Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Madaktari
wenzao wa Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya Nchini Australia
wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa moyo kwa njia ya kufungua kifua na
kuziba tundu la moyo. Kulia ni Dkt. Bingwa wa Upasuaji Hussein Hassan
akifuatiwa na madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo kwa watoto Dk.
Godwin Godfrey (kushoto) na Dkt. Benjamin Bierbach.
Madaktari bingwa wa moyo
pamoja na wauguzi kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa
kushirikiana na Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya Nchini
Australia wakiendelea na kazi ya kumfanyia mgonjwa upasuaji wa moyo kwa
njia ya kufungua kifua na kuziba tundu lililopo kwenye moyo. Taasisi
hizo hivi sasa ziko katika kambi maalum ya siku sita ya upasuaji kwa
wagonjwa wa moyo, katika kambi hiyo wagonjwa 20 wanarajiwa kupata
matibabu.
Picha na Anna Nkinda – JKCI
No comments :
Post a Comment