Monday, December 7, 2015

RAIS DR. JOHN POMBE MAGUFULI AKUTANA NA MWAKILISHI WA BENKI YA DUNIA

pom9
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimpa pole Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Bi. Bella Bird alipokutana naye Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015
PICHA NA IKULU

MWENYEKITI WA CCM JAKAYA MRISHO KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA CCM

pom1 
Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho kikwete akiongozana na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli , Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015
pom2 
Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho kikwete akiongozana na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli , Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015
pom3 
Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho kikwete akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015
pom4 pom5 
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipigiwa saluti na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015
pom6 pom7 
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim. wengine ni Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais Mhe samia Suluhu Hassan na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015
pom8

Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi asimamishwa kazi.

3
Na Raymond Mushumbusi- Maelezo
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaban Mwinjaka kuanzia  leo ( Disemba 7, 2015) na atapangiwa kazi nyingine.
Rais Dkt. Magufuli pia amevunja Bodi ya Bandari na kutengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Bandari Prof. Joseph Msambichaka na Mkurugenzi Mkuu wa Bandari Bw. Awadhi Massawe.
Aidha amewasimamisha kazi Wakuu wa Vitengo vitano vya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Bandari ya Dar es Salaam kutokana na kashfa ya ukwepaji kodi wa makontena 329 kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Uamuzi huo umetangazwa leo na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Wakuu wa vitengo waliosimamishwa kazi ni pamoja aliyekuwa Meneja Mapato Bw Shaaban Mngazija ambaye kwa sasa amehamishiwa Makao Makuu Kitengo cha Fedha, Mkuu wa Bandari Kavu (ICD) Bw. Rajab Mdoe, Mkurugenzi wa Fedha Bw.Ibin Masoud na Meneja wa Bandari Msaidizi-Fedha Bw. Apolonia Mosha.
Wengine waliosimamishwa kazi ni Wasimamizi wanane wa Bandari Kavu (ICD) ambao ni Bi. Happygod Naftari, Bw.Juma Zaaar, Bw.Steven Naftari Mtui, Bw.Titi Ligalwike,Bi. Lydia Prosper Kimaro, Bw.Mkango Alli, Bw.John Elisante na Bw.James Kimwomwa ambaye amehamishiwa Mwanza.
Hata hivyo Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa alipofanya ziara ya kushtukiza katika Bandari ya Dar es salaam Novemba 27 mwaka huu aligundua utendaji mbovu ndani ya Bandari ya Dar es salaam na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na katika kufuatilia utekelezaji wa maagizo watendaji wa mamlaka hizo wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi.

SYMPOSIUM TO MARK HUMAN RIGHTS DAY 08 DEC 2015

The United Nations Systems in Tanzania in collaboration with the Commission of Human Rights and Good Governance (CHRAGG), Ministry of Constitutional and Legal Affairs  cordially invites the media to the Symposium to commemorate the 2015 Human Rights Day to be held at the Peacock Hotel, along Bibi Titi Road, Mnazi Mmoja on Tuesday,08 December, 2015, at 0800-1200 pm.
The focus of the symposium is Linkage between Sustainable Development Goals (SDGs) and Human Rights. The debate aim to engage government officials and youth on the newly adopted Sustainable Development Goals specifically focusing on Goal # 2 ( Quality Education); Goal 10 ( Reduced inequalities among and within nations); SDG 15 (Life on Land) and SDG 16 ( Peace Justice and Strong institutions) .
The Panelists at the symposium will come from the United Nations Tanzania, Haki Elimu; CHRAGG and ESRF.
There are 17 SDGs and 169 targets that were unanimously adopted by all 193 member states at the UN general Assembly on 25 September 2015. The SDGs build on the goal-setting agendas of United Nations conferences and the widely successful Millennium Development Goals that have improved the lives of millions of people. The new agenda recognizes that the world is facing immense challenges, ranging from widespread poverty, rising inequalities and enormous disparities of opportunity, wealth and power to environmental degradation and the risks posed by climate change. 
The UN General Assembly proclaimed 10 December as Human Rights Day in 1950, to bring to the attention ‘of the peoples of the world’ the Universal Declaration of Human Rights as the common standard of achievement for all peoples and all nations.

Muhumbili yapatiwa msaada wa mashine ya kisasa ya Digital ya X-Ray

TC3 
Mkuu wa Idara ya Mionzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk Flora Lwakatare akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu matumizi ya mashine mpya ya X-ray ya digitali.  Dk Lwakatare amesema mashine hiyo ina uwezo wa kupiga picha na kutumwa nje ya nchi kwa ajili ya ushauri wa kitaalamu zaidi. Mashine hiyo haihitaji chumba cha kusafishia picha wala dawa za kusafishia.
TC4 
Mkuu wa Idara ya Mionzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk Flora Lwakatare akitoa maelezo kuhusu idadi ya wagonjwa waliopata huduma ya kipimo cha CT Scan baada ya mashine hiyo kukamilika.
TC1 
Pichani ni misaada ya shuka 200, neti 150 na Televisheni nne ikipokelewa leo  katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
TC2 
Pichani ni misaada ya shuka 200, neti 150 na Televisheni nne ikipokelewa leo  katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
………………………………………………………………………………
Hospitali ya Taifa  Muhimbili (MNH) imepata mashine mpya na ya kisasa ya Digital X-ray ambayo wataalamu wake hawatalazimika kutumia filamu kusafisha picha kama ilivyozoeleka katika  mashine za kawaida.
Mashine hiyo imegharimu Dola 200,000 za Marekani ambazo zimetolewa na serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii  ambayo ina uwezo wa kusafirisha picha nje ya nchi ili kupata ushauri wa kitaalamu.
Akilelezea kuhusu maendeleo ya mashine ya MRI na CT-SCAN  , Mkuu wa Idara ya Mionzi wa MNH,  Dk Florah  Lwakatare amesema matengenezo ya mashine hizo  yamekamilika na kwamba hadi sasa wagonjwa 148 wamepimwa  kwa kutumia mashine ya MRI , wakati wagonjwa 304 wamepimwa kwa kutumia CT-SCAN .
Katika hatua nyingine Hospitali ya Taifa Muhimbili leo imepokea msaada wa mashuka 200, vyandarua 150 ,  Televisheni nne , Decoder 4 pamoja  na Tv Stand 4.
Akikabidhi msaada huo ambao umetolewa na Kampuni ya Mr. Uk Electronics Limited ya Dar essalaam, mwakilishi wa kampuni hiyo    John Solomon   ametoa wito kwa jamii kuwa na moyo wakujitolea na kushirikiana na serikali katika kuboresha huduma mbalimbali za jamii ikiwemo  huduma za afya .

NEC Yataoa Tamko Kuhusu Uchaguzi wa Wabunge Arusha Mjini na Handeni.

cr1 
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (ambao hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu uchaguzi wa wabunge unaotarajiwa kufanyika Tarehe 13/12/2015 katika jimbo Handeni na Arusha Mjini,(kushoto) ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura Bw.Clarence Nanyaro kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi.Na Anitha Jonas –MAELEZO
cr2 
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva(ambaye hayupo katika picha) leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waaandishi wa habari kuhusu taratibu zitakazo tumika katika uchaguzi wa wabunge katika jimbo la Arusha na Handeni.
cr3 
Mwandishi wa Habari kutoka Kituo cha Utangazaji ITV Bi:Ufoo Saro akimuuliza swali Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva (ambaye hayupo katika picha)kuhusu suala la ulinzi utakao kuwepo kwa wananchi wa majimbo hayo wakati wa kupiga kura.

DK.SHEIN AMUAPISHA MKUU WA WILAYA MICHEWENI PEMBA

dr1 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Nd,Abeid Juma Ali kuwa Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba,kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar,hafla ya kiapo  ilifanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,{Picha na Ikulu}
dr2 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Nd,Ali Khamis Juma  kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha kabla alikuwa Naibu katibu Mkuu Wizara ya Uwezeshaji Ustawi wa Jamii Vijana Wanawake na Watoto Zanzibar,hafla ya kiapo hicho ilifanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,{Picha na Ikulu}
dr3 
Baadhi ya Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Mkuu mpya wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba Nd,Abeid Juma Alina Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Nd,Ali Khamis Juma leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.{Picha na Ikulu}
dr4 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu mpya wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba Nd,Abeid Juma Ali (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Nd,Ali Khamis Juma (kulia) baada ya kuwaapisha kushika nyadhifa hizo leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.{Picha na Ikulu}

Watumishi wa Umma Kusaini Kiapo cha Ahadi na Uadilifu

index 
Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu(kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es  Salaam kuhusu utekeleza wa Ahadi ya Uadilifu kwa Watumishi wa Umma nchini ambao ulizinduliwa Agosti Mosi mwaka huu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA) Bw. Charles Senkondo
Picha na Magreth Kinabo – (MAELEZO).
………………………………………………………………………………………………..
Na Lilian Lundo-Maelezo
Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeanza rasmi kutekeleza Ahadi ya Uadilifu kwa watumishi wa Umma nchini ambao ulizinduliwa Agosti Mosi mwaka huu.
Akiongea na vyombo vya habari leo, Katibu Mkuu Hab Mkwizu amesema utekelezaji huo umeanza rasmi Disemba, 2015 ambapo kila mtumishi wa Umma ataweka saini  ya kiapo  kwa kuzingatia  taratibu zilizowekwa na  mazingira ya Taasisi husika.
“Utaratibu wa Utekelezaji wa Ahadi ya Uadilifu kwa watumishi wa Umma umetolewa kupitia waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma  Na. 2 wa mwaka 2015 kuhusu utekelezaji wa Ahadi ya Uadilifu kwa viongozi, watumishi wa Umma na sekta binafsi wa tarehe 1 Agosti, 2015.” Alisema Mkwizu.
Mkwizu aliongezea kwa kusema, uanzishwaji wa Ahadi ya Uadilifu  ni muendelezo wa uundwaji wa vyombo vya kusimamia maadili baada ya ongezeko kubwa la ubadhirifu, utoro sehemu za kazi na kushuka kwa nidhamu katika kipindi cha miaka ya themanini na tisini.
Alivitaja vyombo vingine ambavyo vilianzishwa kusimamia ahadi na uadilifu kuwa ni Sekretariate ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).
Mkwizu alivitaja vipengele ambavyo mtoa ahadi anatakiwa kuvitamka ni, kuwa mzalendo wa nchi yake na kutii Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kuhudumia Umma na watumishi wenzake kwa heshima, kutimiza wajibu wa kutoa huduma bora kwa umma, kutoa huduma bora kwa usawa kwa watu wote na kutofanya ubaguzi wa dini, siasa, kabila, udugu, ukanda, jinsia, urafiki au hali ya mtu.
Vipengele vingine ni kutumia rasilimali za Umma kwa manufaa ya Umma, kutotoa siri za Serikali au mteja kwa watu wasiohusika isipokuwa kwa maslahi ya Umma, kufanya kazi kwa nidhamu ya hali ya juu, kutoomba kushawishi, kutoa wala kupokea rushwa na kutotumia madaraka kwa manufaa binafsi ya ndugu, rafiki au jamaa.
Aidha, Mkwizu ametoa wito kwa waajiri wote kuhakikisha kuwa utekelezaji wa Ahadi na Uadilifu unakamilika  ifikapo tarehe 31/12/2015 na kuwasilisha Ofisi ya Rais – UTUMISHI kabla ya tarehe 25/02/2016 na utekelezaji wake kuwa kila ifikapo Juni 30 ya kila mwaka. Fomu za Ahadi ya Uadilifu zinapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Rais – UTUMISHI yenye anwani www.utumishi.go.tz.

RAIS MAGUFULI AVUNJA BODI YA MAMLAKA YA BANDARI

MSAMBICHAKA 1
* Atengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mkuu TPA
* Amsimamisha kazi Katibu Mkuu Uchukuzi
* Waziri Mkuu awasimamisha kazi watumishi wengine 13 wa bandari
RAIS Dkt. John Pombe Magufuli amevunja Bodi ya Mamlaka ya Bandari (TPA) na kutengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Bandari, Prof. Joseph Msambichaka pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Bandari, Bw. Awadhi Massawe.
Dkt. Magufuli pia ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaban Mwinjaka kuanzia leo (Jumatatu, Desemba 7, 2015), na kwamba atapangiwa kazi nyingine.
Akitangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari kwenye mkutano uliofanyika leo ofisini kwake Magogoni, jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema hatua hizo zimechukuliwa kufuatia ziara mbili za kushtukiza alizozifanya katika mamlaka ya bandari Novemba 27 na Desemba 3, mwaka huu.
Waziri Mkuu amesema Rais Magufuli amevunja bodi hiyo na kutengua uteuzi wa viongozi hao kutokana na utendaji mbovu wa muda mrefu wa Mamlaka ya Bandari na kwa kitendo cha viongozi hao kutochukua hatua kwenye vyanzo.
Pia alisema Katibu Mkuu amesimamishwa kazi kwa sababu ya kutosimamia kwa makini mashirika mawili ya Bandari na Reli ambayo yako chini ya wizara yake ambako yeye mwenyewe alizuru Shirika la Reli (TRL) Desemba 3, 2015 na kukuta kuna ubadhirifu wa sh. bilioni 16.5/-.
“Tarehe 3 Desemba mwaka huu nilifanya ziara ya kushtukiza pale TRL nikakuta wametumia visivyo sh. bilioni 13.5/- walizopewa na Serikali. Pia nilikuta wamekopa sh. bilioni 3/- kutoka benki ya TIB lakini nazo wamezitumia nje ya utaratibu. Fedha hizi zilikuwa ni za kusaidia kuboresha miradi ya shirika lakini wao wamezitumia visivyo. Uchunguzi bado unaendelea,” alisema Waziri Mkuu.
Wakati huo huo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi kuanzia leo viongozi watano wa sekta zilizotoa ruhusa ya makontena kutoka ndani ya bandari pamoja na watumishi wanane wa bandari kavu ambao walihusika na ukwepaji kwa makontena 2,387.
“Viongozi hawa hawakuwemo kwenye ripoti ya ukaguzi lakini ni wahusika wakuu. Hawa ndiyo waliotoa ruhusa ili makontena yaende kwenye ICDs. Nao ni aliyekuwa Meneja Mapato ambaye kwa sasa amehamishiwa Makao Makuu kitengo cha Fedha, Bw. Shaban Mngazija; aliyekuwa Mkurugenzi wa Fedha na Mkuu wa Bandari Kavu (ICD) – ambaye amehamishiwa Makao Makuu kwa Naibu Mkurugenzi Co-operate Services, Bw. Rajab Mdoe; Kaimu Mkurugenzi wa Fedha, Bw. Ibin Masoud; na Meneja Bandari Msaidizi – Fedha, Bi. Apolonia Mosha
Pia amewasimamisha kazi wasimamizi wanane wa Bandari Kavu (ICDs) ambao ni Happygod Naftari, Juma Zaar, Steven Naftari Mtui, Titi Ligalwike, Lydia Prosper Kimaro, Mkango Alli, John Elisante na James Kimwomwa ambaye alihamishiwa Mwanza lakini kuanzia sasa anasimamishwa kazi huko huko aliko.
“Bila wao kuidhinisha hakuna kontena linaweza kutoka au kwenda kokote. Watumishi wote hao wawe chini ya ulinzi na waisaidie polisi kupata taarifa hayo makontena ni ya nani na yana thamani gani,” Waziri Mkuu alisema.
Waziri Mkuu Majaliwa aliwaeleza waandishi wa habari kwamba Desemba 3, mwaka huu aliamua kurudi tena bandarini kufuatilia na kuangalia hatua ya udhibiti wa upitishaji wa bidhaa mbalimbali kinyume cha utaratibu. “Ziara yangu ilinipitisha hatua zote za upitishaji mizigo ambazo pia kwa mujibu wa Taarifa ya Ukaguzi wa Ndani ya tarehe 30 Julai 2015, Mamlaka ya Bandari iligundulika kuwepo kwa mianya mingi ya ukwepaji kodi ikiwemo makotena 2,387 yaliyopitishwa kati ya Machi – Septemba 2014 kinyume cha utaratibu”.
“Vitendo hivi vinaonyesha kuwa bandari yetu hupitisha makontena mengi bila ya kulipiwa kodi na hakuna hatua yoyote inayochukuliwa. Serikali haitavumilia kuona watu wachache au kikundi chochote kilichojipanga kuhujumu mifumo au kuiibia Serikali kwa namna yoyote ile kwa manufaa ya wachache kwani bandari ni eneo muhimu ambalo likisimamiwa vizuri, linaweza kukusanya fedha nyingi na kuchangia Pato la Taifa,” alisema.
Desemba 3, mwaka huu, Waziri Mkuu alimpa saa tatu tu Kaimu Meneja wa Bandari, Bw. Hebel Mhanga amletee ofisini majina ya watumishi wote waliohusika na ukwepaji kodi huo. Pia alimpa Meneja huyo wiki moja kuhakikisha kuwa mamlaka hiyo inabadilisha mfumo wa utozaji malipo kutoka kwenye billing system na badala yake kuweka mfumo wa malipo wa kielektroniki (e-payment). Mwisho wa kukamilisha zoezi hilo ni Desemba 11, 2015.

No comments :

Post a Comment