Tuesday, November 22, 2016

WAZIRI NAPE AMJULIA HALI MKUU WA MKOA WA TANGA, MARTINE SHIGELLA




Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akimjulia hali Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela aliyelazwa katika wodi ya Sewahaji Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam.Kwa taarifa zilizopo hali ya Mhe. Shigela inaendelea vizuri.(PICHA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI WHUSM)

 Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Madaktari wenzao  kutoka Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya Nchini Australia wakitoa huduma ya  matibabu ya moyo bila ya kupasua kifua (Catheterization) kwa mgonjwa, kwenye taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. (PICHA NA ANNA NKINDA-JKCI)

Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Madaktari wenzao  kutoka Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya Nchini Australia wakitoa huduma ya  matibabu ya moyo bila ya kupasua kifua (Catheterization) kwa mgonjwa. Kushoto ni Afisa Muuguzi Ayoub Mchau, akifuatiwa na Dkt. Daniel Maclennan na kulia ni Dkt. Peter Kisenge.



Waziri Mkuu, Kaasim Majaliwa  akiteta  na  Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda  wakati alipokwenda kwenye hospitali ya mkoa wa Dodoma kumjulia hali Mzee Xavery Kayanza Pinda ambaye ni baba mzazi wa Waziri Mkuu Mstaafu Novemba  22, 2016. Mzee Pinda amelazwa kwenye hospitali hiyo kwa matibabu
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda wakati alipokwenda kwenye hospitali ya Mkoa wa Dodoma kumjulia hali baba mzazi wa Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee Xavery Kayanza Pinda Novemba 22, 2016.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia jambo kati yake na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda baada ya kuwasili kwenye hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako alikwenda kumjulia hali baba mzazi wa Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee Xavery Kayanza Pinda Novemba 22, 2016. Kulia ni Paroko wa Kanisa Kuu Katoliki la Dodoma , Padri Wisi Onesmo na wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


 Ofisa Mkuu wa Biashara wa Kampuni ya Simu ya Tigo,  Shavkat Berdiev (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu kampuni hiyo kutangaza ofa ya Krismas ya Smartphone. Kushoto ni Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga.
 Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga, akizungumza kwenye mkutano huo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.


Na Dotto Mwaibale

Kampuni inayooongoza kwa maisha ya kidijitali Tigo Tanzania  leo imetangaza  kuzindua ofa  mpya  ya Tecno Y3+ Music Smartphone  ambayo imejengewa ndani yake  zana kubwa  ya kuchezesha  ambayo inatoa nafasi ya kutiririsha  kupitia mtandao na hivyo kuwawezesha wateja kufurahia na kusherehekea na wapendwa wao wakati wa kipindi hiki cha kipekee  kinachohusiana na Sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.

No comments :

Post a Comment