Wednesday, November 23, 2016

Watoa Huduma za Afya Nchini Watakiwa Kufanya Kazi kwa Bidii

bakar1

Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohamed Bakari akizungumza katika kongamano la siku tatu la wanachama wa Chama cha Wafiziotherapia Tanzania (APTA) ambalo limeanza Leo jijini Dar es Salaam.

bakar2

Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohamed Bakari akizumgumza katika mkutano huo leo.

…………………………………………………………
Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohamed Bakari amewataka watoa huduma za afya nchini kufanya kazi kwa bidii ili kutoa huduma bora kwa wagonjwa.
Profesa Bakari ametoa kauli hiyo Leo wakati akifungua kongamano la siku tatu la Chama cha Wafiziotherapia Tanzania (APTA) ambalo linafanyika jijini Dar es Salaam.
Mganga Mkuu amewataka kuzingatia maadili ya kazi kwani serikali ya sasa inawataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuongeza uzalishaji na kutoa huduma bora katika maeneo yao ya kazi.
“Mnatakiwa kuwa na nidhamu na kuwahudumia vizuri wagonjwa. Fanyeni kazi kwa bidii kwani ndani ya nchi kuna mabadiliko makubwa ya kiutendaji,” amesema Profesa Bakari.
Kongamano hilo limewakutanisha wataalamu wa afya kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Kilimanjaro Christian Medical Centre KCMC) na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

No comments :

Post a Comment