Friday, September 9, 2016

UNESCO YAZINDUA RIPOTI YA UFUATILIAJI WA ELIMU DUNIANI (GEM) 2016


 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez akielezea siku ya kisomo duniani na dhumuni la UNESCO kuanzisha siku hiyo.
 Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta akizungumzia juhudi za serikali za kuhakikisha kila mtanzania anajua kusoma.
  Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, Basilina Levira akitoa taarifa jinsi hali ilivyo kwa watu wazima ambao wanajua kusoma na wasiojua kusoma.
Afisa Mradi wa Elimu wa UNESCO, Faith Shayo akielezea mradi wa XPRIZE ambao unasimamiwa na UNESCO ukiwa na malengo ya kukuza teknolojia ya dunia kwa kutumia uwezo walionao watoto katika maeneo mbalimbali nchi
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez akitoa maelezo kuhusu Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez akimkabidhi mgeni rasmi, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta, Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM)

 Wageni waalikwa katika maadhimisho ya siku ya kisomo duniani wakionyesha Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM) wakiongozwa na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez (wa kwanza kushoto).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez akimkabidhi mgeni rasmi, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta, sanduku la Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM).
 Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya kisomo, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta akigawa Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM) kwa baadhi ya wafanyakazi wa wizara yake.


Na Mwandishi wetu
Katika kutambua umuhimu wa kusoma na kuandika Tanzania na mataifa mengine duniani zimeungana kwa pamoja kuadhimisha siku ya Kisomo Duniani ambayo huadhimishwa kila Septemba, 8 ya kila mwaka ambapo pamoja na maadhimisho hayo pia iliambatana na Uzinduzi wa Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani (GEM).

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez alisema kuwa dhumuni la UNESCO kuweka siku hii ya Septemba 8 kila mwaka kuwa siku ya kisomo kimataifa ili kuziunganisha jamii zote za kimataifa duniani kuweka na kuendeleza nguvu na juhudi kwa watu kujua kusoma na kuandika ili kuleta maendeleo katika jamii mbalimbali.

“Kauli mbiu hii inatufungulia milango ya uelewa juu ya malengo na mafanikio ya miongo mitano iliyopita ambayo yaliwekwa ya kutaka kila mtu anajua kusoma,” alisema Bi. Rodrieguez na kuongeza.

“Tunataka kujua ni changamoto gani zinazoikabili sekta ya elimu katika kusoma na kuandika na tunataka kufahamu namna ya kukabiliana na changamoto hizo ili kufikia malengo ambayo UNESCO iliyakusudia kufikiwa ya kila mmoja awe anajua kusoma.”

Kwa upande wa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta ambaye alimuwakilisha Mgeni Rasmi, Katibu Mkuu wa wizara hiyo alisema serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imejizatiti kuondoa tabaka la wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa vijana na watu wazima kwa kujenga uwiano sawa wa utoaji wa elimu kwa watu wote.

“Wizara imejipanga vizuri, na lengo kubwa la wizara ni kuhakikisha tunakuwa na mtanzania aliye elimika na aliye na stadi, maarifa na uwezo wa kutumia elimu aliyoipata,” alifafanua Bureta.

Vile vile Bw. Bureta amesema kwa sasa wizara ipo kwenye mpango wa kukuza stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) ambao unaanzia chini kwa wanafunzi wa awali mpaka shule za msingi.

Katika mpango huo walimu wamekuwa wakipata mafunzo mbalimbali ya namna ya kumuwezesha mwanafunzi kujua Kusoma Kuandika na Kuhesabu katika ngazi ya elimu ya awali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, Basilina Levira amesema kwamba kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012, asilimia 78 ya vijana na watu wazima ndio waliokuwa wakijua kusoma na kuandika.

Akaongeza kuwa mwaka 2015 idadi hiyo ya wanaojua kusoma na kuandika ilishuka na kufikia asilimia 77 ambapo ilipelekea wizara hiyo kutoka na mikakati inayokusudia kuondoa kabisa tabaka la watu wasiojua kusoma na kuandika nchini.

Aidha, Basilina amesema kuwa Serikali ilipitisha sheria ya vyumba vya madarasa ya shule zote nchini kutumika kufundishia vijana na watu wazima ambao hawajui kusoma na kuandika muda wa jioni baada ya wanafunzi wa kawaida wanapomaliza masomo yao.

Amefafanua kwa kusema kuwa, wizara imeandaa programu ambayo iko kwenye mfumo wa Televisheni na picha za video (DVD) yenye masomo 65 ya kujifunza kusoma, kuandika na kuhesabu, ambapo kwa kutumia programu hiyo mwanafunzi anaweza kujua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa muda wa miezi 4 mpaka 6.
Mafunzo hayo kwa njia ya Televisheni na Picha za Video tayari yameanza kutumika kwa wilaya za Ilemela, Dodoma Manispaa, Songea Manispaa, Bagamoyo, Mkuranga, Temeke, Ilala na Kinondoni, ambapo asilimia 65 ya vijana na watu wazima wasiojua kusoma na kuandika wamejitokeza kujiunga na Elimu hiyo huku idadi kubwa ikiwa ni ya wanawake.

Siku ya Kisomo Duniani huadhimishwa Duniani kote kila ifikapo Septemba, 8 ya kila ya mwaka, ambapo mwaka huu 2016 maadhimisho hayo yametimiza miaka 50 tangu yalipoanza kuadhimishwa mwaka 1966.

Kauli mbiu ya siku ya kisomo duniani kwa mwaka huu ni ‘Tunasoma yaliyopita, Tunaandika yajayo, Elimu endelevu’ ambayo kwa lugha ya kiingereza ni ‘Reading the future, Writing the past’.
Mgeni rasmi, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta akionyesha Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM) baada ya kuipokea kutoka kwa Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez

MKUU WA MKOA MARTINE SHIGELLA ATEMBELEA BANDARI YA TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella, (wapili kulia), akiwa ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika (wapili  kushoto), Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Mhandisi Zena Saidi (wakwanza kulia), Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa, (wakwanza kushoto) wakifurahia jambo wakati wakiwa kwenye ziara ya kuitembelea Bandari ya Tanga Septemba 9, 2016
 Kushoto ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa kwanza kulia aliyekaa kwenye boti wakati alipofanya ziara ya kuitembelea bandari hiyo
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa kwanza kulia akitazama maeneo ya bahari akiwa kwenye boti wakati alipoitembelea kuona namna ya utendaji wao  katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi na kushoto ni Kaimu Meneja wa Bandari wa Tanga Henry Arika
 Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika wa pili kutoka kulia akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kulia wakati alipofanya ziara ya kuitembelea Bandari hiyo kuona namna inayofanya kazi kwa ufanisi,
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akishuka kwenye boti la Bandarini akisaidiwa kushuka wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella aliyoitembelea bandari hiyo kuona namna inavyofanya kazi zake
Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akipanda ngazi kuelekea kwenye meli ya mizigo iliyotia nanga Bandari ya Tanga wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella ambaye aliitembelea Bandari hiyo anayefuatia ni Mkuu huyo wa mkoa
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akipanda ngazi kuelekea kwenye meli ya mizigo iliyotia nanga bandari ya Tanga wakati wa ziara yake ya kuitembelea Bandari hiyo
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akipanda ngazi kuelekea kwenye meli hiyo akifuatiwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga,Faidha Salim wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella

 Kaimu Meneja wa Bandari wa Tanga Henry Arika akipanda ngazi kuelekea kwenye meli ya mizigo iliyotia nanga kwenye bandari ya Tanga wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kuitembelea Bandari hiyo kuona shughuli zake anayefuatia ni PRO wa Bandari ya Tanga,Moni Jarufu
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella katikati akiteta jambo na PRO wa Mamlaka ya Bandari ya Tanga,Moni Jarufu wakati wa ziara yake

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa kwanza kushoto akionyeshwa kitu na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,(Ras) Mhandisi Zena Saidi wakati wa ziara yake ya kuitembelea Bandari hiyo jana
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi wakiteta jambo wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa kuitembelea Bandari hiyo kuona namna inayofanya kazi zake kulia ni PRO wa Bandari ya Tanga,Moni Jarufu

(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha Blog) 

Kaimu Katibu Tawala mkoani Mwanza, Projestus Rubanzibwa, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza, kwenye kikao cha Utambulisho wa Mradi wa kuongeza Ujuzi na Idadi ya Wakunga katika maeneo ya Vijijini katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi, kilichofanyika hii leo Jijini Mwanza.
Amesisitiza kwamba Wakuu wa Vyuo vya vya Ukunga nchini wanao wajibu wa kuhakikisha kwamba wanatoa mafunzo bora kwa wahitimu wa vyuo hivyo ili watakapohitimu masomo yao waweze kusaidia kutoa huduma bora afya.
Mradi wa kuongeza Ujuzi na Idadi ya Wakunga katika maeneo ya Vijijini, unatekelezwa na Shirika la Jhpiego kwa kushirikiana na Taasisi ya Wakunga nchini Canada, Shirika la Amref, Serikari ya Canada, Taasisi ya Wakunga Tanzania na Wizara ya Afya nchini, lengo likiwa ni kuboresha huduma za afya kwa akina mama na mtoto ili kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi maeneo ya Vijijini nchini.
Na BMG
Kaimu Mganga Mkuu mkoa wa Mwanza, Dr.Silas Wambura, akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu mkoa wa Mwanza, ambapo amesema mkoa wa Mwanza unakabiriwa na upungufu mkubwa wa idadi wa wakunga pamoja na vifaa tiba hali ambayo inasababisha kuwepo kwa vifo vya akina mama na watoto.
Dr.Dustan Bishanga ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za Mama na Mtoto Shirika la Jhpiego, amesema lengo la mradi huo ni kuhakikisha unaongeza Ujuzi na Idadi ya Wakunga maeneo ya Vijijini hapa nchini ambapo wahitimu wa masomo ya Sayansi katika maeneo hayo watakuwa wakipewa ufadhiri wa masomo kwa makubaliano ya kurudi kwenye maeneo yao ili kutoa huduma za afya. Mradi huo unatarajiwa kufikia tamati mwaka 2021.
Kikao cha Utambulisho wa Mradi wa kuongeza ujuzi na idadi ya Wakunga katika maeneo ya Vijijini mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi kilichofanyika hii leo Jijini Mwanza.
Dr.Dustan Bishanga ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za Mama na Mtoto Shirika la Jhpiego, akizungumza na wanahabari kwenye kikao hicho.
Martha Rimoy ambaye ni Mratibu wa Taifa wa Chama cha Wakunga Tanzania (TAMA), amesema bado maeneo mengi nchini yanakabiloiwa na upungufu wa Wakunga kutokana na idadi ya Wakunga wanaohitimu vyuoni kutoendana na idadi ya ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya huku wengine pia wakishindwa kwenda kufanya kazi maeneo ya Vijijini kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mazingira duni.
Gustav Moyo ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za Uuguzi na Ukunga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, amesema hali ya upungufu wa Wakunga nchini hususani maeneo ya Vijijini si nzuri hivyo Serikali inatumia jitihada mbalimbali ikiwemo kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi ili kutatua changamoto hiyo. 
Amesema asilimia kubwa ya mikoa ya Kanda ya Ziwa inakabiliwa na upungufu huo na kwamba Serikali itakuwa ikitolea kipaumbele kwenye mikoa hiyo pindi inapotoa ajira kwa Wakunga.
Kikao hicho kimewajumuisha wadau mbalimbali wa afya wakiwemo Wakunga, Waganga Wakuu wa Wilaya na Maafisa Elimu ambao watakuwa na wajibu wa kuwahamasisha wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi ili kuongeza idadi ya Wakunga.
Wadau wa afya kutoka Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Tabora, Kigoma na Mara wameshiriki kwenye kikao hicho.

 Hili ndilo gari lililoacha njia na kupinduka kwenye msafarawa makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan huko kijiji cha Nanguruwe mkoani Mtwara leo Septemba 9, 2016.
MSAFARA wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama  Samia Suluhu Hassani ambao ulikuwa unaelekea Wilayani Tandahimba ukitokea Mtwara umepata ajali mapema leo asubuhi Septemba 9, 2016, baada ya garilililobeba wasaidizi wake kuacha njia na kupinduka.
Mkuu wa mkoa wa Mtwara Bi. Halima Dendego, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo. 


“Leo ikiwa ni siku yatatu ya ziara ya Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mama yetu Samia Suluhu Hassan, moja ya magari yaliyokuwa kwenye msafara namba ST 234 ilipata matatizo ya kupinduka, na wasaidizi wanne wa Makamu wa Rais, wameumia lakini wamekimbizwa hospital ya Ligula na wanaendelea na matibabu nahali zao zinaendelea vizuri.” Amefafanua Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Halima Dendego
Taarifa za awali zinasema, watukadhaa waliokuwemo ndani ya gari hilo akiwemo dereva wamejeruhiwa na kukimbizwa hospitali ya Rufaa Mkoani Mtwara, Ligula kwa matibabu.
Ajali imetokea mbele kidogo ya kijiji cha Nanguruwe kilichopo Halmashauri ya wilaya ya Mtwara
Awali kabla ya gari hilo lililobeba wasaidizi wa rais kuacha njia na kupinduka, gari liliokuwa limebeba waandishi wa habari wa liliacha njia na nusura lipinduke.
Picha zilizotumwa kutoka eneo la tukio, zinaonyesha, Muhudumu wa afya akiwahudumia majeruhi hao ambao walilazwa katikati ya barabara huku gari linalodaiwa kuwabeba watu hao, likiwa nje ya barabara na limepondeka
Barabara ya kutoka mtwara kuelekea tandahimba si ya kiwango cha kuridhisha na kuruhusu magari kwenda mwendokasi hali iliyosababisha magari hayo kuacha njia na moja kupinduka kabisa na kusababisha majeruhi.

 Wanaodaiwa kuwa wasaidizi wa Makamu wa Rais, wakipatiwa huduma ya kwanza baada la ajali hiyo


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akitembelea kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba mkoani Mtwara.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba Mhandisi.Leonce namna gesi inavyopokelewa na kuchakatwa na kusafirishwa kwa watumiaji
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akiangalia mfumo wa uendeshaji na usalama wa kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba mkoani Mtwara.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na wafanyakazi wa kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba mkoani Mtwara.
                                        .......................................................................

Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewataka wafanyakazi wa kiwanda cha kuchakata gesi asilia kilichopo Madimba mkoani Mtwara wawe wazalendo na wafanye kazi kwa bidii katika kulinda na kuutunza uwekezaji huo mkubwa ambao serikali inautegemea katika uzalishaji wa nishati ya umeme wakati taifa linaelekea kwenye nchi ya viwanda.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wafanyakazi na watendaji wa kiwanda hicho baada ya kutembelea kiwanda kwa mara ya kwanza tangu ashike wadhifa huo kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa kiwandani hapo akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Mtwara.
Amesema kiwanda cha kuchakata gesi asilia ni hazina kubwa  kwa Taifa hivyo ni kikalindwa na kutunzwa ipasavyo kutokana na umuhimu wake katika uzalishaji wa nishati ya umeme kwa maendeleo ya nchi.

Makamu wa Rais pia amewashukuru na kuwapongeza wafanyakazi wa kiwanda hicho cha kuchakata gesi asilia cha Madimba na amewahakikishia kuwa serikali itaendelea kuwajali na kuwathamini katika utendaji wao wa kazi na kwamba serikali itahakikisha wafanyakazi wa kiwanda hicho wanapewa motisha ya kutosha ili waongeze maradufu utendaji wao wa kazi ili malengo ya serikali ya kuleta maendeleo kwa wananchi kupitia viwanda inatimia kwa sababu taifa litakuwa na nishati ya umeme ya uhakika.
Makamu wa Rais amewataka watendaji wa Shirika la Maendeleo la Petroli (TPDC) ambalo linasimamia mradi huo kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kusaidia huduma za jamii katika vijiji vinavyozunguka mradi huo kila mwaka ili wananchi waweze kuwa walinzi wa mitambo hiyo.
Akitoa maelezo mafupi ya mradi huo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. James Mdoe amesema kiwanda hicho kina uwezo wa kuchakata gesi ya futi za ujazo milioni 210 kwa siku.



Bw Donsun Lee ambaye ni Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International akikagua pump kwenye moja ya kisima kwenye shule ya Msingi Makalala, anayetizama ni Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi
 Bw Donsun Lee ambaye ni Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International akimsikiliza kwa makini Mhandisi wa Maji wa Mji wa Mafinga Eng Eradius.
Baadhi ya wanafunzi na waalimu wa shule ya Msingi Makalala wakiwa katika picha ya pamoja na Mrs Lee na Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi

 Na Fredy Mgunda,Iringa

MBUNGE wa jimbo Mafinga mjini Cosato Chumi ameendeleza juhudi zake za kuwatafutia maendeleo wananchi wa jimbo lake kwa kufanya kazi kwa ukaribu na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali za nje ya nchi ya Tanzania pamoja na taasisi za ndani.
Hivi karibu balozi wa korea nchini Tanzania Bw Song Geum Young akiwa na NGO ya Kutoka Korea ya World share  alitembelea jimbo la mafinga mjini kwa lengo la kujionea changamoto za jimbo hilo na kutafuta njia za kutoa msaada wa kutatua baadhi ya changamoto hizo na walitoa msaada wa taa ndogo za solar kwa kaya masiki mia saba.
Baada ya balozi huyo kurudi jijini Dar es Salaam alimuagiza Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International Bw Donsun Lee kutembelea jimbo la mafinga mjini na kuzifanyia tafiti kwa kina baadhi ya changamoto za jimbo hilo ambazo alikuwa amezianisha hapo awali ili kuweza kusaidia kuzitatua.
Aidha mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International Bw Donsun Lee alifanikiwa kutembelea baadhi ya shule za jimbo la mafinga mjini na kuzifanyia tafiti changamoto zilizopo kama uhaba wa maji na kuahidi kuzitatua kwa kuwa ameshazifanyia utafiti.
“Leo nimetembelea Shule za Msingi Makalala, Mkombwe, Ndolezi na Mwongozo na Shule ya Sekondari Luganga na nimejionea shida ya upatikanaji wa maji hivyo kwa kuwa NGO yetu inajihusisha na uchimbaji wa visima hivyo tumewasilisha taarifa hizi makao makuu ya ofisi zetu na tunasubili majibu”alisema Bw Donsun Lee.
Bw Donsun Lee alimpongeza mbunge wa jimbo mafinga mjini Cosato Chumi kwa juhudi alizozifanya za kuwashawishi kutembelea jimbo hilo na kujionea baadhi ya changamoto  ambazo wanaweza kuzitatua kwa kushiriana na mbunge huyo.

Katika ziara hiyo Bw Lee na timu yake walitembelea Shule za Msingi Makalala, Mkombwe, Ndolezi na Mwongozo na Shule ya Sekondari Luganga.
Aidha baada ya tafiti hizo, Bw Lee atawasilisha taarifa zake Makao Makuu ya NGO ya Serving Friends International huko Seoul, Korea.
Nia ya kufanya tafiti hizo ni kuiweka Katika Mipango Halmashauri ya Mji wa Mafinga kwa sababu ndo utaratibu wa NGO hiyo ambayo kwa Sasa wanachimba visima mkoani Singida
Kwa upande wake mbunge wa jimbo la mafinga Cosato Chumi amemshukuru Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International Bw Donsun Lee kwa kufanikisha kufanya tafiti ambazo amejine mwenye na kuleta matumaini kwa wananchi wa jimbo hilo la kutatuliwa tatizo la maji kwa kuchimbiwa visima na taasisi hiyo.
Chumi ameongeza kuwa haya ni matokeo ya ziara ya Balozi wa Korea ambaye alitembelea jimbo la Mafinga Mwezi mmoja uliopita na kujionea changamoto hizo.
Lakini mbunge Chumi amewataka wananchi wa jimbo la mafinga kufanya kazi kwa kujituma na kuunganisha na nguvu za mbunge wao ili kupata maendeleo kwa kasi inayotakiwa.
“Unakuta mbunge nahangaika kuwaletea maendeleo wananchi wangu kama hivi mnavyoona lakini ukienda vijiweni unakuta wananchi wanacheza bao,pooltable na wengi wanapiga soga zisizo na malengo,wakati wangeutumia muda huo kufanya kazi jimbo la mafinga mjini litakuwa na maendeleo ya kasi sio muda”.alisema Chumi

No comments :

Post a Comment