Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
BAADA ya mkuu wa mkoa wa Pwani
,mhandisi Evarist Ndikilo,kutoa agizo la kukamatwa kwa uongozi wa
kampuni ya ALPHA CHOICE LTD na KAASAL COMMODITIES LTD kutokana na
kukiuka mkataba wa mnada wa korosho msimu huu ,makampuni hayo yamelipa
kiasi cha fedha ili kujinasua katika agizo hilo..
Viongozi wa makampuni hayo
wameanza kulipa fedha ambayo walidaiwa kushindwa kulipa kwa wakati zaidi
ya sh.bil 5.794 za mnada huo.
Mhandisi Ndikilo,akizungumza na
waandishi wa habari juu ya jambo hilo alisema,viongozi hao wamelipa
baadhi ya fedha ambazo walikuwa wakidaiwa na wakulima wanyonge wa
korosho mkoani hapo.
Alieleza kampuni ya ALPHA CHOICE ltd imekamilisha malipo ya kiasi cha sh.bil .4,202,514,402 ilizokuwa ikidaiwa.
Aidha kwa upande wa kampuni ya
KAASAL COMMODITIES ltd imelipa sh.mil.342,200,768 ambapo awali ilikuwa
ikidaiwa bil.1,591,608,288.
Mhandisi Ndikilo alisema kwamba
kwasasa kampuni ya KAASAL COMMODITIES bado inadaiwa kiasi cha
sh.bil.1,298,407,520 huku ikiahidi kumalizia deni hilo desemba 19 mwaka
huu.
Kufuatia kampuni hiyo kushindwa
kukamilisha deni lake zuio la kusafirisha korosho zake za Mtwara lipo
pale pale na litaendelea hadi hapo itakapokamilisha deni .
Hata hivyo kutokana na kampuni ya
ALPHA CHOICE ltd kulipia deni lake mkuu wa mkoa huyo ameiruhusu kuchukua
korosho zilizokuwa kwenye maghala na kusafirisha.
Mhandisi Ndikilo,alizikumbusha
kampuni hizo na nyingine zinazonunua korosho mkoani Pwani,kuheshimu
mikataba ya ununuzi wa korosho inayowekwa.
“Nazishukuru kampuni hizo kwa
kutii agizo langu na kulitekeleza kwa muda mfupi lakini haifai
kushurutishwa kwa mambo ambayo yanakwenda kimikataba namna hii’
“Haipaswi kuvutana wakati sheria
na taratibu zinajulikana,hawa wakulima wanatumia nguvu zao kupambana na
umaskini sasa ikitokea watu wachache wakawahujumu inakuwa haina tija
katika mustakabali mzima wa maisha yao”alisema mhandisi Ndikilo.
Wiki iliyopita mkuu wa mkoa wa
Pwani,aliyakalia kooni makampuni hayo mawili kwa kuamuru viongozi wa
kampuni hizo wakamatwe na kufunguliwa mashtaka kwa kushindwa kufuata
makubaliano ya mkataba wa mnada wa mwaka huu .
Sambamba na agizo hilo alimuomba
mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendego kuzuia korosho zilizonunuliwa na
makampuni hayo hadi pale watakapolipia korosho walizonunua mkoani Pwani.
Taratibu za makubaliono ya minada zinamtaka mnunuzi akishinda zabuni aandae malipo ndani ya siku saba.
Taratibu za makubaliono ya minada zinamtaka mnunuzi akishinda zabuni aandae malipo ndani ya siku saba.
No comments :
Post a Comment