Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akikagua gwaride kabla ya kutunuku Kamisheni kwa Maafisa Wapya
586 wa jeshi la Wananchi wa Tanzania kundi la 58/15 katika chuo cha
kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akikagua gwaride kabla ya kutunuku Kamisheni kwa Maafisa Wapya
586 wa jeshi la Wananchi wa Tanzania kundi la 58/15 katika chuo cha
kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akitunuku kamisheni kwa maafisa wapya 586 wa jeshi la Wananchi
wa Tanzania kundi la 58/15 katika chuo cha Mafunzo ya kijeshi cha
Monduli TMA mkoani Arusha
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akimpongeza Afisa Mpya wa cheo cha Luteni Usu, Nasra Rashid
ambaye alifanya vizuri zaidi kuliko Maafisa Wanafunzi wanawake katika
chuo cha kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya wananchi General
Davis Mwamunyange mara baada ya kuwasili kwenye chuo cha Mafunzo Kijeshi
cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Maafisa
Wanafunzi wakipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli kabla
ya kutuniwa Kamisheni
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha
Monduli TMA Meja Jenerali Paul Peter Massao kabla ya kutunuku Kamisheni
kwa Maafisa Wapya 586 katika chuo hicho cha Monduli.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wapya
aliowatunuku Kamisheni katika cha Mafunzo Kijeshi cha Monduli TMA mkoani
Arusha. Wengine katika picha ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya wananchi
Jeneral Davis Mwamunyange , Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha
Monduli TMA Meja Jenerali Paul Peter Massao, Waziri wa Ulinzi Dkt.
Hussein Mwinyi pamoja na Maafisa wa ngazi za juu katika Jeshi la Ulinzi.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akiwasalimia wananchi wa Ngarenaro waliomsimamisha wakati
akitokea kwenye chuo cha Mafunzo ya Kijenshi cha Monduli mkoani Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akitembea kikakamavu mara baada ya kutoka kukagua gwaride
katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha Monduli TMA mkoani Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akisisitiza jambo wakati akizungumza na wanaanchi wa kona ya
Mbauda mkoani Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akifurahia jambo na Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis
Mwamunyange katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha Monduli mara baada ya
kutazama picha za Majenerali wastaafu waliongoza Jeshi la Wananchi
katika miaka ya nyuma.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri
Jeshi mkuu Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mkuu wa majeshi
ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi
cha Monduli mara baada ya kutazama picha za Majenerali wastaafu
waliongoza Jeshi la Wananchi katika miaka ya nyuma.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dkt. John Pombe
Magufuli akizungumza na wakazi wa Kona ya Nairobi eneo la Arusha Tech
mara baada ya kutoka kutunuku Kamisheni kwa maafisa Wapya katika Chuo
cha Mafunzo ya Kijeshi cha Monduli mkoani Arusha. PICHA NA IKULU
…………………………………………………………………………………………………..
Na Mahmoud Ahmad,Monduli
Amiri jeshi mkuu na Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli amewatunuku
Kamisheni wahitimu wapatoa 586 kutoka Chuo cha Kijeshi TMA kilichopo
Monduli Mkoani Arusha.
Raisi dkta jpm ambaye hii ni
mara ya pili kuwatunuku maofisa hao wakijeshi katika chuo hicho cha
kijeshi aliweza kuwapa zawadi mbalimbali kwa wale waliofanya vizuri
katika mafunzo yao.
Aidha Raisi Magufuli
alifurahiswa na kitendo cha Askari wanawake wapatao 6 miongoni mwa
wahitimu 586 waliopata fursa ya kutunukiwa vyeo na kuibua shangwe na
nderemo kwa wageni waliohudhuria Kamisheni hiyo
“Leo nimewatunuku vyeo vya kuwa
watumishi katika Jeshi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nafasi
hiyo naomba Mungu awasaidie’’alisema Raisi wakati akiwatunuku
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo
hicho cha kijeshi TMA Meja Jenerali Paul Masau akitoa taarifa fupi juu
ya mafunzo ya wahitimu hao mbele ya Rais Magufuli kuwa wahitimu wote
waliohitimu mafunzo hayo ni Raia wa Tanzania.
Aliongeza kuwa kati ya wahitimu
hao kuna marubani ,Madaktari,na wengi wao ni wahitimu wa kidato cha
sita katika masomo ya Sayansi ambao watakuja kuongeza ufanisi kwa
utendaji kazi katika jeshi kwa siku za usoni ili jeshi hilo liende
kisasa zaidi.
‘’Miongoni mwa wahitimu wapo
madaktari 80, marubani 6 wa ndege,huku 500 ni vijana ambao wamehitimu
kidato cha sita katika masomo ya Sayansi na kufaulu vizuri ambao
watasaidia katika kulijenga zaidi jeshi letu kwa siku za usoni’’alisema
Meja Jenerali Masau.
NAIBU SPIKA ACKSON AFUNGUA SEMINA KWA WABUNGE KUHUSU UELEWA WA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu (Wenye Ulemavu), Dk Abdallah Possi (kulia), akiwasilisha
mada katika semina ya Wabunge kukuza na kuimarisha usawa wa watu wenye
ulemavu nchini, kwenye Ukumbi wa Bunge wa Msekwa mjini Dodoma jana.
Kutoka kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Bukene, Seleman Zedi (CCM) na Naibu
Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson.PICHA ZOTE NA RICHARD
MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson akifungua semina hiyo
Mkuu wa wilaya Bukombe aagiza maafisa tarafa kusimamia hifadhi ya mavuno kwa wananchi
Mkuu
wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Amani K. Mwenegoha ameagiza maafisa tarafa
kusimamia kwa karibu shughuli za hifadhi ya mavuno yaliyopatikana katika
Mvua za vuli Msimu wa 2015/2016 kwa kuhamasisha wananchi wenye
mavuno mengi kila mahali kuhifadhi vizuri ili mavuno hayo yasiharibike
na kuweka akiba ya kutosha kwaajili ya kaya zao.
Pia ameagiza Wakulima
washauriwe kuuza ziada tu ya mavuno yao kwaajili ya kukidhi mahitaji yao
muhimu na kila kaya isimamiwe kuhakikisha imehifadhi mazao ya chakula
cha kuwatosha huku akiagiza Wafugaji washauriwe kuvuna sehemu ya
mifugo yao kwaajili ya kukidhi mahitaji yao muhimu na kununua nafaka
kwaajili ya kaya zao.
Amesisitiza maelezo haya
yawafikie viongozi ngazi za kata,vijiji na vitongoji kwaajili ya
utekelezaji na taarifa iwasilishwe kwa Mkuu wa Wilaya kabla ya
13/05/2016.
Imetolewa na
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bukombe
Geita
06 Mei, 2016
MAKATIBU WAKUU WA VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA WAKUTANA NCHINI ZIMBABWE
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akitoa mada
kwenye Kongamano la siku Nne la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya
Ukombozi Kusini mwa Afrika. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls
Zimbambwe lilianza tarehe 4 – 8 Mei, 2016. Vyama hivyo ni ANC ya Afrika
Kusini, FRELIMO ya Msumbiji, MPLA ya Angola, SWAPO Party ya Namibia na
CCM ya Tanzania.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akimpongeza Katibu Mtendaji Mkuu wa ZANU-PF Ndugu Ignatius Morgen Chombo kwa kufanikisha Kongamano la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika na anaeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa FRELIMO Ndugu Eliseu Machava. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016

Picha ya pamoja ya Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika(FLM) wanaoshiriki Kongamano la siku Nne la kutafakari uimarishaji na uendelezaji wa ushirikiano wao na namna ya kukabiliana na changamoto walizonazo. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa ANC ya Afrika Kusini Ndugu Ndugu Gwede Mantashe, Katibu Mkuu wa FRELIMO ya Msumbiji Ndugu Eliseu Machava, Katibu Mkuu wa CCM ya Tanzania Ndugu Abdulrahaman Kinana, Makamu Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomnisti cha China (CPC) Ndugu Guo Yezhou, Katibu Mtendaji Mkuu wa ZANU-PF ya Zimbabwe Ndugu Ignatius Morgen Chombo, Katibu Mkuu wa MPLA ya Angola Ndugu Juliao Mateus Paulo na Katibu Mkuu wa SWAPO Party ya Namibia Ndugu Nangolo Mbumba. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa ANC ya Afrika Kusini, Ndugu Gwede Mantashe kwenye Kongamano la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika(FLM) linalofanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akimpongeza Katibu Mtendaji Mkuu wa ZANU-PF Ndugu Ignatius Morgen Chombo kwa kufanikisha Kongamano la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika na anaeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa FRELIMO Ndugu Eliseu Machava. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016

Picha ya pamoja ya Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika(FLM) wanaoshiriki Kongamano la siku Nne la kutafakari uimarishaji na uendelezaji wa ushirikiano wao na namna ya kukabiliana na changamoto walizonazo. Kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa ANC ya Afrika Kusini Ndugu Ndugu Gwede Mantashe, Katibu Mkuu wa FRELIMO ya Msumbiji Ndugu Eliseu Machava, Katibu Mkuu wa CCM ya Tanzania Ndugu Abdulrahaman Kinana, Makamu Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomnisti cha China (CPC) Ndugu Guo Yezhou, Katibu Mtendaji Mkuu wa ZANU-PF ya Zimbabwe Ndugu Ignatius Morgen Chombo, Katibu Mkuu wa MPLA ya Angola Ndugu Juliao Mateus Paulo na Katibu Mkuu wa SWAPO Party ya Namibia Ndugu Nangolo Mbumba. Kongamano hilo linafanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa ANC ya Afrika Kusini, Ndugu Gwede Mantashe kwenye Kongamano la Makatibu Wakuu wa vilivyokuwa Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika(FLM) linalofanyika Victoria Falls, Zimbabwe tarehe 4 – 8 Mei 2016
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA KUU LA UWT TAIFA DODOMA LEO
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya
CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia ngoma alipowasili katika
Ofisi za Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM mjini Dodoma leo Mei
7,2016 kwa ajili ya kufungua mkutano wa Baraza Kuu la UWT Taifa.
Wajumbe
wa Mkutano wa Baraza Kuu la UWT Taifa wakimsikiliza Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM
Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan, alipokua akifungua Mkutano wa Baraza Kuu
la UWT Taifa wenye lengo la kukumbushana katika majukumu ya kiutendaji
kwenye ngazi mbalimbali za Jumuiya hiyo pamoja na kumpongeza Makamu wa
Rais kwa kuchaguliwa Mwanamke wa kwanza katika Ngazi hiyo Kuu ya
kitaifa. Mkutano huo umefunguliwa leo Mei 7,2016 katika Ukumbi wa
Halmashauri Kuu ya CCM mjini
Wajumbe
wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la UWT Taifa wakimkabidhi zawadi za aina
mbalimbali Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe
wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya
kumpongeza kwa kuchaguliwa Mwanamke wa kwanza katika Ngazi Kuu ya
kitaifa wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la UWT Taifa uliofunguliwa leo
Mei 7,2016 katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM mjini Dodoma
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya
CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Mkutano wa Baraza Kuu la
UWT Taifa wenye lengo la kukumbushana katika majukumu ya kiutendaji
kwenye ngazi mbalimbali za Jumuiya hiyo pamoja na kumpongeza Makamu wa
Rais kwa kuchaguliwa Mwanamke wa kwanza katika Ngazi hiyo Kuu ya
kitaifa. Mkutano huo umefunguliwa leo Mei 7,2016 katika Ukumbi wa
Halmashauri Kuu ya CCM mjini Dodoma.
Wajumbe
wa Mkutano wa Baraza Kuu la UWT Taifa wakimsikiliza Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM
Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan, alipokua akifungua Mkutano wa Baraza Kuu
la UWT Taifa wenye lengo la kukumbushana katika majukumu ya kiutendaji
kwenye ngazi mbalimbali za Jumuiya hiyo pamoja na kumpongeza Makamu wa
Rais kwa kuchaguliwa Mwanamke wa kwanza katika Ngazi hiyo Kuu ya
kitaifa. Mkutano huo umefunguliwa leo Mei 7,2016 katika Ukumbi wa
Halmashauri Kuu ya CCM mjini Dodoma.
Wajumbe
wa Mkutano wa Baraza Kuu la UWT Taifa wakimsikiliza Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM
Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan, alipokua akifungua Mkutano wa Baraza Kuu
la UWT Taifa wenye lengo la kukumbushana katika majukumu ya kiutendaji
kwenye ngazi mbalimbali za Jumuiya hiyo pamoja na kumpongeza Makamu wa
Rais kwa kuchaguliwa Mwanamke wa kwanza katika Ngazi hiyo Kuu ya
kitaifa. Mkutano huo umefunguliwa leo Mei 7,2016 katika Ukumbi wa
Halmashauri Kuu ya CCM mjini Dodoma.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya
CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Semina ya Mafunzo kwa
ajili ya kuwajengea Uwezo Viongozi na Makada wa Chama cha Mapinduzi CCM
iliyofunguliwa leo Mei 7,2016 katika ukumbi wa MORENA Mjini Dodoma.
akamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya
CCM Taifa Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati akiwa bkatika picha ya
pamoja na Viongozi na Makada wa Chama cha Mapinduzi CCM baada ya
kufungua Semina ya Mafunzo kwa ajili ya kuwajengea Uwezo Viongozi na
Makada wa Chama cha Mapinduzi CCM iliyofunguliwa leo Mei 7,2016 katika
ukumbi wa MORENA Mjini Dodoma.
UVCCM Z’BAR YAWATAKA VIONGOZI KUTEKELEZA AHADI
……………………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.
UMOJA wa vijana wa Chama cha
Mapinduzi(UVCCM) Zanzibar umewataka vijana wa umoja huo katika Mkoa wa
Kaskazini Unguja kuwakumbusha viongozi waliopo madarakani kwa sasa
kutekeleza kwa haraka ahadi walizotoa wakati wa kuomba ridhaa ya kuingia
madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa Marudio uliofanyika mwaka huu.
Umesema vijana wana haki ya
kutumia vikao halali vinavyokubalika katika utaratibu wa kiuongozi ndani
ya UVCCM kuwakumbusha viongozi wa chama hicho kutekeleza kwa vitendo
ahadi walizotoa kwa wananchi wa Zanzibar.
Akizungumza katika ziara ya
UVCCM katika Mkoa huo, Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar,
Abdulghafar Idrissa huko katika ofisi ya jimbo la Jimbo la Kitope
iliyopo Kinduni Unguja.
Alifafanua kwamba CCM ni chama
chenye viongozi makini wanaoahidi na wakatekeleza hivyo hakuna haja ya
vijana kuendelea kulalamika badala yake wafuate utaratibu kuwakumbusha
wahusika watekeleze majukumu yao kwa wananchi.
“ Vijana kumbukeni kuwa kwamba
nyie ndiyo mliowaweka madarakani hao Marais, wabunge, wawakilishi na
madiwani hivyo msiwaogope kuwakumbusha kwa kufuata taratibu wajibu wao
wa kutekeleza ahadi zao kwenu na wakikataa basi rudini kwetu mtwambie na
tutayafanyia kazi.”, alisema Idrissa.
Idrissa alisisitiza vijana hao
kuendelea kuwa wamoja ili waweze kunufaika na fursa mbali mbali
zilizopo katika chama na serikali iliyopo madakani.
Alisema umoja na mshikamano ndiyo
njia pekee itakayowawezesha vijana kubuni fursa za maendeleo kwa lengo
la kujikwamua katika wimbi la umasikini nchini.
Amos Makalla azindua mashindano ya UMISSETA Copa Coca Cola mkoani Mbeya
Mkuu
wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akihutubia wadau wa michezo na wanafunzi
wakati wa Uzinduzi wa mashindano ua UMISSETA ambayo mwaka huu
yamedhaminiwa na kampuni ya Coca Cola.Uzinduzi huo ulifanyika katika
uwanja wa Sokoine ambapo kulifanyika michezo mbalimbali na burudani za
kila aina zilikuwepo.
Meneja
wa Kiwanda cha Coca Cola tawi la Mbeya, Gary pay (kulia) akiteta jambo
na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla ndani ya Uwanja wa Sokoine Mbeya
kwenye uzinduzi wa mashindano ya UMISSETA
Mkuu wa Mkoa Amos Makalla akigagua moja ya timu wakati wa uzinduzi wa michuano hiyo kwenye uwanja wa mpira wa Sokoine.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali walihudhuria katika uzinduzi hyuo wa mashindano ya UMISSETA wakiwa katika uwanja wa Sokoine.
Burudani za muziki pia zilikuwepo kama kinavyoonekana kikundi hiki kikitumuiza katika uzinduzi huo.
Mkuu wa Mkoa Amos Makalla akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa mashindano ya UMISSETA mkoani humo.
Serikali yabaini tani 4,579.2 zilizokuwa zimefichwa Kwenye maghala
rank mvungi-Maelezo
Taasisi ya kuzuia na Kupambana na
rushwa (TAKUKURU) yabaini kuwepo kwa sukari iliyofichwa tani 4,579.2
iliyonunuliwa toka Kiwanda cha Sukari Kilombero.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa
leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Valentine
Mlolowa Taasisi hiyo imeanza uchunguzi dhidi ya swala hilo kwa
kushirikiana na Jeshi la Polisi.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa
mnamo tarehe 05 Mei, 2016 timu ya uchunguzi ilitembelea maghala yaliyopo
Tabata Jijini Dar es salaam na kubaini uwepo wa sukari hiyo.
TAKUKURU tayari imetembelea
Maghala ya mfanyabiasha Haruni Daudi Zacharia ambaye ni Mkurugenzi
Mtendaji wa Al-Naeem yaliyoko Mbagala na Tabata ambaye ni miongoni mwa
wafanyabiashara wakubwa wa sukari hapa nchini na anayetuhumiwa kuficha
bidhaa hiyo. Ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Aidha uchunguzi uliofanywa na
Taasisi hiyo ulibaini kuwepo kwa njama za dhati za kutouza sukari
iliyokutwa katika maghala hayo kulikofanywa na mfanyabiashara huyo kwani
hata sehemu ya Maghala ilipo sukari hiyo hapakuwa na dalili za upakiaji
wa sukari hiyo ili iweze kusambazwa.
Taarifa hiyo imeendelea kufafanua
kuwa katika eneo la Kitumbini kumekuwa na wananchi wengi wanaohitaji
bidhaa hiyo na wachache sana waliweza kuuziwa licha ya ukweli kwamba
sukari ilikuwepo.
Katika uchunguzi wake TAKUKURU
pia imebaini kuwepo kwa mikakati ya dhati iliyokuwa ikifanywa na
mfanyabiasha huyo kwa kununua sukari yote toka viwanda vya ndani na
kisha kuihifadhi na kuuza bidhaa hiyo kidogo kidogo kwa wastani wa tani
250 kwa siku wakati alikuwa na uwezo wa kuuza zaidi jambo lililochangia
uhaba wa sukari katika soko.
Kuficha bidhaa ni kosa la uhujumu
uchumi na ni kinyume na Aya ya 3 Jedwali la kwanza Sheria ya Uhujumu
Uchumi Sura ya 200 [Chapisho la Mwaka 2002]. Serikali haitavumilia
hujuma za namna hii na itachukua hatua kali dhidi ya mfanyabiashara
yeyote ataekwenda kinyume na sheria hii.
TAKUKURU imetoa wito kwa
wafanyabiashara wote wa sukari kuacha vitendo vya kuficha sukari na
vyombo vya uchunguzi vinafuatilia kote nchini na yeyote atakayebainika
kufanya hujuma hizo atakabiliwa na mkondo wa Sheria.
Abdallah
Moto mkazi wa Kijiji cha Kigwa B wilaya ya Uyuwi Mkoani Tabora akitoa
maoni yake kwa Kamati ya kukusanya Maoni ya kuboresha Sera ya Taifa ya
Ardhi ya 1995 kuhusu suala la kupewa kipaumbele utoaji wa hati miliki
kwa wanavijiji.
Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Ardhi.
……………………………………………………………………………………………………………………………….
Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi imeanza zoezi la ukusanyaji wa maoni na kuipitia
upya Sera ya Taifa ya Ardhi ya 1995 ili kuiboresha. Zoezi hilo limeanza
Mwaka huu wa 2016 ambapo linashirikisha kanda nane za Ardhi ambazo ni
Kanda ya Dar es salaam, Kanda ya Mashariki, Kanda ya Kusini, Kanda ya
Nyanda za Juu Kusini Magharibi, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kati, Kanda
ya Ziwa na Kanda ya Kaskazini.
Na kwa sasa kamati maalumu ya
kukusanya maoni ipo mkoani Tabora ikikusanya maoni ya wananchi na wadau
mbalimbali wa sekta ya Ardhi ili kupata sera iliyoridhiwa na wengi.
Katika sekta ya Ardhi Serikali ya
Tanzania imekuwa ikitekeleza Sera ya Taifa ya Ardhi ya 1995 kwa
takribani miaka 20 hadi sasa, hata hivyo zimejitokeza changamoto nyingi
ambazo zinalazimu kufanya mapitio ya sera hiyo.
Migogoro na malalamiko
yanayotokana na ardhi ni changamoto zinazo chukua nafasi kubwa katika
jamii yetu na imekuwa ikiigharimu kwa kiasi kikubwa katika kuitatua.
Kuongezeka kwa migogoro hii
imekuwa ni changamoto zinazoikabili sekta ya ardhi pamoja na watumiaji
mbalimbali wa ardhi hususan wakulima na wafugaji, wawekezaji, wananchi,
vijiji na hifadhi.
Hata hivyo, kuongezeka kwa
mahitaji ya ardhi kwa ajili ya uwekezaji hususan katika sekta za kilimo,
madini, viwanda na wananchi kutonufaika na uwekezaji unaofanywa katika
ardhi na hivyo kusababisha migogoro baina ya wananchi na wawekezaji.
Aidha kutokuwepo kwa mipango ya
matumizi endelevu ya ardhi mijini na vijijini na hata sekta ya ardhi
kuvamiwa na madalali ni changamoto iliyoifanya Serikali kuamua kuipitia
upya Sera ya Taifa ya Ardhi ya 1995.
Changamoto zote kwa pamoja,
zimelazimika kufanyika kwa mapitio ya Sera ya Taifa ya Ardhi ya 1995 ili
kutoa mwelekeo mpya na usimamizi wa ardhi kwa manufaa ya watanzania
wote.
Ardhi ni Sekta mama na hivyo basi
Sera ya ardhi ni sera mama katika masuala yote ya maendeleo ikiwemo
kilimo na mifugo, ambayo shughuli zake zinafanyika kwenye ardhi.
Na sasa Wizara ya Ardhi, Nyumba
na Maendeleo ya Makazi imeanza zoezi la ukusanyaji wa maoni na kuipitia
upya Sera ya Taifa ya Ardhi ya 1995 ili kuiboresha. Zoezi hilo limeanza
Mwaka huu wa 2016 ambapo linashirikisha kanda nane za Ardhi ambazo ni
Kanda ya Dar es salaam, Kanda ya Mashariki, Kanda ya Kusini, Kanda ya
Nyanda za Juu Kusini Magharibi, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kati, Kanda
ya Ziwa na Kanda ya Kaskazini.





No comments :
Post a Comment