Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akizungumza na na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara
Ligula kufuatia tukio la mmoja wa Madaktari kupigwa na mwananchi. Kulia
ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.
………………………………………
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akemea tabia inayotaka kujengeka ndani ya jamii ya kuwashambulia
watumishi wa afya hasa Madaktari na Wauguzi.
Amevitaka
vyombo ya dola kuwachukulia hatua wananchi wanaojihusisha na vitendo
hivi ambavyo vitaathiri utoaji wa huduma za afya kwa wananchi hasa wa
kipato cha chini.
Mhe
Ummy amewasili Mtwara jana akiongozana na Mganga Mkuu wa Serikali Prof.
Mohammed Kambi ambapo alifanya mazungumzo na watumishi wa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula.
Amewaonya
wananchi kutoitumia vibaya dhamira ya dhati ya Rais Dkt. John Magufuli
na Serikali ya kuimarisha nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma
kwa kujichukulia sheria mkononi.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akizungumza na mmoja wa wazee aliyefika kupata matibabu katika Hospitali
ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula mara baada kuwasili hospitalini hapo
kuzungumza na wafanyakazi.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akizungumza na baadhi ya wananchi waliokusanyika nje ya hospitali
kufuatia tukio la mwananchi kumpiga daktari.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akisikiliza maoni kutoka kwa mmoja wa wananchi aliyefika hospitalini
hapo.
Mh.
Ummy Mwalimu akizungumza na na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
wa Mtwara Ligula kufuatia tukio la mmoja wa Madaktari kupigwa na
mwananchi. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Kambi.
Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula wakimsikiliza Mh. Ummy Mwalimu (hayupo pichani).
Mh. Ummy Mwalimu akisikiliza hoja mbalimbali za madktari wa hospitali hiyo.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akikagua neti ya mmoja wa mama aliyejifungua katika Hospitali ya Rufaa
ya Mkoa wa Mtwara Ligula.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akifurahi kumuona mmoja wa watoto aliyezaliwa katika wodi ya wazazi
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula mara baada ya kufanya
mazungumzo na watumishi wa hospitali hiyo.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu
akifurahi jambo na mmoja wa kina mama alipotembelea wodi ya wazazi
katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara Ligula.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungukia baadhi ya maeneo ya hospitali hiyo.
TANZANIA YAPOKEA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 116.4 KUTOKA JAPAN
(Na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
Kamati ya kudumu ya Bunge ya miundombinu yapongeza mradi wa daraja la Kigamboni
Picha zote na Raymond Mushumbusi MAELEZO
BENKI YA KILIMO YAJIDHATITI KUSAIDIA UPATIKANAJI WA MASOKO NCHINI
UFAFANUZI KUHUSU KIMA CHA CHINI CHA MAFAO YA WASTAAFU (MINIMUM PENSION BENEFITS)
…………………………………………………………………
Hivi karibuni Mamlaka imekuwa
ikipokea Malalamiko mengi kutoka kwa wanachama na wadau mbalimbali wa
Sekta ya Hifadhi ya Jamii kuhusu kuwepo kwa tofauti ya kima cha chini
cha malipo ya mafao ya wastaafu. Malalamiko haya yanajitokeza kufuatia
kutolewa kwa Tangazo la Serikali Na. 285 la mwaka 2015 kuhusu
kupandishwa kwa kima cha chini cha Mafao kwa baadhi ya wastaafu.
Kufuatia malalamiko hayo, Mamlaka inatoa ufafanuzi kama ifuatavyo:
- Mnamo mwezi Julai mwaka 2015, Wizara ya Fedha kupitia Tangazo la Serikali Na. 285 la tarehe 30/6/2015 (the Public Services Retirement Benefits (Minimum Pensions) Order, 2015 (Government Notice No GN N. 285 of 30/06/2015) baada ya kuridhiwa na Bunge, ilipandisha kima cha chini cha malipo ya mafao kwa wastaafu chini ya kifungu cha 30 cha Sheria ya PSPF. Kwa mujibu wa Tangazo hilo, kima cha chini kwa malipo ya pensheni ya kila mwezi kiliongezeka kwa kiasi cha shilingi 45,000/- pamoja na asilimia 10 ya mafao ya zamani na hivyo kufanya kima cha chini kupanda kufikia kiasi cha takribani Shilingi laki moja (100,000/=).
- Mamlaka inapenda kufafanua kwamba, ongezeko hilo liliwalenga wastaafu waliokuwa kwenye mfumo wa pensheni wa zamani wa kutochangia (Non-Contributory) wanaolipwa mafao yao na Hazina kupitia Mfuko wa PSPF na HALIKUWAHUSU wastaafu waliopo katika Mifuko ya Msingi (Mandatory Schemes) yaani NSSF, PPF, LAPF, PSPF na GEPF.
- Aidha, ni muhimu ikaeleweka kwamba, utaratibu wa kuweka kima cha chini cha mafao kwa wanachama wa Mifuko ya Msingi (Mandatory Schemes) yaani NSSF, PPF, LAPF, PSPF, GEPF, NHIF & WCF umeainishwa katika kifungu cha 25 cha Sheria ya Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii, Sura ya 135 kikisomwa pamoja
na kifungu cha 36 cha Sheria hiyo.
Kwa mujibu wa vifungu hivyo, kima cha chini cha malipo ya mafao ya
wastaafu hupangwa na Mamlaka baada ya kufanya tathimini (Actuarial
Valuation) na kushirikisha wadau. Lengo la kufanya tathimini kabla ya
kupandisha kima cha chini cha malipo ya mafao ni kujiridhisha juu ya
uwezo wa Mfuko husika kubeba ongezeko linalopendekezwa. Kwa kupitia
utaratibu huu, mwaka 2014 Mamlaka ilitengeneza na kutoa Kanuni za
Uwianishaji wa Mafao (Pensheni Benefit Harmonisation Rules). Kanuni hizi
pamoja na mambo mengine zinaainisha kima cha chini cha malipo ya mafao
kwa wastaafu kuwa ni asilimia 40 ya kima cha chini cha mshahara wa Sekta
husika. Kununi hizi zinatumika kwa Mifuko ya Msingi ambayo ni NSSF,
PPF, LAPF, PSPF & GEPF.
- Vile vile katika jitihada za kuendelea kuimarisha Sekta, Mamlaka imekamilisha zoezi la kufanya tathimini ya Mifuko na Taarifa ya Mtathmini hiyo ipo katika hatua ya majadiliano na wadau wakiwemo wawakilishi wa wanachama. Pamoja na mambo mengine, taarifa hiyo itakuja na mapendekezo mahsusi ya namna bora ya kuboresha mafao ya wanachama. Hivyo, Mamlaka inawasihi wanachama na wadau wengine wote wawe na subira wakati huu ambao taarifa ya Mtathimini inafanyiwa kazi.
Imetolewa na Kitengo Cha Mawasiliano
Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii
S.L.P 31846
Tovuti: www.ssra.go.tz
Dar Es Salaam
WADAU WA SEKTA YA USAFIRI WA ANGA WAKUTANA KUJADILI USAFIRI WA ANGA ( CIVIL AVITIATION MASTER PLAN) DAR ES SALAAM
PICHA NA MPIGA PICHA WETU
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI YAANZA VIKAO VYA MAPITIO YA RASIMU YA BAJETI YA WIZARA HIYO KWA MWAKA 2016/17
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Prof. Mbarawa afanya ziara kushtukiza KOJ Kurasini.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), akisalimiana na
wafanyakazi wa Mashirika mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa
yanayohudumia wakimbizi katika Kambi ya muda ya NMC, iliyoko mkoani
Kigoma, kushoto ni Mratibu wa Wakimbizi Mkoani Kigoma, Tonny Samwel
Laiser.Naibu Waziri yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.
Msimamizi wa Kambi ya muda ya
NMC, Jordan Emmanuel (wa kwanza kushoto), akimuonyesha Naibu Waziri wa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, jinsi mfumo wa
jiko la kupikia chakula kambini hapo unavyofanya kazi.Naibu Waziri
yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.
Sehemu ya vitanda vipya vikiwa
katika moja ya mabweni ya Kambi ya muda ya wakimbizi ya NMC , tayari kwa
kufungwa na kuanza kutumika na wakimbizi wanaohifadhiwa kambini hapo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), akizungumza na
Mkuu wa Wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma, Peter Toima Kiroya (wa kwanza
kushoto), wakati walipotembelea iliyokua kambi ya Karago iliyotumika
kuhifadhi wakimbizi.Kulia ni Mkuu wa Kambi ya Wakimbizi Mtendeli,
Innocent Mwaka.Naibu Waziri yuko mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akifafanua jambo
kwa Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani Ofisi ndogo ya
Kibondo, Dost Yousafzai(kushoto), wakati alipotembelea iliyokuwa kambi
ya Wakimbizi ya Karago,Wilayani Kibondo mkoani Kigoma.
Mkuu wa Shirika la Kuhudumia
Wakimbizi Duniani Ofisi ndogo ya Kibondo,Dost Yousafzai (kushoto),
akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni(kulia), wakati ya ziara ya Naibu Waziri
kutembelea ilipokuwepo kambi ya wakimbizi ya Karago, wilayani Kibondo.
Naibu Waziri yuko mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wakimbizi wa
Burundi (hawapo pichani) wanaoishi katika kambi ya Mtendeli, iliyoko
wilayani Kakonko mkoani Kigoma.Naibu Waziri yuko Mkoani Kigoma kwa ziara
ya kikazi.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
ZIARA YA NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI-MKOANI KIGOMA
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
SERIKALI YAJIPANGA KUWASAIDIA WAKULIMA KUPAMBANA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI
Wageni
rasmi katika mkutano huo, Wa kwanza kushoto ni Mtafiti kutoka Taasisi
ya Mtandao wa Kutathimini Sera za Chakula, Kilimo na Maliasili
(FANRPAN), Njongenhle Nyoni, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti
wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida na Mkuu wa Kitengo cha
Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bi. Shakwaanande
Natai.
Mkuu wa Kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bi. Shakwaanande Natai akielezea Kilimo Salama (CSA).
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuendelea na mkutano huo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dkt. Tausi
Kida (kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo,
Mifugo na Uvuvi, Bi. Shakwaanande Natai.
Karl Deering kutoka Taasisi ya CARE akizungumzia Mpango wa Kilimo Salama Afrika (ACSAA)
Baadhi ya wageni katika mkutano huo wakichangia hoja
Washiriki wa mkutano wakiwa katika makundi kujadili kuhusu Kilimo Salama (CSA)
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uwezeshaji wa ESRF, Doris Likwelile akifunga mkutano.
UBALOZI WA INDIA NCHINI WAADHIMISHA ITEC DAY
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Mh. Angellah Kairuki
(Mb) akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Ushirikiano wa Kiufundi
na Kiuchumi kati ya Tanzania na India (ITEC DAY) yaliyofanyika katika
Kituo cha Utamaduni cha India jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Mh. Angellah Kairuki
(Mb) akiwasha mshumaa kuashiria uzinduzi wa maadhimisho ya Siku ya
Ushirikiano wa Kiufundi na Kiuchumi kati ya Tanzania na India (ITEC
DAY) yaliyofanyika katika Kituo cha Utamaduni cha India jijini Dar es
Salaam. Anayeshuhudia ni Balozi wa India nchini Tanzania Mh. Sandeep
Arya .
Balozi
wa India nchini Tanzania Mh. Sandeep Arya (kushoto) akikabidhi zawadi
kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Mh.
Angellah Kairuki (Mb) wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ushirikiano wa
Kiufundi na Kiuchumi kati ya Tanzania na India (ITEC DAY)
yaliyofanyika katika Kituo cha Utamaduni cha India jijini Dar es
Salaam.
PICHA NA MPIGA PICHA WETU
SERIKALI KUSAIDIANA NA TAASISI YA MILLEN MAGESE MAPAMBANO DHIDI YA TATIZO LA ENDOMETRIOSIS
Hati za viwanja vya Bayport zatolewa kwa mtindo wa aina yake
Meneja
Biashara wa Bayport Financial Services, Thabit Mndeme, kushoto
akimpatia hati ya kiwanja cha Vikuruti, mteja wao Ibrahim Yusuph Ismail,
nyumbani kwao Kariakoo jijini Dar es Salaam, leo mchana. Kwa wiki hii
tu Bayport imeamua kuwapelekea hati za viwanja wateja wao katika maeneo
yao ya makazi na maofisini kwao.
Meneja
Biashara wa Bayport Financial Services, Thabiti Mndeme, kushoto
akizungumza jambo wakati anamkabidhi hati yake ya kiwanja mteja wao
Neema Jameson Nawita, jijini Dar es Salaam leo mchana.
No comments :
Post a Comment