Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro kwenye ukumbi wa Ofisi za Mamlaka hiyo Desemba 6, 2016.
Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa hifadhi ya Ngorongoro kupeleka pembe za
faru aliyekufa kwa maradhi mwaka 2015 zipelekwe ofisini kwake Desemba 8,
ni baada ya kugundua hujuma za kumuhamisha faru huyo kumpeleka kwenye
hoteli ya kitalii kwenye hifadhi moja ya hifadhi za taifa.(PICHA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU)
Baadhi
ya watumishi wa Mamlka ya Hifadhi ya Ngorongoro wakimsikiliza Waziri Mkuu,
Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Ofisi za Mamlaka hiyo
Desemba 6, 2016
Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania
Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha vyeo Maafisa Wakuu wawili wa
JWTZ kuwa Meja Jenerali kuanzia
tarehe 03 Disemba 2016.Maafisa Wakuu
hao ni;
Brigedia Jenerali George William Ingram ambaye ni Mkuu wa Kamandi
ya Jeshi la Anga, (pichani kulia), na Brigedia Jenerali Michael Wambura Isamuhyo, (pichani kushoto), ambaye ni Mkuu
wa Jeshi la Kujenga Taifa.
Taarifa ya Makao Makuu ya JWTZ iliyotolewa jana Desemba 6 imesema,
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Adolf Mwamunyange kwa niaba ya Rais na
Amiri Jeshi Mkuu anawapongeza na kuwatakia kheri katika vyeo vyao vipya.

No comments :
Post a Comment