Monday, April 18, 2016

JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. MOHAMED CHANDE OTHMAN AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA JAJI MKUU WA MAHAKAMA YA CHINA MHE. ZHANG JIANNAN LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

 
 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akiwa ameongozana na Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan (kuahoto) mara baada ya kumpokea katika viwanja vya Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam. Mhe. Zhang Jiannan pamoja na ujumbe wake yupo nchini kwa ziara ya kikazi kwenye Mahakama ya Tanzania kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi na kuimarisha ushirikiano baina ya Mahakama ya Tanzania na China. 
 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akisalimiana na baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China mara baada ya kuwakaribisha   Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam.
  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja kati ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China uliolenga kukuza ushirikiano na kubadilishana uzoefu wa utendaji wa Mahakama za Tanzania na China leo jijini Dar es salaam. 
 Baadhi ya Majaji wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa mkutano wa pamoja ulioongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania na Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China.
   Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na wale wa Mahakam Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China wakibadilisha uzoefu wa shughuli za kimahakama na masuala mbalimbali ya utendaji wakati wa mkutano wa pamoja ulioongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania na Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China jijini Dar es salaam.
 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo. Kushoto ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan
 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) akimweleza jambo Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang Jiannan wakati wa mkutano huo.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akieleza namna Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China inavyofanya kazi leo jijini Dar es salaam wakati wa kikao cha pamoja kilichowahusisha Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na China. Wengine  ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) na Jaji Kiongozi Mhe. Shaban Lila.  
 Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akipokea zawadi ya kinyago kutoka kwa Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman.
  Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman mbele ya Jengo la Mahakama ya Rufaa.
 Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Shaban Lila(kulia) akimweleza jambo jaji wa Mahakamu Kuu ya Jamhuri ya Watu wa China mara baada ya kumkaribisha Ofisini kwake Mahakama Kuu leo jijini Dar es salaam.
Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Shaban Lila(kulia) akiwa katika mazungumzo na Jaji wa Mahakama Kuu ya China na baadhi ya Majaji kutoka  Mahakama hiyo waliomtembelea Ofisini kwake Mahakama Kuu jijini Dar es salaam.
 Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang (wa pili kutoka kushoto mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman (katikati) na baadhi ya watendaji wa Mahakama ya Tanzania mbele ya Jengo la Mahakama ya Rufaa leo jijini Dar es salaam.
 Jaji wa Mahakama Kuu ya Watu wa Jamhuri ya China, Mhe. Zhang ( kushoto) akiagana na  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman (kulia) mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo naye leo jijini Dar es salaam. Picha/Aron Msigwa.
……………………………………………………………………………………
Na Mwandishi- Mahakama ya Tanzania
Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Juu Nchini China Mheshimiwa Zhang Jiannan yuko Nchini kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuimarisha uhusiano na ushirikiano uliopo baina ya nchi za Tanzania na China.
Katika ziara yake Nchini, Mheshimiwa Jiannan ambaye anamwakilisha Jaji Mkuu wa China, leo alikutana na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman na kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi wa Mahakama zao.
Akizungumzia changamoto za Mahakama nchini China, Mheshimiwa Jiannan alisema hivi sasa Mahakama za China zinakabiliwa na upungufu wa Majaji ikilinganishwa na idadi ya kesi zinazosajiliwa.
Kwa Upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania alisema baadhi ya changamoto zinazoikabili Mahakama ya Tanzania ni pamoja na upungufu wa Mahakama za mwanzo.
Alisema ili kukabiliana na upungufu huo, Tanzania inahitaji kuwa na Mahakama za Mwanzo 3000 nchi nzima. Hivi sasa kuna Mahakama za Mwanzo karibu 960 nchini kote ambazo hazitoshi ikilinganishwa na Idadi ya kata zilizopo Nnchi mzima.Jaji Mkuu wa Tanzania alimshukuru Jaji Mkuu Kiongozi wa China kwa kuitembele Mahakama ya Tanzania.
Katika ziara yake nchini, Jaji Jiannan ameongoza ujumbe wa Majaji na

Wizara yakemea mauaji ya mtoto sumbawanga

download (2)
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto inalaani vikali tukio La mauaji ya mtoto wa kike, umri miaka 9, ambaye alininajisiwa kwa zamu na watu wasiojulikana, na hatimaye kumkata mapanga yaliyosababisha kuuawa kwa mtoto huyo mdogo, katika kijiji cha Kapanga, wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa.

WANAFUNZI 65 WA SHULE YA SEKONDARI CHALINZE WANUSURIKA KIFO BAADA YA BWENI LAO KUTEKETEA KWA MOTO

images (1) 
VICTOR MASANGU, BAGAMOYO
WANAFUNZI  65 wa shule ya sekondari chalinze iliyopo Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wamenusurika kupoteza maisha baada ya bweni moja la kulalia  kuteketea kabisa  kwa moto wakati wao wakiwa darasani kwa ajili ya kujisomea masomo ya usiku  

Madiwani Wete Kisiwani Pemba wala kiapo kupambana na wakwepa kodi

8022
Na Masanja Mabula –Pemba
MADIWANI wa wadi kumi zinazounda Baraza la Mji Wete Kisiwani Pemba  , wamekula kiapo cha utii na kuahidi kushirikiana na Uongozi wa Baraza hilo katika kupambana na wafanyabiashara wanaokwepa kulipa kodi
Watendaji wengine wa Mahakama wanne kutoka nchini China.

Halmashauri yatenga bajeti ya milioni 162 kuisaidia shule ya walemavu

03 mnazi mmoja Lindi
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Halmashauri ya Wilaya ya Lindi iliyopo Mkoa wa Lindi imetenga jumla ya shilingi milioni 162 katika mwaka wa fedha 2016/17 kwa ajili ya kuisaidia shule ya Msingi Nyangao.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi. Olliver Vavunge alipokuwa akikanusha kuhusu madai ya wazazi kutaka shule hiyo ifungwe kwa sababu ya ukosefu wa huduma muhimu

Uchukuzi SC netiboli kuivaa CDA Dodoma kesho


UC2 
Kocha wa soka Elutery Muholeli (wanne kulia) mwenye jezi za manjano akitoa maelekezo kwa wachezaji.
UC3
Mazoezi mpira wa Netball  yakiendelea 
UC4 
Matalena Mhagama (mwenye fulana nyeupe kulia) akisubiri mpira.
…………………………………………………………………………………………………………
Mwandishi Wetu
TIMU ya netiboli ya Uchukuzi SC iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kesho itarusha karata yake ya kwanza kwa kuumana na wenyeji CDA Dodoma katika mchezo wa netiboli, utakaofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri..

CHIKAWE ATEULIWA BALOZI WA TANZANIA NCHINI JAPAN


CHIKAIMG-20160418-WA0070

Taasisi ya Graca Machel mdau muhimu wa elimu ya mtoto wa kike nchini, ikiwa na lengo la kuielimisha jamii.

GRANa Eleuteri Mangi-MAELEZO
Mtoto huanza kujifunza kulingana na mazingira yake yanayomzunguka, mafunzo hayo yanamuwezesha kupata uzoefu wenye athari ya kujenga akili, tabia ama uwezo wa kimaumbile ili aweze kuyamudu mazingira yake

TAMKO KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI LILILOTOLEWA NA MHE. UMMY MWALIMU WAZIRI WA AFYA LEO

um1
Kama mnavyofahamu, Serikali kupitia Wizara yangu imeweka utaratibu wa kutoa kila wiki taarifa ya mwenendo wa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu nchini  ili kuifahamisha jamii hali ilivyo na hatua zinazochukuliwa na Wizara  kudhibiti ugonjwa huu. Hadi kufikia tarehe 17 April 2016, jumla ya wagonjwa 20,882 wametolewa taarifa, na kati ya hao ndugu zetu 329 wamepoteza maisha tangu ugonjwa huu uliporipotiwa Agosti 2015.

Meneja wa bondia Francis Cheka “Chief Ndambile” awania ukatibu mkuu Kifa


ni1
Mkurugenzi wa Kampuni ya Advanced Security  Limited, Juma Ndambile ambaye pia ni meneja wa bondia Francis Cheka  akimwaga sera baada ya kupitishwa kuwania nafasi ya Ukatibu Mkuu kwa Chama Cha Soka cha Manispaa ya Kinondoni (KifA)
ni2
Mkurugenzi wa Kampuni ya Advanced Security  Limited, Juma Ndambile (wa kwanza kushoto) akiwa na bondia wake Francis Cheka  wakati wa kukabidhi mkanda wa ubingwa Super Middle kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Nape Nnauye (wa kwanza kulia).

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AZINDUA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MKOANI MOROGORO LEO

ng1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Mwenge wa Uhuru kiongozi wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2016  George Jackson Mbijima kutoka mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kukimbiza mwenge huo katika Mikoa na wilaya zote za Tanzania.
ng2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasha  Mwenge wa Uhuru kuzindua rasmi mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2016 leo Aprili 18, 2016  sherehe iliyofanyika katika uwwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro. Kulia ni Waziri wa Uwezeshaji Ustawi wa Jmii, Vijana, Wanawake na Watoto –  Zanzibar Mhe. Modelin Kastiko.
ng3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Taifa kwenye Sherehe za uzinduzi wa Mwenge wa Uhuru kitaifa zilizofanyika leo april 18, 2016 katika Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.
ng4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Taifa kwenye Sherehe za uzinduzi wa Mwenge wa Uhuru kitaifa zilizofanyika leo april 18, 2016 katika Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.
ng5
Halaiki
(Picha na OMR)

CCM Z’BAR YATAKA WAHANGA WA MAFURIKO WASAIDIWE.

7 
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewataka viongozi wa serikali na chama kuharakisha kutoa misaada kwa waathirika wa mafuriko bila ya kujali tofauti zao za kisiasa.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vuai wakati akitembelea maeneo mbali mbali ya Zanzibar yaliyoathiriwa na mafuriko hayo

KICHUYA MCHEZAJI BORA MWEZI MACHI

Mshambuliaji Shiza Ramadhan Kichuya wa timu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Machi kwa Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu wa 2015/2016.
Kichuya alionyesha kiwango cha juu katika mwezi huo uliokuwa na raundi nne, hivyo kuisaidia timu yake kushinda mechi mbili kati ya tatu ilizocheza.
Katika mechi hizo ambazo zote Kichuya alicheza, alifanikiwa kufunga mabao mawili kati ya matano yaliyofungwa na timu yake. Alifunga dhidi ya Coastal Union kwa ushindi wa mabao 3-0, na JKT Ruvu Stars ambapo Mtibwa Sugar ilishinda mabao 2-1.
Uwezo aliouonyesha kwa mwezi huo ulisababisha Kocha wa Taifa Stars, Charles Mkwasa amwite kwa mara ya kwanza kwenye kikosi chake kwa ajili ya mechi dhidi ya Chad iliyofanyika Machi 23, 2016 jijini N’Djamena.
Washindani wa karibu wa Kichuya walikuwa washambuliaji Mbaraka Yusuf wa Kagera Sugar, na Abdulrahman Mussa wa JKT Ruvu Stars ambao pia waling’ara kwa upande wa timu zao kwa mwezi huo.
Kichuya ambaye huu ni msimu wake wa pili kwenye Ligi Kuu, kwa kunyakua tuzo ya mchezaji bora kwa Machi atazawadiwa kitita cha sh. 1,000,000 (milioni moja) na wadhamini wa Ligi hiyo, kampuni ya Vodacom.
Wachezaji bora wa miezi mitatu iliyopita ni kiungo Thaban Kamusoko wa Yanga (Desemba 2015), beki Shomari Kapombe wa Yanga (Januari 2016) na mshambuliaji Mohamed Mkopi wa Tanzania Prisons (Februari 2016).

TFF YALAANI VURUGU ZA MASHABIKI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limelaani kitendo cha baadhi ya mashabiki wa mpira wa miguu kufanya vurugu mara baada ya mchezo kati ya Simba SC dhidi ya Toto Africans uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
TFF imesikitishwa na kitendo hicho cha mashabiki wa klabu ya Simba SC, na kusema inalaani kitendo hicho ambacho sio cha kiuana michezo, huku ikiwataka wanachama, washabiki kuheshimu viongozi wa klabu zao waliopo madarakani na kama kuna masuala ya kujadili wakayajadili katika vilabu vyao.
Mashabiki wa klabu ya Simba walifanya vurugu kwa kurusha mawe, wakilenga kuwadhuru viongozi wa klabu hiyo pamoja na wachezaji, magari waliyokuwa nayo baada ya timu yao kupoteza mchezo dhidi ya Toto Africans kwa bao 1- 0.
Jeshi la Polisi baada ya kuwasishi mashabiki kuondoka eneo la uwanja punde tu mchezo ulipomalizika, mashabiki hao walikaidi na kuendelea kurusha mawe hali iliyopelekea jeshi kutumia mabomu ya machozi kuwatanya katika eneo hilo.
Kufutia kitendo hicho, Jeshi la Polisi lilihakikisha bus la timu ya Simba SC na viongozi wake wanaondoka salama uwanjani baada ya kuwatawanya mashabiki hao, kwa kupitia mlango wa karakana ya wachina waliojenga uwanja huo.
Aidha TFF imeviomba vyombo vya Usalama na Ulinzi kuwachukulia hatua kali mashabiki waliohusika na kitendo hicho, kwani kufanya vurugu ni kosa la jinai na wanapaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

PIZZA HUT OPENS IT’S FIRST STORE IN DAR ES SALAAM, TANZANIA

pizza1
Vikram Desai Pizza Hut Owner adressing  Journalist  at Mkuki Mall in Dar es salaam last week.
pizza2 
Pizza Hut, a division of Yum! Brands, the world’s largest restaurant company, today announced the opening of its first restaurant in Tanzania.
Pizza Hut is the world’s largest pizza chain with $12 billion in global sales and more than 15,000 restaurants in over 90 countries.
Dough Works Ltd, the franchise holders of Pizza Hut for Tanzania, has worked very hard in securing Pizza Hut’s placement in the country, which shows the confidence from Yum! Brands in the Tanzanian economy and the investors of Dough Works Ltd.
Dough Works Ltd has committed to a multi million dollar investment in the Pizza Hut brand and the launch of it’s first of many stores, which is located at the newly built Mkuki Mall on Nyerere Road, Dar es Salaam.
The company has plans for rapid expansion and growth with a target of over 30 stores across the country, creating over 500 new jobs in the Quick Service Restaurant sector.
Dough Works Ltd Director Vikram Desai says “We would like to thank all the regulators and vendors for being very supportive and extending guidance on the opening of Pizza Hut in Tanzania and we look forward to working together very closely on building the QSR sector in the country.”
The new Pizza Hut restaurant features ultra-modern design, digital menu boards, a children’s play area, and indoor/outdoor seating for over 80 people.

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO MHE. SAIDI MECK SADIKI ATEMBELEA LANGO LA LONDOROSI HIFADHI YA TAIFA KILIMANJARO

mec1 
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh. Saidi Meck Sadiki   (watatu kutoka kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Siha Dk. Charles Mlingwa ( wa kwanza kulia) wakiwasili katika lango la Londorosi, Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro. Katikati ni mwenyeji wao Betrita Loibooki, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro.
mec2 
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro akiwasilisha taarifa fupi ya Hifadhi ya Kilimanjaro kwa Mkuu wa  Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Saidi Meck Sadiki akiwa katika lango la Londorosi.
mec3 
Mkuu wa Idara ya Utalii Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro, Charles Ngendo akionyesha maeneo ya hifadhi kwenye ramani kufafanua taarifa ya Mkuu wa Hifadhi.
mec4 
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Saidi Meck Sadiki akiongea na watumishi wa hifadhi, wilaya na mkoa katika lango la Londorosi.
mec5 
Watumishi wa Hifadhi ya Kilimanjaro, Wilaya ya Siha na Mkoa wa Kilimanjaro wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.
mec6Akiongozwa na Mhifadhi Imani Kikoti, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro alipata fursa ya kutembea kwa miguu kupanda mlima kuelekea uwanda wa Shira.
mec7 
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na ujumbe wake kutoka mkoani na Wilaya ya Siha wakipewa maelezo juu ya vivutio  na jiolojia ya uwanda wa Shira kutoka  kwa Charles Ngendo, Mhifadhi Utalii wa Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro.
mec8 
Picha ya pamoja ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro alipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro. Hapa akionekana na msafara wake na viongozi wa hifadhi ya Kilimanjaro wakiwa uwanda wa Shira (mita 3962)

No comments :

Post a Comment