Thursday, September 1, 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA AZINDUA RIPOTI YA HALI YA HEWA BARANI AFRICA



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea Kutoka kwa Mwenyekiti Mwenza na Mwenyekiti wa Masula ya Uhusiano wa Kimataifa  wa   Taasisi ya The Investment Climate Facility for Africa (ICF), Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa,  Ripoti ya Hali ya Hewa Barani Afrika, kwenye  hoteli ya Serena jijini Dar Septemba 1, 2016.  (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimaina na  Mwenyekiti Mwenza na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya  Taasisi ya The Investment Climate Facility for Africa (ICF), Neville Isdell na Katikati ni Mwenyekiti Mwenza na Mwenyekiti wa Masula ya Uhusiano wa Kimataifa wa ICF, Ris Mstaafu, Benjamin Mkapa  katika hafla ya kuzindua Ripoti ya Hali ya Hewa Barani Afrika, kwenye  hoteli ya Serena jijini Dar Septemba 1, 2016.

 Mkuu wa mkoa wa Geita, Meja Jenerali (Mstaafu) Ezekiel Kyunga (kushoto)akipokea moja kati ya madawati 185 yenye thamani ya shillingi milioni 31 jana, toka kwa Meneja wa Tigo kanda ya ziwa, Edgar Mapande ikiwa ni mpango wa kampuni ya simu za mkononi Tigo kutoa madawati kupitia kauli mbiu “ Dawati kwa kila mwanafunzi ni msingi wa elimu bora fiesta 2016 kwa kishindo cha Tigo imooo”

 Mkuu wa mkoa wa Geita, Meja Jenerali (Mstaafu) Ezekiel Kyunga(katikati)  akiwa ameketi kwenye dawati mara baada ya kukabidhiwa madawati 185 toka kampuni ya simu za mkononi Tigo hafla iliyofanyika shule ya msingi Mwatulole jana mkoani humo, Wengine pichani kulia ni Meneja wa Tigo kanda ya ziwa, Edgar Mapande na Afisa elimu mkoa wa Geita, Catheline Mashala.

Mkuu wa mkoa wa Geita, Meja Jenerali (Mstaafu) Ezekiel Kyunga akiwa ameketi na wanafunzi wa shule ya msingi Mwatulole mara baada ya kukabidhiwa madawati 185 toka kampuni ya simu za mkononi Tigo hafla iliyofanyika shule ya msingi Mwatulole jana mkoani humo, Pembeni mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi.
 Kampuni ya Tigo Tanzania  leo imekabidhi madawati 185 yenye thamani ya shilingi milioni 31  yatakayogawiwa shule nne katika mkoa wa Geita  ikiwa ni sehemu ya mkakati wake unaoendelea nchi nzima wa kutoa msaada wa madawati  ambayo yatainufaisha mikoa 14 bega kwa  bega na tamasha la Tigo FIESTA 2016.  
Mkakati wa kutoa msaada wa madawati katika msimo huu wa Fiesta unajulikana, “‘Dawati kwa kila mwanafunzi ni msingi wa elimu bora; Fiesta 2016 kwa Kishindo cha Tigo Elimu bora, Imooooo!’
Akizungumza katika sherehe za kukabidhi madawati hayo  zilizofanyika katika Shule ya Msingi Mwatulole, Meneja wa Kikanda wa Tigo Kanda ya Ziwa Edgar Mapande, alisema  umekuwepo uhitaji mkubwa wa madawati katika shule za msingi na kutokana na kuwepo kwa uhaba wa madawati  imebainika kuwa ni moja ya sababu zinazoathiri uwezo wa kujifunza  pamoja na ufanisi wa masomo miongoni mwa  wanafunzi  katika  shule zetu nyingi za msingi.
“Lengo letu kama kampuni ni kuhakikisha kuwa tunaboresha mazingira ya kujifunzia katika shule zetu za msingi na tunayo furaha  kwamba msimu wa FIESTA 2016 unaleta mabadiliko kwa  kizazi cha baadaye  ambacho ni wanafunzi walio katika shule za msingi kwa kuhakikisha hawakai tena chini sakafuni,” alisema Mapande.
Makabidhiano ya madawati hayo yalishuhudiwa na Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu  Ezekiel Kyingu     ambaye alisema kuwa madawati hayo 185 yataboresha kwa kiwango kikubwa  mazingira ya kujifunza  kwa watoto katika mkoa huo  na kutoa witom kwa watu wengine wenye mapenzi mema  kujitokeza  na kujiunga na juhudi hizo za kuondoa uhaba wa madawati uliobakia katika mashule  mkoani humo.
Kyingu  alizitaja shule  zitakazonufaika na  madawati hayo  na idadi yake katika mabano kuwa ni Mwatulole (50), Nyankumbu (45), Ukombozi (45),  na Kivukoni (45).
 “Tunawashukuru sana Tigo  kwa kutuunga mkono katika juhudi zetu kwa kupunguza idadi ya uhaba wa madawati  katika shule za msingi mkoani Geita. Tunaamini  madawati haya 185  yatatufikisha mbali  katika  kuwawezesha mamia ya watoto kuwa katika mazingira mazuri ya kujifunzia yanayotakiwa kwa ajili ya mafanikio katika kuelekea kuwa viongozi wa baadaye,” alisema Kyingu.

 Mradi mkakati wa madawati wa Tigo Fiesta ulianzia mkoani Mwanza na hadi sasa Tigo imeshatoa madawati wilayani Kahama na mkoani Kagera.

MAADHIMISHO YA 14 YA SIKU YA WAHANDISI YAANZA DAR, RAIS MAGUFULI MGENI RASMI

 Baadhi ya ahandisi wakiwa kwenye maadhimisho ya 14 ya siku ya Wahandisi, kwenye ukumbi wa MlimaniCity jijini Dar es Salaam asubuhi hii.Rais John Pombe Magufulindiye mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayoambao kauli mbiu yake ni "Kuibadili Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati kupitia viwanda"



Baada ya juzi Agost 30,2016 Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kuzindua aina mpya ya Kondomu iitwayo Zana Kondomu mkoani Mbeya, Uzinduzi kama huo unatarajiwa kufanyika mkoani Mwanza Septemba 05,mwaka huu.

Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni (pichani), jana alisema mkoa wa Mwanza unatarajia kupokea ugeni kutoka wizara hiyo ambao utajumuisha wataalamu mbalimbali wa afya watakaokuwa wakitoa semina na elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo kutumia vyombo vya habari, wakielezea juu ya uzinduzi wa kondomu hiyo.

Alisema miongoni mwa dhumuni la kuzindua aina hiyo mpya ya Kondomu, ni kusaidia katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukwimwi ambapo Wizara itakuwa ikigawa bure kondomu hizo zenye ubora kwa wananchi, kote nchini.
Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni
Baadhi ya Wanahabari mkoani Mwanza, wakimsikiliza Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza.



NA THOMAS NYINDO-TUME YA MIPANGO
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tabora Dkt. Thea Ntara, (anayezungumza pichani) amewataka maafisa mipango na wachumi kuibua miradi ya maendeleo inayotekelezeka ili kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi.
Dkt. Ntara amesema miradi mingi inayoibuliwa imekuwa haitekelezeki na siyo endelevu hivyo kuna haja ya kuzingatia mwongozo wa uwekezaji wa umma ili kuleta maendelea endelevu katika maeneo yao.
Katibu Tawala amesema hayo katika Mafunzo ya Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma yanayoratibiwa na Tume ya Mipango kwa Maofisa na watendaji wa Idara za Sera na Mipango wa mikoa ya Tabora, Kigoma, Shinyanga na Katavi.
Akizungumza katika mafunzo hayo yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Ntara amesema maafisa mipango na wachumi wanatakiwa kutoa msaada wa kitaalam kwa uongozi wa wilaya na mkoa katika kuibua na kutekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo yao.
Dkt. Ntara amesema mafunzo hayo yanalenga katika kuleta mabadiliko chanya katika kuibua, kutekeleza na kufuatilia miradi ya maendeleo.
Amesema fedha za miradi ya maendeleo haziwezi kupatikana kwa urahisi kama maafisa mipango na wachumi hawataandaa andiko la miradi kitaalam. “Tunaposhindwa kuibua miradi mizuri, tunashindwa kupata fedha kutoka serikalini na kwa wafadhili wengine,” alisema Dkt. Ntara.
Awali akimkaribisha Katibu Tawala, Kaimu Naibu Katibu Mtendaji wa Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya Mipango, Dkt. Lorah Madete alisema Serikali  imeandaa Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma (Public Investment Management Operational Manual) kwa lengo la kuimarisha utendaji, uwajibikaji na kuleta ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma zinazoelekezwa katika miradi ya maendeleo.
Dkt. Madete amesema vipaumbele vya Serikali katika miaka mitano ijayo vimeainishwa kwenye Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 – 2020/21 ambao una lenga zaidi katika kuweka mazingira rafiki ya uanzishwaji wa viwanda kwa ajili ya mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya binadamu. Kwa hiyo mafunzo hayo ni hatua muhimu katika kuboresha, kusimamia utekelezaji, pamoja ufuatiliaji na kufanya tathmini ya miradi ya maendeleo.



Dkt. Lorah Madete, Kaimu Naibu Katibu Mtendaji, Klasta ya Uchumi Jumla, Tume ya Mipango, akitoa neno kwa Maofisa na watendaji wa Idara za Sera na Mipango kutoka mikoa ya Tabora, Kigoma, Shinyanga na Katavi ambao ni washiriki wa mafunzo yanayohusu Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma kabla ya kumkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Dkt. Thea Ntara  (wa pili kushoto) Wengine ni Dkt. Jehovaness Aikaeli, Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya Uchumi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Bibi Rukia S. Manduta, Katibu Tawala Msaidizi, Mipango na Uratibu Mkoa wa Tabora.

No comments :

Post a Comment