Thursday, September 22, 2016

MADEREVA 10 WA TANZANIA WALIOTEKWA NCHINI CONGO WAREJEA NCHINI NA KUSEMA WALIPONEA TUNDU LA SINDANO KUUAWA



 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba (katikati), akizungumza na madereva 10 wa Tanzania waliotekwa na watu wanaodaiwa kuwa ni waasi Jamhuri ya Demokrasia ya Conco (DRC), wakati wa hafla fupi ya kuwapokea iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam leo jioni. Kulia ni Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba na kushoto ni Mkurugenzi  Idara ya Afrika katika wizara hiyo, Balozi Samweli Shelukindo.
 Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.
 Mmiliki wa Kampuni ya Simba Logistic ambayo magari yake na madereva walitekwa, Azim Dewj (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo ya kuwapokea madereva hao.
 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakisubiri kuchukua taarifa za kuwapokea madereva hao.
 Madereva hao wakipokelewa uwanjani hapo.
 Madereva hao wakiwa chumba cha mkutano cha uwanja huo wakati wa mapokezi yao.
Dereva  Mbwana Said (kulia), akielezea jinsi walivyotekwa.
 Dereva Kumbuka Seleman (kulia), akisimulia jinsi alivyotoroka na kutoa taarifa ya kutekwa kwao.
Dereva  Athuman Fadhili (kulia), akisimulia walivyookolewa na majeshi ya Congo na jinsi walivyojificha porini na kutembea umbali mrefu kwa kutambaa ambapo ilifika wakati waliomba bora wafe kuliko mateso waliyokuwa wakipata.
 Hapa ni furaha ya kukutana na ndugu jamaa na wafanyakazi wenzao.
 Picha ya pamoja na viongozi waliowapokea.
 Ndugu, Jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzao wakiwa nje ya jengo la VIP uwanjani hapo wakisubiri kuwapokea.
 Mapokezi yakiendelea.
Ni furaha ya kukutana na wapendwa wao.
Hapa Dereva Mbwana Said akikumbatia na mjomba wake Kassim Salim katika hafla hiyo kwa Mbwana ilikuwa ni furaha na majonzi. 
Mbwana Said (katikati), aamini macho yake baada ya kukutana na mke wake Mariam pamoja na mtoto wake Kauzari.

Na Dotto Mwaibale

MADEREVA 10 wa Tanzania waliotekwa na watu  wanaodhaniwa ni waasi Jamhuri ya Demokraia ya Congo (DRC) wamesema waliponea tundu la sindano kuuawa.

Kauli hiyo imetolewa na madereva hao katika hafla ya kuwapokelewa iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam leo jioni.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Mbwana Said alisema analishukuru jeshi la Congo kwa jitihada kubwa walioifanya kwa ajili ya kuokoa maisha yao." 

" Tunaishukuru serikali ya Congo kwa kutuokoa kwani tulikuwa katika wakati mgumu na leo kuungana tena na ndugu zetu" alisema Said.

Alisema walilazimia kutembea kwa muda mrefu huku risasi zikirindima kati ya majeshi ya serikali na waasi hao hadi walipofanikiwa kutuokowa kutoka kwenye mikono ya waasi hao. 

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba aliishukuru serikali ya Congo kwa jitihada iliyoifanya na kufanikiwa kuwaokoa madereva hao.

Balozi wa Congo nchini Jean Mutamba aliwataka madereva hao kuacha viza na nyaraka zao ubalozini pindi wanapo safiri na kurudi ili iwe rahisi kuwatambua pale wanapopata matatizo.

"Tukio hilo limetokea kwa bahati mbaya na kutoa wito kuwa waendelee kusafiri kwa kufuata taratibu zilizopo," alisema Mutamba.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712727062)


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisisitiza umakini kwa wananchi waliojitokeza kwenye Kikao cha Mafunzo ya namna bora ya kushiriki katika kilimo chambogamboga na matunda kupitia umwagiliaji
Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo akiwasihi wananchi kutumia njia za kisasa katika kilimo cha umwagiliaji na kufuata taratibu wanazoelekezwa na wataalamu wa kilimo
Baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali vya ujasiriamali sawia na wajumbe washiriki kwenye mafunzo hayo wakifatilia kwa makini Muelimishaji
Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo
Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu na kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe wakifatiliakwa makini mafunzo ya namna bora ya kujishughulisha na kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia Gree House
Kutoka Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Hassan Tati, Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo
Dc Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kufunga mafunzo hayo
Na Mathias Canal, Singida

Uongozi wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida umeahidi kuvisaidia vikundi mbalimbali ambavyo vitakubali kujihusisha na kilimo cha mbogamboga na matunda (Perishable Crops) sambamba na kilimo hicho kwa kutumia Kitalu Nyumba (Green House).

Kauli ya serikali imetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati akifunga mafunzo kwa wajasiriamali, wakulima na wafugaji yaliyoendeshwa na Asasi isiyo ya kiserikali ya Right Way For Development (RIWADE) kwenye ukumbi wa Mikutano katika Shule ya Sekondari Ikungi na kuhudhuriwa na watu 115 ambao wanatokea katika Kata 24 kati ya Kata 28 zilizopo Wilayani humo.

Katika Mafunzo hayo jumla ya Vikundi 39 vimehudhuria ambavyo vimetakiwa kujishughulisha zaidi kukimbia kilimo cha mazoea ambacho wakulima hulima msimu mmoja hadi mwingine na hatimaye kujihusisha na kilimo cha umwagiliaji ambacho kinatumia muda mchache kukamilika na kuanza kwa mavuno.

DC Mtaturu amevitaka vikundi hivyo kwa pamoja kutumia vyema fursa ya Makao makuu ya serikali kuhamia Mjini Dodoma kwani itakuwa taswira chanya katika kukuza soko la mazao yao pasina kupata ugumu wa uuzaji.

Amesema kuwa Mkoa wa Singida mara nyingi umekuwa ukitajwa kama mkoa masikini nchini Tanzania kati ya mikoa 10 ambayo ipo mkiani katika maendeleo ya kiuchumi kwa sababu ya wananchi wenyewe kutofanya ubunifu katika kilimo chao jambo ambalo linasababisha uzalishaji mdogo na kupelekea kipato kuendelea kuwa duni ilihali maandalizi ya mashamba ni makubwa.

Mtaturu amesema kuwa wananchi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa serikali katika kukamilisha adhma yake katika uwekezaji na Tanzania ya viwanda kwani endapo watakubali kulima kilimo cha kisasa na kuwa na uzalishaji mkubwa itakuwa rahisi kwa serikali kuanzisha viwanda vya kusindika mazao.

Kwa upande wake muwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE ambayo imesajili kwa lengo la kiwasaidia vijana wasio na ajira waweze kufanya kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Mazingira Mhandisi Ayubu Massau alisema kuwa wananchi wanapaswa kufikia kilimo cha kuachana na kuuza mazao yao kwa madalali badala yake kuuza moja kwa moja kwa mtumiaji jambo ambalo litatoa fursa chanya ya mafanikio makubwa katika pato la mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo amepigia chepuo zaidi kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) na kusema kuwa ndicho kilimo pekee chenye uwezo wa kuwatoa wananchi kwenye kadhia ya umasikini kwani kilimo hichp kupitia umwagiliaji wa kisasa unatumia maji machache na matokeo yake ni makubwa kama wakulima watafuata taratibu zote za utunzaji wa shamba.

Massau alisema kuwa umefika wakati wa wananchi kuachana na vyama vya kufa na kuzikana badala yake kujihusisha zaidi na vyama vya kujikwamua kiuchumi kupitia vikundi mbalimbali.

Naye Moses Msai ambaye ni Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida alisema kuwa wakulima wanapaswa kutambua kuwa sekta pekee yenye uwezo wa kuajiri watu wengi na kuwatoa kwenye lindi la umasikini ni Sekta ya Kilimo hivyo ni vyema kufanya kilimo cha kisasa kwani ndicho kitakacho wanufaisha wananchi.

Ametoa fursa kwa wananchi kujiunga na RIWADE kwani watapata fursa ya kuunganishwa na wataalamu ili kuelekezwa namna bora ya kulima kilimo cha umwagiliaji.

Hata hivyo Mjasiriamali na mkulima aliyeshika nafasi ya Kwanza kanda ya kati katika sekta ya kilimo Hassan Tati aliwasihi wakulima hao waliopatiwa mafunzo kuwa mafanikio kwenye kilimo ni makubwa endapo wakulima watafuata taratibu za kilimo na kuwasikiliza wataalamu.

Tati amesema kuwa hakuna ajira nzuri duniani kama kuwekeza kwenye kilimo lakini amewasihi wananchi kuing'ang'ania Asasi ya RIWADE kwani ni taasisi muhimu kwa kila mmoja kwa kujitolea kutoa mafunzo ya kilimo na ufugaji.

Asasi isiyo ya kiserikali ya Right Way For Development (RIWADE) ilianzishwa Mwezi June 2016, ikiwa ni dhima ya kutengeneza na kutoa fursa kwa watanzania wote ili waweze kupata elimu ya ujasiriamali na namna ya kutengeneza mitaji kwa ajili ya ukuaji endelevu wa kijamii na kiuchumi.



 Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gdwin GOndwe akisalimiana na mkazi wa kijiji cha nyasa.
 Mkuu waa Wilaya ya Handeni,Mh Godwin Gondwe  Jana alifanikiwa kusuluhisha mgogoro wa mpaka uliokuwa ukivihusisha vijiji viwili vya kata ya kang'ata wilayani Handeni .Vijiji hivyo ni Madebe na Nyasa ambao walikua hawafahamu mpaka wao unaishia wapi,suluhu hiyo ilifanikiwa kumalizwa na mkuu wa wilaya na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Handeni ,Bwa.William Makufwe.
DC Gondwe pia aliwataka wananchi na viongozi wajikite katika shughuli za kimaendeleo badala ya kujikita kwenye suala la mipaka ,Kwa madai  wapate maeneo ya kulima wakati wakigombania maeneo ili wauze. Amewaonya wasiuze ardhi kiholela  na kufanya vizazi vijavyo kuwa watumwa kwenye ardhi yao.
 Mkuu wa wilaya Mh.Godwin Gondwe akimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Handeni,Ndugu William Makufwe (pichani kushoto) akitoa ufafanuzi kwa wananchi wa vijiji vya nyasa na madebe.
 Mwenyekiti wa kijiji cha nyasa  na madebe wakipeana pongezi baada ya kujua mipaka yao huku wakisistizwa kujikita zaidi katika masuala ya maendeleo.
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Gondwe akipeana mkono wa pongezi na Mwenyekiti wa kijiji cha Nyasa baada ya kupata mpaka wa maeneo yao.
Mkuu wa wilaya ya handeni Mh.Gondwe akizungumza na wananchi wa vijiji vya nyasa na madebe akiwakataza wasiuze ardhi kiholela na wasigombanie maeneo ili wayauze.

Wafuasi wa CUF, wakiwa wamemzunguka Mbunge wa jimbo la Temeke kupitia CUF, Abdallah Mtolea, baada ya kushinda kesi ya kupinga ushindi wake iliyofunguliwa na aliyekuea mgombea wa jimbo hilo kupitia CCM, Zuberi Mtemvu Mahakama Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo Septemba 21, 2016.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkurugenzi wa Benki ya Dunia wa nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia, Bella Bird (kulia kwake) na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman (kulia) baada ya kuweka jiwe la msingi la jengo la Hakimu Mkazi Mahakama ya Pwani na Mahakama ya wilaya ya Kibaha Septemba 21,2016. Wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo. (PICHA NA OFISI YA  WAZIRI MKUU)

  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyesha   Mpango Mkakati na Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania  baada ya kuuzindua mjini Kibaha, Septemba 21, 2016. Wengine pichani kutoka kushoto ni Dkt. Hassison Mwakyembe, Waziri wa Katiba na Sheria, Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande na Naibu Spika wa Bunge, Dkt Ackson Tulia
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisaidiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othaman kukata utepe wakati alipozindua  Mpango Mkakati na Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania  mjini Kibaha, Septemba 21, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman  baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge  Dkt, Tulia Ackson baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarest Ndikilo akizungumza  katika   uzinduzi  Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha Septemba 21, 2016
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji  akizungumza katika   uzinduzi  Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha Septemba 21, 2016.
Mkurugenzi wa Benki ya Dunia katika nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia, Bella Bird  akizungumza katika   uzinduzi  Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha Septemba 21, 2016
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman akizungumza katika uzinduzi  katika   uzinduzi  Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha Septemba 21, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyesha Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania  baada ya kuuzindua mjini Kibaha Septemba 21, 2016. Wengine pichani kutoka kushoto ni Dkt. Hassison Mwakyembe, Waziri wa Katiba na Sheria, Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande na Naibu Spika wa Bunge, Dkt Ackson Tulia
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi wa Benki ya Dunia wa Nchi za Tanzania, Burundi, Malawi na Somalia, Bella Bird kitabu cha Mradi wa Maboresho  ya Huduma za Mahakama ya Tanzania  baada ya kuuzindua mjini Kibaha Septemba 21, 2016. Kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman  na kulia ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua  Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania ulifanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa mjini Kibaha Septemba 21, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifunua kitambaa kuashiria ufunhuzi wa  jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha  Sptemba 21, 2016

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman  baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi  Evarest Ndikilo baada ya kuwasili kwenye eneo inapojenjwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Pwani na Mahakama ya Wilaya ya Kibaha kuzindua Mpango Mkakati na Mradi  wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ya Tanzania Septemba 21, 2016
 Baadhi ya watumishi wa serikali na wananchi wengine
 Baadhi ya watumishi wa serikali na wananchi wengine
Waziri Mkuu katika picha ya pamoja

OFISI YA URATIBU WA SHUGHULI ZA SMZ YAPOKEA MTAMBO MAALUM WA MAWASILIANO YA NDANI

Meneja Mkuu wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nd. Ali Ibrahim Kilupi kushoto akimkabidhi msaada wa mtambo maalum wa mawasiliano ya Simu za ndani { Inter call } Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Joseph Abdulla Meza kwa ajili ya Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam. Wa kwanza kutoka Kulia anayeshuhudia tukio la makabidhiano hayo ni Mratibu Mkuu wa Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam Ndugu Issa Mlingoti Ali.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Meza akiuwasilisha msaada huo wa Mtambo wa mawasiliano ya Simu kwa mlengwa Mratibu Mkuu wa Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam Ndugu Mlingoti.
                                                                                         Picha na – OMPR – ZNZ.
 
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Joseph Abdulla Meza alisema jamii na hasa wananchi Wazalendo wenye uwezo wanapaswa kuendelea kujenga tabia ya kusaidia nguvu katika kupambana na changamoto zinazoikabili serikali pamoja na wananchi katika maeneo mbali mbali nchini.

Alisema mfumo uliozoeleza kwa kipindi kirefu sasa katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ni ule uliotegemewa zaidi wa kupokea misaada kutoka Mashirika, taasisi na mataifa ya nje ya nchi.

Ndugu Joseph Abdulla Meza alitoa kauli hiyo wakati akipokea msaada wa mtambo maalum wa mawasiliano ya ndani { Inter call }kwa ajili ya Ofisi ya Uratibu wa Shughuli za SMZ Mjini Dar es salaam uliotolewa na Uongozi wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nungwi hafla iliyofanyika Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Alisema wakati umefika kwa wananchi wenyewe kurejesha ari iliyowahi kutekelezwa miaka ya nyuma katika nia ya kujenga nchi kwa kushirikiana kwenye Nyanja zote zinazohusika za kujenga Taifa lenye nguvu za Kiuchumi, maendeleo na ustawi wa Jamii.

{ Tumezoea kupokea misaada kutoka nje ya nchi lakini ni vyema tukapaswa kujenga tabia ya Wananchi wenyewe kusaidia changamoto zinazotukabili sisi pamoja na Serikali yetu “. Alisema Nd. Meza.

Katibu Mkuu huyo wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliushukuru Uongozi wa Hoteli ya Kendwa Rocks kwa uamuzi wake wa kusaidia nguvu za kiuwezeshaji changamoto zinazozikabili baadhi ya Taasisi za Umma Nchini.

Mapema Meneja Mkuu wa Hoteli ya Kendwa Rocks Nd. Ali Ibrahim Kilupi alisema Taasisi yake imeamua kutoa Mtambo huo ili kuwasaidia watendaji wa Ofisi ya Uratibu wa shughuli za SMZ kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

HALI YA TAHADHARI YATANGAZWA CHALOTTE KUFUATIA KUENDELEA KWA GHASIA

WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI WAAGIZWA KUWA NA KIWANGO CHA UFAULU KUANZIA ASILIMIA 41

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deogratius Ndejembi akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na Wakuu wa Shule za sekondari Wilayani humo
Na Mathias Canal, Dodoma

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deogratius Ndejembi amewaagiza wakuu wa shule za Sekondari zote za Wilaya hiyo kuhakikisha wanafikia ufaulu kuanzia asilimia 41% ili kuakisi hali ya ukuaji wa ufaulu nchini na kupata wanafunzi waliopikwa vyema darasani ili kuwa na wasomi wenye weledi pasina mashaka.

Dc Ndejembi amesema kuwa hatarajii kusikia shule mojawapo Wilayani humo ikiwa imeshika mkia Kiwilaya, Mkoa ana Taifa kwani kufanya hivyo ni kuonyesha jinsi ambavyo walimu hawakujiandaa vyema katika kuwaimarisha wanafunzi darasani ili kufikia ufaulu mahususi na kulijenga Taifa letu katika misingi bora ya elimu.

Ndejembi alisema kuwa anataraji kushirikiana na Afisa elimu sekondari ili kutoa hamasa kwa shule ambazo zitafanya vyema katika mitihani yao ili kuamsha ari kwa shule zingine Wilayani humo.
Walimu hao wametakiwa kutofanya kazi kwa mazoea, kuwa na hofu ya Mungu, na kufanya kazi kwa uzalendo mkubwa katika kufundisha wanafunzi kwani walimu wana wajibu mkubwa wa kuwafanya wanafunzi kufaulu katika mitihani yao.

Sambamba na hayo pia Dc Ndejembi amewataka walimu hao kutokuwa na madaraja kati yao na wanafunzi wao kwani kufanya hivyo ni kutengeneza chuki kutoka kwa wanafunzi kwenda kwa walimu ambapo pia inapelekea kuyachukia masomo yanayofundishwa na walimu hao.

BARCELONA YABANWA NA ATLETICO MADRID KATIKA MCHEZO WA LA LIGA

MTUKUTU MARIO BALOTELLI AENDELEA KUTAKATA NCHINI UFARANSA

VILLARREAL YATIBUA MIPANGO YA REAL MADRID KUWEKA REKODI

Real Madrid imepoteza nafasi ya kuvunja rekodi ya kushinda michezo 17 mfululizo katika Ligi ya La Liga baada ya kulazimishwa sare ya goli 1-1 na Villarreal.

Wenyeji Madrid walijikuta wakifungwa goli baada ya Sergio Ramos kuuzuia kwa mkono mpira na Bruno Soriano kufunga kwa mkwaju wa penati.

Hata hivyo baadaye Sergio Ramos alirekebisha makosa yake baada ya tu ya kuanza kipindi cha pili kwa kufunga kwa kichwa mpira wa kona.
                Sergio Ramos akiwa ameupiga mpira kwa kichwa ambao ulienda kujaa wavuni
                     Cristiano Ronaldo alidhibitiwa vilivyo na kushindwa kutikisa nyavu
 

No comments :

Post a Comment