Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi wa
Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha waliojitokeza kumsalimia wakati
akielekea Monduli kwa ajili ya kufunga zoezi la Onesha uwezo Medani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisoma bango mara baada ya
kukabidhiwa na mwananchi mmoja katika eneo la Kona ya Nairobi Mkoani
Arusha
Umati mkubwa uliojitokeza katika eneo la Mianzini Mkoani Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa
Arusha katika eneo karibu na chuo cha Arusha Tech. Wananchi hao
walifunga barabara ili wapate nafasi ya kumuona Mheshimiwa Rais Dkt.
Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Mianzini Mkoani Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu
wa Majeshi ya Ulinzi Nchini General Davis Mwamunyange wakati waufungaji
wa zoezi la Onesha Uwezo Medani lililofanyika Monduli nje kidogo ya Jiji
la Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Mkuu
wa Majeshi ya Ulinzi Nchini General Davis Mwamunyange wakati akielekea
kupewa maelezo ya zoezi zima la Onesha Uwezo Medan.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya
Maafisa wa jeshi katika tukio hilo la Ufungaji.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akielekea kwenye uwanja wa
maonesho akiwa pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini General Davis
Mwamunyange.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya
pamoja na Maafisa wa ngazi za juu wa Jeshi mara baada ya kufunga zoezi
la Onesha Uwezo Medani Monduli Mkoani Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katikati akishuhudia
matukio ya zoezi la Onesha Uwezo Medani Monduli Mkoani Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipewa maelezo ya zana
mojawapo ya Kivita katika Zoezi la Onesha Uwezo Medani Mkoani Arusha.
Picha na IKULU
…………………………………………………………………………………………………………..
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunga “Zoezi la Onesha Uwezo
Medani” lililoandaliwa na kutekelezwa na Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
ambalo ni sehemu ya Jeshi la wananchi Tanzania katika eneo la
Lang’arurusu nje kidogo ya Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli Mkoani
Arusha.
Akizungumza na Askari na Maafisa
wa Jeshi la wananchi Tanzania kabla ya kufunga zoezi hilo, Rais Magufuli
amesema katika awamu yake ya tano ya uongozi amedhamiria kulitumia
Jeshi la wananchi Tanzania katika kujenga uchumi, ikiwemo kuanzisha
viwanda na kampuni za ujenzi ili kuharakisha maendeleo.
Ametoa mfano wa kiwanda cha
Nyumbu ambacho kipo chini ya jeshi la wananchi Tanzania na kueleza kuwa
wakati umefika wa kukiimarisha na kukiendeleza kiwanda hicho, ili kiweze
kufanya uzalishaji mkubwa kwa manufaa ya nchi ikilinganishwa na hali
ilivyo hivi sasa.
“Zipo nchi nyingi ambazo
majeshi yao yanatumika katika uchumi na yanafanya kazi nzuri ya kupigiwa
mfano, wakati umefika na sisi kufanya hivyo. Hata hizi sare za jeshi na
viatu, hatuna sababu ya kuvinunua kutoka nje ya nchi, tunaweza
kutengeneza sisi wenyewe” Alisisitiza Rais Magufuli.
Rais Magufuli amelipongeza Jeshi
la wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kuandaa “Zoezi Onesha Uwezo Medani”
ambalo limethibitisha uwezo, weledi na utayari lilionao katika jukumu
lake la kiulinzi.
Ameahidi kuwa ataendeleza juhudi
zilizofanywa na viongozi wenzake waliotangulia za kuliimarisha kwa
vitendea kazi na maslai ya wanajeshi ili liweze kutekeleza wajibu wake
bila vikwazo.
Pamoja na kuwapongeza Askari na
maafisa wa Jeshi la wananchi Tanzania walioshiriki katika zoezi hilo,
Rais Magufuli ameagiza Askari Mgambo na Askari wa Jeshi la kujenga Taifa
(JKT) walioshiriki zoezi hilo kuajiriwa na jeshi la wananchi Tanzania.
Akitoa maelezo ya awali kabla ya
hotuba ya Rais Magufuli, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt.
Hussein Ali Mwinyi, amesema Wizara yake itaongeza na kusimamia juhudi
za kuliboresha jeshi hilo kwa zana, vifaa na maslai kwa wanajeshi ili
kuwajengea uwezo na morali ya kutekeleza majukumu yao ya kuilinda nchi,
pamoja na kutoa msaada stahiki kwa nchi zenye kuhitaji ulinzi wa amani
popote duniani.
Kwa upande wake Mkuu wa majeshi
ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Adolf Mwamunyange amemhakikishia Rais
Magufuli kuwa Jeshi la wananchi Tanzania lipo imara na litaendelea
kutekeleza majukumu yake kwa weledi, nidhamu ya hali ya juu na uzalendo
mkubwa.
Kabla ya kuwahutubia maafisa wa
jeshi la wananchi, Askari na wananchi waliohudhuria ufungaji wa “Zoezi
Onesha Uwezo Medani”, Rais Magufuli ameoneshwa zana mbalimbali za kivita
ikiwa ni pamoja na kushuhudia upigaji wa mizinga ya masafa mafupi,
masafa ya kati na masafa marefu.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Arusha
22 Januari, 2016
Nyota wa kikapu wa Malawi kuzikabili timu za Dar es salaam
Mratibu
wa Sprite BBall Kitaa Karabani Karabani akiongea na waandishi wa habari
leo jijini Dar-es- Salaam kuhusu mechi za kirafiki zitakazochezwa
Jumamosi na Jumapili katika uwanja wa BBK Park na timu kutoka Malawi. Wa
kwanza kulia waliokaa ni mkurugenzi wa ufundi chama cha mpira wa kikapu
Malawi Obed Nyirongo, wengine ni wachezaji wa timu ya Bricks na Brave
Hearts.
Mkurugenzi
wa ufundi chama cha mpira wa kikapu Malawi Obed Nyirongo kiongeana
waandishi wa wa habari leo jijini Dar-es- Salaam kuhusu mechi za
kirafiki zitakazochezwa Jumamosi na Jumapili katika uwanja wa BBK Park
na timu kutoka Malawi wa Sprite BBall Kitaa. Wa kwanza kushoto waliokaa
ni mratibu wa Sprite BBall Kitaa Karabani Karabani na wengine ni
wachezaji wa timu ya Bricks na Brave Hearts.
*************************
Miamba
miwili ya mpira wa kikapu kutoka nchini Malawi imewasili jijini Dar es
Salaam leo kwa ajili ya mfululizo wa mechi za kirafiki za kimataifa
dhidi ya timu za bigwigs Jogoo, East Zone One, Mbezi na West Zone Three.
Mechi hizo zenye hamasa ya aina yake zitachezwa kwenye uwanja Bball
Kitaa Park, karibu na Ukumbi wa Gymkhana.
Kulingana
na ratiba iliyotolewa na mratibu wa Bball Kitaa Karabani Karabani pazia
la michezo hiyo litafunguliwa kesho ambapo East Zone One watakipiga na
Bricks, mchezo unaotabiriwa kuwa ni mgumu na wa kusisimua. Siku hiyo
hiyo Mbezi watacheza na Associate Team, mchezo ambao pia unatazamiwa
kuwa na ushindani mkubwa.
Michezo
hiyo bado itaendelea kuwateka wakazi wa jiji la Dar es Salaam, ambapo
West Zone Three watapambana na Bricks kabla ya Jogoo kuwakaribisha
Associate team. “Tuna furaha kubwa kuandaa michezo hii ya kirafiki. Ni
moja ya sehemu muhimu katika kudumisha mahusiano, vile vile kuendeleza
vipaji vinavyochipukia”, Karabani alisema.
Ujio
wa Bricks na Associate teams jijini Dar es Salaam imeonekana si jambo
geni baada ya timu za East Zone One na West Zone Three kwenda Malawi
mwaka jana. Zikiwa nchini humo, timu hizo zilishinda mechi zao kadhaa.
Karabani
ambaye michuano yake ya mpira wa kikapu iko chini ya udhamini wa
Sprite, amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuibua na kukuza vipaji vya
vijana kwa kipindi cha miaka mitatu ambapo michuano hiyo imekuwa
ikifanyika. Vilevile michuano hii inatoa fursa ya kuendeleza ushirikiano
baina ya maeneo mbalimbali ya ndani ya nje ya nchi.
“Lengo
letu ni kuanzisha michuano ngazi ya kanda mwishoni mwa mwaka huu,
ambapo mabingwa kutoka Tanzania, Malawi, Zambia na Zimbabwe”, Karabani
alisema na kuongeza kuwa uzinduzi wa michuano hiyo utafanyika nchini
Malawi
Kwa
upande wake, Meneja Biashara wa Coca-Cola nchini, Maurice Njowoka
alisema anajisikia furaha kubwa kutokana na heshima waliopewa kuisapoti
michuano hiyo hapa nchini na kusisitiza kuwa kampuni yake itaendeleza
ushirikiano wake na wadau wa mchezo wa kikapu kuzidi kuutangaza mchezo
huo.
“Sote
tunafahamu kuwa mpira wa kikapu ni moja ya michezo maarufu na yenye
nguvu nchini, hasa miongoni mwa vijana ambao wanahitaji aina hii ya
msaada ili kuhamasika na kuweza kuendeleza vipaji vyao”, Njowoka
alisema.
TIGO WAZINDUA UDHAMINI WA MBIO ZA NUSU MARATHON MJINI MOSHI
ASHANTI YAONDOLEWA KOMBE LA SHIRIKISHO
Kikao cha Kamati ya Mashindano ya
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kilichoketi jana na kupitia
taarifa mbalimbali za michezo ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports
Federation Cup) mzunguko wa pili, kimeiondoa klabu ya Ashanti United
kwenye michuano hiyo na nafasi yake kuchukuliwa na klabu ya Africa Lyon.
Katika kikao hicho kamati
ilipokea malalamiko ya klabu ya Africa Lyon dhidi ya Ashanti United kwa
kumchezesha mchezaji Enock Balagashi kwa jina la Awesu Abdu katika
mchezo namba 3, uliochezwa tarehe 15 Disemba, 2015 na Ashanti kuibuka na
ushindi kwa mikwaju ya penati.
Kamati imejiridhisha baada ya
kupitia taarifa ya mchezo huo, na kubaini klabu ya Ashanti United
ilifanya udanganyifu wa kumtumia mchezji huyo kwa jina la mchezaji
mwingine, huku ikitambua kuwa kufanya hivyo ni makosa na mchezo huo
ulikuwa ukionyeshwa moja kwa moja kwenye kituo cha luninga cha Azamtv.
Kwa mujibu wa Kanuni no. 41 (12)
ya uthibiti wa viongozi kufungiwa miezi 12, Kamati imemfungia Katibu
Mkuu wa klabu ya Ashanti kutojihusisha na masuala ya mpira wa miguu kwa
kipindi cha miezi 12.
Aidha Kamati pia kwa kutumia
kanuni ya 37 (15) ya udhibiti wa wachezaji, mchezaji Enock Balagashi
amefungiwa kwa kucheza mpira kwa kipindi ch amiezi 12 na faini ya
shilingi laki tatu (300,000).
Kamati imevitaka vilabu vya ngazi
zote nchini kuheshimu vipindi vya usajili kwa kufanya usajili wa
wachezaji watakaowatumia, na kuheshimu kanuni na taratibu zinazoendesha
michuano inayoandaliwa na TFF.
Africa Lyon watacheza dhidi ya Azam FC mznguko wa tatu siku ya Jumatatu katika Uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.
Watumishi NEC wapongezwa kwa kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2015
Afisa Ufuatiliaji toka Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bw. Ambrose Manyanda akielezea mafao
mbalimbali yanayotolewa na mfuko huo kwa watumishi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) hawapo pichani, wakati wa kikao kazi kilichofanyika
mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
: Afisa Ushirika toka Manispaa ya
Ilala Bi. Mihayo Malunde akielezea umuhimu wa Watumishi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuanzisha kikundi cha akiba na mikopo (SACCOS)
wakati wa kikao kazi kilichofanyika mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi Bw. Ramadhan Kailima (aliyesimama) akiwakaribisha wajumbe na
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya uchaguzi wakati Wajumbe hao na Mwenyekiti
walipokwenda kuwashukuru na kuwapongeza watumishi wa tume hiyo kwa
kuweza kufanikisha zoezi la uchaguzi kwa mafanikio makubwa.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi Jaji Damian Lubuva akiongea na watumishi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) wakati alipokwenda kuwashukuru na kuwapongeza watumishi
wa tume hiyo kwa kuweza kufanikisha zoezi la uchaguzi kwa mafanikio
makubwa mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi Bw. Ramadhan Kailima (aliyesimama) akifurahia jambo na
watumishi wa tume hiyo wakati Wajumbe na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya
uchaguzi walipokwenda kuwashukuru na kuwapongeza watumishi wa tume
hiyo kwa kuweza kufanikisha zoezi la uchaguzi kwa mafanikio makubwa
Picha zote na Eliphace Marwa -Maelezo
RIPOTI YA TATHMINI MAZINGIRA YA KISHERI KATIKA MWITIKIO WA UKIMWI TANZANIA YA ZINDULIWA DAR ES SALAAM
Mkurugenzi
Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar (ZAC), Dk.Ali Ali (katikati), Kaimu
Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania
(TACAIDS), Jumanne Issango (kushoto) na Naibu Mkurugenzi Mwakilishi wa
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo (UNDP), Titus
Osundina wakikata utepe kwa pamoja kuashiria uzinduzi wa ripoti ya
tahmini ya mazingira ya kisheria katika mwitikio wa ukimwi katika
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanyika Makao Makuu ya Tacaids Dar
es Salaam leo asubuhi.
Viongozi
hao wakiwaonesha wageni waalikwa na wadau mbalimbali ripoti hiyo.
Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Sheria wa Tacaids, Elizabeth Kaganda na
kilia ni Dk.Bwijo Bwijo kutoka UNDP.
Naibu
Mkurugenzi Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
Maendeleo (UNDP), Titus Osundina, akihutubia wakati wa uzinduzi wa
ripoti hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar (ZAC), Dk.Ali Ali (kushoto), Kaimu Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya
Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Jumanne Issango (katikati) wakimpongeza Naibu
Mkurugenzi Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo (UNDP), Titus Osundina baada ya kuhutubia.
Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Jumanne Issango (katikati) wakimpongeza Naibu
Mkurugenzi Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo (UNDP), Titus Osundina baada ya kuhutubia.
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Wanahabari wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Uzinduzi ukiendelea.
| Wadau wakiwa katika uzinduzi huo. |
| Picha ya pamoja na viongozi. |
Wasanii wa Hisia Threatel
Group kutoka Sandali Temeke jijini Dar es Salaam wakionesha igizo
linalohusu ukimwi katika uzinduzi huo.
ZANTEL YATOA 20 M/- KUSAIDIA WANAFUNZI WENYE UONI HAFIFU KISIWANDUI
MKURUGENZI Mkuu wa Zantel, Benoit
Janin akisaini barua ya kampuni yake kwa ajili ya kuwa mlezi wa darasa
la wanafunzi wenye ulemavu wa uoni wa skuli ya msingi Kisiwandui mjini
Zanzibar. Zantel pia walikabidhi msaada wa shilingi milioni 20 kwa ajili
ya kununulia vifaa vya matumzi ya wanafunzi hao. Wengine kutoka kulia
ni Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo Bi. Taifa Ahmed Khamis, Mkurugenzi wa
Elimu ya Maandalizi na Msingi, Bi. Safia Ali Rijali, na mwisho kushoto
ni Shinuna Kassim, Mkurugenzi wa Mipango ya Biashara wa Zantel.
MKURUGENZI Mkuu wa kampuni Zantel,
Benoit Janin akimkabidhi Mwalimu Mkuu, Bi. Taifa Ahmed Khamis mfano wa
hundi ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya kununulia vifaa vya wanafunzi
wenye ulemavu wa uoni wa skuli ya msingi Kisiwandui.
…………………………………………………………….
Na Salum Vuai
KAMPUNI ya simu ya Zantel, leo imeukabidhi uongozi wa skuli ya msingi Kisiwandui hundi ya shilingi milioni 20, kwa ajili ya kununulia vifaa vya wanafunzi wenye uoni hafifu.
Hundi hiyo ilikabidhiwa kwa mwalimu mkuu wa skuli hiyo Bi. Taifa Ahmed Khamis, na Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Bw. Benoit Janin, katika hafla fupi iliyofanyika skulini hapo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Janin alisema msaada huo ni sehemu ya mikakati ya kampuni yake, katika kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata elimu bora bila kujali tofauti za kimaumbile.
Alieleza kuwa, ni wajibu wa kampuni hiyo kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata msaada kama wanavypata watu wengine, na pia kuweza kuwaandaa kwa ajili ya kuweza kufikia malengo yao kama walivyokusudia.
“Kama sehemu ya jamii, tumedhamiria kuwasaidia kuwasaidia wanafunzi wenye ulemavu kwa kuwapatia vifaa wanavyovihitaji ili waweze kupata elimu bora,” alieleza Mkurugenzi huyo.
Aidha, alisema kuanzia leo, kampuni yake imeamua kuwa mlezi wa darasa la wanafunzi wenye uoni hafifu katika skuli hiyo, kwa kuwapatia mahitaji yao ili waweze kusoma bila matatizo.
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo Bi. Taifa Ahmed Khamis, akiushukuru uongozi wa Zantel, alisema msaada huo ni wa kipekee na utarahisisha ufundishaji kwa wanafunzi hao wenye matatizo ya uoni, na hivyo kuwawezesha kupata elimu bora kama ilivyo kwa wengine.
“Tunawashukuru Zantel kwa kuziona changamoto zinazotukabili, na hakika msaada huu utatusaidia katika kuwafundisha wanafunzi hawa na pia kuwawezesha kufikia malengo yao,” alifafanua.
Alitaja miongoni mwa changamoto hizo kuwa ni mashine za nukta nundu, karatasi za kuchapishia, miwani pamoja na fimbo maalumu kwa watu wasioona (white canes).
Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Maandalizi na Msingi Bi. Safia Ali Rijali, pamoja na kuishukuru Zantel katika kusaidia jitihada za serikali kuleta maendeleo, alisema elimu ni muhimu kwa kila mwananchi hata wenye ulemavu.
Aliwasisitiza wazazi na walezi kutowatenga watoto wenye ulemavu kwa kuwakosesha haki ya kusoma, kwani wakipewa fursa wanaweza kufanya makubwa na kuwa mfano kwa wengine.
Alitoa mfano wa mwanafunzi mmoja asiyeona aliyekuwa akisoma Kisiwandui, kwa namna alivyokuwa mahiri hata akaweza kuchukua digrii ya sheria.
Mkurugenzi huyo ameziomba taasisi na kampuni nyengine kuiga mfano wa Zantel kujikita katika kusaidia jamii kwa mahitaji mbalimbali, yakiwemo ya kielimu, kiafya na mengine.
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO-ZANZIBAR- JANUARI 22, 2016
KAMPUNI ya simu ya Zantel, leo imeukabidhi uongozi wa skuli ya msingi Kisiwandui hundi ya shilingi milioni 20, kwa ajili ya kununulia vifaa vya wanafunzi wenye uoni hafifu.
Hundi hiyo ilikabidhiwa kwa mwalimu mkuu wa skuli hiyo Bi. Taifa Ahmed Khamis, na Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Bw. Benoit Janin, katika hafla fupi iliyofanyika skulini hapo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Janin alisema msaada huo ni sehemu ya mikakati ya kampuni yake, katika kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata elimu bora bila kujali tofauti za kimaumbile.
Alieleza kuwa, ni wajibu wa kampuni hiyo kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata msaada kama wanavypata watu wengine, na pia kuweza kuwaandaa kwa ajili ya kuweza kufikia malengo yao kama walivyokusudia.
“Kama sehemu ya jamii, tumedhamiria kuwasaidia kuwasaidia wanafunzi wenye ulemavu kwa kuwapatia vifaa wanavyovihitaji ili waweze kupata elimu bora,” alieleza Mkurugenzi huyo.
Aidha, alisema kuanzia leo, kampuni yake imeamua kuwa mlezi wa darasa la wanafunzi wenye uoni hafifu katika skuli hiyo, kwa kuwapatia mahitaji yao ili waweze kusoma bila matatizo.
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo Bi. Taifa Ahmed Khamis, akiushukuru uongozi wa Zantel, alisema msaada huo ni wa kipekee na utarahisisha ufundishaji kwa wanafunzi hao wenye matatizo ya uoni, na hivyo kuwawezesha kupata elimu bora kama ilivyo kwa wengine.
“Tunawashukuru Zantel kwa kuziona changamoto zinazotukabili, na hakika msaada huu utatusaidia katika kuwafundisha wanafunzi hawa na pia kuwawezesha kufikia malengo yao,” alifafanua.
Alitaja miongoni mwa changamoto hizo kuwa ni mashine za nukta nundu, karatasi za kuchapishia, miwani pamoja na fimbo maalumu kwa watu wasioona (white canes).
Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Maandalizi na Msingi Bi. Safia Ali Rijali, pamoja na kuishukuru Zantel katika kusaidia jitihada za serikali kuleta maendeleo, alisema elimu ni muhimu kwa kila mwananchi hata wenye ulemavu.
Aliwasisitiza wazazi na walezi kutowatenga watoto wenye ulemavu kwa kuwakosesha haki ya kusoma, kwani wakipewa fursa wanaweza kufanya makubwa na kuwa mfano kwa wengine.
Alitoa mfano wa mwanafunzi mmoja asiyeona aliyekuwa akisoma Kisiwandui, kwa namna alivyokuwa mahiri hata akaweza kuchukua digrii ya sheria.
Mkurugenzi huyo ameziomba taasisi na kampuni nyengine kuiga mfano wa Zantel kujikita katika kusaidia jamii kwa mahitaji mbalimbali, yakiwemo ya kielimu, kiafya na mengine.
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO-ZANZIBAR- JANUARI 22, 2016
AHUKUMIWA MIAKA 19 JELA KWA KUIBA MBUZI MKOANI MBEYA
Na Ezekiel Kamanga,,Mbozi.
…………………………………………….
MAHAKAMA ya mwanzo vwawa mjini wilayani Mbozi mkoani Mbeya imemuhukumu Patrick Moses(19) mkazi wa Ilembo kutumikia jela miaka mitano baada ya kukiri kosa la kuiba Mbuzi mmoja mwenye thamanai ya Sh 85,000 mali ya Bahati Mtafya.
Akisoma
hukumu hiyo hakimu wa mahakama hiyo,lazima Mwaijega alisema kutokana
kifungu cha sheria 268 na mshitakiwa kukiri kosa hivyo mahakama imeamuru
mshitakiwa kutumikia kifungo hicho ili iwe fundisho kwake na kwa
wengine wenye nia ya kutenda kosa kama hilo.
Mshitakiwa
alipopewa nafasi ya kujitetea aliiomba mahakama kumpunguzia adhabu
kwani anategemewa na familia yake,hata hivyo hakimu Mwaijega amesema
kifungo hicho cha miaka mitano amepunguziwa pia kwa kuwa ni kosa lake la
kwanza na kwamba.
Awali imeelezwa mahakamani na mwendesha mashitaka wa polisi Hamis Mohamed kuwa January 20,mwaka huu saa 11 jioni mshitakiwa
alivamia nyumbani kwa Bahati Mtafya (38) na kuiba mbuzi mmoja mwenye
thamani ya Sh. 85,000 huku akijua kufanya vyo ni kosa kisheria namba 229
sura ya 16 kanuni ya adhabu.
Aidha
mwendesha mashitaka huyo aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa
mshitakiwa ili iwe fundisho kwake na kwa wale wenye nia ya kutendakosa
kama hilo kutokana na wimbi kubwa la vijana kujikita katika wizi na
kuacha kufanya kazi halali.
Katika
hatua nyingine mshitakiwa huyo alipandishwa kizimbani hapo kujibu
tuhuma ya wizi wa kuku 23 wenye thamani ya Sh laki 4 mali ya Evance
Mwakenja mkazi wa Ilembo Vwawa
Imeelezwa
mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa polisi Hamis Mohamed kuwa
tukio hilo lilitokea januari 20 mwaka huu saa 8 usiku ambapo mshitakiwa
aliiba kuku 23 wenye dhamani ya Sh.laki 4 mali ya Evance Mwakenja huku
akijua kufanya hivyo nikosa kisheria.
Hata
hivyo mshitakiwa alikana shitaka linalomkabili na hakimuwa mahakama
hiyo Chirstina Mlwilo amesema shauli hilo litaanza kusikilizwa Januari
27 mwaka huu,pia hakimu huyo amesema dhamana kwa mshitakiwa ipo wazi kwa
ahadi ya Sh.laki 4 pamoja na kuwa na wadhamini wawili wenye vitambulisho vya mpiga kura.
Hata hivyo mshitakiwa ameludiswa maabusu kwa kushindwa kutimiza masharti la dhamana pamoja na kuanza kutumikia kifungo cha miaka mitano ya wizi wa mbuzi.
Serikali kuendelea kutoa elimu ya Uzalishaji na matumizi endelevu ya rasilimali
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya
Mipango Miji kutoka Wizara ya Ardhi,|Nyumba na Maendeleo ya Makazi
George Pangawe akizungumza na Waandishi wa Habari (Hawapo Pichani)
kuhusu wananchi kuzingatia sheria na kanuni za mipango miji nchini pale
wanapotaka kuendeleza ardhi kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya
Mazingira kutoka Baraza la Taifa la Mazingira Carlos Mbuta na kulia ni
Mkuu wa Idara ya Mipango Miji, Ardhi na Mazingira Manispaa ya Kinondoni
Bi. Juliana Letara
Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya
Mazingira kutoka Baraza la Taifa la Mazingira Carlos Mbuta akizungumza
na Waandishi wa Habari (Hawapo Pichani) kuhusu elimu ya uzalishaji na
matumizi endelevu ya rasilimali ili waweze kunufaika na rasilimali hizi
ambapo elimu hiyo imeingizwa katika mitaala ya elimu hapa nchini kulia
ni Msaidizi Idara ya Mipango Miji kutoka Wizara ya Ardhi,|Nyumba na
Maendeleo ya Makazi George Pangawe.
Mkuu wa Idara ya Mipango Miji,
Ardhi na Mazingira Manispaa ya Kinondoni Bi. Juliana Letara akisisitiza
jambo kwa Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam kulia ni Msaidizi
Idara ya Mipango Miji kutoka Wizara ya Ardhi,|Nyumba na Maendeleo ya
Makazi George Pangawe na kushoto ni
Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya Mazingira kutoka Baraza la Taifa la Mazingira Carlos Mbuta
Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya Mazingira kutoka Baraza la Taifa la Mazingira Carlos Mbuta
Baadhi ya Waandishi wa Habari
wakifatilia mkutano uliondaliwa na, Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Baraza la mazingira na Manispaa ya Kinondoni
uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam
(Picha na Frank Mvungi-MAELEZO)
……………………………………………………………………………………………………………………………….
Hassan Silayo-MAELEZO
Serikali kuendelea kutoa elimu ya Uzalishaji
na matumizi endelevu ya rasilimali kwa wananchi ili waweze kunufaika na
rasilimali zote zilizopo katika maeneo yao kote nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es
salaam na Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya Mazingira kutoka Baraza la Taifa
la Mazingira (NEMC) Bw.Carlos Mbuta wakati wa mkutano na vyombo vya
Habari ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali katika kuelimisha umma
kuhusu matumizi sahihi ya rasilimali ikiwemo ardhi.
Akifafanua Mbuta amesema kuwa Elimu hiyo
itawasaidia wananchi kungamua na kufanya maamuzi sahihi pale wanapotaka
kutumia rasilimali zilizopo katika kujiletea maendeleo.
’Elimu ya mazingira imejumuishwa katika
mitaala ya shule zetu hapa nchini ili kujenga uelewa kuhusu matumizi
sahihi ya rasilimali alisisitiza Mbuta
Akizungumzia faida za Elimu ya Mazingira
kutlowa mashuleni mbuta alibainisha kuwa itasaidia kujenga kizazi chenye
uelewa na uwezo wa kutumia rasilimali zilizopo kwa kuzingatia sheria na
kanuni.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Idara
ya Mipango Miji kutoka Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw.
George Pangawe alitoa wito kwa wananchi kufuata taratibu zote za
kisheria pale wanapotaka kuendeleza Kipande chochote cha ardhi.
Aliongeza kuwa Serikali kupitia Wizara yake
inasimamia matumizi sahihi ya uendelezaji wa ardhi na kuwataka wananchi
kuunga mkono juhudi za Serikali katika kusimamia Sheria na Kanuni
zinazosimamia Sekta ya ardhi.
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya
Makazi kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Mazingira pamoja na
Halmashuri zote nchini zimekuwa zikisisitiza kuhusu elimu ya uzalishaji
na matumizi endelevu ya rasilimali ili ziweze kuwanufaisha wananchi.
MH. MAJALIWA AONGOZA MKUTANO WA WABUNGE
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akifungua mkutano wa wabunge, bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016.
Kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai na kushoto ni Katibu wa Bunge Dkt.
Thomas Kahilillah. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Spika wa Bunge Job Ndugai
akizungumza kumkaribisha Mwenyekiti wa Mkutano wa Wabunge, Waziri Mkuu,
Kassim Majliwa kufungua mkutano huo bungeni mjini Dodoma Januari 22,
2016. Kulia ni Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilillah. (Picha na Ofisi
ya Waziri Mkuu)
Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge,
Nenelwa Mwihambi akitoa mada katika mkutano wa wabunge ulioongozwa na
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, buneni mjini Dodoma Januari 22, 2016.
Watatu kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai na kulia ni Katibu wa Bunge,
Dkt. Thomas Kashilillah.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Wabunge, Jenista Mhagama wa
Peramiho (kushoto) na January Makamba wakiteta katika mkutano wa
wabunge, bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
George Masaju akitoa mada katika mkutano w wabunge , bungeni mjini
Dodoma Januari 22, 20167. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisalimiana na Mbunge wa Mafinga mjini Cosato Chumi kwenye viwanja vya
Bunge mjini Dodoma Januari 22, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akifurahia jambo na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari wakati
aaliposalimiana naye kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januari 22,
2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa
akisalimiana na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari kwenye
viwanja vya Bunge mjini Dodoma Januari 22, 2016. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)

No comments :
Post a Comment