Thursday, September 22, 2016

DARAJA LA SALENDER JIJINI DAR ES SALAAM KUJENGWA UPYA, LITAKUWA NA UREFU WA KILOMITA 1.4, RAIS MAGUFULI AKABIDHIWA MCHORO




Hivi ndivyo daraja la Salender litakavyokuwa kama ambavyo mchoro huu wa daraja hilo uluivyokabidhiwa kwa Rais John Pombe Magufulo, kutoka kwa Balozi wa Korea hapa nvhini Song Geum-Young, Ikulu jijini Dar es Salaama leo Septemba 22, 2016.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea picha ya mfano wa Daraja jipya la Salenda litakojengwa kuanzia maeneo ya Hospitali ya Agha Khan na kupita baharini  hadi eneo la Coco beach jijini Dar es Salaam kutoka kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Song Geum-Young aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo. Daraja hilo litakuwa na urefu wa kilomita 7 na kati ya hizo kilomita 1.4 zitapita baharini na ujenzi wake unatarajiwa kuanza mwezi Juni mwakani. (PICHA NA IKULU)

 Rais akiagana na balozi huyo wa Korea baada ya mazungumzo yao
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kumkaribisha  Balozi wa Russia hapa nchini Yuri Popov aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo, leo Septemba 22, 2016

.
Katibu Msaidizi Tume ya Maadili (Kanda ya Kusini) Be. Muhuwa R. Kapangawazi akitoa mada kuhusu Maadili ya Utumishi wa Umma na Tamko la Ahadi ya Uadilifu wakati wa kikao cha kawaida cha Baraza la wafanyakazi Ofisi ya Rais, Ikulu, katika Ukumbi wa Mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2016
Kaimu Mshauri wa Kitaalamu Ofisi ya ushauri wa Mafuta na Gesi ofisi ya Rais Ikulu, Dkt. Emma Msaky,
akitoa mada kuhusu utendaji wa ofisi yake wakati wa kikao cha kawaida cha Baraza la wafanyakazi Ofisi ya Rais, Ikulu, katika Ukumbi wa Mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2016.(PICHA NA IKULU)


Katibu Mkuu Ikulu Mhe Peter Ilomo (wa nne kutoka kulia) akiongoza kikao cha kawaida cha Baraza la wafanyakazi Ofisi ya Rais, Ikulu, katika Ukumbi wa Mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2016


Katibu Mkuu Ikulu Mhe Peter Ilomo (wa nne kutoka kulia) na viongozi wengine pamoja na wajumbe wakipata picha ya pamoja baada ya kikao cha kawaida cha Baraza la wafanyakazi Ofisi ya Rais, Ikulu, katika Ukumbi wa Mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2016


JONAS KAMALEKI- MAELEZO
JAJI wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Jacob Mwambejele amemkabidhi Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi ripoti ya uchunguzi baada kukamilika kwa uchunguzi huo.
Tukio hilo limefanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo ripoti iliyohusu uchunguzi wa Mgogoro wa muda mrefu kuhusu kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani, Kilosa, mkoani Morogoro.
Katika makabidhiano hayo Jaji Mwambejele amesema kwa kushirikiana na timu yake, Wizara ya Ardhi, Vijiji vya wilayani Kilosa na uongozi wa Mkoa wa Morogoro wamekamilisha ripoti hiyo ndani ya siku 60 kama adidu za rejea zilivyowataka.
Jaji Jacob Mwambejele amesema uchunguzi huo uliangalia baadhi ya mambo ikiwemo kama uanzishwaji wa kijiji cha Mabwegere ulianzishwa kisheria na sheria zilifuatwa katika uanzishwaji huo, kama ulikuwepo usahihi wa kisheria katika upimaji wa eneo hilo na kama wanavijiji walishirikishwa, alisema Lukuvi.
Jaji huyo ameyataja maeneo mengine ya uchunguzi huu kuwa yalikuwa pamoja na kuchunguza kama upimaji ulizingatia mipaka, kuchunguza maeneo mengine yenye migogoro na kuchunguza jambo jingine lolote ambalo litasaidia katika kuleta suluhu ya mgogoro huo.
Kwa upande wake, Waziri Lukuvi ametoa shukrani zake kwa Jaji Mwambejele na timu yake, waziri Lukuvi amesema ripoti hiyo imekalika kwa wakati na inataraji kumaliza mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 25.
“Mapendekezo yaliyotolewa ndani ya ripoti ya Jaji, tutayafanyia kazi haraka iwezekanavyo ili kumaliza mgogoro wa Mabwegere ambao umedumu kwa miaka mingi,” alisema Lukuvi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi mapema mwaka huu alimteua  kwa mamlaka yake chini ya kifungu 18 (1) cha Sheria ya Ardhi sura 113 Jaji Jacob Mwambejele wa Mahakama Kuu- Kitengo cha Biashara kuchunguza mgogoro wa Kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani vya Mfuru, Mbigiri, Mandengwa, Dumila , Matongolo na Maboiga vilivyopo Wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro ili kupata suluhisho la kudumu la mgogoro huo.


 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita (kulia), akizungumza katika na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa Tovuti ya mtaa huo iliyofanyika Hoteli ya Best Western Plus Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta. 
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita, akitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya tovuti hiyo.
 Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (katikati), akikata utepe kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kionondoni, aliyekuwa mgeni rasmi, kuashiria uzinduzi rasmi wa tovuti hiyo. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta, Mwenyekiti wa mtaa huo, Kimweri Mhita, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Masaki, Richard Mwakyulu na Mjumbe wa Kamati ya Mtaa huo, Rose Mkisi.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea kabla ya uzinduzi huo.
 Wajumbe wa kamati ya mtaa huo wakishiriki kwenye uzinduzi huo.
 Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo,  Peter Mkongereze akizungumza kwenye hafla hiyo.
 Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta (kulia), akizungumza katika hafla hiyo.
 Mmoja wa waendeshaji wa tovuti hiyo, Benjamin Chaula (kulia), akielezea jinsi itakavyokuwa ikifanya kazi.Kushoto ni Norbert Baranyikwa.
 Makofi yakipigwa baada ya uzinduzi wa tovuti hiyo.
Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.


Na Dotto Mwaibale

SERIKALI ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam imezindua tovuti yake ili kurahisisha mawasiliano na shughuli za maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tovuti hiyo Dar es Salaam leo asubuhi Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Masaki, Kimweri Mhita alisema tovuti hiyo imeanzishwa kwa lengo la  kuwasiliana na kuwashirikisha katika shughuli za maendeleo raia wa kigeni wanaoishi katika mtaa huo.

"Kutokana na jiografia ya eneo letu kulikuwa na changamoto kuwa ya kuwashirikisha wenzetu katika masuala mbalimbali kutokana na kutokuwa na mawasiliano tukaona tuanzishe tovuti yetu itakayosaidia kuondoa changamoto hiyo" alisema Mhita.

Alisema kupitia tovuti hiyo itasaidia kuwatambua wafanyabiashara waliopo katika mtaa huo ambao wameanza kujisajili pamoja na wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, Katibu Tarafa wa Kata ya Magomeni, Fullgence Sakafu alisema kuanzishwa kwa tovuti hiyo katika wilaya hoyo wilaya hiyo mtaa huo umeonesha njia hivyo akaomba mitaa mingine kuiga mfano huo.


Alisema tovuti hiyo itasaidia kuweka wazi mipango ya maendeleo katika mtaa huo pamoja na kuhimizana kwenye kampeni ya kufanya usafi inayoendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuwa.

Alhaji Adam Kimbisa

NA K-VIS BLOG

MWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya vyombo vya habari vya Chama Cha Mapinduzi, (CCM), Al-Hajj Adam Kimbisa, amejiuzulu wadhifa wake.
Taarifa iliyotolewa na msemaji wa chama hicho, Christopher Ole Sendeka na kusambazwa kwa vyombo vya habari leo Septemba 22, 2016, imesema pamoja na Kimbisa, pia bodi nzima nayo imejiuzulu.
Kimbisa na bodi hiyo, wamechukua uamuzi huo ikiwa ni siku chache baada ya Rais John Pombe Magufuli, kufanya ziara ya kushtukiza kwenye ofisi za magazeti ya Uhuru na Mzalendo, ambapo pamoja na mambo mengine alikumbana na malalamiko mengi kubwa ni kuwepo kwa maslahi duni na kushuka kwa morali ya kufanya kazi ambapo, wafantakazi wa makagazeti hayo, walimueleza Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho, kuwa hawajalipwa mishahara kwa zaidi ya miezi mitano.
Hakuna sababu zaidi zilizotolewa za kujiuzulu kwa mwanasiasa huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki akishika nafasi ya kuwa mwenyekiti wa Wabunge wa bunge hilo wanaotoka Tanzania.
 

No comments :

Post a Comment