……………………………………………………….
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Mhe. Rais Dkt. Magufuli amemteua
aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
kwenye Serikali ya Awamu ya Nne Mahadhi Juma Maalim kuwa Balozi wa
Tanzania nchini Kuwait kufuatia uamuzi wa Serikali kufungua Ofisi ya
Ubalozi katika nchi hiyo rafiki.
Vile vile Rais ameagiza Wizara
ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa
kuwarejesha nyumbani mara moja Mabalozi wawili ambao mikataba yao
imeisha na kuwataka Mabalozi hao kukabidhi kazi kwa Afisa Mkuu au
Mwandamizi aliyechini yao leo hii.
Mabalozi hao ni Bi Batilda Salha Buriani, aliyeko Tokyo, Japan, Dkt. James Alex Msekela, aliyeko Rome, Italia.
Kwa mujibu wa Balozi Sefue, Rais
pia amemrejesha nyumbani Balozi wa Tanzania aliyeko London, Uingereza,
Bwana Peter Allan Kallaghe ambaye anarejea Wizara ya Mambo ya Nje,
Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa ambapo
atakapopangiwa kazi nyingine.
Balozi Sefue alisema kuwa hadi
sasa vituo vya Ubalozi ambavyo viko wazi ni London nchini Uingereza
kufuatia kurejea nchini kwa Balozi Peter A. Kallaghe, Brussels nchini
Ubelgiji kufuatia aliyekuwa Balozi, Dkt. Deodorous Kamala kuchaguliwa
kuwa Mbunge, Rome nchini Italia, kufuatia kuisha kwa mkataba wa Dkt.
James Alex Msekela na Tokyo nchini Japan, kufuatia kuisha kwa mkataba wa
Bibi Batilda Buriani.
Vituo vingine vya Ubalozi
ambavyo viko wazi ni Kuala Lumpar nchini Malaysia, kufuatia aliyekuwa
Balozi Dkt. Aziz Ponray Mlima kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya
Mambo ya Nje, Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa na
Brasilia nchini Brazil, kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa Balozi, Bwana
Francis Malambugi.
Wakati huo Balozi Sefue alisema kuwa Rais ametengua uteuzi wa Mhandisi Madeni Juma Kipande kabla hajathibitishwa kwenye cheo cha
Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi kutokana na utendaji kazi usioridhisha.
High Level Meeting For Identification of Education Priorities for formulation of the Education Sector Development Plan (ESDP) and the 5 Year Development Plan
Dar es Salaam, 25 January 2016
The United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO) is supporting the Ministry of Education, Science and Technology in developing the Education Sector Development Plan (ESDP) for 2017-2021. The Plan intends to direct the Government of Tanzania’s quinquennium goals, objectives and strategies for its Mainland’s education sector.
In close collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), UNESCO will facilitate a two days High Level workshop from 26th to 27th January 2016, at the National Council for Technical Education (NACTE).
Overall, the workshop aims to identify education priorities required for formulation of outcomes, strategies and outputs of the education sector for the next 5 years
The meeting will be chaired by the Commissioner of Education, Professor Eustella Bhalalusesa and will bring together Senior government officials from MoEST and Education Institutes, the President’s Office Regional Administration and Local Government (PO-RALG), Development Partners and Civil Society Organizations representatives as well as members of the Academia. The UNESCO team, will be led by the International Institute for Education Planning (IIEP) and further composed by experts from the UNESCO Institute of Lifelong Learning (UIL), the Education and TVET Units of the HQs and the Dar es Salaam Office.
The workshop proceedings will enable the alignment of the ESDP with the Education priorities of the Five Year Development Plan (FYDPII), taking into consideration as well the key national and international policies and agendas including the new Education and Training Policy (2014) and the Education 2030 Agenda and Framework for Action.
Following the prioritization, the exercise will continue with a smaller number of Government officials for the further formulation of the expected outcomes and targets for identified priorities.
For more information please contact;
Petro Makuru (makurupetro@gmail.com) and Faith Shayo, (f.shayo@unesco.org)
The United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO) is supporting the Ministry of Education, Science and Technology in developing the Education Sector Development Plan (ESDP) for 2017-2021. The Plan intends to direct the Government of Tanzania’s quinquennium goals, objectives and strategies for its Mainland’s education sector.
In close collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), UNESCO will facilitate a two days High Level workshop from 26th to 27th January 2016, at the National Council for Technical Education (NACTE).
Overall, the workshop aims to identify education priorities required for formulation of outcomes, strategies and outputs of the education sector for the next 5 years
The meeting will be chaired by the Commissioner of Education, Professor Eustella Bhalalusesa and will bring together Senior government officials from MoEST and Education Institutes, the President’s Office Regional Administration and Local Government (PO-RALG), Development Partners and Civil Society Organizations representatives as well as members of the Academia. The UNESCO team, will be led by the International Institute for Education Planning (IIEP) and further composed by experts from the UNESCO Institute of Lifelong Learning (UIL), the Education and TVET Units of the HQs and the Dar es Salaam Office.
The workshop proceedings will enable the alignment of the ESDP with the Education priorities of the Five Year Development Plan (FYDPII), taking into consideration as well the key national and international policies and agendas including the new Education and Training Policy (2014) and the Education 2030 Agenda and Framework for Action.
Following the prioritization, the exercise will continue with a smaller number of Government officials for the further formulation of the expected outcomes and targets for identified priorities.
For more information please contact;
Petro Makuru (makurupetro@gmail.com) and Faith Shayo, (f.shayo@unesco.org)
MATUKIO KUTOKA BUNGENI -MJINI DODOMA Januari 25, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
TAMKO KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI LILILOTOLEWA NA MHE. UMMY MWALIMU (MB); WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
Kwa mujibu wa Takwimu za kuanzia
tarehe 18 hadi 24 Januari 2016, ni kuwa jumla ya Mikoa ambayo imeripoti
kuwa na wagonjwa ni 15 ambapo idadi ya wagonjwa 524 na vifo 10
vimeripotiwa. Idadi ya wagonjwa walioripotiwa wiki hii imepungua
ukiliinganisha na idadi ya wiki iliyoishia tarehe 17 ambapo kulikuwa na
wagonjwa 621 na vifo 14 ambalo ni punguzo la asilimia (16%). Mkoa wa
Morogoro bado umeendelea kuripoti idadi kubwa zaidi ya wagonjwa
ukilinganishwa na Mikoa mingine, (Manispaa ya Morogoro 89, Halmashauri
ya Morogoro 36, Mvomero 17), ukifuatiwa na mikoa ya Mwanza (Ukerewe 36,
Nyamagana 19 na Ilemela 13), Simiyu (Bariadi DC 29 na Bariadi municipal
23), Manyara (Simanjiro 48), Mara (Musoma Manispaa 11, Musoma DC 8,
Rorya 8 na Butiama 8), Geita (Geita DC 21 na Geita TC 6) na Mbeya (Kyela
26).
Mikoa mingine ambayo bado pia imeendelea kuripoti wagonjwa ni pamoja na Dodoma (Wagonjwa 22), Arusha (21), Tabora (18), Singida (18), Lindi (12), Rukwa (7), Kilimanjaro (6) na Kagera (2).
Mwanzoni mwa mwezi Januari mwaka huu, Wizara yangu kwa kushirikiana na wadau ilituma timu ya jopo la wataalam kutoka ngazi ya Taifa kwenda kusaidiana na wataalam waliopo katika ngazi ya mkoa na halmashauri katika mikoa 7 iliyokuwa inatoa taarifa ya kuwa na wagonjwa wengi zaidi. Mikoa hiyo ni Arusha, Manyara, Mwanza, Simiyu, Singida, Mara na Morogoro. Mafanikio ya kazi iliyofanywa na Jopo hilo yameanza kuonekana kwani katika Mikoa hiyo saba idadi ya wagonjwa wa kipindupindu imeanza kupungua. Pamoja na mafanikio hayo zipo changamoto ambazo timu hizo ilizibaini kuwepo ambazo zinachangia kulegalega kwa juhudi za kupambana na Kipindupindu nazo ni;
i. Kuwepo na idadi ndogo ya kaya ambazo zinamiliki na kutumia vyoo bora hususani katika maeneo ambayo yameathirika zaidi na ugonjwa huu.
ii. Kutokuwepo kwa miundombinu stahiki ikiwemo vyoo na maji katika Maeneo ya mikusanyiko kama masoko na minada kutokuwa na
iii. Wananchi kutokutii sheria zilizopo kwa kuendelea kuuza chakula bila kuzingatia kanuni za afya na kuuza matunda yaliyokwisha katwakatwa maeneo yasiyo salama.
iv. Utiririshaji wa maji taka kwenye vyanzo vya maji, pamoja na kujisaidia maeneo ya wazi na pembezoni karibu na vyanzo vya maji.
v. Kuwepo kwa idadi ndogo ya watu wanaopata maji safi na salama ya kunywa. Aidha utakasaji wa maji katika ngazi ya kaya kwa kuyachemsha au kwa kutumia vidonge vya kutakasia bado ni changamoto kubwa.
vi. Wagonjwa wa Kipindupindu kuchelewa kufika Kambi za Matibabu.
Kutokana na changamoto hizo, napenda kuikumbusha jamii kuwa kipindupindu ni ugonjwa unaochochewa na mazingira machafu ikiwemo ukosekanaji wa vyoo na hivyo kuletea vinyesi vyenye vimelea kuwa chanzo kikuu cha maambukizi, utiririshaji wa maji taka na vinyesi ambao unaweza kupelekea kuchafuka kwa vyanzo vya maji, kutokuzingatia kanuni za afya wakati wa utayarishaji wa vyakula na matunda, Kula vyakula au vinywaji au pombe za kienyeji zisizoandaliwa kwa kufuata kanuni za afya na kugusa matapishi ya mgonjwa wa kipindupindu au kwenye kitu chochote kilichochafuliwa na kinyesi au matapishi ya mgonjwa.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inaendelea kusisitiza kwa jamii kuzingatia yafuatayo:
– Kunywa maji yaliyo safi na salama.
– Kuepuka kula chakula kilichoandaliwa katika mazingira yasiyo safi na salama.
– Kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka hasa kabla ya kula na baada ya kutoka chooni.
– Kutumia vyoo wakati wote na kutokujisaidia ovyo katika vyanzo vya maji vya mito, maziwa na mabwawa.
– Kutokutiririsha maji taka na vinyesi ili kuepuka uchafuzi wa vyanzo vya maji.
Mikoa mingine ambayo bado pia imeendelea kuripoti wagonjwa ni pamoja na Dodoma (Wagonjwa 22), Arusha (21), Tabora (18), Singida (18), Lindi (12), Rukwa (7), Kilimanjaro (6) na Kagera (2).
Mwanzoni mwa mwezi Januari mwaka huu, Wizara yangu kwa kushirikiana na wadau ilituma timu ya jopo la wataalam kutoka ngazi ya Taifa kwenda kusaidiana na wataalam waliopo katika ngazi ya mkoa na halmashauri katika mikoa 7 iliyokuwa inatoa taarifa ya kuwa na wagonjwa wengi zaidi. Mikoa hiyo ni Arusha, Manyara, Mwanza, Simiyu, Singida, Mara na Morogoro. Mafanikio ya kazi iliyofanywa na Jopo hilo yameanza kuonekana kwani katika Mikoa hiyo saba idadi ya wagonjwa wa kipindupindu imeanza kupungua. Pamoja na mafanikio hayo zipo changamoto ambazo timu hizo ilizibaini kuwepo ambazo zinachangia kulegalega kwa juhudi za kupambana na Kipindupindu nazo ni;
i. Kuwepo na idadi ndogo ya kaya ambazo zinamiliki na kutumia vyoo bora hususani katika maeneo ambayo yameathirika zaidi na ugonjwa huu.
ii. Kutokuwepo kwa miundombinu stahiki ikiwemo vyoo na maji katika Maeneo ya mikusanyiko kama masoko na minada kutokuwa na
iii. Wananchi kutokutii sheria zilizopo kwa kuendelea kuuza chakula bila kuzingatia kanuni za afya na kuuza matunda yaliyokwisha katwakatwa maeneo yasiyo salama.
iv. Utiririshaji wa maji taka kwenye vyanzo vya maji, pamoja na kujisaidia maeneo ya wazi na pembezoni karibu na vyanzo vya maji.
v. Kuwepo kwa idadi ndogo ya watu wanaopata maji safi na salama ya kunywa. Aidha utakasaji wa maji katika ngazi ya kaya kwa kuyachemsha au kwa kutumia vidonge vya kutakasia bado ni changamoto kubwa.
vi. Wagonjwa wa Kipindupindu kuchelewa kufika Kambi za Matibabu.
Kutokana na changamoto hizo, napenda kuikumbusha jamii kuwa kipindupindu ni ugonjwa unaochochewa na mazingira machafu ikiwemo ukosekanaji wa vyoo na hivyo kuletea vinyesi vyenye vimelea kuwa chanzo kikuu cha maambukizi, utiririshaji wa maji taka na vinyesi ambao unaweza kupelekea kuchafuka kwa vyanzo vya maji, kutokuzingatia kanuni za afya wakati wa utayarishaji wa vyakula na matunda, Kula vyakula au vinywaji au pombe za kienyeji zisizoandaliwa kwa kufuata kanuni za afya na kugusa matapishi ya mgonjwa wa kipindupindu au kwenye kitu chochote kilichochafuliwa na kinyesi au matapishi ya mgonjwa.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inaendelea kusisitiza kwa jamii kuzingatia yafuatayo:
– Kunywa maji yaliyo safi na salama.
– Kuepuka kula chakula kilichoandaliwa katika mazingira yasiyo safi na salama.
– Kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka hasa kabla ya kula na baada ya kutoka chooni.
– Kutumia vyoo wakati wote na kutokujisaidia ovyo katika vyanzo vya maji vya mito, maziwa na mabwawa.
– Kutokutiririsha maji taka na vinyesi ili kuepuka uchafuzi wa vyanzo vya maji.
RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA)
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni
Sefue akizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es salaam
wakati alipotangazia umma wa watanzania kuhusu hatua ambazo Rais Dk.
John Pombe Magufuli amechukua dhidi ya Dickson Mwaimu Mtendaji Mkuu wa
Mamlaka ya Taifa ya Vitambulisho vya taifa NIDA kutengua uteuzi wake na
kumsimamisha kazi mara moja pamoja na wasaidizi wake ambao ni Joseph
Makani Mkurugenzi wa TEHAM, Bi. Rahel Mapande Sfisa Ugavi Mkuu Bi.
Sabrina Nyoni Mkurugenzi wa Sheria na George Ntalima Afisa Usafirishaji
kwa kuwasimamisha kazi mara moja kupisha uchunguzi.
Taarifa zilizomfikia Rais
zinaonesha kuwa NIDA hadi sasa imetumia shilingi Bilioni 179.6 kiasi
hicho ni kikubwa na Rais angependa kufanyika uchunguzi na ukaguzi jinsi
fedha hizo zilivyotumika, maana Rais amekuwa akipokea malalamiko ya
wananchi kuhusiana na kazi ndogo ya utoaji wa vitambulisha vya taifa .
Hivyo Rais ameelekeza mamlaka ya
udhibiti wa manunuzi ya Umma PPRA wafanye ukaguzi wa manunuzi yote
yaliyofanywa na NIDA, TAKUKURU na CAG kufanya uchunguzi kwa pamoja ili
kubaini kama kulikuwa na vitendo vya rushwa na ukiukwaji wa taratibu au
la.
(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-IKULU)
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni
Sefue akizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es salaam ,
kulia ni Kaimu mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano IKULU Bw. Gerson
Msigwa.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni
Sefue akiangalia wakati Kaimu mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano
IKULU Bw. Gerson Msigwa alipomruhusu mmoja wa waandishi wa habari
kuuliza swali katika mkutano huoIkulu jijini Dar es salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa iliyokuwa ikitolewa na Balozi Ombeni Sefue Ikulu leo.
Mkutano ukiendelea.
No comments :
Post a Comment