Kuelekea Miaka 55 ya Uhuru wa
Tanzania Bara, Serikali imepongezwa kwa Mafanikio yaliyofikiwa katika
kipindi chote tangu awamu ya kwanza hadi awamu ya tano inayoongozwa na
Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Watanzania walio wengi
wanakupongeza Mhe. Rais kwa kazi nzuri unayofanya, mengi tumeyashuhudia
katika kipindi kifupi cha uongozi wako na tunakuombea Mwenyezi akulinde
ili Watanzania wanufaike na yale mema uliyopanga kuwafanyia.
Tumeshudia shirika la ndege
Tanzania (ATCL) likiwa na ndege mpya,mikakati ya ujenzi wa reli yenye
viwango vya Kimataifa (Standard gauge) na mabadiliko makubwa katika
kuwaletea wananchi maendeleo.
Hakika tuna kila sababu ya
kujivunia na kumshukuru Mungu kwa zawadi hii aliyotupatia ambayo ni Rais
Dkt. John Pombe Magufuli,hakika umevaa viatu vya Baba wa Taifa Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere kwa falsafa yako ya “HAPA KAZI TU” inayoakisi
falsafa ya Baba wa Taifa ya “UHURU NA KAZI”.
Kufanya kazi kwa bidii ni
kielelezo cha uhuru wetu na msingi wa Kujenga uchumi wa Viwanda
utakaosaidia kukuza uchumi kwa kasi zaidi katika kipindi hiki ambapo
maendeleo yanahitaji watu kufanya kazi kwa bidii na weledi.
Uhuru wetu umekuwa kielelezo cha
Mafanikio tuliyoyapata katika nyanja mbalimbali ikiwemo
elimu,afya,maji,miundombinu,ujenzi na nyingine nyingi.
Tarehe 9 desemba kila mwaka ni
siku yakutafakari hatua tuliyofikia na kuongeza juhudi kwa kufanya kazi
bila kuchoka ili kuijenga Tanzania mpya ambayo tayari misingi imejengwa
na Kazi kubwa inafanywa na Rais wetu katika kuhakikisha kuwa Tanzania
inakuwa nchi ya asali na maziwa.
Kuimarika kwa huduma za Afya
katika Hospitali ya taifa Muhimbili ni kielelezo kuwa tumeweza
kuitekeleza ile dhana ya Uhuru ni Kujitegemea na kwa hali hiyo
tunamuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye nyakati
zote alisisitiza umuhimu wa kujenga uwezo wa kujitegemea kwa Taifa
letu.
Serikali katika awamu zote tangu
awamu ya kwanza hadi sasa zimekuwa zikiweka kipaumbele katika Sekta
zote zinazochangia ustawi wa maisha ya wananchi hali iliyochangia
kuongezeka kwa shule za msingi ,Sekondari na Vyuo Vikuu ambapo wakati wa
uhuru hakukuwa na chuo Kikuu hata kimoja, sasa tunavyo vyuo Vikuu 48.
Je hayo si mafanikio makubwa
katika Kipindi cha miaka 55?ni wazi kuwa nchi yetu imefakiwa katika
sekta ya elimu na sekta nyingine pia ambazo kwa kiasi kikubwa
zimechochea ukuaji wa uchumi wa Taifa Letu.
Elimu bure ni miongoni mwa
dhamira ya Serikali ya Awamu ya tano ya kuwaletea wananchi wake
maendeleo na kuzidi kuendeleza azma ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere ya kupambana na maadui watatu ambao ni ujinga,maradhi
na umasikini.
Miundo mbinu ya barabara
imeimarishwa ikiwemo barabara za Lami na madaraja ambayo yamerahisisha
mawasiliano kati ya Mkoa na Mkoa,Wilaya na Wilaya,Kata na Kata hadi
ngazi ya vijiji wananchi wanafurahia matunda ya Uhuru wao na rasilimali
za Taifa.
Sekta ya maji pia imeimarika
ukilinganisha na wakati wa uhuru ambapo moja ya miradi mikubwa
iliyotekelezwa na Serikali ni mradi wa maji wa ziwa Victoria hadi
shinyanga na mwingine ni ule wa upanuzi wa mitambo ya Ruvu juu na Ruvu
Chini ambayo imeanza kumaliza tatizo la maji katika Jiji la Dar es
salaam.
Wananchi wote bila kujali
itikadi zetu tunalo jukumu la kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa
rasilimali za Taifa na miundo mbinu iliyopo kwa maslahi ya taifa kwa
kuwafichua wale wote wanaokwaamisha au kuhujumu nia njema ya Serikali
katika kuwaletea wananchi maendeleo.
Sherehe za Uhuru huadhimishwa
kila mwaka inapofika tarehe 9 mwezi Desemba ambapo mwaka huu Kitaifa
zitafanyika Jijini Dar es salaam na Kuongozwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa mara ya kwanza tangu
achaguliwe mwaka mmpja uliopita.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni
“Tuunge Mkono Jitihada za Kupinga Rushwa,Ufisadi na Kuimarisha Uchumi
wa Viwanda kwa Maendeleo yetu.”
Kauli mbiu hii inasadifu yale
ambayo kiongozi wetu mkuu anayasimamia hivyo ni wajibu wetu Watanzania
kuunga mkono juhudi hizi zakuwakwamua Watanzania na kuongeza kasi ya
ukuaji wa uchumi wetu.
No comments :
Post a Comment