Sunday, September 4, 2016

MAJALIWA AWASILI DODOMA KWA AJILI YA BUNGE




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Lugimbana  baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma Septemba 4, 2016 kwa ajili ya vikao vya Bunge vinavyotarajiwa kuanza Septemba 6, 2016. (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)


Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa akisalimiana Septemba 4, 2016  na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma kwa ajili ya vikao vya Bunge vinavyotarajiwa kuanza Septemba 6, 2016
Wasanii wa Clever Boys ambao wameingia fainali ya mashindano yaliyodhaminiwa na Vodacom Tanzania ya Dance 100%, wakichuana kwenye nusu fainali ya  mashindano   hayo katika viwanja vya Don Bosco  jijini Dar es Salaam


Mmoja wa Majaji wa mashindano yanayodhaminiwa na Vodacom Tanzania ya Dance100%, Super Nyamweli (kulia) akionyesha umahiri wake wa kucheza kwenye nusu fainali ya  mashindano hayo jijini Dar es Salaam huku akishangiliwa na mmoja wa majaji wenzake Khalila Kellz

Wasanii wa Clever Boys ambao wameingia fainali ya mashindano yaliyodhaminiwa na Vodacom Tanzania ya Dance 100%, wakichuana kwenye nusu fainali ya  mashindano   hayo katika viwanja vya Don Bosco  jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)Mhandisi,Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa bodi mpya.kesho

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira leo itazindua bodi mpya yake iliyoteuliwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji  Mhandisi Gerson Lwenge Julai Mosi mwaka huu baada ya ile ya awali kumaliza muda wake ambayo ilidumu kwa kipindi cha miaka mitatu.

Katika uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ambayo inatarajiwa kuanza asubuhi.

Akizungumza jana,Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa aliwaambia waandishi wa habari kuwa halfa hiyo pia itatumika kutambua na kupongeza juhudi zinazofanywa na bodi,menejimeni na wafanyakazi wa mamlaka hiyo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)Mhandisi,Joshua Mgeyekwa kushoto aliyesimama na PRO wa Mamlaka hiyo
Alisema licha ya wafanyakazi hao lakini pia wateja wao kwa kuiwezesha mamlaka hiyo kuwa bora kwa utoaji wa huduma za maji safi miongoni mwa mamlaka 23 za maji safi na usafi wa mazingira hapa nchini kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo tokea mwaka 2012/2013.
Aidha alisema pia mamlaka hiyo imepata leseni ya daraja la kwanza baada ya kukithi vigezo vya mdhibiti wa huduma za nishati na maji hivyo kuwa mamlaka ya kwanza ya maji safi na usafi wa mazingira hapa nchini kufikia hatua hiyo ya juu katika ufanisi wa utendaji wa mamlaka.

  “Waandishi wa habari kama mnavyojua mamlaka yetu ina cheti cha ithibati ya Ubora (ISO 9001) ambacho imekipata tangu mwaka 2007 tokea kipindi hicho mamlaka imekuwa ikifanya kazi zake kwa viwango vya kimataifa katika usimamizi wa mfumo wa kumhudumia mteja kwa kufuata vigezo vya ubora “Alisema.

Waandishi wa habari mkoani Tanga wakifuatilia hotuba ya mkurugenzi huyo
  “Lakini pia cheti hiki huuishwa kila baada ya miaka mitatu kwa kukidhi vigezo vya utoaji wa huduma vinazohitajika ,uhuishaji ulifanyika miaka 2010 na 2013 kwa kupata ISO 9001:2008 na mwaka huu Tanga Uwasa imekuwa taasisi ya kwanza nchini chini ya kampuni ya Ithibati ya SGS Tanzania kupata cheti cha Ithibati cha 9001:20015.

Aidha aliongeza kuwa mafanikio makubwa sana ambayo hayo yametokana na juhudi za pamoja kati ya bodi ya wakurugenzi, menejimenti,wafanyakazi,wateja na wadau wa Tanga Uwasa.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha
 Rais John Pombe Magufuli, akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam usiku huu Septemba 3, 2016. Rais alikuwa kwenye ziara ya siku mbili visiwani Zanzibar kuwashukuru wananchi kwa kuichagua CCM.(PICHA NA IKULU).

Mkuu wa mkoa  wa Mara Dkt. Charles Mlingwa  na  Meneja  wa   Tigo  kanda  ya  ziwa, Edgar Mapande  wakinyanyua mikono   juu   mara  baada  ya  makabidhiano  ya  madawati 135 kwa  wilaya ya Rorya na jumla ya   madawati 235 kwa  mkoa  wa Mara, hafla  iliyofanyika  shule yamsingi  Utegi wilayani  Rorya  jana
Mkuu  wa  Mkoa  wa Mara Dkt. Charles Mlingwa  akiongea na wazazi,walimu na wanafunzi wa shule ya msingiUtegi wilayani Rorya wakati wa hafla ya kukabidhi  madawati   kwa  shule hiyo  jana. Jumla  ya madawati 235 yalitolewa kwa mkoa huo. Pichani kutoka kushoto Meneja waTigo Mkoa wa Mara, Edwin Kisamo,Meneja wa Tigo kanda ya  ziwa, Edgar Mapande ,Mkuu wa wilaya ya  Rorya, Simon Chacha  na   Mwenyekiti wa  Halmashauri  mka Mara, Albert Machiwa
Meneja wa Tigo  Mkoa wa Mara, Edwin Kisamo akiongea na walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Utegi  wilayani Rorya wakati   wa  hafla ya kukabidhi madawati kwa shule hiyo jana.
Meneja wa  Tigo  kanda ya  ziwa, Edgar Mapande  akiongea na  walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Utegi wilayani Rorya wakati wa hafla ya kukabidhi  madawati kwa shule  hiyo  jana, Wengine  pichani  kushoto  kwake  ni  mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt.Charles  Mlingwana  Mkuu wa wilaya ya   Rorya, Simon Chacha.
Mkuu wa Mkoa  wa Mara Dkt. Charles Mlingwa  akipokea  madawati 235 kwa  mkoa   wa Mara toka  kwa  Meneja  wa Tigo kanda ya  ziwa, Edgar Mapande  kwenye hafla  iliyofanyika  shule  ya  msingi   Utegi  wilayani   Rorya    jana

Wanafunzi wa  shule  ya   msingi   Utegi   wakiwa  wameketi kwenye madawati waliopewa na kampuni ya simu za mkononi Tigo    jana.


Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Nelson Mlela akifafanua jambo kwa Kamati ya  Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira walipotembelea kuangalia utendaji kazi wa Bandari ya Dar es Salaam leo Septemba 3,2016 . (PICHA ZOTE NA OFISI YA BUNGE)


Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Khatib Said Haji Mbunge wa Konde akichangia hoja katika kikao baina ya wadau wa biashara na Kamati hiyo walipokutana kujadili masuala mbalimbali ya kibiashara katika Bandari za Tanzania leo Septemba 3,2016.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania Mhandisi Deusdedit Kakoko(kushoto) akifafanua jambo mbele ya Kamati ya  Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu masuala mbalimbali ya kibiashara katika Bandari za Tanzania leo Septemba 3, 2016 kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Dkt Dalaly Peter Kafumu Mbunge wa Igunga.


Mwenyekiti wa Kamati ya  Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Dkt Dalaly Peter Kafumu Mbunge wa Igunga akizungumza na uongozi wa Bandari na watendaji wa Wizara husika walipokutana kujadili masuala mbalimbali ya kibiashara katika Bandari za Tanzania leo Septemba 3, 2016.


Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini TAFF Bw. Otieno Ogobo akitoa maoni yake kwa Kamati ya  Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira walipokutana kujadili masuala mbalimbali ya kibiashara katika Bandari za Tanzania leo Septemba 3, 2016.


Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Jocktan Kyamuhanga akifafanua jambo mbele ya Kamati ya  Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu masuala mbalimbali ya ukusanyaji mapato katika Bandari za Tanzania leo Septemba 3,2016 .

Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Nelson Mlela akifafanua jambo kwa Kamati ya  Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira walipotembelea kuangalia utendaji kazi wa Bandari ya Dar es Salaam leo Septemba 3,2016


Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Anatropia Theonest Mbunge wa Viti maalum (Chadema) akichangia hoja katika kikao baina ya wadau wa biashara na Kamati hiyo walipokutana kujadili masuala mbalimbali ya kibiashara katika Bandari za Tanzania leo Septemba 3, 2016.

No comments :

Post a Comment