Monday, August 22, 2016

MICHUANO YA OLIMPIKI RIO 2016 YAFUNGWA KWA SHAMRASHAMRA


KISHINDO CHA UZINDUZI WA MSIMU WA TIGOFIESTA 2016 CHAZIZIMA JIJINI MWANZA USIKU WA JANA

 
Mkali wa singeli ManFongo na Shilole wakilivamia jukwaa la Tigo Fiesta 2016 katika tamasha hilo kubwa liliofanyika usiku wa jana jijini Mwanza na kukutanisha wasanii nguli katika muziki wa kizazi kipya na Msanii wa kimataifa toka Nijeria Wizkid . 
Umati wa wakazi wa Jiji la Mwanza wakitoa shangwe wakati burudani mbalimbali zikiendelea katika Tamasha la Tigo Fiesta 2016 viwanja vya CCM Kirumba hapo usiku wa jana. 
Alikiba alikuwa kivutio kwa mashabiki wengi mara baada ya kufanya suprize na kutoa burudani ya kukata na shoka huku mashabiki zake wakifuatisha nyimbo zake moja baada ya nyingine katika Tamasha la Tigo Fiesta 2016 katika viwanja vya Kirumba Jijini Mwanza.  
Benpol akilishambulia jukwaa la Tigo Fiesta 2016 lilifnayika jana katika viwanja vya CCM kirumba Jijini Mwanza.  
Msanii wa kizazi kipya Dayna Nyange akitumbuiza umati uliohudhuria Tamasha la Tigo Fiesta 2016 jijini Mwanza hapo usiku wa jana.

NEYMAR AONGOZA KUSHANGILIA BRAZIL IKISHINDA KATIKA MPIRA WA WAVU

GARETH BALE AIONGOZA REAL MADRID KUPATA USHINDI


Mshambuliaji Gareth Bale ametumia sekunde 72 kufunga goli lake la kwanza kwa msimu huu na kisha kuongeza la pili wakati Real Madrid ikiifunga Real Sociedad kwa mgoli 3-0 katika mchezo wa La Liga.

Mchezaji Marco Asensio, 20, naye alifunga goli akionekana kuongozwa vyema na Bale na kuifanya Real Madrid kutoonekana kumkosa mshambuliaji wake nyota Cristiano Ronaldo ambaye hakushuka dimbani.
                       Gareth Bale akiruka juu na kupiga mpira wa kichwa uliojaa wavuni
          Beki Markel Bergara akiteleza na kumkata buti Mateo Kovacic wa Real Madrid

No comments :

Post a Comment