Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akizungumza na viongozimbalimbali toka
Tanzania na Vietnam kwenye halfa ya kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya
Kisoshalisti Mhe. Truong Tan Sang iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es
Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti
Mhe. Truong Tan Sang akizungumza na viongozi mbalimbali toka Tanzania na
Vietnam katika halfa ya kumkaribisha iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es
Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akigonga glass na Rais wa Jamhuri ya
Kisoshalisti Mhe. Truong Tan Sang ikiwa ni ishara ya ushirikiano kati ya
Tanzania na Vietnam katika halfa ya kumkaribisha iliyofanyika Ikulu
Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti
Mhe. Truong Tan Sang (Kulia) akiwa amenyanyua glass juu pamoja na Mke wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Waziri
Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa,Majaliwa ikiwa ni ishara ya kutakia heri kati
ya Tanzania na Vietnam katika halfa ya kumkaribisha iliyofanyika Ikulu
Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti
Mhe. Truong Tan Sang (Kulia) akiwa amenyanyua glass juu pamoja na Mke wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Waziri
Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa,Majaliwa ikiwa ni ishara ya kutakia heri kati
ya Tanzania na Vietnam katika halfa ya kumkaribisha iliyofanyika Ikulu
Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti
Mhe. Truong Tan Sang wakitoa heshima kwa nyimbo za mataifa hayo mawili.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na
Usalama Generali Aldof Davis Mwamunyange (Wa pili kulia) akifatilia
hotuba za Rais wa Tanzania na Vietnam katika halfa ya kumkaribisha
iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi
Inspecta Generali Ernest Mangu, wa pili kushoto ni Mkuu wa Jeshi la
Magereza Kamishna Jenerali Casmir Minja, katikati ni Mkuu wa Usalama
Rashid Othman na kushoto ni Kamanda wa Kanda maaalum Dar es Salaam
Kamishna Simon Sirro.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John
Kijazi (katikati) akifatilia halfa ya kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya
Kisoshalisti Mhe. Truong Tan Sang iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es
Salaam kushoto ni Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson na kushoto ni Mnadhimu Mkuu mstaafu wa
Jeshi la wananchi la Tanzania Luteni Generali Abdulrahman Shimbo.
Picha zote na Raymond Mushumbusi MAELEZO
CHAKULA CHA JIONI ALICHOANDAA RAIS MAGUFULI KWA HESHIMA YA RAIS WA VIETINAM
Mkewa Rais Mama Janeth Magufuli
alimwongoza Mke wa Rais wa Vietinam, Mai Ti Hahn (kushoto) kwenda
kwenye chakula cha jioni alichoandaa Rais John Magufuli ikulu jijini Dar
es salaam Machi 9, 2016 kwa heshima ya Rais wa Vietinam, Truong Tang
Sang. Wapili kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa na kulia ni
Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na
Mkewe Salma wakiingia kwenye ukumbi wa Ikulu jijini Dar es salaam
kushiriki chakula cha jioni alichoandaa Rais John Magufuli ikulu
jijini Dar es salaam Machi 9, 2016 kwa heshima ya Rais wa Vietinam,
Truong Tang Sang. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Katibu wa CCM, Abdulrahman Kinana
akizungumza na Balozi Celestine Mushy wa Wizara ya Mambo ya Nje,
Ushirikiano wa Afrika ya Mashari, Kikanda na Kimataifa katika chakula
cha jioni alichoandaa Rais John Magufuli ikulu jijini Dar es salaam
Machi 9, 2016 kwa heshima ya Rais wa Vietinam, Truong Tang Sang. (Picha
na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Rais John Magufuli akiteta na
Rais Mstaafu Ali Hasan Mwinyi na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika
chakula cha jioni alichomwandalia Rais wa Vietinam, Truong Tang Sang,
Ikulu jijini Dar es salaam Machi 9,2016. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Rais John Magufuli akizungumza
na Marais Wstaafu Ali Hasan Mwinyi na Jakaya Kikwete Waziri Mkuu
katika chakula cha jioni alichomwandalia Rais wa Vietinam, Truong Tang
Sang, Ikulu jijini Dar es salaam Machi 9,2016. Kulia ni Waziri Mkuu,
Kasim Majaliwa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na Mwenyekiti wa Chama cha UDP,John Cheyo chakula cha jioni
ambacho Rais John Magufuli alimwandalia Rais wa Vietinam, Truong Tang
Sang, Ikulu jijini Dar es salaam Machi 9,2016. Kulia ni Waziri Mkuu,
Kasim Majaliwa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu awahakikishia fursa za Uwekezaji wa Vietnam
Na Anitha Jonas – MAELEZO
Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa amewahakikishia
wawekezaji kutoka Vietnam kuwepo kwa fursa za uwekezaji nchini.
Majaliwa ameyasema hayo jana
katika kongamano la ujumbe wa Rais wa Vietnam Mheshimiwa Troung Tan Sang
pamoja na wadau wa uwekezaji kutoka nchini humo ambapo wanatarajia
kufanya ziara ya siku nne nchini wakitazamia fursa za uwekezaji nchini.
“Nchi yetu inamazingira mazuri ya
uwekezaji, usalama wakutosha na pia kuna uhahika wa soko kwani ipo
mikataba ya kikanda ya kukuza masoko katika nchi wanachama kama EAC na
SADC kwani katika nchi hizo kuna watu zaidi ya milioni 300”, alisema
Majaliwa.
Akiendelea kuzungumza na
wawekezaji hao Waziri Mkuu alisema serikali ya Tanzania imekuwa
ikiboresha Mazingira ya uwekezaji nchini na hiyo imechangia ongezeko la
wawekezaji.
Mbali na hayo Majaliwa alisema
serikali imekuwa ikiboresha sheria na kuimarisha ushirikishwaji wa wadau
wa sekta binafsi lengo likiwa ni kuchochea mazingiraya uwekezaji ikiwa
ni kuimarisha uchumi wa taifa pamoja na kukuza kipato cha kila
mtanzania.
Hata hivyo Waziri Mkuu
aliipongeza Kampuni ya VIETTEL Tanzania Ltd kutoka Vietnam ambayo
imewekeza katika Sekta ya Mawasiliano kwani imewasaidia watanzania wengi
wa vijijini kupata mawasiliano.
RAIS WA ZANZIBAR AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA VIETNUM, AKUTANA NA MAALIM SEIF
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi akisalimiana na Rais wa Vietnam Truong Tan Sang,
jana Ikulu Jijini Dar es Salaam akipofika kwa mazungumzo na ujumbe
aliofuatana nao,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Ujumbe wake (kushoto) wakiwa
katika mazungumzo na Ujumbe wa Rais wa Vietnam Truong Tan Sang jana
Ikulu Jijini Dar es Salaam akiwa nchini kwa ziara ya Kikazi,[Picha na
Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia)akiagana na mgeni wake
Rais wa Vietnam Truong Tan Sang(kushoto) baada ya mazungumzo yao
yaliyofanyika jana Ikulu Jijini Dar es Salaam(katikati) mawair mbali
mbali wa Vietnum walioungana na Rais Truong,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto)akifuatana na Rais wa
Vietnam Truong Tan Sang(katikati) baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika
jana Ikulu Jijini Dar es Salaam(kulia) Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa Dkt. Augustin Mahiga,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamo wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad katika Hoteli ya
Serena Jijini Dar es Salaam jana akiwa katika mapumziko baada ya kuugua
kwa matatizo ya kiafya,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiteta na Makamo wa Kwanza wa
Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad jana katika Hoteli ya Serena
Jijini Dar es Salaam alipofika kuonana nae kiwa katika mapumziko baada
ya kuugua kwa matatizo ya kiafya,[Picha na Ikulu.]
Watanzania wameaswa kuwa na tabia kuwekea akiba benki.
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Dodoma
Watanzania wameaswa kujenga tabia
ya kujiwekea akiba kupitia mabenki kwa manufaa yao na taifa kwa kwa
ujumla ikiwa ni mchango wao katika kutekeleza kaulimbiu ya Mhe. Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili kufikia
malengo waliojiwekea katika kujiletea maendeleo endelevu.
Hayo yamesemwa na Meneja wa Fedha
na Utawala kutoka Bodi ya Bima na Amana (DIB) iliyo chini ya Benki Kuu
ya Tanzania (BoT) Richard Malisa wakati akitoa mada juu ya bodi hiyo
katika semina ya waandishi wa habari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa
lengo la kuwajengea uwezo waandishi hao katika kuandika, kutoa na
kusambaza habari za sekta ya uchumi biashara na fedha.
“Pesa zinapowekwa na kuwa benki
hutumika kuchangia kuinua na kuimarisha usalama wa akiba ya mtu binafsi
na kwa upande wa nchi zinatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo
ikiwemo kuinua sekta ya elimu, afya, maji, ujenzi wa barabara na
kilimo” alisema Malisa.
Katika kuonesha umuhimu wa bodi
hiyo nchini, Malisa alisema kuwa taasisi ama mtu binafsi anapoweka pesa
zake benki, hiyo ni amana kubwa na muhimu kwa kuwa tabia hiyo ya uwekaji
pesa ina tija na inaongeza usalama wa pesa ambayo ni njia salama
ikilinganishwa na kutumia njia za zamani za watu kuweka pesa kwenye
godoro ambayo sio salama.
Faida nyingine za mtu binafsi ama
taasisi kuweka pesa zao benki ni kuongeza mtaji wake kwa kupata riba
kulingana na muda pesa hizo zinapokuwa benki na mteja anauhakika pesa
yake ipo salama kwa kuwa ipo mikononi mwa Bodi ya Bima na Amana endapo
litatokea tatizo lolote kwenye benki alipoweka pesa zake.
Katika kufanikisha na kutekeleza
majukumu yake, DIB inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uelewa
mdogo wa mtu mmoja mmoja katika masuala ya kibenki na fedha kwa undani
wake ili aweze kufanya maamuzi yatakayomfanya awe bora zaidi kiuchumi
ikilinganishwa na hapo awali kabla ya kufahamu masuala ya kibenki na
fedha ikiwemo kuongeza nidhamu ya matumizi.
Akitolea mfano Malisa amewaasa
Watanzania wawe makini wanapochukua mikopo ambapo alisema kuwa watu
wasikope kwa kufuata mkumbo ama kwa shinikizo fulani, bali wakepo kwa
lengo la kuwekeza ili kuinua hali zao za kiuchumi katika maisha.
Hadi kufikia Juni 30, 2015 Bodi
ya Bima na Amana ina akiba ya jumla ya kiasi cha Sh. biloni 220.5
ikilinganishwa na wakati ilipokuwa inaanzishwa na Serikali mwaka 1994
ambapo kianzio kilikuwa kiasi cha Sh. bilioni 1.5.
Aidha, katika semina hiyo Bw.
Bernard Dadi kutoka Kurugenzi ya Mifumo ya Malipo ya Taifa alisema kuwa
BoT itaendelea kuboresha mifumo ya malipo ya hundi, kielektroniki ili
kuongeza ufanisi kwenye mifumo hiyo, kuongeza usalama, kuongeza njia
mbalimbali za malipo ili kupunguza malipo kwa fedha taslimu na kuongeza
kasi ya malipo yaweze kuwa ya wakati kwa wateja popote walipo ndani na
nje ya nchi.
Ili kuendana na wakati BoT
kupitia Kurugenzi ya Mifumo ya Malipo ya Taifa katika kuwahudumia
wananchi katika masuala ya fedha na mabenki, imeanza kutumia mfumo wa
TACH unaohusisha malipo ya hundi na malipo madogo ya kielektroniki (EFT)
ambao umeanza kutumika tarehe 30 Aprili 2015 nchini.
Mfumo wa TACH unatumika na
mabenki kutuma na kupokea hundi za wateja wao ikiwemo kulipa malipo
madogo madogo yaliyojumishwa pamoja, mishahara, pension na hata malipo
ya mtu mmoja mmoja.
Kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa
TACH nchini, awali hundi zilikua na muda tofauti wa siku za
kuhakiki kulingana na kanda hali iliyopelekea muda wa siku za kuhakiki
za hundi ulikua ni siku 3, 7 na 14 kutegemeana na kanda.
Baada ya kuanzishwa mfumo wa TACH
hali imekuwa tofauti ambapo kwa mfumo huo sasa, hundi zote za Tanzania
popote zitakapowasilishwa zitakuwa zinafanyiwa kazi ndani ya siku moja
ya kuzihakiki hundi hizo (T+1) mpaka hapo itakapolipwa.
Hatua hiyo imewapunguzia muda wateja ili waweze watapata hela zao mapema na hivyo kuzitumia kwenye shughuli zao za kiuchumi.
Aidha, Bw. Dadi aliongeza kuwa
nchi washirika wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zenyewe zinatumia
unaojulikana kama EAPS ikiwa ni jitihada za kuunda umoja wa kiuchumi
miongoni mwa nchi hizo.
Mfumo huo wa malipo umeunganisha
mifumo ya malipo (RTGS) ya nchi washiriki wa Afrika Mashariki ili
kurahisisha malipo kati ya nchi washirika.
Kwa maana hiyo mabenki ya
kibiashara ya nchi husika zina uwezo wa kutumiana na kupokea pesa za
wateja wao kwa kutumia sarafu za nchi wanachama kufanya muamala.
Hadi sasa, mfumo huo umeunganishwa kwa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, wakati Burundi na Sudan ya Kusini wako mbioni kujiunga.
KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI CHA MKOA WA LINDI CHAFANYIKA
Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Jordan Rugimbana akisoma hotuba ya ufunguzi wa kikao cha Kamati ya Ushauri mkoa.
Waziri
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la
Mtama Mhe. Nape Nnauye akizungumza kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri
mkoa wa Lindi.
Wajumbe wa Kikao cha Ushauri cha mkoa wa Lindi.
Mbunge wa Jimbo la Lindi mjini Mhe. Hassan Kaunje akichangia maoni yake kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa wa Lindi.
Kamati ya Ulinzi na usalama ya mkoa
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo akutana na mkurugenzi wa radio France Internationale
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura akimkaribisha
Mkurugenzi wa Radio France Internationale(RFI) Bi.Cecile Megie ofisini
kwake alipomtembelea kwa ajili ya kufahamiana na kuboresha mahusiano
yaliyopo kwa miaka saba sasa.
Ujumbe kutoka Radio France
International (RFI) wakifurahia jambo wakati wa kikao na Naibu Waziri wa
Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura(Hayupo
pichani).
Mkurugenzi wa Radio France
Internationale (RFI) Bi.Cecile Megie(kushoto) akizungumza na Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura
kuhusu msaada ambao wameipa shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) ili
kusaidia katika kufikisha matangazo yake mbali Zaidi.
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura(kulia) akimpa zawadi ya
kahawa kutoka Tanzania Mkurugenzi wa Radio France Internationale(RFI)
Bi.Cecile Megie(kushoto) baada ya mazungumzo mafupi ofisini kwa Naibu
Waziri uyo kuhusu kuimarisha mahusiano baina ya nchi izi mbili katika
masuala ya Habari kati ya TBC na RFI.
Jennifer Mgendi alipania Tamasha la Pasaka
Na Mwandishi Wetu
MWIMBAJI na Msanii mahiri wa Filamu Tanzania, Jennifer
Mgendi amelipania Tamasha la Pasaka linalotarajia kuanza Machi 26-28
katika mikoa ya Geita, Mwanza na Kahama.BAKITA waaswa kuhamasisha matumizi ya Lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura akizungumza na
Katibu Mtendaji BAKITA (hayupo pichani) alipotembelea ofisi za Baraza
la Kiswahili Taifa (BAKITA) kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na
Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji Baraza la
Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Selemani Sewange (katikati) akifafanua
jambo kwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi.
Anastazia James Wambura (kushoto) alipotembelea ofisi za BAKITA kufahamu
mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es
Salaam. Kulia ni maafisa Utamaduni kutoka Wizara hiyo.
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (kushoto)
akikabidhiwa kitabu kiitwacho Furahia Kiswahili kilichoandaliwa na
BAKITA alipotembelea ofisi za BAKITA kufahamu mambo mbalimbali
yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam. Anayemkabidhi ni
Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Seleman Sewange
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura akipitia
Kamusi kuu ya Kiswahili aliyopewa baada ya kutembelea ofisi za BAKITA
kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo jana jijini Dar
es Salaam.
Mtaalamu kutoka Idara ya Istilahi
na Kamusi Taasisi ya BAKITA Bw. Mayolwa John (kushoto) akimwelezea
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia
James Wambura (kulia) kazi zinazofanywa na Idara hiyo alipotembelea
ofisi za BAKITA kufahamu mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hiyo
jana jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mtendaji Baraza la
Kiswahili Taifa (BAKITA) Dr. Selemani Sewange
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Anastazia James Wambura (wapili
kushoto) akiangalia mfumo wa mradi wa kukuza kiswahili katika kompyuta
ulioandaliwa na BAKITA alipotembelea Taasisi hiyo kufahamu mambo
mbalimbali wanayoyafanya jana jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni
Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili Taifa Dr. Selemani Sewange na
kushoto ni Afisa Utamaduni Bw. Christopher Mhongole.
TAMKO LA WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KUHUSU SIKU YA FIGO DUNIANI, TAREHE 10 MACHI, 2016
Siku ya Figo Duniani huadhimishwa
duniani kote kila AlhamisI ya pili ya mwezi Machi tangu mwaka 2006.
Mwaka huu itaadhimishwa leo tarehe 10/3/2016.
Kaulimbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Figo mwaka 2016 ni “Chukua Hatua Mapema Kuepuka Magonjwa ya Figo kwa Watoto”. Kauli mbiu hii inalenga kuhamasisha jamii juu ya matatizo ya figo yanayoikabili jamii yetu hususani watoto.
WATOTO CHINI YA MIAKA 5 KUNUFAIKA NA UPIMAJI WA AFYA BURE KUTOKA KWA BANGO SANGHO
Mwenyekiti
wa Umoja wa Jamii ya watu kutoka India, Bengali waliopo Tanzania (Bango
Sangho), Kunal Banerjee akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na
kambi ya upimaji afya kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano
inayotayotaraji kufanyika katika Shule ya Msingi Kibugumu iliyopo
Kigamboni jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mmoja wa madaktari
watakaoendesha zoezi la upimaji afya kwa watoto hao Dkt. Ali Mzige
kutoka Kliniki ya Al Hilal ya jijini Dar es Salaam.
Mmoja
wa madaktari watakaoendesha zoezi la upimaji afya kwa watoto hao Dkt.
Ali Mzige kutoka Kliniki ya Al Hilal ya jijini Dar es Salaam akifafanua
jambo kuhusiana na umuhimu wa kupima afya za watoto katika mkutano na
waandishi wa habari.
“Tunataka
kusaidia marafiki zetu wa Tanzania na katika kuendelea hilo tutatoa
huduma ya bure kwa watoto kupima afya zao na tunataka wazazi wawalete
watoto ili wapime afya,” alisema Banerjee.
Mtaalamu
wa afya ya uzazi kutoka Kliniki ya Al Hilal, Bi. Husna Abdallah akitoa
msisitizo kwa akina mama kuzingatia kanuni za afya ya uzazi wakati wa
mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam.
Mwandishi
wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Zawadi Chogongwe (kulia)
akiuliza swali kwa wataalamu wa afya wakati wa mkutano na waandishi wa
habari kuhusiana na kambi ya upimaji afya kwa watoto wenye umri chini ya
miaka mitano inayotayotaraji kufanyika katika Shule ya Msingi Kibugumu
iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.
UZINDUZI WA MRADI WA UIMARISHAJI MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA MKOA WA SHINYANGA
Hapa
ni katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga
ambako kumefanyika uzinduzi wa mradi wa Uboreshaji Mifumo ya Sekta za
Umma unaojulikana kwa jina la Public Sector Systems Strenghening (PS3)
unaofadhiliwa na shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).
Lengo la mradi huo ni kuimarisha mifumo ya ya sekta za umma yakiwemo masuala ya utawala bora,rasilimali watu,fedha utoaji taarifa na tafiti tendaji katika halmashauri za wilaya na taifa kwa ujumla. Mkutano wa uzinduzi huo utakaofanyika kwa siku mbili Machi 09,2016 hadi Machi 10,2016 umehudhuriwa na Kiongozi wa timu ya mradi,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga,wakuu wa wilaya,meya wa manispaa ya Shinyanga,wenyeviti wa halmashauri za wilaya,wataalam kutoka kutoka ofisi ya Waziri mkuu na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi,mashirika na taasisi za umma na binafsi-Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde yupo eneo la tukio ametusogezea picha 30 ,Tazama hapa chini
Kaimu katibu tawala mkoa wa Shinyanga Dkt Ntuli Kapologwe ambaye pia ni mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga akitambulisha wageni mbalimbali waliohudhuria mkutano huo wa uzinduzi wa mradi wa uimarishaji mifumo ya sekta za umma Public Sector Systems Strenghening(PS3) utakaotekelezwa kwa muda wa miaka mitano na utafanya kazi na serikali kuu pamoja na halmashauri 97 katika mikoa 13 ya Tanzania bara.
Lengo la mradi huo ni kuimarisha mifumo ya ya sekta za umma yakiwemo masuala ya utawala bora,rasilimali watu,fedha utoaji taarifa na tafiti tendaji katika halmashauri za wilaya na taifa kwa ujumla. Mkutano wa uzinduzi huo utakaofanyika kwa siku mbili Machi 09,2016 hadi Machi 10,2016 umehudhuriwa na Kiongozi wa timu ya mradi,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga,wakuu wa wilaya,meya wa manispaa ya Shinyanga,wenyeviti wa halmashauri za wilaya,wataalam kutoka kutoka ofisi ya Waziri mkuu na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi,mashirika na taasisi za umma na binafsi-Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde yupo eneo la tukio ametusogezea picha 30 ,Tazama hapa chini
Kaimu katibu tawala mkoa wa Shinyanga Dkt Ntuli Kapologwe ambaye pia ni mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga akitambulisha wageni mbalimbali waliohudhuria mkutano huo wa uzinduzi wa mradi wa uimarishaji mifumo ya sekta za umma Public Sector Systems Strenghening(PS3) utakaotekelezwa kwa muda wa miaka mitano na utafanya kazi na serikali kuu pamoja na halmashauri 97 katika mikoa 13 ya Tanzania bara.
Wakuu wa wilaya tatu za mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini,wa kwanza kushoto ni Vita Kawawa kutoka wilaya ya Kahama,akifuatiwa na Josephine Matiro kutoka wilaya ya Shinyanga na Hawa Ng’umbi kutoka wilaya ya Kishapu
Mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga akizindua mradi wa PS3 ambapo alisema mkoa wa Shinyanga ni miongoni mwa mikoa 13 nchini ambayo itanufaika na mradi huo ambapo alidai umeanza kwa wakati muafaka kwani sasa serikali iliyopo madarakani inataka mabadiliko katika kuhakikisha kuwa serikali inahudumia wananchi ipasavyo
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam (kushoto) akifuatilia hotuba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga.Rufunga alisema mradi huo utakuwa na tija kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa halmashauri 6 za mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga aliwataka watendaji wa serikali katika ngazi ya mkoa na mamlaka za serikali za mitaa kutoa ushirikiano katika kutekeleza mradi wa Uboreshaji Mifumo ya Sekta za Umma kutokana na kwamba wao ndiyo wana mawasiliano ya moja kwa moja na wananchi wa kawaida.
Tunamsikiliza mgeni rasmi……
Mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa uimarishaji mifumo ya sekta za umma unaofadhiliwa na shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID)
Meneja wa Mradi wa PS3 Dkt Emmanuel Malangalila akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo ambapo alisema mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano umeandaliwa na shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) Kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania na kutekelezwa na mashirika saba likiwemo shirika la Abt Associates Inc ambalo ndiyo mtekelezaji mkuu.
No comments :
Post a Comment