Thursday, October 27, 2016

BALOZI SEIF AFUNGUA MKUTANO WA KIKANDA WA KIMATAIFA WA SEKTA YA MAFUTA NA GESI ASILIA, ZANZIBAR

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wa pili kutoka kulia akiwa pamoja na Viongozi waandamizi kabla ya kuufungua Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi na kufanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Park Hyatt Mjini Zanzibar.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia wakimsikiliza Balozi Seif wakati akiufungua Mkutano huo.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia wakimsikiliza Balozi Seif wakati akiufungua Mkutano huo.
Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia.
 
Picha na – OMPR – ZNZ.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema licha ya juhudi kubwa zinazochukuliwa na Mataifa na Taasisi za Kimataifa kuunga mkono miradi ya Kiuchumi inayoanzishwa na Serikali, lakini bado nguvu za pamoja kwa Taasisi za ndani zinahitajika katika kushirikiana na Serikali kiuendeleza miradi hiyo.

Alisema zipo jitihada zinazofanywa na Serikali kuandaa Sera,mipango na Mikakati ya kujiandaa na miradi mipya kama Mafuta na Gesi asilia ambayo kufanikiwa kwake mbali ya kuinua pato la Taifa lakini pia inaweza kutoa ajira kubwa itakayopunguza wimbi la Vijana wasiokuwa na kazi za kujikidhi kimaisha.

Balozi Seif Ali Iddi alitoa kauli hiyo wakati akiufungua Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi na kufanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Park Hyatt Mjini Zanzibar.

Alisema ingawa usimamizi wa kuendesha miradi ya sekta ya Mafuta na gesi asilia hupangwa na kupewa dhamana wawekezaji kulingana na kiwango cha taaluma walichonacho, hata hivyo jukumu la kusimamia sera litabakia kuwa mikononi mwa wazalendo wenyewe ili kujilinda mapema na changamoto za kimazingira zisizoepukika katika kuendesha miradi hiyo.

UJERUMANI WAIPIGA JEKI SAUTI ZA BUSARA 2017

DK. SHEIN AWAHAKIKISHIA WAZANZIBAR WATAENDELEA KUWA NA AFYA NJEMA, ELIMU BORA NA WAKIISHI KWA AMANI NA UTULIVU

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Sayansi za Afya Mbweni Dr. Haji Mwita Haji alipomuwakilisha Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein katika mahafali ya Pili ya Chuo cha Madaktari Zanzibar na yale ya 23 ya Chuo cha Taaluma za Sayanzi za Afya Mbweni.
Balozi Seif akisalimiana na wahadhiri walioendesha mafunzo ya Udaktari Zanzibar kutoka Chuo Kikuu cha Matanzas cha Nchini Jamuhuri ya Watu wa Cuba Tawi la Zanzibar hapo katika viwanja vya chuo cha Taaluma ya Sayansi za Afya Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
 Baadhi ya wahitimu waliomaliza mafunzo ya Udaktari chuo cha Udaktari Zanzibar wakila kiapo cha utii katika kukabiliana na majukumu yao watakayopangiwa hapo baadaye.
Baadhi ya wahitimu waliomaliza mafunzo ya Udaktari chuo cha Udaktari Zanzibar wakila kiapo cha utii katika kukabiliana na majukumu yao watakayopangiwa hapo baadaye.
Mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Matanzas cha Nchini Jamuhuri ya Watu wa Cuba Dr. Zailit Gonzalet Cruiz akimuhudhurisha Mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Udaktari katika chuo cha Udaktari Zanzibar.

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA) YAONGEZA VYANZO VIWILI VYA MAJI .

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,Prof Faustine Bee (kushoto) akimuongoza Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge kuelekea katika chanz cha Mkashilingi kilichopo wilyani Hai kwa ajili ya uzinduzi, kulia kwa Waziri ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA).Joyce Msiru.
Waziri wa Maji na Uwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge akizungumza wakati wa uzinduzi wa chanzo cha maji cha Mkashilingi kilichopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wakimsilikiliza Waziri wa Maji na Umwagiliaji (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa chanzo cha Mkashilingi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadiki akizungumza katika uzinduzi huo.

TANZANIA YAWAKARIBISHA WAKOREA KUSINI KUWEKEZA SEKTA YA VIWANDA

Mkuu wa kitengo cha utafutaji Rasilimali, kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar, Sabra Issa Machano, akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania Zanzibar, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akimpongeza Mkuu wa kitengo cha utafutaji Rasilimali, kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar, Sabra Issa Machano, baada ya akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania Zanzibar, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akifuatilia kwa makini wakati Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji kutoka kituo cha uwekezaji Tanzania-TIC, John Mnali, akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Mjini Seoul, Korea Kusini. Kulia kwake ni Mkuu wa Kitengo cha Utafutaji Rasilimali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar-Sabra Issa Machano.
Mkurugenzi wa Uhamasishaji uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania-TIC, John Mnali (Katikati), akibadilishana mawasiliano na mmoja wa wafanyabiashara walioonesha nia ya kuweka nchini Tanzania baada ya Mkurugenzi huyo kuwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), akibadilishana mawasiliano na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya MarineBio, Heo Yun-Young, ambaye kampuni yake inataka kuwekeza kiwanda cha kusindika zao la mwani linalopatikana katika Bahari Kuu ya Hindi nchini Tanzania.

DK. SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA, SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akitoa maelekezo wakati alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 27/10 /2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja
Baadhi ya maafisa wa Vikosi vya SMZ wakiwa katika kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 cha Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ,kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi vya SMZ wakiwa katika kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 cha Uongozi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ,kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein

UBALOZI WA PAPA, MAKANISA YAAMUA KUJENGA OFISI DODOMA

WAZIRI MBARAWA APOKEA RIPOTI YA AWALI YA UPIMAJI WA MIPAKA KATIKA KIWANJA CHA NDEGE CHA KIA.

MAJALIWA AKUTANA NA ASKOFU MKUU BEATUS KINYAIYA WA DODOMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Beatus Kinyaiya kabala ya mazungumzo yao, Ofisini kwa Waziri Mkuu mjini Dodoma Oktoba 27, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Beatus Kinyaiya (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii, Peter Maduki (kushoto), Ofisini kwake jijini Dar es salaam Oktoba 27, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Beatus Kinyaiya, Ofisini kwake mjini Dodoma Oktoba 27, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

ABU DHABI YAAHIDI KUENDELEZA KUKUZA UHUSIANO NA TANZANIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425


OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ikulu, Dar es Salaam,

Mrithi wa Mfalme wa Abu Dhabi na Kaimu Rais, Mtukufu Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan amemuahidi Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli kuwa nchi hiyo imedhamiria kuendeleza na kukuza zaidi uhusiano wake na Tanzania hususani katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Mtukufu Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan ametoa ahadi hiyo kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi Bw. Mohamed Al Suwaidi aliyekutana na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli leo tarehe 27 Oktoba 2016.

Mfuko wa maendeleo wa Abu Dhabi unashirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali na katika mazungumzo ya leo Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo ameonesha nia ya kushirikiana zaidi na Tanzania katika maeneo ya ujenzi wa miundombinu ikiwemo reli na barabara, usafiri wa anga na madini.

Pamoja kumshukuru Mrithi wa Mfalme wa Abu Dhabi na Kaimu Rais Mtukufu Sheikh Mohamed bin Zayed Al Nahyan, Rais Magufuli ameialika nchi hiyo kupitia mfuko wake wa Maendeleo na wadau wengine wa maendeleo kuja kuwekeza hapa nchini katika miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa bandari, ujenzi wa viwanda, kilimo, uvuvi, gesi na kushirikiana katika ujenzi wa reli ya kati ambayo itazinufaisha nchi nyingine saba za Afrika Mashariki na kati ambazo hazina bandari.

Tanzania imeamua kujenga reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) na tayari katika bajeti yetu tumetenga Shilingi Trilioni 1 kwa ajili ya kuanza ujenzi, hivyo tunawakaribisha Mfuko wa Maendeleo wa Abu Dhabi kushirikiana nasi, wapo wengi ambao wamejitokeza kushirikiana nasi lakini na nyie pia tunawakaribisha, mnaweza kuchukua sehemu ya reli na mkaijenga” amesema Rais Magufuli.

Aidha, Dkt. Magufuli ameutaka mfuko huo kufupisha muda unaotumika katika mchakato wa kuanza utekelezaji wa miradi ili kuharakisha matokeo yake na manufaa kwa wananchi.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Oktoba, 2016

BILIONEA WA MAKASINO JAMES PACKER AVUNJA UCHUMBA NA MARIAH CAREY

IKUNGI HALF MARATHON 2016

REAL MADRID YAFANYA KUFURU KWA KUISHUSHIA MVUA YA MAGOLI LEONESA

Timu ya Real Madrid imeishushia kipigo cha paka mwizi timu ndogo ya daraja la tatu ya Cultural Leonesa kwa kuichakaza kwa magoli 7-1 katika mchezo wa kombe la Copa del Rey.

Katika mchezo huo ambao Madrid waliwapumzisha Cristiano Ronaldo, Gareth Bale na Karim Benzema, walipata goli la kwanza baada ya mchezaji wa zamani wa West Brom beki Gianni Zuiverloon, kujifunga

Magoli mengine ya Real Madrid yalifungwa na Marco Asensio na Alvaro Morata waliofunga magoli mawili na Nacho na Mariano walifunga moja kila mmoja.
                 Gianni Zuiverloon akiwa amempoteza mahesabu kipa wake na kujifunga 
                                                     Marco Asensio akifunga goli la pili la Real Madrid

CHELSEA YAZAMA MBELE YA WEST HAM HUKU MASHABIKI WAKIPIGANA

Ugomvi baina ya mashabiki wa West Ham na Chelsea umeibuka mwishoni mwa mchezo wao wa jana wa kombe la EFL, ambao Chelsea walilala kwa magoli 2-1 kwenye dimba la London.

Chupa za plastiki na viti vilirushwa na mashabiki mwishoni mwa mechi hiyo huku mamia ya mashabiki wakorofi wakihusika na tukio hilo baya kutokea katika soka.

Katika mchezo huo Cheikhou Kouyate alifunga kwa kichwa kabla ya mapumziko na kisha Edimilson Fernandes akaongeza la pili kwa shuti la yadi 18 huku Gary Cahill akiifungia Chelsea goli pekee katika dakika ya 90.
Kipa wa Chelsea akiruka bila ya mafanikio kuzuia mpira wa kichwa uliopigwa na Cheikhou Kouyate
                       Edimilson Fernandes akiachia shuti lililzaa goli la pili la West Ham
                    Mashabiki wakizozana punde tu baada ya kumalizika kwa mechi hiyo

JUAN MATA AIPELEKA MANCHESTER UNITED ROBO FAINALI KOMBE LA EFL

Juan Mata amefunga goli na kuipatia ushindi Manchester United dhidi ya majirani zao Manchester United katika mchezo wa kombe la EFL na kutinga hatua ya robo fainali.

Mhispania huyo aliachia shuti la chini lililojaa wavuni akiunganisha mpira uliogongwa nyuma na Zlatan Ibrahimovic na kujihakikishia kukutana na West Ham robo fainali.

Paul Pogba aligonga mwamba muda mchache kabla ya kufungwa goli hilo, ambapo mpira katika mchezo huo ulichangamka katika kipindi cha pili.
                                    Juan Mata akiachia shuti lililomshinda kipa na kujaa wavuni 
                Kipa na wachezaji wa Manchester City wakiwa hoi baada ya kutinga goli hilo

No comments :

Post a Comment