Monday, August 1, 2016

ESRF YAWAKUTANISHA WADAU MBALIMBALI KUICHAMBUA BAJETI YA SERIKALI KATIKA SEKTA YA AFYA NA VIWANDA

TAASISI ya Utafiti ya Uchumi na Jamii (ESRF) imewakutanisha wasomi na wawakilishi wa taasisi za umma na kibinafsi kuchambua bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/2017 katika Sekta ya Afya na Viwanda ili kuona inavyoweza kutatua changamoto zinazokabili Sekta hizo kwenye mdahalo uliokutanisha wasomi, wawakilishi wa Taasisi za Umma na Binafsi na kufanyika makao makuu ya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Akifungua mdahalo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dkt.Tausi Kida alisema, Taasisi yake imeona ni vema kuwakutanisha wadau kujadili bajeti hiyo katika sekta ya Afya na Viwanda, kwa vile zinagusa uchumi wa wananchi.
Akiwasilisha mada juu ya bajeti ya Serikali 2016/2017na changamoto zinazoikabili sekta ya Afya, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki Cha Afya na Sayansi Shirikishi, Cha Muhimbili, (MUHAS), Profesa Phares Mujinja alisema, ingawa bajeti iliyotengwa kwenye sekta ya Afya ni kubwa, lakini bado kuna changamoto kadhaa kwa vile Wizara hiyo imepanuka kutokana na kuhudumia maeneo mengi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii, (ESRF), Dkt.Tausi Kida, akitoa hotuba ya ufunguzi wa mdahalo uliolenga kujadili changamoto zinazoikabili bajeti ya mwaka 2016/2017 kwenye sekta ya Afya na Viwanda, kwenye makao makuu ya ESRF jijini Dar es Salaam. Mdahalo huo umewakutanisha wasomi, wawakilishi wa Taasisi za Umma na Binafsi. (Picha zote na K-VIS MEDIA/Khalfan Said).
 
Profesa Mujinja alitolea mfano wa ununuzi wa madawa ambapo, zaidi ya asilimia 90 ya madawa yanayotumika huagizwa kutoka nje na hivyo fedha nyingi za kigeni hutumika.
Katika majumuisho yake, Profesa Mujinja alisema, ni vema Serikali ielekeze nguvu zake kwenye uanzishwaji wa viwanda vya kuzalisha madawa na vifaa tiba hapa nchini ili kwenda sambamba na malengo ya taifa ya maendeleo endelevu.
Akizungumzia kuhusu changamoto za bajeti kwenye eneo la Viwanda, muwasilisha mada Profesa Prosper H. Ngowi kutoka Chuo Kikuu Cha Mzumbe kampasi ya Dar es Salaam, alisema, fedha zilizotengwa kwenye Sekta ya Viwanda ni Shilingi Bilioni 81, 871,992,000, ambapo asilimia 51 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na asilimia 49 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Kwa mtazamo wake, Profesa Ngowi alisema, mgawanyo huo ni mzuri na sio kwa kiwango kikubwa kwani hakuna tofauti na bajeti ya mwaka 2015/2016, na kuonyesha wasiwasi wake muda ambao Serikali inatoa fedha hizo kuhudumia maeneo yaliyokusudiwa.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki Cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), Cha Muhimbili, Profesa Phares Mujinja, akitoa mada juu ya changamoto zinazoikabili bajeti ya Serikali ya 2016/2017 kwenye Sekta ya Afya wakati wa mdahalo huo.
 
“Bajeti ya 2016/2017 ni Asilimia 70.3% ya ile ya 2015/2016 na kwamba wizara hivi sasa ni kubwa kutokana na kuongezeka kwa sekta ya Uwekezaji.” Alifafanua.
Wakichangia mada hizo, wengi wa washiriki wameonyesha wasiwasi wao kuhusu kufanikiwa kwa malengo ya serikali kwenye Sekta hizo kutokana na muonekano wa bajeti yenyewe na mahitaji halisi ya sasa ya utoaji huduma kwenye Sekta hizo ili kufikia malengo ya kukuza uchumi wa nchi kumekuwepo kwa mtazamo kuwa biashara nchini zinaanguka kutokana na mkazo wa kukusanya mapato.
Akifunga mdahalo huo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Utawala na Ujenzi wa Maendeleo wa ESRF, Doris Likwelile, aliwashukuru washiriki kwa michango yao mbalimbali na kwamba mawazo yao yatawezesha utayarishaji wa mtazamo wa wadau kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/2017 kwenye Sekta hizo mbili za Afya na Viwanda.

WAZIRI MKUU: WAKURUGENZI WATAKAOTOA TAARIFA ZA UONGO KUONDOLEWA

JIL 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitasita kuwaondoa katika nyadhifa zao Wakurugenzi wote watakaoshiriki katika kutoa taarifa za uongo kuhusu miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao.
“Serikali inatoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ambapo  kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakiandika taarifa za uongo kuwa mradi umekamilika wakati haujajengwa, hivyo wakurugenzi watakaoshiriki kutoa taarifa zisizokuwa sahihi wataondolewa,” alisema.
Waziri Mkuu ameyasema hayo jana jioni (Jumapili, Julai 31, 2016) wakati akipokea taarifa ya mkoa wa Morogoro mara baada ya kuwasili mkoani hapa kwa ziara ya kikazi ya siku tatu.
Alisema alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wakurugenzi katika halmashauri zote nchini kuhakikisha wanatembelea miradi yote inayojengwa katika maeneo yao ili kufanya ukaguzi na kujiridhisha kama thamani yake inalingana na kiasi cha fedha kilichotolewa.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amesema Serikali aihitaji Halmashauri kutoa ajira za mikataba kwenye kada zilizopo katika muundo wa ajira hivyo ameziagiza halmashauri zote nchini kufanya mapitio ya watumishi wa mikataba.
“Tumeruhusu kuajiri kwa mikataba walimu wa masomo ya sayansi kwa kipindi cha miaka miwili tena kwa waliostaafu. Kuna kada zilizoko katika muundo wa ajira hizo hatuhitaji watumishi wa mikataba wakiwemo madereva msiwatumikishe kwa mikataba watakosa stahili zao,” alisema.
Akizungumzia suala la watumishi hewa mkoani Morogoro Waziri Mkuu alisema ni vema wakaendelea kufanya uchunguzi na ifikapo mwisho wa mwezi huu wawe wamekamilisha taarifa na kuanza kuchukua hatua kwa waliohusika kwa waliohusika.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk. Stephen Kebwe katika taarifa yake aliyoiwasilisha kwa Waziri Mkuu alisema mkoa unaendelea kutekeleza agizo la Rais Dk. John Magufuli la kuzitaka taasisi zote za Serikali kufanya uhakiki wa mishahara hewa na malipo batili ya watumishi.
Alisema mkoa umebaini watumishi hewa 315 ambao wameisababishia Serikali hasara ya sh. bilioni 2.132 ambapo timu ya uhakiki bado inaendelea na zoezi hilo na taarifa kamili itatolewa mara kazi hiyo itakapo kamilika.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 01, 2016.

RAIS DKT. MAGUFULI ALIPOHUTUBIA MKUTANO GEITA MJINI

1 2 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Geita mjini mara baada ya kuwasili kutoka Kahama.
3 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka katika viwanja vya mikutano vya Geita mjini mara baada ya kuhutubia.
4 
Wananchi wa Geita wakionesha furaha yao wakati Rais Dkt. Magufuli alipokuwa akihutubia mkutano viwanjani hapo.
PICHA NA IKULU

TAASISI ZATAKIWA KUANZISHA MFUMO WA KUPIMANA

2 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Lt. Mstaafu Chiku Galawa (Kulia) wakati alipotembelea ofisini kwake kupata taarifa ya hali ya miundombinu katika mkoa huo.
4 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Meneja wa wakala wa barabara nchini (Tanroads) mkoa wa Mbeya Eng. Paul Lyakurwa wakati alipokagua barabara ya Ikana-Makamba –Chitete iliyopo mkoa wa Songwe.
5 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akikagua kituo cha kukuza mawimbi ampilification station kilichopo miangalau mkoani Rukwa. Kulia kwake ni Meneja wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Mkoa wa Katavi na Rukwa Bw. Peter Kaguru.
6 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Zelothe Stephen akitoa taarifa ya hali ya Miundombinu katika mkoa huo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipomtembelea ofisini kwake.

MKUTANO WA LOWASSA NA WANAFUNZI MUHIMBILI WAZUILIWA

Na Dotto Mwaibale
……………………..
UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Shirikishi Muhimbili (MUHAS) umezuia mkutano uliokuwa ufanywe na baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowaasa.
Mkutano huo ambao ulikuwa ufanyike na baadhi ya vijana wa kikristo ambao ni wanafunzi wa chuo hicho ulikuwa pangwa kufanyika juzi chuoni hapo kuanzia saa za mchana.
Akizungumza mtandao wa www. habari za jamii.com  mmoja wa wanafunzi hao ambaye hakupenda kutaja jina lake alisema maandalizi yote ya mkutano huo ambao ulikuwa baada ya ibada yalikuwa yamekamilika.
“Tulifanya taratibu zote ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo ambao ulitukubalia na kumualika ndugu Lowassa lakini tumeshangazwa na zuio lililotolewa na uongozi wa chuo” alisema mwanafunzi huyo.
Mwanafunzi huyo alisema kuwa saa sita mchana wakati wakimsubiri mgeni rasmi Edward Lowassa awasili mkuu wa chuo hicho na viongozi wengine waliwaita na kuwaeleza kwamba mkutano huo umewekewa zuio kutoka juu hivyo hautafanyika bila ya kutoa sababu .
Msemaji wa Lowassa Abubakar Lihongo alisema wanafunzi hao baada ya kuzuiliwa kufanya mkutano huo walimuomba radhi Lowassa na kumueleza watamualika tena kipindi kingine wakiwa tayari.
“Mimi naona zuio hilo linatokana na masuala ya kisiasa lakini kuna barua ya wanafunzi hao ipo katika mitandao ya kijamii mkiipata mnaweza kupata picha halisi” alisema Liongo.
 

No comments :

Post a Comment