Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipata ufafanuzi wa mikakati ya uwekezaji kwenye
miundombinu ya umeme wa gesi asilia na jua kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa
Kampuni ya KOYO ya Japan, Bw. Norio Shoji wakati alipokutana na ujembe
wa kampuni hiyo ofisini kwake jijini Dar es salaam May 9, 2016. (Picha
na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Viongozi wa Kampuni ya
Japan ya KOYO na kampuni ya Kitanzania ya SSF Limited ambazo kwa
pamoja zimekusudia kushirikiana ili kuwekeza kwenye miundombinu ya
umeme wa gesi asilia na jua nchini. Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini
kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam May 9, 2016. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya KOYO ya
Japan, Bw. Norio Shoji baada ya kukutana na Mtendaji huyo na ujumbe
wake ofisini kwake jijini Dar es salaam May 9, 2016. Kampuni hiyo
ikishirikiana na Kampuni ya Kitanzania ya SSF Limited inakusudia
kuwekeza kwenye miundombinu ya umeme wa gesi asilia na jua nchini.
(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa
Kampuni ya Japan ya KOYO na kampuni ya Kitanzania ya SSF Limited
ambazo kwa pamoja zimekusudia kushirikiana ili kuwekeza kwenye
miundombinu ya umeme wa gesi asilia na jua nchini. Waziri Mkuu alifanya
mazungumzo na viongozi hao ofisini kwake jijini Dar es salaam May 9,
2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Watanzania wahamasishwa kujitokeza kushiriki shindano la kuongeza kipato
Mtaalam
Mshauri wa Master Card Foundation Gabriel Kivuti akieleza jambo kwa
waandishi wa habari juu ya kushiriki shindano la kuongeza kipato
lijulikanalo kama “Scaling Competition” kwa makundi yanayoruhusiwa
kushiriki shindano hilo kuwa ni pamoja na vikundi vya akiba, bima ndogo
ndogo na mifumo ya umoja wa fedha, fomu za maombi na mwongozo wa
kushiriki shindano hilo zinapatikana katika tovuti ya www.frp.org .
Mtaalam
Mshauri wa Master Card Foundation Gabriel Kivuti akifafanua jambo
katika semina ya namna shirika hilo linavyofanya kazi na jinsi ya
kushiriki shindano la mwaka 2016 ili kupata washindi watakaopata msaada
wa kifedha na kuboresha ushirikishwaji wa kifedha kwa wakulima wadogo
Afrika.
…………………………………………………………………
Na: Lilian Lundo – Maelezo
Watanzania wameombwa kujitokeza
kwa wingi kushiriki shindano la kuongeza kipato lijulikanalo kama
“Scaling Competition” kwa kutuma maombi yao shirika la “Master Card
Foundation, Fund For Rural Prosperity” ili kupanua na kuimarisha
upatikanaji wa fedha Vijijini Tanzania.
Hayo yalisemwa na Mtaalam
Mshauri wa Master Card Foundation Gabriel Kivuti leo, jijini Dar es
Salaam katika semina ya namna shirika hilo linavyofanya kazi na jinsi ya
kushiriki shindano la mwaka 2016 ili kupata washindi watakaopata msaada
wa kifedha na kuboresha ushirikishwaji wa kifedha kwa wakulima wadogo
Afrika.
“Master Card Foundation inafanya
kazi na mashirika yenye maono ili kuleta zaidi upatikanaji wa elimu,
mafunzo ya ujuzi na huduma za kifedha kwa watu wanaoishi katika umaskini
barani Afrika, ikiongozwa na dira ya kuboresha mafunzo na kuongeza
ushirikishwaji wa upatikanaji wa kifedha ili kupunguza umaskini,”
alisema Kivuti.
Kivuti alisema kuwa, kaya nyingi
za vijijini barani Afrika hazishirikishwi katika masuala ya kifedha na
zaidi ya asilimia 70 za familia Kusini mwa Jangwa la Sahara sehemu
kubwa ya mapato yao yanatokana na shughuli za kilimo, wakati huohuo
watoa huduma za kifedha wanakabiliana na changamoto kadhaa katika
kuifikia jamii, hivyo Master Card likaamua kusaidia miradi ambayo ina
uwezo wa kuleta mabadiliko chanya.
Aidha, Kivuti alitaja makundi
yanayoruhusiwa kushiriki shindano hilo kuwa ni pamoja na vikundi vya
akiba, bima ndogo ndogo na mifumo ya umoja wa fedha, fomu za maombi na
mwongozo wa kushiriki shindano hilo zinapatikana katika tovuti ya www.frp.org .
Jumla ya dola za Kimarekani
milioni 10.6 zimetolewa kwa washindi wa mwaka 2015 kwa ajili ya
maendeleo Vijijini, kampuni zilizoshinda ni APA Insurance Ltd kutoka
Kenya, Finserve Afrika Ltd/Equitel kutoka Uganda, M-KOPA LLC kutoka
Tanzania, Musoni Kenya Ltd kutoka Kenya na Olam Uganda Ltd kutoka
Uganda. Kupitia kampuni hizo takribani watu milioni nane wanaoishi
maeneo ya Vijijini watakuwa na fursa ya kupata huduma za kifedha ifikapo
mwaka 2020
WAZIRI MKUU KUMWAKILISHA RAIS MAGUFULI LONDON
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
anatarajiwa kuondoka nchini leo jioni (Jumanne, Mei 10, 2016) kwenda
London, Uingereza kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi unaojadili suala
la kupambana na rushwa (Anti-Corruption Summit 2016) utakaofanyika Mei
12, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari
leo mchana, Waziri Mkuu alisema anaenda kumwakilisha Mheshimiwa Rais,
Dk. John Pombe Magufuli kwa sababu siku hiyo hiyo, atalazimika
kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri
Museveni.
“Mheshimiwa Dk. Magufuli ni
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), na siku hiyo hiyo,
mmoja wa marais wa nchi wanachama anaapishwa. Kwa hiyo amelazimika
kwenda kuhudhuria sherehe hizo,” alifafanua Waziri Mkuu.
Akizungumzia kuhusu mada ya
mkutano huo, Waziri Mkuu amesema Tanzania inafanya vema katika mapambano
dhidi ya rushwa na kwamba baadhi ya nchi zimeanza kuvutiwa na juhudi
ambazo Serikali imekuwa ikichukua.
“Waziri Mkuu wa Uingereza ameandaa
mkutano huu na alimwalika Mheshimiwa Rais Magufuli ili ahudhurie akiwa
ni miongoni wa wakuu wa nchi 60 watakaohudhuria mkutano huo. Tanzania ni
miongini mwa nchi mbili kutoka bara la Afrika ambazo zimealikwa
kushiriki. Nchi nyingine ya kutoka Afrika ni Nigeria,” alisema.
Waziri Mkuu atafuatana na Jaji
Mkuu wa Tanzania, Othman Chande, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa
Kimataifa na Kikanda, Balozi Dk. Augustine Mahiga, Mkurugenzi wa
TAKUKURU, Bw. Valentino Mlowola, wataalamu wa sekta ya rushwa na
wanasheria
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
2 MTAA WA MAGOGONI,
- L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
JUMANNE, MEI 10, 2016.
WAZIRI MKUU: SERIKALI ITAAGIZA TANI 70,000 ZA SUKARI
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye makazi yake jijini Dar es salaam.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
……………………………………………………………………….
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
amesema Serikali itaagiza kutoka nje ya nchi tani 70,000 za sukari
ambapo kati ya hizo, tani 11,957 zimeshawasili nchini na zitaanza
kusambazwa kesho (Jumatano).
Ametoa kauli hiyo leo mchana
(Jumanne, Mei 10, 2016) wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye
mkutano uliofanyika nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Akitoa ufafanuzi wa sukari ambayo
imekwishawasili nchini, Waziri Mkuu alisema tani 2,000 zitapelekwa mikoa
ya Kaskazini, tani 3,000 (mikoa ya Kanda ya Ziwa), tani 2,000 (mikoa ya
Kusini), tani 2,000 (Nyanda za Juu Kusini) na tani 2,000 (mikoa ya
Kanda ya Kati).
“Tani nyingine 24,000 za sukari
zitawasili Ijumaa hii na hadi zitoke bandarini itakuwa kama Jumapili kwa
hiyo zinaweza kusambazwa kuanzia Jumatatu. Tani nyingine 20,000
zitawasili baadaye, ama mwishoni mwa mwezi huu au mapema mwezi Juni,”
alisema Waziri Mkuu.
Amesema anawataka Watanzania
wasihofu kuhusu uhaba wa sukari uliojitokeza hivi karibuni kwani
umesababishwa na watu wachache. “Mheshimiwa Rais ameagiza watu
waliohodhi bidhaa hii wakamatwe na sukari isambazwe. Lakini pia
tunaagiza kwa muda mfupi kwa sababu viwanda vyetu vinatarajia kuanza
uzalishaji ifikapo Julai,” alisema.
Amewataka wasambazaji wa sukari
waziuze kwa wafanyabishara wadogo ili wao wawawuzie wananchi kwa bei
elekezi ya sh. 1,800. Pia amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya
kuhakikisha wanasimamia zoezi la ukaguzi ili kubaini zaidi wale
waliohodhi bidhaa hiyo.
Akifafanua kuhusu mkakati wa
Serikali kuongeza uzalishaji wa sukari nchini, Waziri Mkuu amesema nia
ya Serikali ni kuhakikisha tatizo la uhaba wa sukari nchini linakwisha
ifikapo 2019. “Wananchi wasiogope, Serikali imechukua hatua kwa udhibiti
mzuri ili tusije kuporomosha soko letu la ndani,” alisema.
“Tunao mkakati wa kuboresha
viwanda vya ndani, wenye viwanda wenyewe au kwa ubia na wawekezaji
kutoka nje, wanaweza kufungua mashamba kwenye maeneo matatu tuliyotenga
kwa ajili hiyo,” alisema.
“Serikali imetenga maeneo matatu
yanayofaa kwa kilimo cha miwa huko Bagamoyo, Ngerengere na Kigoma. Huko
wanaweza kulima na kujenga viwanda vya sukari na uzalishaji ukawa
unapanda mwaka kwa mwaka hadi tutakapoweza kuimaliza hii gap iliyopo,”
alisema.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
2 MTAA WA MAGOGONI,
- L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
JUMANNE, MEI 10, 2016.
SERIKALI YAPIGA MARUFUKU KUPAKIA MIZIGO KUPITA KIASI.
Na Benedict Liwenga, MAELEZO, Dodoma.
………………………………………..
SERIKALI imepiga marufuku upakiaji wa mizigo kupita kiasi (lumbesa) katika magunia kuanzia mwaka ujao wa fedha.
Kauli hiyo imetolewa
jana Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji,
Mhe. Charles Mwijage (Mb) wakati akijibu hoja mbalimbali za Wabunge
wakiochangia hotuba ya Wizara yake.
Amesema kuwa, kuanzia mwaka ujao wa fedha, Vyombo vy Dola vitakamata wafanyabiashara wote watakaokuwa wanapakia lumbesa.
Mhe. Mwijage alisema
kuwam upakiaji huo wa mizigi kupita kiasi unawasababishia wizi kwa
wakulima ambapo ametoa wito kwa wakulima na wafanyabiashara nchini
kutumia vipimo halali wakati wanaponunua na kuuza mazao yao mbalimbali.
Katika hatua nyingine, Waziri huyo ametoa wito kwa wakulima kuacha tabia ya kuuza mazao yao yakiwa shambani au kabla ya kukomaa.
Alisema kuwa hali hiyo inawarudisha nyuma na kuwapunja wakati wangesubiri mazao yakomae wangepata fedha za kutosha.
11 WA KWANZA DHIDI YA YANGA HAWA HAPA
Katika kikosi hicho mlinda mlango
Juma Kaseja anaendelea kusimama langoni sambamba na walinzi wa kulia
na kushoto, John Kabanda na Hassan Mwasapili.
Wengine katika kikosi hichi ni kama ifuatavyo
1.Juma Kaseja 2. John Kabanda
3. Hassan Mwasapili 4. Tumba Lui 5.Haruna Shamte 6.Kenny Ally 7. Seleman
Mangoma 8. Ramadhan Chombo 9. Salvatory Nkulula .10 Geoffrey Mlawa 11
Joseph Mahundi
SUB: Hanningtony Kalyesubula, Hamidu Mohamed, John Jerome,Ditram Nchimbi,Haruna Moshi,Raphael Daud na Yohana Moriss.
Mchezo huu namba 218 umepangwa
kuanza saa 10:00 na utachezeshwa na mwamuzi Jimmy Fanuel kutoka
Shinyanga, huku kiingilio kwa mashabiki kikiwa ni shilingi 5000 tu.
NAPE: UANACHAMA WA TFF KATIKA FIFA UPO.
Na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
…………………………………..
Kufuatia majadiliano na vikao
mbalimbali vilivyofanyika mwaka 2005-2010, kumbukumbu zinaonyesha kuwa
suala la uanachama wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na
Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) lilifanyiwa kazi kwa ukamilifu
na Serikali za pande zote mbili kwa ushirikiano na Vyama vyote viwili.
Hayo yamesemwa leo na
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (Mb)
wakati akijibu swali la Mhe. Mbunge wa Dimani Hafidh Ali Tahir lenye
kipengele a,b na c lililotaka kujua ni nini matokeo ya Kamati iliyoundwa
na Waziri Mkuu.
Mhe. Nnauye ameeleza
kwamba, kwa kutambua umuhimu wa ZFA kupata uanchama wa FIFA, mwaka 2010
ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwamba, ukiongozwa na aliyekuwa
Naibu Waziri Kiongozi, Mhe. Juma Shamhuna pamoja na aliyekuwa Naibu
Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Joel Bendera
walikwenda Zurich, Switzerland ambako walikutana na Rais wa FIFA wa
wakati huo.
Aidha, Mhe, Nnauye
amefafanua kuwa, katika msafara huo walifuatana na viongpozi wa TFF na
ZFA na madhumuni ya safari hiyo ilikuwa ni kuwasilisha maombi ya ZFA
kupewa uanachama wa FIFA.
“Mwezi Juni 2011, FIFA
iliiandikia ZFA ikiwajulisha kuwa kwa mujibu wa taratibu zilizopo,
isingewezekana Zanzibar kupata Uanachama wa FIFA kwa kuwa wananchama wao
ni nchi zinazotambuliwa na Jumuiya ya Kimataifa kama ilivyoelezwa
katika aya ya 10 ya Katiba yao”, alisema Mhe. Nnauye.
Mhe. Nnauye aliongeza
kuwa, suala la usajili wa TFF au ZFA linafahamika vyema ndani ya
Serikali ya Mapinduzi pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
“Hata hivyo, naomba
kulihakikishia Bunge lako Tukufu kuwa, uanachama wa TFF katika FIFA upo
kwa mujibu wa muafaka wa pande zote mbili.
Kwa kuzingatia
utaratibu wa FIFA kuhusiana na suala hilo, Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo imewaelekeza TFF nao wako tayari kufanya maridhiano na
ZFA ili kukamilisha utaratibu wa wazi wa kukidhi mahitaji ya Zanzibar
kushiriki katika masuala ya FIFA kupitia TFF bila kuathiri ushiriki wa
klabu za Zanzibar katika mashindano yanayoandaliwa na Shirikisho la
Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
SERIKALI YATENGA SHILINGI BILIONI 59.5 KWA AJILI YA KUWAWEZESHA WANANCHI VIJIJINI.
Na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
…………………………………….
SERIKALI imetenga Shilingi bilioni
59.5 katika Bajeti ya mwaka 2016/17 kwa ajili ya kuwawezesha Wananchi
vijijini kwa kutoa shilingi milioni 50 kwa kila kijiji na mtaa.
Taarifa hiyo imetolewa
leo Bungeni na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Watu wenye Ulemavu,
Mhe. Dkt. Abdallah Possi (Mb) wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti
Maalum, Mhe. Esther Mahawe aliyetaka kujua ni lini fedha zingetolewa na
Serikali imejipanga vipi kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wananchi juu ya
njia bora ya kutumia fedha hizo.
Dkt. Possi amesema
kuwa, fedha hizo zitatolewa mara baada ya kuidhinishwa na Bunge hilo na
baada ya kukamilisha taratibu mahususi zinazolenga kuhakikisha uwepo wa
tija katika matumizi ya fedha hizo.
Ameongeza kuwa, kuhusu
mpango bora wa Elimu ya Ujasiriamali kwa wananchi, Serikali inaendelea
kukamilisha maandalizi ya utaratibu maalum wa utoaji wa fedha hizo ikiwa
ni pamoja na utoaji wa elimu ya Ujasiriamali.
“Baraza la Taifa la
Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI
imepewa kazi ya kuratibu utekelezaji wa mpango huo”, alisema Dkt.
Possi.
MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI DODOMA 10 MEI, 2016.
Waziri
wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi (kulia)
pamoja na Katibu Mkuu, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job
Masima wakiwa katika mazungumzo Bungeni mjini Dodoma kabla ya kuanza kwa
vikao vya asubuhi vya bunge hilo 10 Mei, 2016.
Mkuu
wa Majeshi ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Jenerali Davis
Mwamunyange (kulia) akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Ulinzi na Jeshi
la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi pamoja na Katibu Mkuu,
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima Bungeni mjini
Dodoma kabla ya kuanza kwa vikao vya asubuhi vya bunge hilo 10 Mei,
2016.
Waziri
wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akisoma
taarifa Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa leo 10 Mei,
2016, Bungeni mjini Dodoma.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO, DODOMA.
KAMISHNA MSAIDIZI KITENGO CHA HAKI ZA MTOTO AFUNGUA NYUMBA ZA KUNDI LA WATOTO
Kaimu
Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia,
Steven Gumbo akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa mradi wa nyumba za kundi la watoto wanaoelekea ujanani katika kituo cha kulelea watoto cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Jengo
jipya lililojengwa kwa ufadhili wa Emirates National Bank of Dubai
(ENBD) kwa ajili ya watoto wanaoelekea ujanani katika kituo cha kulelea
watoto cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akimuonesha Kaimu Kamishna msaidizi kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo maeneo mbalimbali ya jengo hilo katika ramani.
Moja ya muonekano wa chumba katika jengo hilo.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap
akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi rasmi wa jengo hilo.
Baadhi
ya walimu na walezi wa watoto katika kituo cha kulelea watoto cha Aman
Center wakifuatilia shughuli mbalimbali katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap akiteta jambo na Kaimu Kamishna kitengo cha haki za mtoto na marekebisho ya tabia, Steven Gumbo wakati wa hafla ya ufunguzi wa jengo hilo.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto cha Aman Center Meindert Schaap
akimkaribisha Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
,Agnes Urassa katika Hafla hiyo.
Baadhi ya watoto wanaolelewa katika kituo cha Aman Center kilichopo mjini Moshi.
DAWASCO KUGHARAMIA GHARAMA ZA UUNGANISHAJI KWA WATEJA WAPYA
| Mhandisi Cyprian Luhemeja. |
Katika kutekeleza agizo la serikali la kuwafikia wateja laki 4 (400,000) ifikapo June
2016 ,Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es salaam (Dawasco) ,linaendelea
na zoezi la uunganishaji wa huduma ya
Maji kwa wananchi wote wa jiji la Dar es salaam pamoja na miji ya Bagamoyo na
Kibaha mkoani Pwani huku ikigharamia gharama zote za uunganishaji ambazo awali
zilikuwa zikilipwa na mteja.
2016 ,Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es salaam (Dawasco) ,linaendelea
na zoezi la uunganishaji wa huduma ya
Maji kwa wananchi wote wa jiji la Dar es salaam pamoja na miji ya Bagamoyo na
Kibaha mkoani Pwani huku ikigharamia gharama zote za uunganishaji ambazo awali
zilikuwa zikilipwa na mteja.
Akiongeana waandishi wa habari hivi Afisa mtendaji mkuu wa Dawasco, Mhandisi Cyprian
Luhemeja ameeleza kuwa kwenye awamu hii ya zoezi la uunganishaji wateja wapya
shirika litagharamia gharama zote za maunganisho ambazo ni gharama za
uunganishaji, mabomba na vifaa vya uunganishaji ambapo mteja atawajibika kurudisha
gharama hizo za maunganisho kidogo kidogo kila mwezi kwa kipindi cha miezi 12
baada ya kupata huduma ya Maji.
Luhemeja ameeleza kuwa kwenye awamu hii ya zoezi la uunganishaji wateja wapya
shirika litagharamia gharama zote za maunganisho ambazo ni gharama za
uunganishaji, mabomba na vifaa vya uunganishaji ambapo mteja atawajibika kurudisha
gharama hizo za maunganisho kidogo kidogo kila mwezi kwa kipindi cha miezi 12
baada ya kupata huduma ya Maji.
“Dawasco itamuunganishia huduma ya maji na kugharamia gharama zote uunganishaji ila
mteja atawajibika kurudisha ile gharama kidogokidogo kila mwezi kwa kipindi cha
miezi 12 baada ya kupata huduma ya Maji hii itasaidia hata wale ambao kipato
chao ni cha chini kuweza kuunganishiwa huduma ya Maji” alisema Luhemeja.
mteja atawajibika kurudisha ile gharama kidogokidogo kila mwezi kwa kipindi cha
miezi 12 baada ya kupata huduma ya Maji hii itasaidia hata wale ambao kipato
chao ni cha chini kuweza kuunganishiwa huduma ya Maji” alisema Luhemeja.
Pia Mhandisi Cyprian Luhemeja ameleeza kuwa zoezi hili la uunganishia wateja wapya ni
la kipindi cha miezi miwili tu cha Mei na Juni 2016 hivyo wananchi wote watumie
fursa hii kwa kufika katika ofisi za Dawasco za kanda ili kupata huduma hiyo.
la kipindi cha miezi miwili tu cha Mei na Juni 2016 hivyo wananchi wote watumie
fursa hii kwa kufika katika ofisi za Dawasco za kanda ili kupata huduma hiyo.
“Zoezi
hili la kugharamia gharama za
uunganishaji huduma ya maji kwa wateja ni kwa kipindi maalum cha miezi miwili
tu ambacho ni Mei na Juni hivyo wananchi watumie fursa hii kujitokeza iliwaweze
kuunganishiwa na katika kipindi chote cha zoezi Ofisi za Dawasco zitakuwa wazi
kuanzia jumatatu hadi jumapili” alisema Luhemeja.
hili la kugharamia gharama za
uunganishaji huduma ya maji kwa wateja ni kwa kipindi maalum cha miezi miwili
tu ambacho ni Mei na Juni hivyo wananchi watumie fursa hii kujitokeza iliwaweze
kuunganishiwa na katika kipindi chote cha zoezi Ofisi za Dawasco zitakuwa wazi
kuanzia jumatatu hadi jumapili” alisema Luhemeja.
Hata
hivyo Dawasco imeeleza kuwa wananchi pamoja wateja wake wameweza kuwasiliana na
kituo cha huduma kwa wateja kupitia
namba 022-2194800 au 0800110064 (bure) ili waweze kupata huduma na maelezo
zaidi kuhusiana na zoezi hilo la uunganishaji huduma ya Maji.
hivyo Dawasco imeeleza kuwa wananchi pamoja wateja wake wameweza kuwasiliana na
kituo cha huduma kwa wateja kupitia
namba 022-2194800 au 0800110064 (bure) ili waweze kupata huduma na maelezo
zaidi kuhusiana na zoezi hilo la uunganishaji huduma ya Maji.
Rais Mstaafu JK akutana na waandishi wa habari kutoka Malaria No More
Rais
Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya
Kikwete akiongea na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kutoka Taasisi
ya “Malaria No More” ya nchini Marekani leo jijjini Dar es salaam,
waandishi hao wapo nchini kwa ziara ya siku tano kujionea namna Tanzania
inavyopambana na ugonjwa wa malaria.(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
Rais
Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya
Kikwete akiongea na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kutoka Taasisi
ya “Malaria No More” ya nchini Marekani leo jijjini Dar es salaam,
waandishi hao wapo nchini kwa ziara ya siku tano kujionea namna Tanzania
inavyopambana na ugonjwa wa malaria. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi ya “Malaria No More” Martin Edlund.
Rais
Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya
Kikwete akiongea na waandishi wa Habari kutoka Taasisi ya “Malaria No
More” ya nchini Marekani leo jijjini Dar es salaam, waandishi hao wapo
nchini kwa ziara ya siku tano kujionea namna Tanzania inavyopambana
kutokomeza ugonjwa wa malaria.
Rais
Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waandishi wa Habari
kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini Marekani leo jijjini Dar
es salaam, waandishi hao wapo nchini kwa ziara ya siku tano kujionea
namna Tanzania inavyopambana kutokomeza ugonjwa wa malaria.
TANZIA UK DIASPORA GLASGOW.
Tunasikitika kuwatangazia msiba wa Mtanzania mwenzetu
Bi Mwasaburi Haji
kilichotokea Jumamosi jioni huko Glasgow Scotland.
Mipango ya mazishi inaendelea na mtajulishwa tarehe ya mazishi.
Msiba uko nyumbani kwa Marehemu
2/1, 105 Mcculloch St. Glasgow, G41 1NT.
Kwa wale mlioguswa mnaweza kutuma rambi rambi zenu kwenye account ya
ndugu wa marehemu
A. AZIZ.
Nationwide.
Account No: 01491791
Sort code: 07 04 36.
Kwa mawasiliano zaidi mnaweza kumpigia ndugu wa Marehemu
A. AZIZ – 07411445644
Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Rajiun.











No comments :
Post a Comment