Monday, April 18, 2016

SYMBION POWER-TANZANIA YATUHUMU KAMPUNI YA DUBAI ENTAL SERVICES AND SOLUTIONS (RSS) KWA KUIKIMBIA TANZANIA BILA KULIPA KODI


NA Mwandishi wa K-VIS MEDIA
Kutoka Washington, DC, imeelezwa kwamba leo tarehe 18 April, 2016; Kampuni ya Symbion Power, imekanusha vikali kile ambacho kimeelezwa na kukuzwa kupita kiasi na Kampuni yenye makazi yake Dubai iitwayo Rental Services and Solutions ( Kampuni itoayo huduma za kukodisha na suluhisho mbali mbali) na washirika wake
Akiongea kutoka Jijini Washington DC, Makamu wa Rais Mwandamizi anayehusika na kitengo cha Mawasiliano na Masuala ya Kijamii katika kampuni ya Symbion Power , Ndugu Adi Raval amesmea. “Kiuhalisia hili ni suala la kodi. Hii kampuni iitwayo RSS na washirika wake walikuwa wakifanya kazi kama wakandarasi waliokamishwa na Kampuni ya Symbion kwa miaka mitatu ; kutoka mwaka 2011 mpaka mwaka 2014. Katika muda huo hawakulipa  hata dola moja ya kodi kwa Serikali ya Tanzania kinyume na inavyotakiwa kwa mujibu wa sheria”.






Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana  (kulia) , Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega (Wapili kushoto) na Mbunge wa  Nachingwea, Hassan Masala baada ya kuwasili kwenye uwanja w ndege wa Dodoma kuhudhuria kikao cha Bunge kinachotarajiw kuanza Arili 19, 2016..

Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya akifunua pazia kuashiria kuweka jiwe la msingi la jengo la biashara na Ofisi la 2D la mjini Morogoro lililojengwa kwa thamani ya Shilingi bilioni 4.3. Jengo hilo ni la ghorofa nne likiwa na eneo la chijni kwa ajili ya maegesho ya magari . Ni mradi wa kwanza kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu mara tuu baada ya kuwashwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Mkurugenzi wa Fedha wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Maagi ambaye alimuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa akiupokea kwenge mbele ya Kiongozi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kukimbiza mwenge huo katika Mikoa na wilaya zote za Tanzania.
Meneja wa Shirika la Taifa, Veneranda Seif akiupokea kwenge mbele ya Kiongozi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kukimbiza mwenge huo katika Mikoa na wilaya zote za Tanzania.
Meneja wa Shirika la Taifa, Veneranda Seif akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo mbele ya Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kukimbiza mwenge huo katika Mikoa na wilaya zote za Tanzania.
Jengo la Biashara la 2D linavyoonekana leo kabla ya kuzinduliwa na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya.
Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa akijiandaa kuupokea Mwenge wa Uhuru.
Wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo wakijiandaa kuupokea Mwenge wa Uhuru.
Mwenge wa Uhuru ukiwasili katika eneo la tukio.
Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Issack Peter akiupokea Mwenge wa Uhuru ulipowasili katika eneo mradi wa 2D.
Kiongozi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya akizungumza baada ya kuzindua jengo hilo ambapo alilipongeza Shirika hilo kwa kazi kubwa wanayofanya kuhakikisha wanawapatia wananchi makazi bora na akalitaka Shirika kuendeleza jitihada hizo ili Watanzania wengi zsaidi wafaidike.
Kiongozi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya akizungumza baada ya kuzindua jengo hilo ambapo alilipongeza Shirika hilo kwa kazi kubwa wanayofanya kuhakikisha wanawapatia wananchi makazi bora na akalitaka Shirika kuendeleza jitihada hizo ili Watanzania wengi zaidi wafaidike.
Wafanyakazi wa Ashirika la Nyumba la Taifa Mkoa wa Morogoro wakiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi.
Kiongozi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2016 George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya akizungumza baada ya kuzindua jengo hilo ambapo alilipongeza Shirika hilo kwa kazi kubwa wanayofanya kuhakikisha wanawapatia wananchi makazi bora na akalitaka Shirika kuendeleza jitihada hizo ili Watanzania wengi zaidi wafaidike.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo. Kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan kwenye Mahakama ya Rufaa jijini Dar es Salaam Aprili 18, 2019. Mkutano huo ulilenga kujenga ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika kubadilishana na kukuza weledi katika sekta ya sheria. 
(Picha na Aron Msigwa wa MAELEZO)



Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akieleza namna Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China inavyofanya kazi leo jijini Dar es salaam wakati wa kikao cha pamoja kilichowahusisha Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na China. Wengine  ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) na Jaji Kiongozi Mhe. Shaban Lila.



Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja kati ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China uliolenga kukuza ushirikiano na kubadilishana uzoefu wa utendaji wa Mahakama za Tanzania na China leo jijini Dar es salaam. 






Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Shaban Lila(kulia) akimweleza jambo jaji wa Mahakamu Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China mara baada ya kumkaribisha Ofisini kwake Mahakama Kuu leo jijini Dar es salaam.






Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (wa pili kutoka kushoto mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman (katikati) na baadhi ya watendaji wa Mahakama ya Tanzania mbele ya Jengo la Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam.





Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akiwa ameongozana na Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan (kushoto) mara baada ya kumpokea katika viwanja vya Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam. Mhe. Zhang Jiannan pamoja na ujumbe wake yupo nchini kwa ziara ya kikazi kwenye Mahakama ya Tanzania kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi na kuimarisha ushirikiano baina ya Mahakama ya Tanzania na China. 




Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang ( kushoto) akiagana na  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman (kulia) mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo naye leo jijini Dar es salaam. 




Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman mbele ya Jengo la Mahakama ya Rufaa.



Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akipokea zawadi ya kinyago kutoka kwa Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman.

No comments :

Post a Comment