Monday, August 22, 2016

WAKILI RINGIA AKANUSHA TAARIFA ILIYOTOLEWA NA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU DK. MENGI KUPANDISHWA KIZIMBANI



Dr. Reginald Mengi, MOAT
Mwenyekiti Mtendaji wa  IPP, Dk. Reginald Mengi.
Kufuatia vyombo vya habari mbalimbali nchini kutoa habari ambayo inamhusu Mkurugenzi wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi kuwa anatakiwa kufika mahakamani Agosti, 24 mwaka huu kujieleza kwanini asifungwe kwa kushindwa kutekeleza hukumu ya kulipa Dola 598,750 (Bil. 1.20), wakili wa Dk. Mengi, Deogratias Ringia amekanusha habari hiyo.
Katika taarifa ambayo imetolewa na wakili Ringia, amesema kuwa akiulizwa na watu mbalimbali kama ni kweli kuna hati imetolewa na Mahakama Kuu ikimtaka mteja wake Dk. Mengi kufika mahakamani kujieleza kwanini asifungwe baada ya vyombo mbalimbali kuripoti kuwa anatakiwa kufika mahakamani lakini jambo hilo halina ukweli.
"Mhusika mkuu katika kesi hiyo ni kampuni nayoitwa KM Prospecting Limited ambayo Dk. Mengi siyo mwanahisa wala mkurugenzi katika kampuni hiyo. Kampuni hiyo ndiyo iliingia kwenye mkataba na wadai iliyopelekea kesi hiyo ya madai," alisema Ringia.
Ringia alisema hatua ya kumuunganisha Dk. Mengi katika kesi hiyo lilikuja baada ya mahakama kuamua hoja mbili zinazohusu kesi hiyo ndipo wadai ambao ni wafanyabiashara Muganyizi Lutagwaba, Eric Mshauri na Charles Mgweo kumuingiza Dk. Mengi katika kesi licha ya kuwa hausiki.
Baadhi ya vyombo vya habari vilivyoandika habari hiyo ni pamoja na gazeti la Jambo Leo, Daily News, The Citizen na mtandao wa Habari Leo Online.
Jambo Leo
Barua ya Mwanasheria wa Mengi 21-Aug-2016 14-39-27-page-001


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiwapungia wananchi wa Inyonga baada ya waziri Mkuu kutawazwa kuwa Chief wa Wakonongo na kupewa jina  la Chief Kayamba wa Kwanza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Inyonga Agosti 22, 2016. Kulia  ni Cheif wa Wakonongo, Kayamba wa Pili. (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakimsikiliza Chifu Kayamba wa Pili  (kulia) wakati  Waziri Mkuu alipotwazwa kuwa Chief wa Wakonongo na kupewa jina la Kayamba wa Kwanza katika mkutano uliofanyika  kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Inyonga wialyani Mlele Agosti 22, 2016

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akionyesha Mpango wa Mafunzo ya Ujasiriamali katika jimbo la Nsimbo mkoani Katavi aliouzindua  kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Katumba akiwa katika ziara ya mkoa huo Agosti 21, 2016

Wananchi wakionyesha mabango wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipowasili kwenye uwanja wa Kashaulili  mjini Mpanda kuhutubia mkutano wa hadhara  Agosti 21, 2016.  Katika hotuba yake Waziri Mkuu alizitolea majibu kero zote zilizoandikwa  kwenye  mabango hayo akiwahusisha watendaji wa Halmashauri, mkoa na wilaya
Wananchi wakionyesha mabango wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipowasili kwenye uwanja wa Kashaulili  mjini Mpanda kuhutubia mkutano wa hadhara  Agosti 21, 2016.  Katika hotuba yake Waziri Mkuu alizitolea majibu kero zote zilizoandikwa  kwenye  mabango hayo akiwahusisha watendaji wa Halmashauri, mkoa na wilaya
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akiwasalimia wananchi wa Mpanda wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipohutubia mkutano wa hadahara kwenye uwanja wa Kashaulili mjini Mpanda Agosti 21, 2016. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Katavi, Meja Jenerali Mstaafu, Raphael Mbuga
 Waziri Mkuu Majaliwa kihutubia wananchi


Wasanii wa kijiji cha Katumba wilayani Mpanda wakicheza ngoma ya Kasimbo  wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipohutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo akiwa katika ziara ya mkoa wa Katavi Agosti 21, 2016

No comments :

Post a Comment