Wednesday, November 23, 2016

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA "MZEE RUKHSA" IKULU JIJINI DAR ES SALAAM



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi ambaye wakati wa utawala wake alifahamka sana na watanzania kama “Mzee Rukhsa”, Ikulu jijini Dar es Salaam. (PICHA NA IKULU)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi Ikulu jijini Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Rais mstaafu wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa kutoka Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Miriam Mmbaga amewataka maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango nchini kufanya kazi kwa uzalendo ili Tanzania iweze kufikia malengo ya maendeleo endelevu (SDG’s) ifikapo mwaka 2030 kama ilivyokusudiwa.

Kauli hiyo aliitoa mjini Dodoma wakati wa ufunguzi wa warsha ya malengo endelevu kwa maafisa hao kutoka kanda ya Ziwa ambayo imeandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango .

Alisema uhamasishaji kuhusu malengo haya ni matokeo ya Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kukamilisha utekelezaji wa Malengo ya Milenia yaliyokamilika mwaka 2015.

Alisema Mpango wa maendeleo endelevu utatekelezwa kati ya mwaka 2015 hadi 2030, hivyo pia na unajulikana kama agenda 2030 na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama mwanachama wa Umoja wa Mataifa pia iliridhia utekelezaji wa malengo hayo.


Mkurugenzi Msaidizi wa Fedha na Mipango, Servus Sagday akielezea madhumuni ya warsha ya siku tatu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) kwa Maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango nchini iliyofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua warsha hiyo inayoendelea mjini Dodoma katika ukumbi wa mikutano Hazina ndogo.

Alisema katika utekelezaji wa mpango huo lazima maafisa hao wawe na uzalendo kwa kufanya kazi kwa maadili.

“Bila kubadili fikra zao malengo hayo hayataweza kufikiwa, tufanye kazi kwa bidii ili ifikapo mwaka 2030 tuweze kujipima na kuweza

kushangilia kwa kufikia malengo ya maendeleo endelevu 17 ambayo yamejikita kwenye sekta mbalimbali,”alisema Mmbaga.

Alisema changamoto iliyopo kwasasa ni namna ya kufikia malengo hayo, hivyo ni lazima kuwa tayari kubadilika katika kufanya kazi na kutafsiri mambo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa kutoka Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Miriam Mmbaga akifungua warsha ya siku tatu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) kwa Maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango nchini inayoendelea katika ukumbi wa mikutano Hazina ndogo mjini Dodoma chini ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

“Tutakuwa tunavutana, tunaangushana na itatupotezea muda wa kufikia kwenye malengo haya lakini kikubwa ni lazima tukubali malengo ni ya kwetu na yapo kwa ajili yetu sisi wenyewe ili mwisho wa siku tuweze kuyafikia,”alisema.

Aliwahimiza kuwa na moyo wa uzalendo ili kufikia malengo hayo katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zilizopo ikiwemo miundombinu.

“Lazima tutambue watumishi wa umma ni jeshi ambalo linatakiwa kupigana na maadui wale ambao wanatuathiri kijamii na kiuchumi na tuna maadui watatu ujinga, maradhi na umaskini, wakati wanapopigana na maadui waliopo kwenye malengo hayo na sisi tuunganishe na hawa maadui watatu,”alisema.
Alisema inawezekana ikapangwa mipango mbalimbali lakini kama hawatabadili fikra zao na hawapo tayari kufanya kazi ili kufikia malengo hayo kazi itakuwa ni ngumu.

Alibainisha tayari miongozo ya bajeti imeshatumwa kwenye mikoa hivyo kwa mujibu wa miongozo hiyo waangalie namna ya kupanga shughuli, miradi ambayo itajikita kufikia maelngo endelevu 17 ya Kitaifa na kidunia.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) -Idara ya Uchumi, Dr. Wilhelm Ngasamiaku akitoa mada kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) na mchakato wake katika warsha ya siku tatu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) kwa Maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango nchini inayoendelea katika ukumbi wa mikutano Hazina ndogo mjini Dodoma chini ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Idara ya Uchumi, Dr. Joel Silas akitoa mada kuhusu uhusiano wa Maendeleo Endelevu (SDG's) na mpango wa maendeleo wa miaka mitano kwenye warsha ya siku tatu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) kwa Maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango nchini inayoendelea mjini Dodoma katika ukumbi wa mikutano Hazina ndogo chini ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Afisa kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Eva Ruhago akifafanua jambo kwa washiriki wa warsha ya siku tatu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) inayoendelea katika ukumbi wa Hazina ndogo mjini Dodoma chini ya ufadhili wa UNDP.
Pichani juu na chini sehemu ya washiriki wakitoa maoni wakati wa majadiliano katika warsha ya siku tatu ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) kwa Maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango nchini inayoendelea mjini Dodoma katika ukumbi wa mikutano Hazina ndogo chini ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Pichani juu na chini ni sehemu ya Maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Mikoa ya Kagera, Kigoma, Mara, Geita, Simiyu, Shinyanga na Mwanza wanaoishiriki warsha hiyo ya siku tatu yenye lengo la kufikisha ujumbe kwa watu wengi zaidi ili kutimiza kaulimbiu ya Malengo hayo isemayo "Hakuna atakayeachwa nyuma" inayolenga kujenga msingi wa malengo shirikishi yanayodhamiria kuleta maendeleo chanya kwa wote.
Mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa kutoka Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Miriam Mmbaga (walioketi katikati) katika picha ya pamoja na Maofisa Maendeleo ya Jamii na Maofisa Mipango kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo Mikoa ya Kagera, Kigoma, Mara, Geita, Simiyu, Shinyanga na Mwanza wanaoshiriki warsha hiyo ya siku tatu inayoendelea mjini Dodoma chini ufadhili wa UNDP

November 25th is the International Day for the elimination of Violence against women in the world. The 16 days up to December 10th the Human Rights Day is a period of global activism dedicated to fight gender violence in all settings.
UZIKWASA, an organization based in Pangani, Tanzania has become known for its innovative interventions that encourage a voice among rural communities and the development of capable grass roots leaders who are committed to fight gender rights violations in Pangani.
UZIKWASA’s multimedia work that has addressed violence against women and girls (VAWG) includes:
-Pangani FM radio programs
*Leadership that Touches (UongoziwaMguso)
*Womens’ Voice (Sauti ya Mwanamke)
-Feature films
*Fimboya Baba (Father’s Stick: Early and forced marriage)
*Chukua Pipi (Sweet deceit, sexual abuse of school children)
*AISHA (Gang rape)
-Comic books
* Varangati
*Halafu series
*AISHA book
-Forum Theatre and Theatre for Development
-A series of TV spots
On December 2 UZIKWASA will participate in the 16 days of activism by launching theMinna Dada Day, abig bang event to create awareness on VAWGin Pangani District.The campaign is designed to start a deep reflection process among the Pangani people and their leaders about atrocities committed against women and girls including Intimate Partner violence.
Minna dada introductory TV Spot

The following four “Minna Dada” TV spots paint a picture of how intimate partner violence affects the lives of local Pangani women. Cinema Zetu of AZAM TV will broadcast the four spots during the next four months.
1.Economic exploitation of women by their male partners

2. Rape in marriage

3.Male partners hindering women to access leadership position

4.Emotional violence through public humiliation




Aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la katiba Zanzibar, Profesa Abdul Shariff akizungumza kuhusu umuhimu wa asasi za kiraia kutoa elimu juu ya Katiba Pendekezwa katika kongamano lililofanyika Unguja lililoandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA pamoja  na IRI.
Mbunge wa Viti maalum Pemba-Zanzibar, Mheshimiwa Zainabu Mussa Bakari akizungumzia Haki na Wajibu wa mwananchi Kikatiba wakati wa ufunguzi wa Kongamano lililowashirikisha vijana mbalimbali kutoka kisiwani Pemba ili kujadili katiba mpya lililoandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA pamoja  na IRI.
Baadhi ya vijana wakipitia katiba wakati wa kongamano lililowakutanisha vijana hao ili kujadili haki na wajibu wa wananachi katika katiba mpya.
Baadhi ya Vijana wakifuatilia mada
Baadhi ya vijana wakichangia mada
Mtaalam wa Katiba, Ndugu Khamisi akizungumzia msingi na muktadha juu ya katika katika kongamano lililofanyaika Unguja uliowakutanisha vijana.
Baadhi ya Vijana wakifuatilia kongamano lililowakutanisha ili kujadili haki na wajibu wa vijana katika katiba mpya.


Na Mwandishi Wetu
Asasi Ya Vijana, Tanzania Youth Vision Association kwa Kushirikiana Na International Republican Institute zimetoa mafunzo ya kuboresha Uwezo wa Vijana kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba nchini katika visiwa vya Unguja na Pemba, Zanzibar.

Mafunzo hayo yameweza kufikia vijana 250 kwa njia ya Warsha na Vijana na wananchi zaidi ya 200,000 kupitia mitandao ya kijamii.

Ndugu Nasser Mtengera (Mkuu wa Idara ya Habari na Utafiti, TYVA) alielezea Lengo kuu la Mafunzo hayo ni kuongeza uelewa na ushiriki wa Vijana katika mchakato wa Mabadiliko ya Katiba. Katika ufunguzi wa mafunzo hayo Chake chake, Pemba Mheshimiwa Zainab Mussa Bakari (Mbunge) alibainisha kuwa wananchi wana haki ya kikatiba ya kushirikishwa katika mchakato wa katiba mpya na kusema nini wanachotaka kiwemo ndani ya katiba.

Mwanaharakati Na Mtetezi wa HAKI za Binadamu ndugu Deus Kibamba (Mwenyekiti - Jukwaa la Katiba Tanzania) alipata kuwaelezea washiriki wa mafunzo hayo historia ya mchakato wa mabadiliko ya Katiba, Ushiriki wa wananchi katika mchakato wa Katiba, hatua muhimu katika Mchakato wa utengenezaji Katiba, Mambo ya Msingi yaliyomo katika Katiba inayopendekezwa na Mambo muhimu kuelekea kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa.

Alidokeza pia, katika mchakato wa Katiba, hasa katika hatua ya Bunge la Katiba ulikosa maridhiano ya Kitaifa. kuna haja ya kuwepo mkutano wa kitaifa utajaowaleta wadau na jopo la wataalamu mbalimbali kwa ajili ya kunyambua yale mambo yanayoendelea kuleta ukakasi linapaswa kufanyika. Alidokeza pia Mchakato wa katiba ulitegemewa kuwa kimbilio la kutatua kero za Muungano.

Afisa kutoka IRI, Tony Alfred aliwatarifu Vijana washiriki kusoma kuhusu Katiba na wanaweza kupata habari na taarifa zaidi kuhusu Katiba kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kwa kutuma Neno "katibayetu" Kwenda 0684996494.

Ndugu Saddam Khalfan (Katibu Mtendaji wa TYVA) aliwashukuru vijana na wadau mbalimbali kwa kuhudhuria na kufanikisha mikutano ya Unguja na Pemba huku akihimiza Mkakati wa ushiriki wa vijana ni mahsusi kwa ajili ya kuhakikisha kuboresha maendeleo ya vijana kwa Tanzania ya sasa na baadae. Tanzania ambayo inatamaniwa na kundi la vijana lakini sambamba na makundi mengine yote.



Vijana wajasiliamali wakiwa katika mafunzo ya kutengeneza urembo wa Shanga baada ya kupata somo kutoka kwa Mkufunzi Peninnah katika mafunzo hayo Biashara kwa Vijana kuelekea Soko la AFrika Mashariki yanayoendelea kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. Picha na Mafoto Blog
Vijana wakichangamkia bidhaa kuanza kutengeza Shanga
Vijana wajasiliamali wakirefresh kwa kucheza mchezo wa kujichangamsha..........
Mkufunzi akitoa maelekezo ya mchezo huo..

No comments :

Post a Comment