Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na
Uchukuzi, Profesa, Makame Mbarawa (kushoto), akihutubia wakati akifungua
Semina ya 26 ya utoaji elimu endelevu kwa Wabunifu Majengo na
Wakadiriaji Majenzi Dar es Salaam leo asubuhi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, Ambwene Mwakyusa akizungumza katika semina hiyo.
Waziri wa Ujenzi,
Mawasiliano na Uchukuzi, Profesa, Makame Mbarawa (kushoto), akipeana
mkono na Msaji wa Bodi hiyo Jehad Jehad baada ya kumaliza kutoa hutuba
yake.
Wadau wa sekta ya ujenzi wakiwa kwenye semina hiyo.
Wadau wa sekta ya ujenzi wakiwa kwenye semina hiyo.
Taswira meza kuu katika semina hiyo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi Waziri Mbarawa.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi, Waziri
Mbarawa (aliyekaa katikati), Wengine kutoka kulia waliokaa ni Mkurugenzi
wa Huduma na Ufundi kutoka Wizara ya Ujenzi, Profesa Mhandisi William
Nshana, Mwenyekiti wa Bodi, Ambwene Mwakyusa, Msajili wa Bodi, Jehad
Jehad na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili, Dk.Adelina Kikwasi.
Na Dotto Mwaibale
WAZIRI wa Ujenzi, Mawasiliano na
Uchukuzi, Profesa, Makame Mbarawa, ameitaka Bodi ya Usajili Wabunifu
Majengo na Wakadiriaji Majenzi kuwafutia leseni wadau wa sekta ya ujenzi
watakao bainika kuomba au kupokea rushwa.
Katika hatua nyingine Profesa Mbarawa
ameitaka Bodi hiyo kuandaa orodha ya wakadiriaji majenzi na wabunifu
majengo wasiyofuta maadili ya kazi zao ili iwekwe hadharani na wasipate
tenda za kufanya kazi popote.
Profesa Mbarawa ametoa kauli hiyo wakati
akifungua Semina ya 26 ya utoaji elimu endelevu kwa Wabunifu Majengo na
Wakadiriaji Majenzi Dar es Salaam leo na kueleza kazi yoyote iwe nzuri
na bora ni lazima kuepuka rushwa na kufuata maadili na kanuni za kazi.
“Napenda niwagize bodi kuanzia sasa
nataka wakadiriaji majenzi na wabunifu majengo na wadau wote wa sekta ya
ujenzi ambao ni wara rushwa muwafutie leseni zao ili wasiweze kupata
tenda au kutoa tenda.Maadili katika kazi zenu ni jambo la msingi na si
vinginevyo,”alisema Profesa Mbarawa.
Mbarawa aliigiza bodi hiyo kuandaa
orodha ya watakao kuwa si waadilifu ili kuonyesha katika jamii kuwa
hawa hawasitahili kupewa tenda ya aina yoyote.
Alisema baada ya kuandaa orodha hiyo ni
vizuri ikatangazwe hata katika vyombo vya habari ili iwe fundisho kwa
wengine wenye vitendo hivyo.
Mbarawa aliwataka wakadiriaji majenzi na
wabunifu majengo nchini kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo katika
serikali ya Awamu ya Tano ili kuweza kjiongezea mitaji.
“Kuna mradi wa ujenzi wa Reli ya kiwango
cha kisasa unakuja na serikali imetenga Sh. Trilioni 1, lazima kutakuwa
na ujenzi wa majengo hiyo ni fursa mbayo mnaweza kuitumia kujiongezea
uwezo, lakini kama mtafanya kazi kwa kuungana njia hiyo inaweza
kuwasaidia kupata tenda hizo.” alisema.
Awali, akizungumza katika semina hiyo,
Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Ambwene Mwakyusa, alisema semina hizo zimekuwa
na faida kwa wakadiriji majenzi na wabunifu, kwani zinawaongezea uwezo
wa kujua mambo mbalimbali na kwamba zimekuwa zikifanyika kila mwaka mara
mbili na zimewanufaisha wadau wa sekta ya ujenzi 5,328.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akishuhudia
Dereva wa Basi la Tahmeed (kulia) akipimwa kilevi na Trafiki Nuru Mvungi kabla
ya Basi lake kuruhusiwa na safari. Masauni alifanya ziara ya kushtukiza katika
Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam pamoja na
Kibaha mkoani Pwani leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa tai) akielekea
Stendi Kuu ya Mabasi ya mikoani Ubungo, jijini Dar es Salaam wakati alipofanya
ziara ya kushtukiza yenye lengo la kukagua mabasi mabovu pamoja na usalama wa
abiria katika Stendi hiyo pamoja na Stendi ya Kibaha mkoani Pwani. Masauni alilizuia Basi la Shambarai lenye namba za usajili T419
BUF na Basi la Karachani (T253 CLZ) ambayo yalikuwa yanaenda Tanga
kutokuendelea na safari zake kutokana na ubovu wa mabasi hayo ambayo yangeweza
kuhatarisha maisha ya abiria. Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani
nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiwauliza abiria wa
Basi la Harambee linalofanya safari zake Dar es Salaam kwenda Arusha, maswali
mbalimbali kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo wakati wanaposafiri. Masauni
alifanya ziara ya kushtukiza katika Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani,
Ubungo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani
nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akikagua mikanda
katika Basi la Shambalai wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Stendi
Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam leo. Picha
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akioneshwa
na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga,
tairi la Basi la Shambalai ambalo halina ubora kwa ajili ya kusafirisha abiria.
Hata hivyo Masauni aliagiza basi hilo lizuiwe kufanya safari na pia kuchukuliwa
hatua kali kwa Mmiliki wa basi hilo pamoja na Dereva. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyevaa tai)
akizungumza na madereva wa Basi ya mikoani pamoja na wa magari madogo ya mizigo
yanayopaki Stendi Kuu Ubungo, jijini Dar es Salaam. Masauni aliwataka madereva
hao kufuata sheria za usalama barabarani. Hata hivyo, madereva hao walilalamika
kuwa hawana mikataba ya kazi zao. Masauni alifanya ziara ya kushtukiza katika
Stendi hiyo, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na
waandishi wa habari, Picha ya Ndege Kibaha, Pwani, mara baada ya kukamilisha
ziara yake ya kukagua mabasi mabovu na usalama wa abiria. Masauni alifanya
ziara ya kushtukiza katika Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani, Ubungo jijini
Dar es Salaam pamoja na Kibaha mkoani Pwani leo. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la
Polisi Mkoa wa Pwani, Bonaventura Mushongi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akihoji
usalama wa mtoto baada ya kugundua siti moja kukaa watoto wawili jambo ambalo
ni hatari kwa usalama wa abiria. Masauni alifanya ziara ya kushtukiza katika
Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani, Ubungo jijini Dar es Salaam. Na baadaye
alielekea Stendi ya Kibaha kuendelea na ukaguzi huo wa mabasi. Picha
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkurugenzi
wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo kushoto akizungumza katika
kikao na Mabalozi wanao ziwakilisha nchi za Afrika hapa nchini.
Mazungumzo yao yalijikita katika kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na
nchi zao. Mkutano huo umefanyika katika Hoteli ya Slipway iliyopo
Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Septemba, 2016
Sehemu
ya Mabalozi kutoka nchi za Afrika wakiwa kwenye Mkutano. Kutoka kulia
ni Balozi wa Uganda hapa nchini, Mhe. Doroth Samali Hyuha, akifuatiwa na
Balozi wa Misri nchini, Mhe. Mohamed Yasser El shawaf na Balozi wa
Msumbiji, Mhe. Monica Patricio Mussa
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika, Bw. Suleiman Saleh wakati wa mkutano kati ya Wizara na Mabalozi wa Afrika waliopo nchini
Mkutano ukiendelea
Meneja
Mkuu wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nd. Ali Ibrahim Kilupi kushoto
akimkabidhi msaada wa mtambo maalum wa mawasiliano ya Simu za ndani {
Inter call } Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd.
Joseph Abdulla Meza kwa ajili ya Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ
Mjini Dar es salaam.
Wa kwanza kutoka Kulia anayeshuhudia tukio la makabidhiano hayo ni
Mratibu Mkuu wa Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam
Ndugu Issa Mlingoti Ali.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Meza akiuwasilisha
msaada huo wa Mtambo wa mawasiliano ya Simu kwa mlengwa Mratibu Mkuu wa
Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam Ndugu Mlingoti.
Picha na – OMPR – ZNZ.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Joseph Abdulla Meza alisema jamii na hasa wananchi Wazalendo wenye uwezo wanapaswa kuendelea kujenga tabia ya kusaidia nguvu katika kupambana na changamoto zinazoikabili serikali pamoja na wananchi katika maeneo mbali mbali nchini.
Alisema mfumo uliozoeleza kwa kipindi kirefu sasa katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ni ule uliotegemewa zaidi wa kupokea misaada kutoka Mashirika, taasisi na mataifa ya nje ya nchi.
Ndugu Joseph Abdulla Meza alitoa kauli hiyo wakati akipokea msaada wa mtambo maalum wa mawasiliano ya ndani { Inter call }kwa ajili ya Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam uliotolewa na Uongozi wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nungwi hafla iliyofanyika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Alisema wakati umefika kwa wananchi wenyewe kurejesha ari iliyowahi kutekelezwa miaka ya nyuma katika nia ya kujenga nchi kwa kushirikiana kwenye Nyanja zote zinazohusika za kujenga Taifa lenye nguvu za Kiuchumi, maendeleo na ustawi wa Jamii.
{ Tumezoea kupokea misaada kutoka nje ya nchi lakini ni vyema tukapaswa kujenga tabia ya Wananchi wenyewe kusaidia changamoto zinazotukabili sisi pamoja na Serikali yetu “. Alisema Nd. Meza.
Katibu Mkuu huyo wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliushukuru Uongozi wa Hoteli ya Kendwa Rocks kwa uamuzi wake wa kusaidia nguvu za kiuwezeshaji changamoto zinazozikabili baadhi ya Taasisi za Umma Nchini.
Mapema Meneja Mkuu wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nd. Ali Ibrahim Kilupi alisema Taasisi yake imeamua kutoa Mtambo huo ili kuwasaidia watendaji wa Ofisi ya Uratibu wa shughuli za SMZ kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi
MKURUGENZI WA AFRIKA AKUTANA NA MABALOZI WA AFRIKA NCHINI KUZUNGUMZIA USHIRIKIANO
OFISI YA URATIBU WA SHUGHULI ZA SMZ YAPOKEA MTAMBO MAALUM WA MAWASILIANO YA NDANI
Meneja
Mkuu wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nd. Ali Ibrahim Kilupi kushoto
akimkabidhi msaada wa mtambo maalum wa mawasiliano ya Simu za ndani {
Inter call } Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd.
Joseph Abdulla Meza kwa ajili ya Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ
Mjini Dar es salaam.
Wa kwanza kutoka Kulia anayeshuhudia tukio la makabidhiano hayo ni
Mratibu Mkuu wa Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam
Ndugu Issa Mlingoti Ali.
Katibu
Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Meza akiuwasilisha
msaada huo wa Mtambo wa mawasiliano ya Simu kwa mlengwa Mratibu Mkuu wa
Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam Ndugu Mlingoti.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Joseph Abdulla Meza alisema jamii na hasa wananchi Wazalendo wenye uwezo wanapaswa kuendelea kujenga tabia ya kusaidia nguvu katika kupambana na changamoto zinazoikabili serikali pamoja na wananchi katika maeneo mbali mbali nchini.
Alisema mfumo uliozoeleza kwa kipindi kirefu sasa katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ni ule uliotegemewa zaidi wa kupokea misaada kutoka Mashirika, taasisi na mataifa ya nje ya nchi.
Ndugu Joseph Abdulla Meza alitoa kauli hiyo wakati akipokea msaada wa mtambo maalum wa mawasiliano ya ndani { Inter call }kwa ajili ya Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam uliotolewa na Uongozi wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nungwi hafla iliyofanyika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Alisema wakati umefika kwa wananchi wenyewe kurejesha ari iliyowahi kutekelezwa miaka ya nyuma katika nia ya kujenga nchi kwa kushirikiana kwenye Nyanja zote zinazohusika za kujenga Taifa lenye nguvu za Kiuchumi, maendeleo na ustawi wa Jamii.
{ Tumezoea kupokea misaada kutoka nje ya nchi lakini ni vyema tukapaswa kujenga tabia ya Wananchi wenyewe kusaidia changamoto zinazotukabili sisi pamoja na Serikali yetu “. Alisema Nd. Meza.
Katibu Mkuu huyo wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliushukuru Uongozi wa Hoteli ya Kendwa Rocks kwa uamuzi wake wa kusaidia nguvu za kiuwezeshaji changamoto zinazozikabili baadhi ya Taasisi za Umma Nchini.
Mapema Meneja Mkuu wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nd. Ali Ibrahim Kilupi alisema Taasisi yake imeamua kutoa Mtambo huo ili kuwasaidia watendaji wa Ofisi ya Uratibu wa shughuli za SMZ kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi







No comments :
Post a Comment