Saturday, January 23, 2016

.SERIKALI YAJA NA MIKAKATI MIPYA YA KUHAKIKISHA UTALII WA NDANI UNAKUA

 ME2
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii,Bi. Uzeeli Kiangi akisisitiza jambo wakati alipokuwa anamkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja. Generali. Gaudence Milanzi kufungua Mkutano Mkutano wa Kamati ya Uwezeshaji Utalii ( Tourism Facilitation Committee- TFC) uliofanyika leo Mpingo House jijini Dar es Salaam wa kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii nchini.
ME1
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja. Generali. Gaudence Milanzi ( kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii Bw. Deogratius Mdamu (kushoto) wakimsikiliza Mjumbe ( hayupo pichani ) wakati wa Mkutano wa Kamati ya Uwezeshaji Utalii ( Tourism Facilitation Committee- TFC) uliofanyika leo Mpingo House jijini Dar es Salaam akiwa anazungumzia changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii nchini na kutoa ushauri ya namna kuuimarisha Utalii wa ndani ambao umekuwa bado ni changamoto kwa wananchi wengi kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini
ME3
 Baadhi ya Wajumbe wa kamati ya Uwezeshaji Utalii ( Tourism Facilitation Committee- TFC) wakiwa wanajadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii nchini kwa kutoa maoni, ushauri na ufumbuzi wa changamoto ikiwa na kuchangia mikakati mbalimbali itakayowezesha kusaidia kuhamasisha Utalii wa ndani.
…………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu
Wakati nchi nyingi Afrika zikiwa zinafanya jitihada mbalimbali za kuimarisha Utalii wa ndani ambao umekuwa ndo wa uhakika katika kuiingizia nchi mapato hata pale majanga yanapotokea, Nayo Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeendelea kuhakikisha kuwa Utalii wa ndani unakua kwa kasi inayotarajiwa.
Baadhi ya Majanga hayo yanayoathiri Sekta ya Utalii ni milipuko ya magonjwa kama Ebola, matukio ya Ugaidi Kenya na kushuka kwa Euro ya Ulaya dhidi ya Dola ya Marekani.
Hivyo Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wadau wa Utalii nchini wamepanga mikakati ya kuhakikisha kuwa Utalii wa ndani unakuwa tegemeo tofauti na sasa ambapo Watalii kutoka nje ndio wamekuwa wamekuwa wakitembelea hifadhi zetu kwa kiasi kikubwa.
Akizungumza kwenye Mkutano wa Kamati ya Uwezeshaji Utalii ijulikanayo kama Tourism Facilitation Committee ( TFC) uliofanyika leo Mpingo House jijini Dar esSalaam , Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili, Meja. Generali. Gaudence Milanzi na Utalii amesema maendeleo ya Utalii yanahitaji sana Utalii wa ndani kuimarika baadala ya kudhani kuwa vivutio vya utalii vilivyopo ni kwa ajili ya wageni kutoka nchi za nje.
Meja. Generali. Milanzi amesema Utalii ni sekta nyeti sana katika kuliingiza Taifa pesa za kigeni lakini hata hivyo ni sekta ambayo imekuwa inaathirika kwa haraka sana pindi majanga yanapotokea nchi jirani hivyo ni lazima jamii ijengewe utamaduni wa kutembelea vivutio vya Utalii ili kuweza kujihakikishia Watalii wa ndani wanakuwa wengi.
Baadhi ya mikakati iliyopendekezwa na Wajumbe wa kamati ya Uwezeshaji Utalii (TFC) ni kuwawezesha maafisa Utalii wa Halmashauri wanatengewa bajeti ya kutosha, wanajengewa uwezo kuhusu ya vivutio vya utalii vilivyopo kwenye maeneo yao pamoja na Idara ya Utalii kufungua ofisi kila kanda ili kuweza kutimiza majukumu yake ipasavyo.
Aidha,viwanja vya ndege vilivyopo nchini viimarishwe ikiwa pamoja na nchi kuwa ndege zake kama ilivyo kwa nchi jirani kama Kenya na Rwanda
Awali , Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii,Bi. Uzeeli Kiangi alisema Mkutano wa TFC hutoa fursa za kuziibua na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii hivyo Sekta Binafsi zinawajibu mkubwa wa kuhakikisha changamoto zinazoikabili sekta zinatafutiwa ufumbuzi
Aliongeza kuwa Idara ya Utalii imekuwa ikishiriki katika maonesho mbalimbali ya kitaifa lengo likiwa ni kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kutembelea vivutio vya Utalii nchini.
Aidha, Prof Wineastor Anderson amesema sekta ya Utalii imekuwa inakua lakini si kwa kiwango cha kuridhisha hivyo jitihada za kutangaza utalii ndani na nje nchi upewe uzito unaostahili kwa kuiwezesha Bodi ya Taifa ya Utalii inatengewa bajeti ya kutosha.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Utalii Tanzania ( TCT) Bw. Richard Rugimbana, amesema Utalii wa ndani ili uweze kukua suala la elimu linahitajika kutolewa ili kuweza kuibadilisha jamii ipende kutembelea vivutio vya Utalii.
Naye Kamanda wa Polisi Jk Ndaki anayeshghulikia dawati la Utalii ( Tourism Police Unit) amewahakikishia usalama wao watalii wa ndani na nje ya nchi kutembelea vivutio vya Utalii bila hofu yoyote kuwa Jeshi la Polisi nchini lipo macho muda wote.

WATU WAWILI WAMEFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA BASI LA BM COACH

12573974_907243602706649_752768834444790439_n
Basi la Kampuni ya BM linavyoonekana baada ya kupata katika eneo la Mikese Mkoani Morogoro chanzo cha ajali hiyo inadaiwa ni mwendo kasi wa Basi hilo uliopelekea kushindwa kusimama.
RPC MKOA WA MOROGORORPC wa Morogoro-Leonard Paul
………………………………………………………….
Tarehe 22/01/2016 majira ya 2130hrs huko eneo la Lubungo Tarafa ya Mikese Wilaya na Mkoa wa Morogoro barabara ya Morogoro/d,Salaam gari yenye namba za usajili T. 916 BQX YUTONG BUS mali ya kampuni ya BM COACH iliyokuwa ikiendeshwa na Aloyce s/o William, 39yrs, Mkaguru, mkazi wa Morogoro ikitokea D’salaam kuelekea Morogoro iligonga Ubavuni mwa gari yenye namba za usajili T. 184 CGX/T. 859 CXB FAW LORI iliyokuwa ikiendeshwa dereva asiyefahamika jina alikimbia baada ya ajali, iliyokuwa ikitokea Morogoro kuelekea D,salaam na kusababisha vifo kwa watu wawili waliokuwa wakisafiri kwa bus; Capten D.G Minga, 35yrs, mkazi wa SKM Mgulani DSM (2) mwanaume ambaye hajatambulika, umri kati ya miaka 35 – 45 na majeruhi kwa watu arobaini na tatu waliokuwa wakisafiri kwa bus hilo na majeruhi thelathini na tatu; Vedastiani d/o Bishagoma, 22yrs, Mhaya, mkazi wa Msasani DSM, Samsoni s/o Jeru, 36yrs, Mchaga, mkazi wa Ubungo DSM, Hadija d/o Omari, 28yrs, Mhehe, mkazi wa Tegeta DSM, Wifrida d/o Bernard, 22yrs, Mfipa, Askari JWTZ Lugalo, mkazi wa D,Salaam, Silvester s/o Sangayau, 38yrs, Mpogoro, mkazi wa Itete, Mwasiti d/o Sultan, 42yrs, Mkutu, mkazi Tabata, Joyce d/o Edward, 32yrs, Muha, mkazi wa Geita, Brayson s/o Chakiuke, 2yrs, Muha, mkazi wa D,salaam, Haridi s/o Siraji , 34yrs, Mpogoro, mkazi wa Modeco, Flora d/o Mganga, 38yrs, Mluguru, mkazi wa Modeco, Msungi d/o Hamisi, 30yrs, Mnyiramba, Kurasini DSM, Mathar d/o Robin, 49yrs, Mchaga, mkazi wa Nanenane, Yasinta d/o Severini, 38yrs, Mluguru, mkazi wa Kihonda, Baturi d/o Bakari, 35yrs, mkazi wa Mafisa , Mkurya, mkazi wa Mafisa, Edwini s/o Ishuba, 22yrs, Mchaga, mkazi wa Kihonda, Juma s/o Chota, 27yrs, Mluguru, mkazi wa Karume Morogoro, Flora d/o Bernard, 22yrs, Mmakonde, mkazi wa Mafisa, Greyson s/o Chagawa, 58yrs, Mpare, mkazi wa Ubungo DSM, Jamila d/o Matola , 25yrs, Vituka DSM, Mwiyao, mkazi wa Yombo Vituka DSM, Francis s/o Chua, 26yrs, Mchaga, mkazi wa Bigwa, Grayson s/o Eliniki , 44yrs, Mpare, mkazi wa Mafiga, Endrew s/o Shaula, 54yrs, Mnyiramba, mkazi wa Tanga, Christopher s/o Masele, 39yrs, Msukuma, mkazi wa Kihonda Magorofani, Peter s/o Agostine Mushi, 42yrs, Mchaga, mkazi wa Vibandani, Rose d/o Michael, 26yrs, Mchaga, mkazi wa Modeco, Wema d/o Tewele. 31yrs, Mbena, mkazi wa Kihonda, Joyce d/o Abisasi, 25yrs, Mjaluo, mkazi wa Morogoro, Saidi s/o Mnyimba, 47yrs, Mluguru, mkazi wa Tabata DSM, Jerani s/o Seif , 37yrs, Mluguru, mkazi wa Kinole, Robert s/o Muba, 46yrs , Mndali, mkazi wa Forest, Hanuari s/o Bakari , 19yrs , Msambaa , mkazi wa Forest, Anither d/o Temu, 39yrs , Mchaga, mkazi wa Bunju DSM , Scolastika d/o Aleni, 24yrs, Msambaa, mkazi wa Mabibo DSM na Bank s/o Omari, 48yrs, Mluguru, mkazi wa Mwembesongo hawa wamelazwa hospitali ya Mkoa wa Morogoro ward namba moja na namba tatu na majeruhi tisa walitibiwa na kuruhusiwa hospitalini hapo. Chanzo cha ajali ni mwendokasi wa gari T. 916
BQX YUTONG BUS.mtuhumiwa amekamatwa.
RPC MOROGORO

MATENGENEZO YA BOMBA KUBWA LA MAJI YA DAWASCO YAENDELEA KAWE-TEGETA.

Kazi ya Kuunganisha Bomba la Maji kutoka mtambo wa uzalishaji wa Ruvu Chini ukiendelea katika eneo la Wazo Tegeta .
Matengenezo ya Bomba hili ndiyo yaliyopelekea kuzimwa kwa mtamb wa uzalishaji maji wa Ruvu Chini ambapo kwa muda wa saa 48 huduma ya maji itakosekana katika jiji la Dar Es Salaam na Bgamoyo.
Afisa Mtendaji mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja a-kizungumza juu ya matengemezo hayo alipotembelea katika eneo hilo kujionea shughuli zinavyoendelea.
Imeandaliwa na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii.

MATUKIO BUNGENI MJINI DODOMA

Q1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Iramba Mashariki, Allan Kiula kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januai 23, 2016.
Q2
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum,Azza Hillal  Hamad kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januai 23, 2016.
Q3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum,Cecilia Daniel Paresso kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januai 23, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Basata yawataka waimbaji nyimbo za Injili kujisajili

basataNa Mwandishi Wetu
……………………………….
BARAZA la Sanaa la Taifa (Basata) limezidi kutoa wito kwa Waimbaji wa muziki wa Injili kujisajili katika baraza hilo ili stahiki zao zitambulike inavyotakiwa.
Mkurugenzi wa ukuzaji Sanaa na Mtukio wa Basata, Maregesi Kwirujira Ng’oko alisema waimbaji wengi wa muziki wa Injili wa Tanzania kuzingatia hilo.
Ng’oko alisema kujisajili Basata kuna faida na fursa nyingi ambazo ni msaada ambao utasaidia kupata haki zao kupitia kazi zao.
Ng’oko alisema kwa kuwa wao ndio wasimamizi wa kazi za sanaa ni jukumu lao kuwakumbusha mara kwa mara wasanii kujisajili.
Aidha Ng’oko alisema wanatoa salamu hizo kwa wasanii pindi inapotokea mikinzano katika ufanikishaji wa kazi zao.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Abihudi Mang’era alisema wanafikiria kuongeza msukumo kwa waimbaji wa muziki wa Injili kuhusu kujisajili Basata katika baadhi ya matukio.
Mang’era alisema wanafikiria kutoa elimu ya kujisajili Basata katika matamasha yao ama kusaka namna ya kufanikisha utambuzi wa waimbaji katika baraza hilo.

SERIKALI YAOMBWA IKAMILISHE TARATIBU ZA UVUNAJI WA MSITU

msitu
Na. Ahmad Mmow, Nachingwea.
……………………………………….
Baadhi ya wananchi na viongozi wa kijiji cha Ngunichile, wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi. Wameiomba serikali kuharakisha na kukamilisha mchakato wa uvunaji wa msitu wa kijiji hicho.
Wananchi na viongozi hao waliyasema hayo mbele ya timu ya waandishi wa habari na maofisa wa Mtandao wa jamii wa usimamizi wa misitu (MJUMITA) waliokwenda kijijini hapo juzi ili kuona mafanikio na changamoto za uhifadhi misitu.
Waliiambia Lindiyetu.com urasimu ambao hawaujui unatokana nanini, umesababisha uvunaji wa mazao ya misitu kwenye msitu waliohufadhi uchelewe kuanza.
Bakari Lilombo aliyejitambulisha ni mwanajamii, alisema kutoanza uvunaji wakati miti imefikia umri wa kuvunwa kunasababisha baadhi ya wananchi kukatatamaa kutokana na kutoona manufaa ya msitu huo.“Uvunaji ungeanza ungeingiza mapato ambayo yangetumika kununua zana za kilimo na kujenga visima vya  vya maji, lakini kwa hali hii tunakata tamaa,”alisema Bakari.
Mzee Hamis Malombe mwanajamii, alisema matarajio ya wananchi nikunufaika na mapato ya mazao ya msitu huo wenye hekta 1800, kupitia huduma za jamii. Hata hivyo wananchi wanakata tamaa na matarajio yao yameanza kutoweka.
Bi Maua Ntila, ambae ni mjumbe waserikali ya kijiji hicho, alisema mapato ambayo yangetokanana mauzo mazao ya msitu huo yangeweza kutumika kuchimba visima na kuboresha zahanati. Jambo ambalo lingekuwa ni ukombozi kwa akinamama wakazi wa kijiji hicho.
Hatahivyo hadi sasa hawajaanza uvunaji, ingawa walitaraji uvunaji ungekuwa umeanza tangu mwaka jana. Kwa upande wake, ofisa mtendaji wa kijiji hicho, Selemani Soya, alisema hatua za awali za maandalizi ya uvunaji zilishafanyika.
Ofisi ya mkurugenzi wa wilaya ya Nachingwea iliwahaidi wangeanza uvunaji mwaka jana mwezi novemba, hata hivyo hadi sasa hawajaanza kuvuna.“Tunapata shida ya kupambana na wavunaji haramu,maana maeneo mengi hayana miti” kwahiyo eneo lenye miti ni msitu huu, kama tungeanza uvunaji naamini wangeogopa na tungekuwa na nafuu sana,”alisema Selemani.
Akijibu malalamiko hayo kwaniaba ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Nachingwea. Ofisa misitu wa halmasiauri hiyo, Paiton Kamnana, alisema uvanaji umechelewa kuanza kwasababu kutokamilika baadhi ya taratibu, nyaraka na nyundo.
Hata hivyo maandalizi yote yamekamilika, kwahiyo muda si mrefu uvunaji utaanza.
“Nyaraka zilishafuata wizarani,nyundo imeshapatikana pia.Ilikuwa jambo lisilowezekana kuanza uvunaji kabla ya kuwapa plan(mpango)”.
Utunzaji wa msitu huo nimatokeo ya elimu iliyotolewa na mashirika yasiyo kiserikali ikiwamo Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania(MJUMITA) kupitia mradi wa kampeni ya mama misitu kwa kushirikiana na serikali.

WAZIRI KITWANGA: KAMATAKAMATA INAYOENDELEA KWA RAIA WA KIGENI NCHINI, HAITAGUSA WENYE VIBALI HALALI

C1
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akizungumza na raia wa China wanaoishi nchini, katika sherehe yao ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake, Waziri Kitwanga alisema Tanzania inatambua ushirikiano mzuri wa miaka mingi uliopo kati yake na China, hivyo raia yeyote wa kigeni anatakiwa afuate taratibu za kuishi nchini, na operesheni inayoendelea ya kuwakamata raia wa kigeni, kamwe haitagusa wenye vibali halali.
C2
Kaimu Balozi wa China nchini, Zhang Biao akizungumza katika sherehe ya raia wa China wanaoishi nchini ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, jijini Dar es Salaam, kabla ya kumkaribisha Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (hayupo pichani) kuja kuzungumza na mamia ya wachina hao waliohudhuria sherehe hiyo. Katika hotuba yake, Waziri Kitwanga alisema Tanzania inatambua ushirikiano mzuri, wa miaka mingi uliopo kati yake na China, hivyo raia yeyote wa kigeni anatakiwa afuate taratibu za kuishi Tanzania, na operesheni inayoendelea ya kuwakamata raia wa kigeni nchini, kamwe haitagusa wenye vibali halali.
C3
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick akimpongeza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto), kwa kutoa hotuba nzuri iliyowafafanulia wachina waishio nchini kuwa Serikali ya Tanzania inawajali na inatambua umuhimu wa ushirikiano wao uliodumu kwa kipindi cha miaka mingi, hivyo raia yeyote wa kigeni anatakiwa afuate taratibu za kuishi Tanzania, na operesheni inayoendelea ya kuwakamata raia wa kigeni nchini, kamwe haitagusa wenye vibali halali. Wachina waishio nchini jana walifanya sherehe ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip na kuhudhuriwa na mamia ya wachina hao. Kulia ni Kaimu Balozi wa China nchini, Zhang Biao.
C4
Raia wa China wanaoishi nchini wakishindana kula Tunda aina ya Tikiti wakati wa Sherehe yao ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, jijini Dar es Salaam. Katika Sherehe hiyo ambayo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (hayupo pichani) alikuwa mgeni rasmi ilihudhuria na mamia ya raia hao wa China. Hata hivyo, Waziri Kitwanga alisema raia yeyote wa kigeni anatakiwa afuate taratibu za kuishi Tanzania, na operesheni inayoendelea ya kuwakamata raia wa kigeni nchini, kamwe haitagusa wenye vibali halali.
C5
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akiwapongeza raia wa China walioshinda mchezo wa bahati nasibu walioucheza katika sherehe yao ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, jijini Dar es Salaam. Waziri Kitwanga katika hotuba yake alisema nchi yake inatambua ushirikiano mzuri wa miaka mingi uliopo kati yake na China, hivyo raia yeyote wa kigeni anatakiwa afuate taratibu za kuishi nchini, na operesheni inayoendelea ya kuwakamata raia wa kigeni, kamwe haitagusa wenye vibali halali.
C6
Kikundi cha Karate kinachoongozwa na raia wa China wanaoishi nchini kikitoa burudani katika sherehe yao ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, jijini Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (hayupo pichani) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hiyo, katika hotuba yake alisema nchi yake inatambua ushirikiano mzuri wa miaka mingi uliopo kati yake na China, hivyo raia yeyote wa kigeni anatakiwa afuate taratibu za kuishi nchini, na operesheni inayoendelea ya kuwakamata raia wa kigeni, kamwe haitagusa wenye vibali halali.
C7
Sehemu ya raia wa China wanaoishi nchini, wakimsikiliza kwa makini, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (hayupo pichani) wakati alipokuwa anatoa hotuba yake kwa Wachina hao katika sherehe yao ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, jijini Dar es Salaam jana. Waziri Kitwanga katika hotuba yake alisema nchi yake inatambua ushirikiano mzuri wa miaka mingi uliopo kati yake na China, hivyo raia yeyote wa kigeni anatakiwa afuate taratibu za kuishi nchini, na operesheni inayoendelea ya kuwakamata raia wa kigeni, kamwe haitagusa wenye vibali halali.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

NAPE ATEMBELEA KITUO CHA UTAMADUNI BUJORA PAMOJA NA CHUO CHA MAENDELEO YA MICHEZO MALYA MKOANI MWANZA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (kulia) akikaribishwa kwenye kituo cha utamaduni wa Kisukuma Bujora na Mlezi na Mshauri wa kituo cha utamaduni pamoja na machifu wa Kisukuma Jaji Mstaafu Mark Bomani
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (katikati) akizungumza na Machifu wa kisukuma kwenye kituo cha Utamaduni Bujora, kulia pichani ni Jaji Mstaafu Mark Bomani na kushoto ni Chifu Charles Kafipa wa Bukumbi mkoani Mwanza
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akipata maelezo juu ya nyumba za asili za wasukuma kutoka kwa Mkurugenzi wa kituo cha Utamaduni wa Kisukuma Padri Fabian Mhoja.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiangalia hesabu za kisukuma kwenye kituo cha Bujora mkoani Mwanza.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akipata maelezo juu ya utamaduni wa kucheza bao kwenye kituo cha Utamaduni wa kisukuma Bujora.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiangalia zana mbali mbali za kiasili kwenye nyumba ya utamaduni Bujora.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akipata maelezo namna machifu walivyokuwa mashujaa na viongozi hodari.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akipata maelezo juu ya chuo cha Bujora
Wapiga ngoma wakipiga kwa ufahari ngoma mbele ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye
Baadhi ya wageni wakiangalia ngoma mbali mbali zikichezwa kwenye kituo cha Bujora mbele ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akihutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye kituo cha utamaduni wa kisukuma Bujora ambapo aliwapongeza kituo hicho kwa kudumisha utamaduni na kuahidi serikali itaendelea kukisaidia.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye ambaye pia amepewa jina la Chifu Sangeja( aliyeshika usinga) akiwa kwenye picha ya pamoja na wasanii kutoka nchini Denmark ambao wanajifunza utamaduni wa Kisukuma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiangalia uwanja wa ndani wa Chuo Cha Maendeleo ya Michezo Malya.
Sehemu ya jukwaa la kukalia la uwanja wa ndai wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya wilayani Kwimba mkoa wa Mwanza.
Wanafunzi  wa Chuo Cha Maendeleo ya Michezo Malya wilayani Kwimba wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akifurahia jambo wakati akizungumza na wanafunzi wa chuo cha maendeleo ya michezo, Malya.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya ambapo aliahidi kutatua changamoto mapema.
wanafunzi wa Chuo Cha Maendeleo ya Michezo- Malya wakionyesha uwezo wao wa kimichezo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye .
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya mkoani Mwanza.

SERIKALI YAJA NA MIKAKATI MIPYA YA KUHAKIKISHA UTALII WA NDANI UNAKUA

 ME2
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii,Bi. Uzeeli Kiangi akisisitiza jambo wakati alipokuwa anamkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja. Generali. Gaudence Milanzi kufungua Mkutano Mkutano wa Kamati ya Uwezeshaji Utalii ( Tourism Facilitation Committee- TFC) uliofanyika leo Mpingo House jijini Dar es Salaam wa kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii nchini.
ME1
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja. Generali. Gaudence Milanzi ( kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii Bw. Deogratius Mdamu (kushoto) wakimsikiliza Mjumbe ( hayupo pichani ) wakati wa Mkutano wa Kamati ya Uwezeshaji Utalii ( Tourism Facilitation Committee- TFC) uliofanyika leo Mpingo House jijini Dar es Salaam akiwa anazungumzia changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii nchini na kutoa ushauri ya namna kuuimarisha Utalii wa ndani ambao umekuwa bado ni changamoto kwa wananchi wengi kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini
ME3
 Baadhi ya Wajumbe wa kamati ya Uwezeshaji Utalii ( Tourism Facilitation Committee- TFC) wakiwa wanajadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii nchini kwa kutoa maoni, ushauri na ufumbuzi wa changamoto ikiwa na kuchangia mikakati mbalimbali itakayowezesha kusaidia kuhamasisha Utalii wa ndani.
…………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu
Wakati nchi nyingi Afrika zikiwa zinafanya jitihada mbalimbali za kuimarisha Utalii wa ndani ambao umekuwa ndo wa uhakika katika kuiingizia nchi mapato hata pale majanga yanapotokea, Nayo Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeendelea kuhakikisha kuwa Utalii wa ndani unakua kwa kasi inayotarajiwa.
Baadhi ya Majanga hayo yanayoathiri Sekta ya Utalii ni milipuko ya magonjwa kama Ebola, matukio ya Ugaidi Kenya na kushuka kwa Euro ya Ulaya dhidi ya Dola ya Marekani.
Hivyo Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wadau wa Utalii nchini wamepanga mikakati ya kuhakikisha kuwa Utalii wa ndani unakuwa tegemeo tofauti na sasa ambapo Watalii kutoka nje ndio wamekuwa wamekuwa wakitembelea hifadhi zetu kwa kiasi kikubwa.
Akizungumza kwenye Mkutano wa Kamati ya Uwezeshaji Utalii ijulikanayo kama Tourism Facilitation Committee ( TFC) uliofanyika leo Mpingo House jijini Dar esSalaam , Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili, Meja. Generali. Gaudence Milanzi na Utalii amesema maendeleo ya Utalii yanahitaji sana Utalii wa ndani kuimarika baadala ya kudhani kuwa vivutio vya utalii vilivyopo ni kwa ajili ya wageni kutoka nchi za nje.
Meja. Generali. Milanzi amesema Utalii ni sekta nyeti sana katika kuliingiza Taifa pesa za kigeni lakini hata hivyo ni sekta ambayo imekuwa inaathirika kwa haraka sana pindi majanga yanapotokea nchi jirani hivyo ni lazima jamii ijengewe utamaduni wa kutembelea vivutio vya Utalii ili kuweza kujihakikishia Watalii wa ndani wanakuwa wengi.
Baadhi ya mikakati iliyopendekezwa na Wajumbe wa kamati ya Uwezeshaji Utalii (TFC) ni kuwawezesha maafisa Utalii wa Halmashauri wanatengewa bajeti ya kutosha, wanajengewa uwezo kuhusu ya vivutio vya utalii vilivyopo kwenye maeneo yao pamoja na Idara ya Utalii kufungua ofisi kila kanda ili kuweza kutimiza majukumu yake ipasavyo.
Aidha,viwanja vya ndege vilivyopo nchini viimarishwe ikiwa pamoja na nchi kuwa ndege zake kama ilivyo kwa nchi jirani kama Kenya na Rwanda
Awali , Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii,Bi. Uzeeli Kiangi alisema Mkutano wa TFC hutoa fursa za kuziibua na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Utalii hivyo Sekta Binafsi zinawajibu mkubwa wa kuhakikisha changamoto zinazoikabili sekta zinatafutiwa ufumbuzi
Aliongeza kuwa Idara ya Utalii imekuwa ikishiriki katika maonesho mbalimbali ya kitaifa lengo likiwa ni kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kutembelea vivutio vya Utalii nchini.
Aidha, Prof Wineastor Anderson amesema sekta ya Utalii imekuwa inakua lakini si kwa kiwango cha kuridhisha hivyo jitihada za kutangaza utalii ndani na nje nchi upewe uzito unaostahili kwa kuiwezesha Bodi ya Taifa ya Utalii inatengewa bajeti ya kutosha.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Utalii Tanzania ( TCT) Bw. Richard Rugimbana, amesema Utalii wa ndani ili uweze kukua suala la elimu linahitajika kutolewa ili kuweza kuibadilisha jamii ipende kutembelea vivutio vya Utalii.
Naye Kamanda wa Polisi Jk Ndaki anayeshghulikia dawati la Utalii ( Tourism Police Unit) amewahakikishia usalama wao watalii wa ndani na nje ya nchi kutembelea vivutio vya Utalii bila hofu yoyote kuwa Jeshi la Polisi nchini lipo macho muda wote.

No comments :

Post a Comment