Wednesday, October 26, 2016

MCHAPALO WA KUADHIMISHA MIAKA 71 YA UN

Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakigonga 'cheers' ya kutakiana kheri na afya njema katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika Oktoba 24, 2016 jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa kwake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) kuzungumza na wageni waalikwa.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika nyumbani kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakigonga 'cheers' ya kutakiana kheri na afya njema katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika Oktoba 24, 2016 jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez baada ya kugonga glass.
Shamra shamra za miaka 71 ya Umoja wa Mataifa zikiendelea jukwaa kuu.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy (kushoto) wakitazama 'documentary' fupi kwenye hafla hiyo.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) pamoja na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida.
MC wa hafla mchapalo ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa, Edgar Kiliba kutoka ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiendesha hafla hiyo.
Wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa wakibadilishana mawazo Anthony Rutabanzibwa (kushoto) na Amon Manyama katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Awa Dabo (katikati) kwenye hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Emslies Travel Ltd. Jaffer Hirji (kushoto) wakati wa hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Baadhi ya wageni waalikwa na waheshimiwa mabalozi wakibadilishana mawazo kwenye hafla hiyo.

Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu (kulia) akiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Picha juu na chini ni baadhi ya wageni waalikwa na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa.






Nguse Nyerere akiwa na baadhi ya Maafisa wenzake wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa.
Edgar Kiliba (katikati) wa ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa akibadilishana mawazo na baadhi ya wageni waalikwa kwenye hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika Oktoba 24, 2016 jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa wakibadilishana mawazo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja.

Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Edgar Kiliba na Beatrice Mkiramweni katika picha ya pamoja.

Baadhi ya madereva wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja kwenye hafla hiyo.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula (Mb) katika hafla ya kushehereka miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika Oktoba 24, 2016 jijini Dar es Salaam.
Geofrey Adroph BLOGGER P.O.BOX 24793, Mob: +255 755 274953 /+255 713 363965, Email: pamojapure@gmail.com. Blog: http://www.pamoja.co.tz/ DAR ES SALAAM, TANZANIA 2016-10-26 14:30 GMT+03:00 Zainul Mzige :
Ziafuatazo ni picha za hafla mchapalo (Cocktail Party) ya kukata na shoka ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu ulipoanzishwa iliyofanyika nyumbani kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali mashuhuri kutoka taasisi mbalimbali za serikali, binafsi pamoja na mabalozi wa nchi mbalimbali.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa India nchini, Sandeep Arya (kulia) mara baada ya Balozi huyo kumaliza mazungumzo na Waziri ambayo yalifanyika ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo. Mazungumzo hayo yalikuwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na India. (Picha na zote Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akimsikiliza Balozi wa India hapa nchini, Sandeep Arya (kulia) wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri huyo ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na India
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akimfafanulia jambo Balozi wa Norway hapa nchini, Hanne-Marie Kaarstad (kulia) wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri Nchemba ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Norway
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akimfafanulia jambo Balozi wa Rwanda, Eugene Kayihura (kulia) wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri Nchemba ofisini kwake, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Norway nchini, Hanne-Marie Kaarstad (kushoto) kwa ajili ya kufanya mazungumzo naye kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Norway na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri huyo, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya

TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA KICHWA KIKUBWA NA MGONGO WAZI MOI MUHIMBILI JIJINI DAR

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Moi akifungua rasmi sherehe za kuadhimisha siku ya mtoto wa kichwa kikubwa na Mgongo wazi Duniani,ambapo alisema wanakazi kubwa ya kutoa matibabu kwa watoto wenye matatizo ya mtindio wa ubongo na mifupa na mpaka sasa watoto takribani 202 wameshafanyiwa upasuaji na zoezi linaendelea Nchi nzima.
Mwenyekiti wa chama cha wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi Bw. Hakim ambaye nae mtoto wake anamatatizo kama hayo akielezea  kuwa kuna umuhimu wa kutoa elimu kwa kuwa watu wengi wanahusisha tatizo hilo na imani potofu, aliongeza kuwa watoto waliofanyiwa upasuaji mkoa wa Mbeya ni 18, Morogoro 12, Mwanza 50, na Izazi 14. na wamefanikiwa kuokoa Maisha ya watoto 185 katika mikoa 16 Tanzania.
Meneja wa Nakiete akitoa neno wakati wa Maadhimisho hayo
Mmoja wa wazazi akiwa na Mwanae mwenye tatizo la Kichwa kikubwa
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Moi (Kushoto) akipokea Msaada kutoka Duka la madawa la Nakiete
Madam Sophia Mbeyela (Kulia) akitoa msaada kwa watoto hao
Baadhi ya wazazi wakiwa na watoto wao wenye vichwa vikubwa
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Moi wapili kutoka kushoto akipokea Msaada viti 15 vya kutembelea 'wheel chair' watoto kutoka kwa Mohamed Punjan Foundation
Baadhi ya wauguzi wakiwa katika maadhimisho hayo
Baadhi ya wazazi na walezi na wazazi wenye kichwa kikubwa na Mgongo wazi wakiwa katika maadhimisho hayo.
Picha zote na Fredy Njeje


Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya YARA Tanzania Ltd, Alexandre Macedo, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Usafirishaji wa mbolea kwa njia ya Reli TRL, Uzinduzi huo umefanyika leo kwenye Ofisi za YARA Tanzania zilizopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji wa TRL, Focus Makoye Sahani.

Azungumzia uzinduzi huo Mkurugenzi huyo alisema kuwa YARA kwa kushirikiana na TRL na SAGCOT, wameamua kuzindua njia hiyo ya usafirishaji ili kupunguza gharama za usafirishaji kwa kutumia barabara na maji ili kuwafikia walengwa kwa wakati na kwa gharama nafuu, ambapo awali kusafirisha Tani moja kutoka Viwandani Ulaya hadi jijini Dar es Salaam, ilikuwa ni Dola za Kimarekani 40, kwa Tani moja na Dar es Salaam hadi Tabora ni Dola za Kimarekani 100 kwa Tani moja kwa njia ya barabara.

Aidha Macedo, alisema kuwa kuamua kutumia usafiri wa Treni sasa usafiri utashuka kwa asilimia 3


 Mfalme Mohammed  wa Morocco akibusu Masahaf kabla ya kumkabidhi Waziri Mkuu Kasim Majaliwa katika hafla fupi ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa msikiti kwenye eneo la BAKWATA Kinondoni jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.  Kulia ni Mufti Mkuu wa Tanzania, Abukary Zubeir. Jumla ya Masahaf 10000 zilikabidhiwa na Mfalme huyo.(Picha n Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Mfalme Mhammed  wa Morocco na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakishuhudia wakati Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakary Zubeir (kulia)  akitia saini Makubaliano ya ujenzi wa Msikiti kwenye eneo la BAKWATA, Kinondoni jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Mkuu wa mkoa wa Tanga, Martine Shigella(Julia), akiwa na ujumbe wa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania, walipotembelea Bandari ya Tanga na kujionea fursa za uwekezaji hapa nchini.

Kaimu Meneja Bandari Tanga, Hendry Arika, akiwafahamisha mabalozi wa nchi za Ulaya wanaowakilisha nchi zao nchini wakati walipotembelea Bandari ya Tanga kuangalia fursa za uwekezaji kufuatia ujio wa mradi wa bomba la mafuta Tanga.
Kaimu Meneja Bandari Tanga, Hendry Arika, akiwafahamisha mabalozi wa nchi za Ulaya wanaowakilisha nchi zao nchini wakati walipotembelea Bandari ya Tanga kuangalia fursa za uwekezaji kufuatia ujio wa mradi wa bomba la mafuta Tanga.


Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Hendry Arika akizungumza na waandishi wa habari leo eneo litakalojengwa bomba la mafuta kijiji cha Chongoleani Tanga wakati wa ziara ya mabalozi 12 kutoka Jumuiya ya Ulaya wanaowakilisha nchini zai nchini.

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Tanga, Daudi Mayeji, akiwaonyesha mabalozi wa nchi  12 za Ulaya wanaoziwakilisha nchini zao nchini ramani ya eneo litakapojengwa bomba la mafuta kijiji cha Chongoleani Tanga ziara waliyoifanya leo.

Mkuu wa Huduma za Fedha kwa njia ya simu wa Tigo Ruan Swanepoel (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu, Wateja Tigo Pesa kuvuna 6.04bn/- (dola 2,763,636) gawio la kumi la robo mwaka. Kulia ni Meneja Masoko na Usambazaji Huduma za Kifedha wa Tigo, Catherine Rutenge.
Meneja Masoko na Usambazaji Huduma za Kifedha wa Tigo, Catherine Rutenge (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.


Na Dotto Mwaibale

Kampuni inayoongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali Tigo imetangaza  gawio jingine  la robo mwaka la shilingi bilioni 6.04 (sawa na dola za Marekani 2,763,636)  kwa watumiaji wa Tigo Pesa  ikiwa ni mara ya kumi katika mfululizo wa kampuni hiyo ya simu kugawa faida hiyo kwa watumiaji wake wa huduma ya fedha kwa njia ya simu.

NA MWANDISHI MAALUM
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  amesema serikali itaendelea kudumisha uhusiano na ushirikiano wa kihistoria  kati ya Tanzania na India ambayo yamedumu kwa muda mrefu hasa katika sekta mbalimbali ikiwemo za elimu,afya na biashara.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo leo 25-Oct-2016 wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa India nchini Sandeep Arya Ikulu jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais amesema mahusiano kati ya Tanzania na India yamesaidia kunufaisha wananchi wa nchini mbili hasa katika masuala ya kibiashara,miradi ya maendeleo na hivyo mahusiano hayo ni muhimu yakaendelezwa na kudumishwa.

Makamu wa Rais katika mazungumzo na balozi huyo wa India hapa nchini Sandeep Arya pia ameiomba serikali kuisaidia Tanzania katika mpango utakaosaidia wakulima kupata taarifa mbalimbali zinazohusu kilimo na masoko ya bidhaa zao kupitia simu za mkononi ili kuondoa usumbufu mkubwa wanaopata wakulima kwa sasa hasa kuhusu masoko.

Kwa upande wake, Balozi wa India nchini Tanzania Sandeep Arya amemhakikishia Makamu wa Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan serikali yake itakuwa bega kwa bega na Tanzania katika kuhakikisha wananchi wa pande Mbili wananufaika na mahusiano yaliyopo.

Balozi Sandeep Arya amesisitiza kuwa serikali ya India itaendelea kuisaidia Tanzania katika uimarishaji wa teknolojia ya habari na mawasiliano pamoja na miradi ya maendeleo na uimarishaji wa shughuli za kiuchumi.

Wakati huo huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Sudan nchini Tanzania Mahgoub Sharfi mazungumzo yaliyolenga pamoja na mambo mengine kuhusu namna ya kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Sudan.
Pichani Makamuwa Rais, akiwa na mazungumzo na Baloziwa Indianchini Tanzania, Sandeep Arya, Ikulu jijini Dar es Salaam, Oktoba 25, 2016. (PICHA NA VPO)

Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu (kushoto) akipewa ushauri na Mtaalam wa magonjwa ya Saratani ya matiti  wa hospitali ya AAR Dkt. Zacharia Kabona wakati wa zoezi la kuwapima ugonjwa huo wafanyakazi wa kampuni hiyo uliofanyika  makao makuu ya kampuni hiyo Mlimani City leo Oktoba 25, 2016 jijinji Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa saratani ya matiti duniani.


Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakipewa ushauri na Mtaalam wa magonjwa ya Saratani ya matiti  wa hospitali ya AAR Dkt. Zacharia Kabona,(kulia) wakati wa zoezi la upimaji wa ugonjwa huo  kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo uliyofanyika  makao makuu ya kampuni hiyo Mlimani City leo jijinji Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa saratani ya matiti duniani.


Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania , wakimsikiliza kwa makini Meneja wa mauzo Happiness Shuma alipokuwa akitoa mada kuhusiana na elimu ya ugonjwa wa saratani ya matiti, wakati wa zoezi la kuwapima wafanyakazi wa kampuni hiyo lililofanyika makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Mlimani city jijini Dar es Salaam,ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa saratani duniani.

Meneja wa mauzo Happiness Shuma  akitoa mada kuhusiana na elimu ya ugonjwa wa saratani ya matiti, wakati wa zoezi la kuwapima wafanyakazi wa kampuni hiyo lililofanyika makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Mlimani city jijini Dar es Salaam,ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya mwezi wa saratani duniani.

No comments :

Post a Comment