Thursday, August 25, 2016

MFUKO WA PSPF WATOA ELIMU YA KUJIUNGA KATIKA MFUKO WA KUJICHANGIA KWA HIARI

ps
 Afisa wa Mfuko wa PSPF Tawi la Zanzibar Bi Fadhila akizungumza wakati wa Mkutano Taasisi zisizo rasmin za Wavuvi, Madereva wa gari za mchanga, Kifusi na Wakulima wa mbogamboga kujiunga na Mpango wa Uchangiaji wa Hiari ya Mfuko wa PSPF uliofanyika katika ukumbi wa Betilyamin Malindi Zanzibar.
Washiriki wa Mkutano huo wakiwa katika Ukumbi wa Mkutano wakimsikiliza Afisa wa Mfuko wa PSPF akitowa maelezo kuhusiana na Mfuko huo. 

Afisa wa Idara ya Uvuvi na Maendeleo Zanzibar Ndg Mohammed Chum akitowa maelezo wakati wa mkutano huo na Mfuko wa PSPF kwa Wavuvi wa Zanzibar kujiunga na Mfuko huo.


Waziri wa Kilimo Maliasili Uvuvi na Mifugo Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed akifungua mkutano wa Wavuvi na Wananchi wasio kuwa katika Sekta Rasmin kujiunga na Mfuko wa PSPF katika Mafao ya Hiari ili kupata huduma muhimu za maendeleo kupitia mfuko huo. 

Waziri wa Uvuvi Mhe Hamad Rashid Mohammed akisisitiza jambo wakati wa kufungua Mkutano wa Wadau Wasiokuwa katika Sekta Rasmin kujiunga na Mfuko wa PSPF kupitia Michango ya Hiara ili kupata fursa mbalimbali zinazotolewa na PSPF kwa Wanchi wa Tanzania.

Afisa wa PSPF Zanzibar Bi Faidha Katavi akitowa maelezo kwa Waziri wa Uvuvi kujiunga na Mfuko huo baada ya kufungua mkutano huo wa kuwahamashisha Wananchi wasio kuwa katika Sekta rasmin kujiunga na Mfuko wa Kujichangia kwa Hiara Mafao yao na kupata fursa zinazotolewa na PSPF kwa Watanzania.  
 Mhe Hamad Rashid akijaza fomu ya Kuchangia kwa Hiari Mfuko wa PSPF baada ya kuufungua Mkutano huo na Wavuvi.
Afisa wa PSPF Bi. Faidha Katavi akitowa maelezo jinsi ya kujiunga na Mfuko wa PSPF Kujichangia kwa Hiara Mafao katika mfuko huo.

Afisa PSPF Ndg. Hadji Jamadari akitowa maelezo jinsi ya kujiunga na Mfuko wa PSPF kwa mafao ya kujichangia kwa hiari kupitia mfuko huo kwa Wananchi wasio katika Sekta rasmin jinsi wanavyoweza kunufaika kupitia kuchangia mafao kwa hiari.
Afisa wa PSPF Ndg Hadji Jamadari akitowa maelekezo kwa Wananchi wanaojiunga katika Mfuko wa PSPF kupitia Michango ya Hiari wakati wa mkutano huo kutowa Elimu ya Mfuko kwa Wananchi wa Zanzibar wasio kuwa katika Sekta Rasmin. 
Afisa wa PSPF Ndg. Hadji Jamadari akitowa maelezo ya moja ya fomu ya kujiunga na Mfuko wa PSPF kupitia Michango ya Hiara kwa Wananchi wasiokuwa katika Sekta rasmin, mkutano huo umewashirikisha Wavuvi, Wachimba Mchanga, Magari ya Mizigo ya Mchanga na Kifunzi na Umoja wa Jumuiya wakulima wa mbogamboga Zanzibar. 

MADIWANI KUTOKA UGANDA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO JIJINI DAR ES SALAAM

mea1
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Isaya Mwita Charles akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano baina ya Wataalamu kutoka Jijini la Dar es Salaam na Madiwani kutoka baadhi ya Halmashauri za Uganda Magharibi na Kaskazini wakati wa ziara yao ya kujifunza masuala mbalimbali leo Jijini Dar es Salaam.Kutoka kulia ni Mratibu wa Taifa wa Mtandao wa Majiji Tanzania (TACINE) Bw. Philotheusy Mbogoro, Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jiji la Dar es Salaam, Phillip Mwakyusa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Koboko, na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mamlaka ya Miji nchini Uganda (UAAU) Mhe. Sanya Wilson.
mea2
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jiji la Dar es Salaam, Phillip Mwakyusa akielezea jambo wakati wa ufunguzi wa mkutano baina ya Wataalamu kutoka Jijini hilo na baadhi ya Madiwani kutkoka Halmashauri za Miji nchini Uganda wakati wa ziara yao ya kujifunza masuala mbalimbali leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Koboko, na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mamlaka ya Miji nchini Uganda (UAAU) Mhe. Sanya Wilson na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Isaya Mwita Charles
mea3
Afisa Uhusiano na Itifaki wa Jiji la Dar es Salaam Gaston Mwakwembe akielezea jambo wakati wa mkutano uliowakutanisha baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Jiji na baadhi ya Madiwani kutoka nchini Uganda leo Jijini Dar es Salaam. Madiwani hao wapo katika ziara ya kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo Menejimenti ya Usafiri, Uchafu, Maji, Rasilimali watu, Fedha na namna ya kuongoza mabaraza ya Madiwani.
mea4
Mhandisi wa Barabara wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Swalehe Nyenye akiwasilisha maada kuhusu mkakati wa kuboresha usafiri katika Jiji la Dar es Salaam leo wakati wa ziara ya baadhi ya Madiwani kutoka Uganda walipo nchini kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo Menejimenti ya Usafiri, Uchafu, Maji, Rasilimali watu, Fedha,Kilimo cha mjini,na namna ya kuongoza mabaraza ya Madiwani.
mea5
Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Godhelp Ringo akifafanua maada kuhusu muundo wa Jiji la Dar es Salaam wakati wa ziara ya baadhi ya Madiwani kutoka Uganda waliopo nchini kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo Menejimenti ya Usafiri, Uchafu, Maji, Rasilimali watu, Fedha,Kilimo cha mjini,na namna ya kuongoza mabaraza ya Madiwani.

MANCHESTER CITY YAMPATA KIPA WA KUCHUKUA MIKOBA YA JOE HART

JESHI LA POLISI ZANZIBAR KUPAMBANA NA WANAOTUMIA KAZI ZA WASANII BILA YA LESENI YA HAKIMILIKI

Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdani Omar Makame akizungumza na wandishi wa habari kuhusu wajibu wa Jeshi la Polisi katika usimamizi wa kazi za wasanii, hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya Polisi Kilimani Zanzibar.(Picha na Mkame Mshenga/Maelezo Zanzibar.)
Jeshi la Polisi Zanzibar limedhamiria kupambana na uharamia wa kazi za hakimiliki kwa kudhibiti maeneo ya uingizaji hakimiliki haramu katika maeneo ya bandarini na uwanja wa ndege .

No comments :

Post a Comment