Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akiimba wimbo wa Amani pamoja na Kwaya ya Kanisa la African Inland Church la Chato Mkoani Geita
mara baada ya kuwasili katika kanisa hilo Agosti 7, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakisali katika ibada ya
Jumapili katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakimsikiliza Mchungaji wa Kanisa
la Anglikana Chato Zacharia Samson mara baada ya kuwasili katika kanisa hilo la
Anglikana Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akihamasisha mchango wa ujenzi wa Kanisa jipya la la Bikira Maria
Parokia ya Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akizungumza na waamini wa kanisa Katoliki wa Parokia ya Chato mara
baada ya Ibada katika kanisa hilo Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akiagana na Padre wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Henry
Mulinganisa mara baada ya kushiriki Ibada katika Kanisa hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akimsalimia Mwalimu wake wa zamani wa Shule ya Msingi Chato Mkoani
GeitaMwalimu Mkuu Mstaafu Jackson
Nyamwaga mara baada ya kumuona wakati akitoka katika Kanisa la African Inland Church la Chato Mkoani Geita.
Shekhe wa Bakwata Wilaya ya Chato Hassan Issa Mnubi
akiongoza dua ya Kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli nje ya Msikiti wa Omar
Bin-L-Khattab Chato Mkoani Geita. PICHA
NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiwapungia mkono waamini wa Kanisa Katoliki Kanisa la
Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita hawapo pichani mara baada ya
kushiriki Ibada katika kanisa hilo
Baadhi
ya Wananchi wakijaza Fomu ya Kujiunga na WOTE SCHEME katika Banda la
PPF Viwanja vya Nane Nane Ngongo Kama Picha Inavyoonekana Afisa
Uhusiano Mwandamizi, Janet Ezekiel akitoa maelekezo ya Jinsi ya Kujaza
Fomu Hizo.
Wananchi waliotembelea Banda la PPF, wakimsikiliza kwa Makini Afisa Masoko PPF Wakati akitoa Elimu Juu ya Mfumo wa WOTE SCHEME.
Baadhi
ya Wananchi wakijaza Fomu ya Kujiunga na WOTE SCHEME katika Banda la
PPF Viwanja vya Nane Nane Ngongo Kama Picha Inavyoonekana Afisa
Uhusiano Mwandamizi, Janet Ezekiel na Afisa Masoko PPF, Wakitoa
maelekezo ya Jinsi ya Kujaza Fomu Hizo
Afisa Uhusiano Mwandamizi, Janet Ezekiel akimkabidhi kadi ya WOTE SCHEME kwa mwananchi aliyejiunga na Mfuko huo.
Akiongea na Lindiyetu.com Bi Janeth ametoa wito kwa wadau mbalimbali kutembelea Banda hilo la PPF kwa ajili kupata elimu na kujiunga na mfuko huo na kufaidika na fursa zinazotolewa na PPF.
Na Stella Kalinga (Ofisi ya Mkoa wa Simiyu)
Mkuu
wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amewataka
viongozi wa kata na vijiji kuwabaini wanufaika wa Mpango wa kunusuru kaya TASAF
III(PSSN) wanaojihusisha na ulevi na kuwaondoa katika orodha ya wanufaika wa
mpango huo.
Mtaka
ametoa agizo hilo wakati alipozungumza na wananchi wa kijiji cha Mwamgoba
wilayani Busega katika zoezi la uhawilishaji fedha za TASAF III PSSN, ambapo
jumla ya shilingi 2,976,000 zimegawiwa kwa wanufaika 82 kijijini hapo.
Mtaka
amesema lengo la mpango wa TASAF III ni kuwatoa watanzania katika hali ya
umaskini kwa kuwapa ruzuku itakayowasadia kupata huduma muhimu ikiwa ni pamoja
huduma za afya, kuwasaidia watoto wao waweze kwenda shule lakini baadhi ya
wanufaika wamekuwa wakitumia fedha hizo kulewa badala ya kuanzisha miradi
midogo midogo kama ufugaji wa kuku, mbuzi na kondoo pamoja na kilimo ili miradi
hiyo iwasaidie kuwaongezea kipato.
“Hatuwezi
kuleta fedha tukifikiri zitawasaidia kujikwamua
katika Umaskini lakini mnashinda baa na vilabuni kulewa , wengine mnaongeza
wake, tukiwabaini mtaondolewa kwenye huu mpango” , alisema Mtaka.
Mtaka
amewataka wanufaika hao kujishugulisha na kilimo na ufugaji na kuondokana na
dhana ya kuwa watakuwa wanufaika wa
mpango huo siku zote, ambapo alieleza azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kuwatoa wananchi
katika umaskini na kuwaondolea changamoto mbalimbali kama kutoa elimu ya bila
malipo na kuanzisha Mfuko wa Huduma ya Afya Watanzania wasio na uwezo waweze
kupata matibabu kwa gharama nafuu na
akatoa wito kwa wanufaika hao kujiunga na Mfuko wa Huduma ya Afya ya Jamii (CHF)ambao
utawasaidia wao wenyewe pamoja na wategemezi wao kupata huduma za Afya katika
Vituo vya kutolea huduma za Afya.
Aidha,
ametoa wito kwa wazazi kuwakumbusha watoto wao wajibu wa kuwatunza kwa sababu
kumekuwa na baadhi ya wazee ambao wametambuliwa kuwa ni maskini, wakati wana
watoto wenye nguvu na uwezo wa kuwasaidia lakini hawatimizi wajibu wao kuwatunza
kwa kuwapa mahitaji muhimu.
Akizungumza
baada ya kukabidhiwa fedha hizo Bibi. Christina Robert ambaye ni mnufaika wa
mpango wa TASAF amesema mpango huo umemsaidia kuondokana na kuishi katika
nyumba ya nyasi na matope na kumuwezesha kujenga nyumba ya matofali na bati.
“Naishukuru
TASAF maana imenisaidia sana, ruzuku niliyopewa mara ya kwanza ilinisaidia
kutibiwa nilipofanyiwa upasuaji, mara ya pili nilitumia tena kwenye matibabu,
mara ya tatu nilinunua kuku na bata, mara ya nne nikanunua bati nikajenga nyumba ya vyumba
viwili”, alisema Christina.
Pamoja
na kusisitiza juu ya matumizi sahihi ya fedha za ruzuku za TASAF Mtaka
amewataka wananchi wa Busega na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla kuongeza juhudi
katika kilimo cha mazao ya mikunde kwa kuwa tayari Serikali ya India imekubali
kununua zaidi ya tani milioni sita ya choroko, dengu na mbaazi kutoka
Tanzania, hivyo wakati utekelezaji wa
makubaliano hayo utakapoanza wananchi walime kwa wingi mazao hayo kwa kuwa
kutakuwa na soko la uhakika.
Jumla
ya kaya 4260 zilibainishwa katika vijiji 41 vya wilaya ya Busega ambapo kaya 53
ziliondolewa katika mpango wa TASAF III PSSN baada ya uhakiki na kubaini kuwa
hazikukidhi vigezo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan amewasili mjini Lindi mchana huu akitokea mkoa wa Dar es Salaam
kwa njia ya barabara ambapo hapo kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
katika kilele cha Sikukuu ya Wakulima Nanenane kitaifa kwenye viwanja
wa Ngongo katika Manispaa ya Lindi.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufunga maonyesho hayo ya Nane nane hapo kesho kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta John Pombe Magufuli.
Alipowasili ikulu ndogo mjini Lindi Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amepokelewa na Mkuu wa mkoa wa LINDI Godfrey Zambi pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali na wa vyama vya siasa.
Katika Msafara wake, Makamu wa Rais ameambatana na Waziri wa Kilimo, Maliasili na Uvuvi wa Zanzibar Mhe. Hamad Rashid.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufunga maonyesho hayo ya Nane nane hapo kesho kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta John Pombe Magufuli.
Alipowasili ikulu ndogo mjini Lindi Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amepokelewa na Mkuu wa mkoa wa LINDI Godfrey Zambi pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali na wa vyama vya siasa.
Katika Msafara wake, Makamu wa Rais ameambatana na Waziri wa Kilimo, Maliasili na Uvuvi wa Zanzibar Mhe. Hamad Rashid.
STAMICO YAWATANGAZIA NEEMA WACHIMBAJI WA MADINI TANZANIA
Katika
kuhakikisha wachimbaji wadogo wananufaika na kazi zao na kuepuka
kuondolewa na wachimbaji wakubwa wameshauriwa kuchukua leseni ndogo za
awali za uchimbaji.
Kaimu
Mkurugenzi wa utafiti na Uchimbaji wa Shirika la Madini (STAMICO) Alex
Rutagwelela (Katikati) akiongea na waandishi wa Habari (Hawapo pichani)
wakati wa maonyesho ya Nane nane Viwanya vya Ngongo - Lindi.
Wito
huo kwa wachimbaji umetolewa na kaimu mkurugenzi wa utafiti na
uchimbaji wa shirika la madini (STAMICO) Alex Rutagwelela alipokuwa
anazungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya ngongo Manispaa ya
Lindi yanapofanyika maonyesho ya nane nane kitaifa.
Rutagwelela
alisema wachimbaji wadogo wanatakiwa kuwa na leseni za awali
zitakazowafanya wawe na haki kwenye maeneo wanayochimba. hivyo kuwa na
uhakika wa kuto ondolewa bila taratibu na wachimbaji wakubwa kwenye
maeneo wanayochimba.
Wananchi
wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Maafisa wa STAMICO walipotembelea
Banda lao katika Maonyesho ya Nane nane yanayoendelea Mkoani Lindi
katika viwanja vya Ngongo.
Aliwahakikishia
wanahabari na wananchi shirika hilo linania ya kuwainua wachimbaji
wadogo kwa kufanyia tathimini maeneo wanayochimba ili waweze kujua kiasi
cha madini na mashapo yaliyopo katika maeneo hayo.
Katika
kuhakikisha wachimbaji wadogo wananufaika na kazi zao na kuepuka
kuondolewa na wachimbaji wakubwa wameshauriwa kuchukua leseni ndogo za
awali za uchimbaji.
Kaimu
Mkurugenzi wa utafiti na Uchimbaji wa Shirika la Madini (STAMICO) Alex
Rutagwelela (Katikati) akiongea na waandishi wa Habari (Hawapo pichani)
wakati wa maonyesho ya Nane nane Viwanya vya Ngongo - Lindi.
Wito
huo kwa wachimbaji umetolewa na kaimu mkurugenzi wa utafiti na
uchimbaji wa shirika la madini (STAMICO) Alex Rutagwelela alipokuwa
anazungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya ngongo Manispaa ya
Lindi yanapofanyika maonyesho ya nane nane kitaifa.
Rutagwelela
alisema wachimbaji wadogo wanatakiwa kuwa na leseni za awali
zitakazowafanya wawe na haki kwenye maeneo wanayochimba. hivyo kuwa na
uhakika wa kuto ondolewa bila taratibu na wachimbaji wakubwa kwenye
maeneo wanayochimba.
Wananchi
wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Maafisa wa STAMICO walipotembelea
Banda lao katika Maonyesho ya Nane nane yanayoendelea Mkoani Lindi
katika viwanja vya Ngongo.
Aliwahakikishia
wanahabari na wananchi shirika hilo linania ya kuwainua wachimbaji
wadogo kwa kufanyia tathimini maeneo wanayochimba ili waweze kujua kiasi
cha madini na mashapo yaliyopo katika maeneo hayo.
MSHINDI WA AIRTEL TRACE MUSIC STAR 2015 AZUNGUMZA NA VIJANA JIJINI MWANZA. PIA KUDONDOSHA BURUDANI USIKU HUU.
Star wa Airtel Trace Music 2015, Mayunga
Andrew Nalimi-MAYUNGA, akizungumza na #BMG kuhusiana na project yake
ambayo anaifanya na star M-Rap.
Na George Binagi-GB Pazzo
Project inaitwa Across Lovers and
Friend Music Tour ambayo Mayunga anaitumia kukutana na mashabiki zake na
kuwapa burudani ikizingatiwa tangu atoke Marekani hakuwahi kufanya tour
kama hiyo kwa ajili ya mashabiki zake.
Mayunga amesema Project hiyo imeanzia
Mwanza na itaendelea katika mikoa mingine na hata nje ya nchi kama vile
Kenya, Uganda, Malawi na Afrika Kusini.
Usiku huu anapiga show Jembe Beach Jijini Mwanza.
Awali Mayunga pamoja na M-Rap kwa
kushirikiana na Star Foundation na Kwanza Online na timu nzima ya Trace
Music, waliweza kukutana na vijana Jijini Mwanza kwa ajili ya kuzungumza
nao kuwahamasisha kutumia vipaji vyao ili kujikwamua kimaisha.
Mayunga akizungumza na BMG
Stella Mutta ambaye ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Star Foundation ya Jijini Mwanza, akizungumza na BMG
Petro Malongo ambaye ni mmoja wa Vijana waliohudhuria Inspiration Event ya hii leo
Mkurugenzi wa Star Foundation akizungumza na Vijana Jijini Mwanza
Mmoja wa viongozi wa Star Foundation akizungumza na Vijana Jijini Mwanza
Baadhi ya Viajana Jijini Mwanza waliohudhuria event hiyo
Mkurugenzi wa Star Foundation
Mayunga (Kushoto) na M-Rap (Kulia)
Vijana katika picha ya pamoja
Picha ya pamoja
GB (L) with Mayunga (R).
Bonyeza HAPA Kusikiliza Mahojiano. Au bonyeza Play hapo chini
Mcheza
sarakasi wa Marekani, Simone Biles anatarajiwa kuiletea medali ya dhahabu nchi
yake kwenye mashindano ya 31 ya Olympic ya Rio, 2016. Mashindano hayo ambayo
yamevuta wanamichezo kutoka kila pembe ya Dunia, yamezinduliwa usiku wa uamkia
leo Agosti 6, 2016 kwenye uwanja wa michezo wa Maracana mjini Rio De Jeneiro
nchini Brazil kwa kurushwa fashifashi angani. Rais wa Mpito wa nchi hiyo, Michel
Temer alitangaza kuanza kwa mashindano hayo ambapo Tanzania nayo inawakilishwa.
Fashifashi (fataki), zikihanikiza anga la uwanja mkubwa kabisa nchini Brazil, Maracana wakati wa uzinduzi huo
Mwanamitindo wa Brazil, Gisele Bundchen
Rais wa Mpito wa nchi hiyo, Michel
Temer
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI) na Mbunge wa Kisarawe
jijini Dar es Salaam, Jaffo Suleiman Said, (katikati), akipokewa na Mkuu
wa Wizalay ya Ikungi mkoani Singida, Miraji Mtaturu, wakati akiwasili
kwenye viwanja vya Maonyesho ya Wakulima Nane Nane, Nzuguni mkoani
Dodoma Agosti 6, 2016. Maonyesho hayo ambayo kitaifa yanafanyika mkoani
Lindi, huwapa fursa wakulima kuonyesha sjughuli zao za kilimo na ufugaji
pamoja na zana za kilimo yatafikia kilele Agosti 8, 2016
Naibu
waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Jafo Suleiman Said akisalimiana na Mkuu
wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne
Mtaturu mara baada ya kuwasili katika uwanja wa maonesho ya nane nane
Nzuguni mjini Dododma
Naibu
waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Jafo
Suleiman Said Jafo akisikiliza kwa makini
maelezo ya kilimo cha mbogamboga yanayofanywa na Jeshi la kujenga Taifa JKT
Naibu
waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Jafo
Suleiman Said Jafo akisikiliza kwa makini
maelezo ya kilimo cha mbogamboga yanayofanywa na Jeshi la kujenga Taifa JKT
Naibu
waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Jafo
Suleiman Said Jafo *watatu kushoto), akizungumza na Luteni AJ
Massawe Meneja wa banda la JKT
Naibu Waziri akipokea
zawadi ya mafuta ya alizeti kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Deogratius Ndejembi
Naibu Waziri katika picha ya pamoja na
na Mkuu wa Wilaya ya ikungi na Kongwa pamoja na watendaji
Mfuko wa LAPF
DAS ILALA, EDWARD MPOGOLO AZINDUA KITABU CHA BAJETI, AKATA KEKI KUNOGESHA MIAKA 16 YA TAASISI YA VIJANA YA TYVA, AWAASA KUANDAA MIPANGO INAYORANDANA NA YA SERIKALI

OfisaTawala wa wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Edward Mpogolo, akiwahutubia Vijana waalikuwa na wanachama wa Taasisi ya Vijana ya TYVA, wakati wa hafla maalum ya maadhimisho ya miaka 16 ya Taasisi hiyo, iliyofanyika leo katika ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam.
Na Bashir Nkoromo
Ofisa Tawala wa Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Edward Mpogolo, pamoja na mambo mengine, Mpogolo amewaasa Vijana wa Taasisi ya Vijana ya TYVA kuhakikisha mipango yao ya kushirikisha Vijana katika shughuli za kimaendeleo, inaendana na mipango ya serikali ili kuwezesha utekelezwaji usiokinzana.
Amesema, iwapo TYVA itapanga kwenye malengo yao mipango inayotofautiana na ile ya serikali kuhusu maendeleo ya vijana na mengineyo, basi utekelezwaji wake unaweza kuwa siyo rahisi kutokana na kukinzana kwa kuwa malengo ya serikali yatakuwa yanaelekeza vingine wakati na wao wamelenga vingine.
Pia aliwataka vijana wa TYVA na wengine kote nchini kuhakikisha wanailinda amani ya Tanzania kwa gharama na nguvu zao zote, akitahadharisha kwamba, amani ni tunu ambayo ikishapotea si rahisi kurejeshwa.
Ameitaka TYVA na Taasisi ngingine za Vijana popote zilipo, kuhakikisha wanakuwa makini dhidi ya watu wasioitakia mema Tanzania, akisema, wapo ndani na nje ya nchi ambao hutamani sana kuona amani ya Tanzania inapotea au inatetereka kwa namna yoyote, na kibaya zaidi kujaribu kujipenyeza kwa makundi ya vijana ili kufanikisha azima zao mbaya.
"Kitu kingine ninacho waasa wakati Taasisi yenu ya TYVA inatimiza miaka 16 sasa, waelimisheni vijana wenzangu, wajihadhari sana, wasije kutekwa na watu waliopo ndani na nje ya Tanzania ili kuwatumia kuharibu amani ya nchi yetu", alisema Mpogolo.
Baadaye Mpogolo alizindua Kitabu cha Mipangokazi au bajeti ya Taasisi hiyo na kukata keki kushiria TYVA kutimiza miaka 16 tangu ilipoanzishwa na kuendelea kwa mafanikio kufanya kazi zake katika nyanja mbalimbali ikiwemo kuhamasisha vijana kushiriki katika shughuli za ujenzi wa taifa.
OfisaTawala Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Edward Mpogolo akizindua mpangokazi au bajeti ya Taasisi ya Vijana ya TYVA, wakati wa maaldhimisho ya miaka 16 ya Taasisi hiyo yaliyofanyika leo katika ukumbi wa British Council Dar es Salaa.. Kushoto ni Mwenyekiti wa TYVA Nuria Mshale
Vijana wakiwa wamenyoosha miko yao wakati Ofisa Tawala wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo (aliyesimama) alipokuwa akiwapiga tafakuri kuhusu umuhimu wa Amani ya Tanzania, alipozungumza nao wakati wa maadhimisho ya miaka 16 ya TYVA yaliyofanyika leo katika ukumbi wa British Council jijini Dar es Salaam.
Mhasibu Mkuu wa TYVA Zuleikha Ibrahim, akiwasilisha keki meza kuu kwa ajili ya mgeni rasmi, Osisa Tawala wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo (kulia) kuikata, kunogesha maadhimisho ya miaka 16 ya TYVA yaliyofanyika leo katika ukumbi wa British Council, Dar es Salaam.
Ofisa Tawala wa wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akikata keki kunogesha maadhimisho ya miaka 16 ya Taasisi ya Vijana ya TYVA, yaliyofanyika katika ukumbi wa British Council, Dar es Salaam, leo. Kulia ni Ofisa Vijana mkoa wa Dar es Salaam, Masalida Sephania Njashi na kushoto ni Mhasibu Mkuu TYVA Zukeikha Ibrahim, na wapili ni Mwenyekiti wa TYVA Nuria Mshare
Keki baada ya kukatwa
Mwenyekiti wa TYVA Nuria Mshare akimlisha keki Ofisa Tawala wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo wakati wa hafla hiyo
Mwenyekiti wa TYVA Nuria Mshare akimlisha keki Ofisa Vijana Dar es Salaam, Masalida Njashi wakati wa hafla hiyo
Mpogolo akimlisha keki Mwenyekiti wa TYVA wakati wa hafla hiyo.
Mpogolo akimlisha keki Mkuu wa Idara ya Ushawishi na Utetezi ya TYVA, Makwita Abdul wakati wa hafla hiyo
Mpogolo akimlisha keki Mhasibu Mkuu TYVA Zukeikha Ibrahim wakati wa hafla hiyo
Ofisa Tawala wa wilaya ya Ilala Edward Mpogolo akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa juu wa Taasisi ya Vijana ya TYVA mwishoni mwa hafla ya TYVA kutimiza miaka 16 tangu kuanzishwa kwake
Geline Fuko (kushoto) akipokea maua kutoka kwa wafanyakazi wenzake wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC),ikiwa ni ishara ya kumpongeza baada ya kutua Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam jana, akitokea
Marekani alikokuwa akihudhuria mafunzo ya vijana wa kiafrika
yaliyoandaliwa na
Raisi Obama.
Na Dotto Mwaibale
SHANGWE ilitawala wakati mtanzania
Geline Fuko alipo wasili Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere
(JNIA) majira ya saa nne usiku jana Agosti 5, 2016 akitokea nchini
Marekani alikohudhuria mafunzo ya viongozi vijana kutoka Bara la
Afrika.
Wafanyakaziwa Kituo cha Sheria na Haki
za Binadamu ambao ni wafanyakazi wenzake wa Geline, familia ya Geline,
ndugu na marafiki walitoa mapokezi ya kishujaa wa wanaharakati huyo
aliyetajwa kuwa mfano wa kuigwa na Rais Obama.
Akizungumza na wanahabari, Geline
alisema amefarijika na hakutarajia kama wazo lake la kuanzishwa kwa
Kanzidata ya Katiba litakuwa wazo kubwa ambalolitakubalika mpaka na
Rais Obama.
Hata hivyo Geline alisema amefurahishwa
na program hiyo ya Mandela Washington Fellowship kwani imewawezesha
washiri kikujifunza mambo mengi na kupata uono mpana zaidi wakufanya
mambo.
Geline iliwahimiza watanzania kutembelea
Kanzidata hiyo iliyopo mtandaoni (http://katiba.humanrights.or.tz/) ili
kuweza kuijua katiba yao na kuweza kujua haki zao kama watanzania.
Mwisho alishukuru wa mapokezi makubwa ambayo pia hakuyatarajia.
Akitoa neno la shukurani kwa Geline kwa
niaba ya LHRC, Mkurugenzi wa Fedha naUtawala-LHRC, Ezekiel Masanja
amempongeza Geline kwa kuitoa kimasomaso LHRC na Tanzania kwa ujumla.
Geline Fuko amepata kutambulika baada ya
Rais Obama kumtaja kama mfano wa kuigwa wa wanaharakati wa haki za
binadamu wakati akizungumza Jumatano Agosti 3, 2016 katika kilele cha
mpango wake wa kuwawezesha vijana wakiafrika unaojulikana kama Mandela
Washington Fellowship.
Raisi Obama alimsifu mwanasheria huyo
kutoka LHRC ambaye ni moja ya vijana 1000 waliokuwa jijini Washington
kwa lengo la kujengewa uwezo ili kuweza kusaidia Maendeleo katika Nyanja
zote za maisha katika nchi zao.
RaisiObamaalisifujuhudizaGelinezakuibuawazo
la kuanzishakwamaraya kwanza Kanzidata ya Katiba nchini Tanzania kwa
kutekeleza wazo hilo chiniya LHRC.
Raisi Obama alikaririwa akisema Marekani itaendelea kushikamana na wanaharakati kama Geline Fuko kutoka Tanzania.
GelinenimwanasherianamwanaharakatiwahakizabinadamuambayeamefanikishakuanzishwakwaKanzidatayaKatibaya
kwanza nayapekeenchini Tanzania inayowawezesha watanzania kusoma Katiba
kupitia simu zao za mkononi”.
Programu ya Mandela Washington
Fellowship yenye lengo la kuwa wezesha vijana wa Kiafrika katika Nyanja
za kiuchumi, kisiasa, kiteknolojia na kijamii ilianzishwa na Rais Obama
mwaka 2014.
Programu hii hujumuisha vijana elfu moja
(1000) kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambao hugharamiwa na serikali
ya Marekani kwenda jijini Washington kwa lengo la kujengewa uwezo zaidi.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kilianzisha Kanzidata ya Katiba mwaka mmoja uliopita mnamo Julai 15, 2015.
Kupitia tovuti maalumu
(http://katiba.humanrights.or.tz/) na simu za mkononi, watanzania
wanaweza kusoma Katiba katika Kanzidata hiyo.
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
Mwenyekiti
wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya ya ikungi ambaye ni Mkuu wa Wilaya Miraji
Jumanne Mtaturu akikagua vijana wa mafunzo ya Mgambo kutoka vijiji vitano vya
Dung’unyi, Munkinya, Kipumbuiko, Samaka na Damankiya vinavyounda Kata ya Dung’unyi
katika Tarafa ya Ikungi
Kundi
la vijana wa Mgambo kutoka Kijiji cha Ighombwe, Jerumani, na Mahonda wakionyesha
umahiri wao katika mafunzo waliyoyapata mbele ya mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa
mafunzo hayo katika Tarafa ya Sepuka
Mwenyekiti
wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya ya ikungi ambaye ni Mkuu wa Wilaya Miraji
Jumanne Mtaturu akiwa kwenye picha
ya pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Ikungi
Kundi
la vijana wa Mgambo kutoka Kijiji cha Ighombwe, Jerumani, na Mahonda
wakimsikiliza mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo katika Tarafa ya
Sepuka
Mwenyekiti
wa kamati ya ulinzi na usalama wa Wilaya ya ikungi ambaye ni Mkuu wa Wilaya Miraji
Jumanne Mtaturu akijadili jambo na
Mshauri wa Mgambo Wilaya ya Ikungi Fortunatus Ndalama
Mkuu
wa Wilaya Miraji Jumanne Mtaturua akizungumza
na watendaji Kata, na viongozi wa vijiji mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya
mgambo yatakayodumu kwa wiki 16
Kutoka
kushoto ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Udalai ya Yono Auction Mart na Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni hiyo Bibi. Scholastica Kevela wakiwa wameshika Tuzo na
Cheti walivyopewa kutokana na kutoa huduma kwa viwango na ufanisi.Tuzo hiyo
inajulikana kwa jina la The Diamond Eye Award for Quality Commitment and
Excellence) imetolewa tarehe 25, Julai 2016 Jijini Rome Italia na Rais wa Asasi
ya Otherways Management & Consulting ya Paris Ufaransa.
Mwenyekiti wa Yono Auction Mart & Co Ltd Bw.
Stanley Kivela akielezea jambo kuhusu Tuzo ya Almas ya Ubora, Uwajibikaji na
Ufanisi (The Diamond Eye Award for Quality Commitment and Excellence) iliyotolewa
na Rais wa Asasi ya Otherways Management & Consulting ya Paris Ufaransa
ambapo takribani nchi 49 dunia zilishiriki mchakato huo huku Tanzania
ikiwakilishwa na taasisi mbili ambazo ni Mamlaka ya Angaa (TCAA) kwa upande wa
Serikali na Yono Auction Mart kwa upande
wa Sekta binafsi
Mkurugenzi
Mtendaji wa Yono Auction Mart Bibi. Scholastica Kevela akiwa ameshika Tuzo
waliyopewa kutokana na kutoa huduma kwa viwango na ufanisi.Tuzo hiyo
inajulikana kwa jina la The Diamond Eye Award for Quality Commitment and
Excellence imetolewa tarehe 25, Julai 2016 Jijini Rome Italia na Rais wa Asasi
ya Otherways Management & Consulting ya Paris Ufaransa.
![]() |
Na Frank Shija, MAELEZO.
|
Serikali
ya awamu ya Tano chini ya Rais Magufuli imeendelea kuungwa mkono na wadau mbalimbali kutokana na
jitihada zake za kurejesha heshima na uadilifu miongoni mwa jamii ya
Watanzania.
Haya
yamebainishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co Ltd Bw. Stanley J.
Kevela aliokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Tuzo iliyopata leo
Jijini Dar es Salaam.
Kevela
ameseme kuwa wao binafsi kama kampuni inayoaminiwa na Serikali na taasisi zake wanayosababu
ya kuunga jitihada zinazoonyeshwa na Serikali katika kupigania maendeleo ya
watu wake kwa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu, ubunifu na ufanisi unaostahili.
“Tunatoa
Tuzo hii muhimu kwetu kwa Mhe. Dkt. Magufuli kama ishara ya kuheshimu mchango
wake katika kuliletea taifa letu maendeleo
na kuhakikisha mambo yanafanywa kwa ufanisi na viwango vyenye ubora wa hali ya juu”. Alisema
Kavela.
Amesema
kuwa tokea Rais Magufuli aingie madarakani mambo mengi yamekuwa yakienda vizuri
hivyo ikiwemo suala la ukusanyaji wa Kodi kazi ambayo wamekuwa wakiisaidia
Serikali kwa muda mrefu sasa.
Aliongeza
kuwa Kampuni yake imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha inatoa huduma
zenye viwango tena kwa uadilifu na uwajibikaji usiotiliwa shaka ndiyo maana
wanamuunga mkono Mhe. Rais kwakuwa naye ni muunini wa falsafa ya uwajibikaji,
uadilifu na ubunifu.
Aidha
Mwenyekiti huyo amesema kuwa katika kuendeleza jitahada za Serikali katika
kukuza ajira wameajiri zaidi ya vijana 200 ambao wako mtaani wakifanya kazi ya
ukusanyaji wa Kodi kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Yono Auction Marts &Co Ltd Bibi.
Scholastica Kevela ametoa rai kwa wadau mbalimbali kuendelea kuiamini Kampuni
hiyo kwa kupata huduma zao zikiwemo wakala wa Udalali wa Mahakama na Ukusanyaji
wa Mapato ya Serikali kwa niaba ya TRA.
Yono
Auction Mart imekuwa ikifanya kazi na Serikali katika Nyanja mbalimba ikiwemo
ukusanyaji wa Kodi kwa niaba ya TRA, udalali wa Mahakama, Uuzaji wa viwanja vya
Serikali na mambio mengine yanayohusu ukusanyaji wa Kodi za Serikali.
Kampuni
ya Yono Auction Marts &Co Ltd ilipata fursa ya kushiriki katika hafla ya
ugawaji wa Tuzo za Diamondo Eye kutokana na Ubora, Uwajibikaji na Ufanisi (The Diamond Eye Award for Quality
Commitment and Excellence) iliyotolewa tarehe 25 Julai 2016 Jijini Rome,
Italy iliyotolewa na Rais wa Asasi ya Otherways Management & Consulting ya
Paris Ufaransa ambapo takribani nchi 49 dunia zilishiriki mchakato huo huku
Tanzania ikiwakilishwa na taasisi mbili ambazo ni Mamlaka ya Angaa (TCAA) kwa
upande wa Serikali na Yono Auction Mart
kwa upande wa Sekta binafsi.
OFISI za Bodi ya Mikopo zilizopo Mwenge,
jijini Dar es Salaam zitakuwa wazi kwa siku mbili, Jumamosi, Agosti 6, 2016
na Jumapili, Agosti 7, 2016 kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri
ili kutoa fursa muhimu kwa wadaiwa wote wa mikopo ya elimu ya juu ambao
hawajaanza kurejesha mikopo kupata taarifa kuhusu madeni yao.
Bodi ya Mikopo imeshaanza kuwachukulia
hatua wadaiwa wa mikopo ya elimu ya juu kwa kutangaza majina yao katika vyombo
vya habari. Hatua zingine zitakazochukuliwa ni pamoja na:
i.
Kufikishwa mahakamani;
ii.
Kutozwa faini;
iii.
Kunyimwa fursa za kupata mikopo;
iv.
Kunyimwa fursa za masomo nje ya nchi; na
v.
Kuzuiwa kusafiri nje ya nchi.
Nyote
mnakaribishwa ili kutumia fursa hii muhimu.
Imetolewa
na:
Bw.
Jerry Sabi,
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji,
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya
Juu,
S.L.P. 76068,
DAR ES SALAAM
Baruapepe: info@heslb.go.tz
‘Kuwa Mzalendo, Rejesha Mkopo wa Elimu ya Juu’
Kutoka
Kushoto ni Eng Sadick Chakka Mhandisi
wa Maji Wilaya ya Ikungi, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji jumanne Mtaturu,
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Wilaya ya Ikungi Rustika Turuka,
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ally J. Mwanga, na Kulia
ni Abel Suri Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi
Jeshi
la polisi Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida limemtia nguvuni Diwani wa Kata ya Iseke
kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Emmanuely Njingu kwa
kosa la kukwamisha shughuli za serikali kwa kuzuia watendaji wa serikali
kufanya kazi yao ikiwemo ukusanyaji wa mapato.
Njingu
ambaye alikuwa mjumbe wa kamati ya fedha awali kabla ya kuwekwa nguvuni na
jeshi la polisi alivuliwa ujumbe wa kamati hiyo kutokana na kukiuka taratibu na
makubaliano ya baraza la madiwani jambo ambalo limepelekea kuhamishiwa
katikakamati nyingine.
Akitoa
taarifa ya kukamatwa kwa diwani huyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya
Ikungi ambaye ni Diwani wa Kata ya Irisia Ally Juma Mwanga amesema kuwa Diwani
huyo amekamatwa kwa mujibu wa sheria hivyo yeye kama mwenyekiti hawezi
kuingilia taratibu, sheria,na kanuni za serikali.
Mwanga
amesema kuwa tarehe 19 mwezi Julai moja ya maadhimio ya kamati ya fedha na
vikao vya baraza ilikuwa ni kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri
lakini diwani huyo amekiuka makubaliano hayo kwa kung’oa mageti ya vizuizi vya
barabarani kwa ajili ya ukaguzi wa mazao jambo ambalo limepelekea kuzorota kwa ukusanyaji
wa mapato ya Halmashauri.
Ameongeza
kuwa Mjumbe yeyote anayekiuka maazimio wanayokubaliana na kutoa siri za kamati
adhabu yake kisheriani kupoteza sifa ya kuwa mjumbe wa kamati husika.
Amesema
diwani huyo ameondoshwa katika nafasi hiyo baada ya maridhiano ya kamati hiyo
na kukubaliana kumuhamishia katika kamati nyingine ya huduma za uchumi.
“Jambo
mkishakubaliana kisheria tena kwenye vikao vya kisheria maana yake linakuwa ni
sheria hivyo kwa kiongozi yeyote akikiuka taratibu za kisheria zinachukua
mkondo wake, kanuni za Halmashauri ni za watu wote hazichagui upande mmoja” Alisema
Mwanga
Hapo
jana Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu alihutubia Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya
hiyo ikiwa ni mara yake ya mwanzo kabisa tangu alipochaguliwa na Rais John
Magufuli kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo ambapo pamoja na kuzungumzia kuwepo kwa
changemoto ya uhaba wa maabara, afya duni na miundombinu pia alizungumzia
kuhusu ukusanyaji hafifu wa mapato jambo ambalo linairudisha nyuma Halmashauri
ya Wilaya hiyo.
Bajeti
ya Wilaya ya Ikungi kwa Mwaka 2013/2014 ilikuwa na Shilingi 509,701,044
namakusanyoyakeyakawa ni 338,325,000 ambapo hata hivyo mwaka ulimalizika kwa
kuwa na upungufuwa shilingi 171,376,044.
Mwaka
2014/2015 ilipangwa bajeti ya shilingi 631,455,000 lakini makusanyo yake yakawa
ni shilingi 457,555,172 ambapo mwaka ulimalizika kwa kukusanya 173,899,828.
Mwaka
wa bajeti 2015/2016 bajeti ya Halmashauri iliyopangwa ilikuwa ni shilingi 1,127,030,000
makusanyo yalikuwa ni 679,283,000 ambapo hata hivyo mwaka ulimalizika kwa kwa
kuwa na upungufu wa shilingi 450,747,000 hivyo kwa miaka mitatu Halmashauri
hiyo imeshindwa kufikia malengo ya ukusanyaji.
Mwanga
amesema kuwa Kutofikiwa malengo hayo kumesababishwa na kutopewa ushirikiano
watendaji katika ukusanyaji wa mapato hii ikiwa ni kufuatia kauli za mazuio
zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa.
Hata
hivyo ametoa Mwito kwa viongozi wa serikali, wanasiasa, taasisi za dini na
wananchi kushirikiana kwa pamoja ili kufikia malengo ya kuifanya Ikungi kukua
kiuchumi .


















































No comments :
Post a Comment