Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki CEAC) na Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Salva
Kiir Mayardit wakati Rais Kiir wakibadilishana hati za makubaliano ya
kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki mara baada ya kusaini
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC) akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzanua Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati na Waziri Mkuu Mh. Majaliwa
Kassim Majaliwa wakimsubiri Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Salva
Kiir Mayardit wakati Rais Kiir alipowasili Ikulu na kupokelewa na kwa
ajili ya kutia kusani mkataba wa kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki
Leo April 15,2016.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzanua Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Rais wa
Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir Mayardit wakati Rais Kiir
alipowasili Ikulu na kupokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC) kwa ajili ya kutia kusani mkataba wa kujiunga na
Jumuiya ya Afrika Mashariki Leo April 15,2016.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzanua Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Rais wa
Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir Mayardit wakati Rais Kiir
alipowasili Ikulu na kupokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC) kwa ajili ya kutia kusani mkataba wa kujiunga na
Jumuiya ya Afrika Mashariki Leo April 15,2016, Kushoto ni Waziri Mkuu
Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa.
Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir Mayardit akikagua gwaride la heshima wakati Rais Kiir alipowasili Ikulu leo.
Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini
Mhe. Salva Kiir Mayardit wakati Rais Kiir akiwapungia mikono viongozi
mbalimbali huku akiongozana na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano
ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Afrika Mashariki (EAC) wakati alipowasili Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki CEAC) na Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Salva
Kiir Mayardit wakati Rais Kiir wakibadilishana hati za makubaliano ya
kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki mara baada ya kusaini
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC), Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini Mhe. Salva Kiir
Mayardit wakati Rais Kiir. Makamu wa Rais Mh. Mama Samia Hassan Suluhu
na Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa wakiwa katika picha ya
pamoja na viongozi mbalimbali waliohudhuria katika hafla hiyo ya utiaji
saini.
SASA TUKO KWENYE KIWANGO KIZURI:KINNAH
Kocha
Mkuu wa Mbeya City Fc Mmalawi Kinnah Phiri amesema sasa ana uhakika
nyota wake wako kwenye kiwango kizuri kufuatia matokeo ya ushindi wa
jumla ya bao 5 kwenye michezo miwili iliyopita kwenye mfululizo wa
mechi za ligi kuu ya Soka Tanzania Bara inayoelekea ukingoni hivi
sasa.
Akizungumza na mbeyacityfc.com
asubuhi ya leo kocha Phiri ameweka wazi kuwa ushindi wa 4-0 dhidi ya
Coastal Union na ule wa 1-0 dhidi ya Mgambo JKT mwishoni mwa juma
lililopita umempa imani kubwa kuwa wachezaji wake sasa wameanza
kuielewa vyema falsafa yake hasa kwa kuweza kufanikisha ushindi bila
kuruhusu kufungwa bao katika michezo hiyo miwili.
Tulianza kucheza kwa mchezo wa kawaida sasa tumeongeza, tunacheza kwa spidi kubwa wachezaji wangu sasa wanajiamini kwa kiwango kikubwa, tumefunga bao 5 bila kuruhusu kufungwa bao lolote, hili ni uhakika tosha kuwa kikosi changu sasa kiko imara kwenye ulinzi na pia kiko vizuri kwenye ufungaji, kwa sasa tuko kwenye mipango mizito kuhusina na mchezo ujao, alisema.
Akiendelea zaidi kocha huyo
aliyewahi kuifundisha kwa mafanikio timu ya taifa ya Malawi alisema
kuwa mara baada ya kurejea kutoka jijini Tanga kwenye mchezo dhidi ya
Mgambo JKT alitoa siku chache za mapumziko kwa wachezaji wake na
kuwataka kujiandaa kwa mazoezi yatakayoanza siku ya jumatatu tayari
kwa mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar uliopangwa kuchezwa mwishoni mwa
mwezi huu.
Baada ya Tanga, nilitoa mapumziko ya siku saba, vijana watarejea jumatatu tayari kwa mazoezi kabla ya kuivaa Mtibwa, nina imani siku saba zitatosha kuwaweka sawa kwa ajili ya mchezo huo, Sifahamu sana kuhusu timu hiyo ya Morogoro, kwenye ratiba inaonyesha watacheza kesho ninaweza kufika kuwaona au nitatumia muda kuangalia mchezo wao kwenye TV, nataka kujua baadhi ya mambo muhimu ili nijiandae vizuri kuweza kupata ushindi.
TAARIFA YA UFAFANUZI KUHUSU MKATABA WA LUGUMI
Ofisi ya Bunge inapenda kutoa
ufafanuzi kuhusu jambo hili kwamba, taarifa hizo si za kweli na zina
lengo la kupotosha umma kutokana na kile kilicho amuliwa na kamati hiyo.
Ukweli kuhusu jambo hili ni kwamba tarehe 5 Aprili, 2016, kamati hiyo
ilikutana na kujadili Taarifa ya Ukaguzi wa hesabu zilizokaguliwa za
fungu 28, Jeshi la Polisi kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2014
ambapo kamati pamoja na mambo mengine ilibaini dosari katika utekelezaji
wa mkataba huo.
Kutokana na dosari hizo, kamati
iliomba Afisa Masuhuli ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi kuwasilisha maelezo ya kina kwa maandishi kuhusu utekelezaji wa
mradi huo kwa Ofisi ya Katibu wa Bunge ili kamati iweze kuchambua na
kujadili maelezo hayo kabla ya kupendekeza kwa Bunge hatua zaidi za
kuchukua. Kufuatia agizo hilo, kamati ilimwandikia pia Katibu wa Bunge
taarifa kuhusu agizo hilo tarehe 12 Aprili, 2016 ili kupatiwa maelezo
hayo kutoka kwa Afisa Masuhuli.
Aidha, Ofisi ya Bunge
ilimwandikia barua Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani tarehe 12
Aprili, 2016 kuwasiilsha Taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya Kamati
Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyotokana na kikao hicho
cha tarehe 5 Aprili 2016 kabla ya tarehe 18 Aprili, 2018 kama
ilivyoshauriwa na kamati . Hivyo ni vyema Umma ukafahamu kuwa
kilichoombwa na Kamati ni Maelezo ya utekelezaji wa Mkataba huo na sio
Mkataba kama inavyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya Habari ambapo Ofisi
ya Bunge iliomba maelezo hayo yawasilishwe kabla ya tarehe 18 Aprili,
2016. Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano Ofisi ya Bunge
DAR ES SALAAM 15 Aprili, 2016.
MOUNT KILIMANJARO WON AFRICA’S LEADING TOURIST ATTRACTION AWARD IN 2016.
Mount
Kilimanjaro, the highest mountain in Africa, and the highest
free-standing mountain in the world, was declared Africa’s leading
tourist attraction in 2016 during the World Travel Awards Africa and
Indian Ocean Gala Ceremony in Zanzibar. The red carpet event attended by
hundreds of tourism industry leaders was hosted by Diamonds La Gemma Dell’est,Nungwi the northern tip of Zanzibar, Tanzania on 9th April 2016.
Tanzania Tourist Board is
honoured to see that Mt. Kilimanjaro has been voted as the leading
tourist destination in Africa. This nomination will definitely
contribute towards our efforts in promoting Destination Tanzania,
especially in making the world know that Tanzania is home to Mt.
Kilimanjaro; the pinnacle wonder of Africa, and as many know, it is
affectionately known as the rooftop of Africa.
Mount Kilimanjaro is the world’s most accessible high snow–capped summit, a beacon for visitors from around the world and is also a UNESCO World Heritage Site.
In addition to Mt. Kilimanjaro, the following Tanzanian tourism companies also won different awards in various categories. http://www.worldtravelawards.com/about
Tanzania Tourist Board
congratulates all companies nominated at the World Travel Awards Africa
& Indian Ocean Gala Ceremony and is confident that their victory is a
very strong tool in the marketing and promotion of destination
Tanzania. Likewise, Tanzania Tourist Board thanks all tourism
stakeholders for voting for Mount Kilimanjaro and other Tanzania tourism
facilities and making them become winners.
———————-
World Travel Awards™ was
established in 1993 to acknowledge, reward and celebrate excellence
across all key sectors of the travel, tourism and hospitality industry.
Today, the World Travel Awards™ brand is recognized globally as the
ultimate hallmark of quality, with winners setting the benchmark to
which all others aspire.
Each year World Travel Awards™
covers the globe with a series of regional gala ceremonies staged to
recognize and celebrate individual and collective successes within each
geographical region.
Issued by
TANZANIA TOURIST BOARD
Wanarorya watakiwa kuwekeza Rorya.
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
15DAR ES SALAAM
Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Felix Lyaniva
ametoa wito kwa wanarorya wanaoishi Jijini Dar es salaam kuwekeza kwenye
fursa zilizopo katika wilaya hiyo iliyopo mkoani Mara.
Ameyasema hayo leo Jijini Dar es salaam
alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu mkutano wa wanarorya
wanaoishi Da es salaam utakaofanyika katika ukumbi wa Karimjee siku ya
jumapili Februari 17, 2016 kuanzia saa nane mchana.
“Wilaya yetu ya Rorya ina fursa nyingi za
uwekezaji zikiwemo za biashara, ardhi yenye rutuba, gesi asilia, mifugo
pamoja na misitu, lakini pamoja na kuwa na fursa za rasilimali zote hizo
bado ni miongoni mwa wilaya ambazo ziko nyuma kimaendeleo hivyo
tunahitaji wanarorya wachukue hatua” alisema Mhe. Lyaniva.
Mhe. Lyaniva ameongeza kuwa licha ya wilaya
ya Rorya kupiga hatua na kuwa Halmashauri haijawa na kasi ya
kuridhisha kutokana na wanarorya waishio nje ya wilaya hiyo kutoshiriki
ipasavyo kwenye fursa za kiuchumi na kwenye utatuzi wa changamoto
mbalimbali zinazoikabili wilaya hiyo.
Aidha, Mhe. Lyaniva ameelezea baadhi ya
changamoto zinazowakumba wananchi wa Rorya zikiwemo za ugonjwa wa
Ukimwi, njaa pamoja na ukosefu wa huduma bora za kijamii kama vile maji
safi na salama, barabara, Hospitali, shule, vyuo vya ufundi pamoja na
vituo vya kutosha vya ulinzi na usalama kwa upande wa Jeshi la Polisi.
Kabla ya mwaka 2007 Rorya ilikua sehemu ya
Wilaya ya Tarime, kwa sasa Rorya imekua wilaya mojawapo kati ya wilaya
nne zilizopo Mkoani Mara.
Dk.Abdalla Possi mgeni rasmi matembezi ya hiyari kuazimisha siku ya watoto wenye usonji
Mwenyekiti wa Chama cha Kuhudumia
Watu Wenye Usonji Tanzania (NAPAT) Dkt.Stella Rwezaula(wa tatu kulia)
akiongea na waandishi wahabari kuhusu matembezi ya hiyari kuadhimisha
siku ya usonji Aprilli 16, kushoto ni Katibu wa Chama cha Kuhudumia Watu
Wenye Usonji (NAPAT) Bi. Ella Mgalla na wengine ni wajumbe.(Picha na
Lorietha Laurence-Maelezo)
…………………………………………………………………………………………………..
Na Lorietha Laurence-Maelezo
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu
Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Dk.Abdalla Possi
anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika matembezi ya hiyari ya kuazimisha
siku ya watoto wenye usonji Aprili 16 mwaka huu.
Akiongea na waandishi wa habari
leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Chama cha Kuhudumia Watu Wenye
Usonji Tanzania (NAPAT) Dkt.Stella Rwezaula ameeleza kuwa lengo la
matembezi hayo ni kutoa elimu kwa jamii kuhusu watu wenye matatizo ya
Usonji.
“Jamii imekuwa ikiwanyima uhuru
watu wenye usonji kwa kuwafungia ndani na hivyo kuwanyima haki zao za
msingi ikiwemo kupata elimu ” alisema Dkt.Rwezaula.
Aliongeza kuwa watu wenye
matatizo ya usonji wanapopatiwa msaada wa haraka na unaostahili ikiwemo
huduma ya afya husaidia kuimarisha hali zao na baadaye kuwa msaada
katika jamii yake.
“Usonji ni tatizo linalotokana na
hitilafu katika ukuuaji wa ubongo wa mtoto na kupelekea mtoto kuwa na
matatizo katika mawasiliano na mahusiano ya kijamii na utambuzi lakini
linapogundulika haraka inasaidia kuimarisha hali ya mtoto“ alisema
Dkt.Rwezaula.
Naye Katibu wa Chama cha
Kuhudumia Watu Wenye Usonji (NAPAT) Bi. Ella Mgalla ametoa wito kwa
wazazi kuwasaidia watoto wenye usonji kwa kuwapeleka katika shule
maalum ili waweze kupata elimu.
Pia ameeleza kuwa changamoto
kubwa wanayokumbana nayo ni ukosefu wa waalimu maluum wa kuwafundisha
watoto wenye usonji pamoja na upungufu wa shule maalum ambapo mpaka
sasa kuna shule 8 Tanzania nzima.
“Ninaiomba serikali iweze
kutusaidia kwa kutoa mafunzo maalum kwa waalimu ambao watakuwa
wakiwahudumia watoto wenye matatizo ya usonji na kuongeza idadi ya shule
ambapo kwa sasa ni mikoa minne tu inayotoa huduma hiyo ikiwemo Dar es
Salaam shule mbili, Arusha shule nne, morogoro shule moja na Mwanza
shule moja” alisema Bi.Mgalla
Chama cha Kuhudumia Watu Wenye
Usonji (NAPAT) kimeanzishwa mwaka 2012 kikiwa kinajumuisha wanachama 53
ambao ni wazazi, walezi na waalimu wa watoto wenye usonji.
WIZARA YAKEMEA MAUAJI YA WAZEE NZEGA
Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na watoto imesikitishwa na kulani viakli matukio ya
mauaji ya wazee kumi (10) yaliyotokea wilaya ya Nzega, mkoani Tabora
kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi, 2016.
Inaelezwa kuwa, miongoni mwa
chanzo cha mauaji ya wazee ni imani za kishirikina, uchu wa kumiliki
mashamba na visasi mambo ambayo Serikali imekuwa ikiyakemea vikali.
Wizara inawataka wananchi kushirikiana na uongozi wa Wilaya ya Nzega,
kuhakikisha kuwa watuhumiwa wa mauaji haya wanakamatwa na kuchukuliwa
hatua kali ili kuwa fundisho kwa watu wengine.
Wizara inasisitiza kwamba wazee
ni binadamu, na wanayo haki ya kuishi na kupata hifadhi ya maisha yao
kwa mujibu wa Sheria za nchi. Vitendo vya mauaji ya kikatili
wanavyofanyiwa wazee vinasababisha hofu kubwa kwa wananchi. Mauaji hayo
yanawakosesha amani na vinadhohofisha ari ya kufanya shughuli za za
maendeleo ya familia na taifa kwa ujumla. Familia inayoishi na mzee
anayewindwa, itatumia muda mwingi kutekeleza jukumu la ulinzi na hivyo
kupunuza tija na uzalishaji wa mwananchi mmoja na familia kawa ujumla.
Kwa kutambua hili Wizara inahimiza wadau wote kuunga mkono jitihada za
Serikali katika ulinzi wa wazee na kuboresha huduma zao ili kuelekeza
nguvukazi katika uzalishaji.
Wizara inapenda kutoa pole kwa
familia ambazo zimeguswa na mauaji ya wazee waliopoteza maisha kwa
kuuawa kinyama. Wizara inaitaka jamii itambue kuwa wazee wana haki ya
kuthaminiwa utu wao, kupata huduma stahiki, na kushiriki haki zote za
msingi bila ubaguzi wowote ambao unaweza kuhatarisha maisha yao ikiwemo
haki yao ya kuishi. Aidha, Jamii ihakikishe kuwa wazee na wananchi wote,
wanaishi katika hali ya usalama, amani na utulivu kwa ajili ya
maendeleo na ustawi wa Taifa letu.
Erasto T. Ching’oro (Msemaji)Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
15/4/2016
WABUNGE WAPONGEZA KUANZISHWA KWA TADB
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,
Mifugo na Uvuvi, Dkt. Florens Turuka (Kulia) akizungumza mbele ya Kamati
ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakati wa kikao cha pamoja kati ya
Kamati hiyo na viongozi kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na
menejimenti ya TADB.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TADB, Dkt. Anaclet Kashuriza (Aliyesimama) akizungumza
mbele ya Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakati wa kikao cha
pamoja kati ya Kamati hiyo na viongozi kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo
na Uvuvi na menejimenti ya TADB.
Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa
Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakifurahia jambo wakati wa
kikao cha pamoja kati ya Kamati hiyo na viongozi kutoka Wizara ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi na menejimenti ya TADB.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa TADB,
Bw. Thomas Samkyi (Kulia) akizungumza mbele ya Kamati ya Bunge ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakati wa kikao cha pamoja kati ya Kamati hiyo
na viongozi kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na menejimenti ya
TADB.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Mary Nagu (Katikati) akifuatilia
maelezo yaMkurugenzi Mwendeshaji wa TADB (hayupo pichani) wakati wa
kikao cha pamoja kati ya Kamati hiyo na viongozi kutoka Wizara ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi na menejimenti ya TADB.
Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa
Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakitoa michango yao wakati
wa kikao cha pamoja kati ya Kamati hiyo na viongozi kutoka Wizara ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi na menejimenti ya TADB.
Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa
Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakitoa michango yao wakati
wa kikao cha pamoja kati ya Kamati hiyo na viongozi kutoka Wizara ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi na menejimenti ya TADB.
Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa
Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakitoa michango yao wakati
wa kikao cha pamoja kati ya Kamati hiyo na viongozi kutoka Wizara ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi na menejimenti ya TADB.
………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi wetu
Wabunge wa Kamati ya Bunge ya
Kudumu ya Kilimo, Mifugo na Maji imeipongeza Serikali kwa kuanzisha kwa
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) yenye lengo la Kusaidia
upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini
Tanzania na kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo
cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi
na kupunguza umaskini.
Wakizungumza na viongozi kutoka
Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na menejimenti ya TADB wakati wa vikao
vya kamati za Bunge vinavyoendelea jijini Dar es Salaam. Wabunge hao
wamesema kuwa TADB imekuja wakati muafaka kwa kuwa itachagiza juhudi za
kuinua na ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini nchini Tanzania.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe.
Dkt. Mary Nagu amesema kuwa licha ya umuhimu wa Sekta ya Kilimo, bado
ukuaji wa sekta hiyo ulikuwa ukikabiliwa na changamoto mbali mbali kuu
ikiwa ni Ufinyu mkubwa wa upatikanaji wa fedha mikopo kwa ajili ya
maendeleo ya kilimo nchini.
“Kwa kweli tunapongeza kwa
kuanzishwa Benki hii kwa kuwa kwa miaka mingi mikopo mingi kutoka
taasisi za fedha imekuwa ikielekezwa zaidi kwenye upande wa biashara za
bidhaa na kuwa na riba kubwa kwenye mikopo ya kilimo,” alisema Mhe.
Nagu.
Wabunge hao wametoa wito kwa Serikali kuiongezea mtaji Bnki hiyo ili kuongeza kasi ya utendaji kazi wa Benki hiyo.
Akizungumza kwenye kikao hicho,
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Florens Turuka
alisema kuwa TADB inajihusisha na aina zote za kilimo kwa ule wigo mpana
wa maana ya kilimo, ambao inahusisha mazao, ufugaji, uvuvi, na bidhaa
zitokanazo na misitu. Na kuongeza kuwa katika kusaidia minyororo ya
thamani ya mazao ya kilimo, TADB itakuwa inatoa fedha kwenye hatua mbali
mbali za Uzalishaji na uongezaji wa thamani kama vile Uzalishaji wa
awali; uhifadhi; usindikaji; uchakataji; usafirishaji; na masoko.
“Uanzishwaji wa Benki ya
Maendeleo ya Kilimo Nchini kama taasisi ya maendeleo ya fedha,
kulitokana na Wizara yangu, na baadaye mawazo ya Wadau mbalimbali chini
ya uratibu wa Baraza la Taifa la Biashara kuhusu jinsi Tanzania
inavyoweza kufikia mapinduzi ya kilimo,” aliongeza Dkt. Turuka.
Kwa mujibu wa Dkt. Turuka,
katika maazimio kumi (10) ya Kilimo Kwanza yaliyofikiwa mwaka 2009,
azimio la tatu lilikuwa kuanzishwa kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo.
Hivyo uanzishwaji wa benki hii ni muendelezo wa Serikali katika kutimiza
na kutekeleza maazimio ya “KILIMO KWANZA”. Hii ilitokana hasa na
kuwepo kwa changamoto mbali mbali kwenye Sekta ya Kilimo ikiwemo
upatikanaji wa fedha na mikopo ya riba nafuu katika kuendeleza sekta ya
kilimo nchini kwa miradi mikubwa ya kilimo, ya kati na midogo inayolenga
kuimarisha minyororo ya thamani ya Kilimo.
Naye Mkurugenzi Mwendeshaji wa
TADB, Bw. Thomas Samkyi alisema kuwa kama yalivyo matarajio ya Serikali,
kuanzishwa na kuanza kufanya kazi kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo
Nchini, kunategemewa kuwa na umuhimu wa kusaidia upatikanaji wa mali
ghafi kwa viwanda vya ndani hivyo kusukuma ndoto ya Serikali kufikia
lengo lake la Kujenga Uchumi wa Viwanda.
Ameongeza pia TADB inatarajia
kuhuisha uwekezaji kwenye Viwanda vidogo vidogo na vya kati vya
usindikaji na uchakataji wa mazao ya Kilimo na mifugo pamoja na
kuboresha kwa upatikanaji wa mikopo na huduma za kifedha kwenye miradi
ya maendeleo ya Kilimo kwa riba nafuu zilizo chini ya viwango vya
kibiashara kwenye soko.
Benki ya TADB ni mali ya Serikali
kwa Asilimia 100 ya Hisa na kwa kuzingatia muundo wa uendeshaji wa
shughuli za Serikali hususan kwenye masuala ya kifedha, Benki ya
Maendeleo ya Kilimo iko chini ya Wizara ya Fedha na Mipango. Hali
kadhalika, benki iko chini ya Uangalizi wa Msajili wa Hazina kama
yalivyo mashirika mengine ya Umma. Hata hivyo, kiutekelezaji, TADB
inajihusisha moja kwa moja na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, kwani
muktadha wa uanzishwaji wake umelenga moja kwa moja kwenye Sekta ya
Kilimo kuliko Sekta nyingine yoyote.
Wakazi Dar ‘kuonja’ daraja la Kigamboni bure kesho
Wakazi wa jiji
la Dar es Salaam na vitongoji vyake kesho wanatapa fursa ya kulitumia
kwa mara ya kwanza Daraja la Kigamboni linalotarijiwa kufunguliwa rasmi
na Rais John Pombe Magufuli siku ya Jumanne ya wiki ijayo ili ‘kuonja’
na kujionea ubora wa daraja hilo kisasa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja mradi kutoka kampuni ya China
Railway Construction Engineering Group ambao wametekeleza mradi huo kwa
ushirikiano na kampuni ya China Railway Major Bridge Group Bw. Zhang Bangxu, alisema siku ya kesho, wataruhusu wakazi hao na magari kupita katika daraja hilolililogarimu Dola za Kimarekani milioni 135 kujengwa.
“Kama wajenzi kesho tutaruhusu
magari kupita kwenda upande wa Kurasini na upande wa Kigamboni siku ya
Jumamosi tu kama ikiwa ni sehemu ya majaribio yetu kitaalamu ikiwa ni
pamoja na kutumia fursa hiyo kufanya majaribio ya mitambo na mashine
zote ambazo zitatumika katika kufanya tozo mbali mbali baada ya kuanza
rasmi kwa mradi,” alifafanua
Kwa mujibu wa Bw. Bangxu,
daraja la Kigamboni ndiyo daraja refu kuliko yote katika ukanda wa
Afrika Mashariki lililotengenezwa kwa kutumia teknolojia ya matumizi ya
kamba (cable) kubeba uzito wa daraja, ambayo itaunganisha jiji la
kibiashara la Dar es Salaam na eneo la Kigamboni na Kurasini. Ujenzi
ulianza mnamo Tarehe moja Februari mwaka 2012.
“Pamoja na kujengwa katika ubora
wa hali ya juu, daraja hili lina jumla ya njia sita yaani njia tatu kwa
kila upande, pamoja na njia mahususi kwa ajili ya waenda kwa miguu na
waendesha baiskeli ambayo ina upana wa mita 2 na nusu (2.5 meters)
katika kila pande. Daraja hilo litaruhusu magari yenye uzito usiozidi
tani 30 kupita.,’’ aliongeza
Bw. Bangxu alisema
kwamba kaskazini mwa daraja hilo, litaungana na barabara lenye urefu wa
kilometa moja ambayo inakatiza reli ya TAZARA kisha kuungana na
barabara ya Mandela. Kwa upande wa Kigamboni, daraja litaungana na
barabara lenye urefu wa Kilometa 1.5 ambayo inaungana na barabara ya
Kigamboni Ferry – Kibada.
Aliongeza kwamba kukamilika kwa
daraja hili ni ishara ya maendeleo kwani inatarajiwa kuchochea kasi ya
maendeleo ya mji wa kisasa wa Kigamboni (Kigambani satellite city),
kutengeneza fursa za ajira katika sekta ya ujenzi wa maeneo ya makazi
pamoja na sekta za huduma ambazo zitastahimili ongezeko kubwa wa idadi
ya wakazi wapya katika mji huo mpya.
Kukamilika kwa daraja hilo
kunatajwa kuwa kutawapafusra wakazi wa Kigamboni na viunga vyake ikiwa
ni kutoa njia mbadala ya kufikia makazi yao, biashara zao au shuguli zao
za ujenzi wa taifa kwa njia ya barabara.
Maeneo ya Kigamboni na Kurasini
kwa sasa hufikika kwa kutumia vivuko viwili vya MV Magogoni na MV
Kigamboni ambazo kwa pamoja zinaumezo wa kubebe abiria 1000 na magari 78
kwa kila safari.
Mradi huo umedhaminiwa kwa kwa
ubia kati ya Shirika la Hifadhi ya Jamii ya Taifa (NSSF) na Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
RAIS WA SUDANI KUSINI, MHE. JENERALI SALVA KIIR MAYARDIT AWASILI NCHINI
Rais wa Sudani Kusini, Mhe.
Jenerali, Salva Kiir Mayardit (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa
Dar es Salaam, Paul Makonda mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya
kikazi ya siku moja, 15 Aprili, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Sudani Kusini, Mhe.
Jenerali, Salva Kiir Mayardit (wa tatu kulia) akisalimiana na Kamanda
Mkuu wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Simon Siro mara
baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius
K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja, 15 Aprili, 2016
Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Sudani Kusini, Mhe.
Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye kofia nyeusi) akishuka katika
ndege ya Shirika la Kenya mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi
ya siku moja, 15 Aprili, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi
Augustine Mahiga (wa tatu kushoto) akiwa tayari kumpokea Rais wa Sudani
Kusini, Mhe. Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye fimbo) mara baada ya
kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K.
Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja, 15 Aprili, 2016
Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Sudani Kusini, Mhe.
Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye fimbo) akisalimiana na baadhi ya
viongozi waliokuja kumpokea mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya
kikazi ya siku moja, 15 Aprili, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Sudani Kusini, Mhe.
Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye fimbo) akipita katikati ya gwaride
la Jeshi mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja, 15
Aprili, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi
Augustine Mahiga (kushoto) akisalimiana na Rais wa Sudani Kusini, Mhe.
Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye fimbo) mara baada ya kuwasili
katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa
ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja, 15 Aprili, 2016 Jijini Dar es
Salaam.
Rais wa Sudani Kusini, Mhe.
Jenerali, Salva Kiir Mayardit (mwenye fimbo) akisalimiana na Katibu Mkuu
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Richard Sezibera (wa pili
kushoto) mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius K. Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja, 15
Aprili, 2016 Jijini Dar es Salaam.
MAKAMPUNI BINAFSI HAYAHUSIKI ULINZI WA NDANI OFISI ZA BANDARI.
Na Jacquiline Mrisho -MAELEZO
DAR ES SALAAM
Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imesema
kuwa makampuni binafsi ya ulinzi yanayofanya kazi bandarini hayahusiki
na ulinzi wa sehemu nyeti za za Mamlaka hiyo.
Akitoa ufafanuzi huo leo jijini Dar es
salaam, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka hiyo Bi. Janeth Ruzangi amekiri
kuwepo kwa makampuni yanayofanya kazi ya ulinzi bandarini na amefafanua
kuwa hayahusiki kwa namna yoyote ile kulinda sehemu za ndani za ofisi
zilizoko bandarini.
“Ninapenda kuwafahamisha wananchi kuwa
Bandari inalindwa na walinzi wa aina tatu ; Jeshi la polisi, Polisi
wasaidizi walioajiriwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (Auxilliary
Police) pamoja na walinzi wa Makampuni binafsi”
Ameongeza kuwa makampuni hayo yanalinda
maeneo ya nje ya bandari yakiwemo maegesho ya magari ya watumishi wa
mamlaka kama ilivyo kwenye ofisi nyingine.
Aidha,amefafanua kuwa Polisi wa bandari
walioajiriwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania wako kwa mujibu wa sheria
zilizotungwa na Bunge na wamepata baadhi ya mafunzo ya kipolisi.
Ikumbukwe kuwa agizo la kuwandoa walinzi wa
makampuni binafsi kwenye maeneo nyeti ya bandari lilitolewa na Waziri
Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa mwezi Februari mwaka huu alipofanya ziara ya
kushtukiza bandarini hapo.
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUHUSU MATUMIZI YA DARAJA LA KIGAMBONI
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano inapenda kutaarifu Umma kuwa Daraja la kigamboni litaanza
kutumika siku ya Jumamosi tarehe 16, Aprili, 2016 kuanzia saa 12:00
asubuhi.
Katika siku za mwanzo, magari
yatapita bila kulipia tozo hadi Serikali itakapokamilisha taratibu na
kutangaza utaratibu wa kulipia. Aidha, watembea kwa miguu na waendesha
baiskeli watavuka bure katika Daraja la Kigamboni. Hata hivyo maguta na
mikokoteni haitaruhusiwa kutumia daraja hilo kutokana na sababu za
kiusalama.
Magari yatakayoruhusiwa kupita
katika Daraja la Kigamboni katika siku hizo za mwanzo ni yale yenye
uzito usiozidi tani 10, hatua ambayo itasaidia kufuatilia mwenendo wa
upitaji wa magari katika daraja, barabara za juu (Interchange) katika
eneo la Kurasini, pamoja na kuhakikisha kwamba magari yanayotoka au
kuingia katika daraja hayasababishi msongamano wa magari katika Barabara
ya Nelson Mandela, Barabara ya Kilwa na maeneo mengine ya jiji. Baada
ya utaratibu kukamilika magari ya aina zote yenye uzito unaoruhusiwa
kisheria yataruhusiwa kupita katika daraja.
Mambo muhimu ambayo madereva na watumiaji wengine wa barabara wanatakiwa kuzingatia ni:-
- Kuzingatia sheria ya Usalama Barabarani ikiwa ni pamoja na kufuata mwendo kasi unaotakiwa ili kuepuka ajali na kuepuka uharibifu miundombinu ya daraja
- Kufuata alama za barabarani zilizowekwa katika ‘Interchange’ ya Kurasini ili kwenda kwenye uelekeo sahihi.
- Kuzingatia alama zilizowekwa kwenye milango (Toll Gates) ya Kituo cha kulipia tozo (Toll Plaza) ili kuepuka uharibifu wa miundombinu ya kituo hicho.
- Madereva na watumiaji wa barabara wengine watakaosababisha uharibifu wa aina yeyote wa miundombinu ya daraja watatozwa faini au kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria.
- Kutunza mazingira kwa kuepuka kutupa takataka katika eneo la daraja.
Aidha, Wizaraya Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano inawataka madereva wa magari ya mizigo wanaoegesha katika
barabara ya Nelson Mandela wakisubiri kuingia bandarini watafute eneo
stahiki la maegesho na kuyaondoa magari hayo kwani hatua za kisheria
zitachukuliwa kwa wale watakaoenda kinyume na agizo hili.
Msongamano wa magari hayo husababisha uharibifu wa barabara na usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa barabara katika eneo hilo.
Imetolewa na;
Eng. Joseph M. Nyamhanga
Katibu Mkuu (Ujenzi)
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
14 Aprili, 2016
No comments :
Post a Comment