Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na waandishi wa habari,
kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, jijini Dar es salaam Desemba
7,2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wapiga
picha wakifuatilia wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipozungumza
na Waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar
es salaam Desemba 7, 2015, Mkurugenzi wa Fullshangweblog Bw. John
Bukuku (kulia) alikuwa ni mmoja wapo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wapiga
picha wakifuatilia wakati Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipozungumza
na Waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar
es salaam Desemba 7, 2015. Mkurugenzi wa Fullshangweblog Bw. John Bukuku
(kulia) alikuwa ni mmoja wapo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim
Majaliwa alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini
Dar es salaam Desemba 7, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
MRADI WA VIJANA WAMFURAHISHA MRATIBU WA UN NCHINI
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Kanali mstaafu Issa Machibya akiongozana na Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez mara tu baada ya kumpokea alipowasili
ofisini kwake akiwa ameongozana na Ofisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara
ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa, Maulidah Hassan, pamoja na Mwakilishi wa Shirika la
Mpango wa idadi ya watu (UNFPA) nchini, Dkt. Natalia Kanem (hawapo
pichani).
Na Mwandishi wetu, Kigoma
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez ameelezea kufurahishwa kwake
na uwapo wa mradi wa kusaidia vijana wa kitanzania kujifunza ujasirimali
na kujitegemea.
Akizungumza
katika shughuli za uzalishaji mali za vijana wa Shirika lisilo la
kiserikali la Nyakitonto Youth Development Tanzania la mjini Kigoma
alisema kwamba shughuli wanazofanya vijana hao zinamsisimua sana.
“Tunafurahi sana mimi na wenzangu kutembelea mradi huu unaofadhiliwa na
Shirika la Kazi Duniani (ILO) ambao unachochea ujasirimali miongoni mwa
vijana. Sote tunajua kwamba vijana wengi wa Kitanzania wanaume kwa
wanawake wameelimika lakini hawana ajira rasmi. Na suala la ujasiriamali
ni kitu ambachio mtu anaweza kujifunza, na ujasiriamali unatoa fursa
kwa vijana kujiunga katika kundi la wafanyakazi kwa kujiajiri wenyewe.
“Tunajua
kwamba kupitia shughuli zinazofadhiliwa na ILO katika ngazi ya jamii na
kwa kufuata maelekezo ya serikalai za mtaa vijana wanaanzisha biashara
mbalimbali binafsi au na jamii. Kiwanda cha kutengeneza sabuni ni mfano
mzuri sana. Tunaona kwamba mradi huu unawaongezea kipato na hivyo kuweza
kusaidia familia zao na kupeleka watoto shuleni na kuboresha lishe .
Kwa ufupi mradi kama huu unasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali
zinazokabili kaya maskini Kigoma” alisema Rodriguez
ILO
Kigoma inaendesha mafunzo ya ujasirimali kwa vijana kwa lengo la
kuwawezesha kujiajiri wenyewe na kuhudumia familia zao kwa kuziwezesha
kupata huduma bora za elimu na afya kutokana na kipato chao.
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Kanali mstaafu Issa Machibya (kushoto)
akibadilishana ‘Business card’ na Mwakilishi wa Shirika la Mpango wa
idadi ya watu (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem.
Alisema
kwamba amefurahishwa na mradi huo ambao unawawezesha vijana kutambua
fursa mbalimbali zilizopo na kuzitumia vyema kufanikisha maendeleo ya
familia zao.
Aidha
alisisitiza haja ya jumuiya ya kimataifa kuusaidia mkoa Kigoma katika
nyanja mbalimbali za kiuchumi hasa katika eneo la ajira kwa vijana
kutokana na ukarimu wa wakazi wa mkoa huo katika kuwapokea na
kuwahudumia wakimbizi kutoka nchi za maziwa makuu kwa upendo.
Rodriguez
alisema pamoja na ombi hilo Mratibu huyo wa shughuli za kimataifa
ambaye ni Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP)
alisema wao kama UN wakifanyakazi pamoja wataendelea kutoa misaada kwa
wakimbizi hasa uanzishaji wa miradi ya kiuchumi kwa vijana na wanawake.
Kwa
upande wake Mwakilishi mkazi wa Shirika la Umoja wa mataifa la Idadi ya
watu (UNPFA), Dkt. Natalia Kanem alisema kuwa kupatiwa mitaji na
kuanzisha vikundi vya uzalishaji kwa vijana na wanawake kunasaidia
kuongeza ajira lakini pia kusaidia kupunguza ongezeko kubwa la idadi ya
watu bila mpangilio.
Katika
risala yao kwa uongozi huo wa Umoja wa Mataifa vijana kutoka Nyakitonto
Youth Development Tanzania wamesema kuwa misaada iliyotolewa kwao
imewasaidia kupata ujuzi na kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ikiwa ni
sehemu ya kujiajiri na kujiongezea kipato ili waweze kuendesha maisha
yao bila utegemezi.
Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma, Kanali mstaafu Issa Machibya akitoa taarifa ya mkoa
wake kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa
Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na ujumbe
ofisini kwa Mkuu huyo wa mkoa.
Hata
hivyo vijana hao katika risala yao iliyosomwa na Meneja miradi wa
shirika hilo, Anjelina Gulanywa walisema kuwa pamoja na mafanikio hayo
wanakabiliwa na changamoto utaalam mdogo, mitaji na vitendea kazi vya
kisasa ili kufanya shughuli zao kuwa na mafanikio zaidi.
Naye
Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Kanali Mstaafu, Issa Machibya alieleza
kuridhishwa kwake na juhudi za Umoja wa Mataifa katika kusaidia miradi
mbalimbali mikoani mwake ambayo inasadia wananchi kukabiliana na
umaskini.
Mkoa
wa Kigoma una mashirika mengi ya Umoja wa Mataifa yakifanya kazi
mbalimbali za maendeleo na za kutoa huduma za kibinadamu kwa wakimbizi.
Mashirika
hayo ya Umoja wa Mataifa yanayotekeleza miradi mbalimbali mkoani Kigoma
ni pamoja na Shirika la Kuhudumia wakimbizi (UNHCR),Shirika la Afya
Duniani ( WHO), Shirika la Mpango wa Idadi ya watu (UNFPA) ,Shirika la
kazi la Kimataifa ( ILO), Shirika la Kuhudumia watoto( UNICEF), Shirika
la Kuhudumia wahamiaji ( IOM), Shirika la Mpango wa Chakula Duniani
(WFP) na Shirika la maendeleo (UNDP).
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akielezea dhumuni la safari yake
katika mkoa wa Kigoma kwa Mkuu wa mkoa huo, Kanali Mstaafu, Issa
Machibya.
Afisa
Mawasiliano wa Shirika la Kimataifa la Kazi (ILO) nchini, Magnus Minja
akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi wa mafunzo ya ujasiriamali kwa
vijana yenye lengo la kuwawezesha kujiajiri wenyewe na kuhudumai familia
zao kwa kuziwezesha kupata huduma bora za elimu na afya kutokana na
kipato chao unaofadhiliwa na shirika hilo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,
Kanali Mstaafu, Issa Machibya.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akiwasilisha Malengo 17 ya Maendeleo
Endelevu (Sustainable Development Golas-SDGs) kwa Mkuu wa Mkoa wa
Kigoma, Kanali mstaafu Issa Machibya. Kulia ni Mwakilishi wa Shirika la
Mpango wa idadi ya watu (UNFPA) nchini, Dkt. Natalia Kanem.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akikabidhi zawadi ya Khanga ya ‘miaka
60 ya UNFPA Tanzania’, kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kanal Mstaafu, Issa
Machibya, huku Mwakilishi wa Shirika la Mpango wa idadi ya watu (UNFPA)
nchini, Dkt. Natalia Kanem akishuhudia tukio hilo.
Malengo
ya maendeleo endelevu sasa yamewafikia Kigoma. Pichani ni Mkuu wa mkoa
wa Kigoma, Kanali Mstaafu, Issa Machibya na baadhi ya wakurugenzi katika
ofisi ya mkuu huyo wa mkoa katika picha ya pamoja na ugeni kutoka Umoja
wa Mataifa Dar es Salaam na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa.
Mkuu
wa mkoa wa Kigoma, Kanali Mstaafu, Issa Machibya akiagana na Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyemtembelea ofisini kwake kabla ya
kuelekea kambi ya wakimbizi Nyarugusu.
STANDARD CHARTERED TANZANIA WINS BANK OF THE YEAR AWARD
Standard
Chartered Bank Tanzania Limited has been awarded the prestigious ‘Bank
of the Year’ award at The Banker Awards 2015. This is the eighth time
that the Bank is winning this award which was announced at a grand gala
dinner programme held at an award ceremony in London last Wednesday
evening.
With
more than fifty lenders operating within its borders, Tanzania has a
healthy and competitive Banking sector. Standard Chartered Bank Tanzania
Limited has stayed ahead of the game by maximising its digital services
to make banking a less time consuming activity for Tanzanians.
The Chief Executive Officer for the Bank in Tanzania, Sanjay Rughani said, “We
are delighted to have won this prestigious award. It is a testimony of
our commitment to serve our clients in this market consistently over so
many years. With a reputation for high quality service, innovation and
connecting Tanzania to neighbours and the world, we have a special offer
to our clients. We are, therefore, proud to be able to make positive
contributions in Tanzania.”
Initiatives
which motivated the accolade from The Banker were Standard Chartered
Bank’s Straight2Bank online service, a fully integrated banking platform
that offers a full range of transactions for clients that continues to
be a market’s leading service. Additionally, in March this year, the
Bank launched the “Straight2Bank Wallet”, a mobile payment service for
corporate clients in Tanzania. The service enables the Bank’s corporate
clients to make almost instantaneous bulk payments directly from their
Standard Chartered Bank accounts into their beneficiaries’ M-PESA and
TigoPesa accounts. The Bank’s corporate and institutional services and
support continues to enable companies operating in Tanzania to fund
their businesses and hedge themselves against currency volatility.
For
the award period under review, Q1 2014 to Q2 2105, Standard Chartered
Bank in Tanzania ran a pan-Bank staff campaign called ‘MySelf MyBrand’
geared towards personalizing service thereby enhancing customer service.
The
Bank also organized a number of client workshops aimed at creating more
awareness on its various products and services as well as enhancing
financial literacy and skills on running profitable businesses and
understanding banking and regulatory requirements.
During
the period, the Bank’s net profits grew by 12% and return on equity
increased to 23%, reflecting a commitment to shareholder returns.
Now
in its 16th year, The Banker Awards is one of the most prestigious
events within the industry. The Banker is the world’s premier banking
and finance magazine, read in over 180 countries around the world. The
Banker is the key source of data and analysis for the industry. Its
unique database of more than 4,000 banks, maps their financial strength
and soundness via Tier I capital, profitability, and their performance
versus their peers.
This
is the eighth time Standard Chartered Bank Tanzania has won the `Bank of
the Year’ award. The bank had earlier won this award consecutively from
2002 – 2005, and thereafter in 2007, 2010 and 2011.
ASYA IDAROUS KHAMSINI ANOGESHA SIKU YA MTANZANIA SEATTLE
Walimbwende
wakiwa tayari kufanya vitu vyao wakiwa na vivazi vya mwanamitindo nguli
Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya
Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Mlimbwende
akiwa kwenye kivazi kutoka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini
kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015
Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Kivazi
chekundu kikiwa na riboni ya punda milia kikimfanya mlimbwende
atabasamu jinsi gani alivyopendeza kivazi toka kwa mwanamitindo nguli
Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya
Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Kivazi
toka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya
Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la
Washington nchini Marekani.
ALBAMU YA NYIMBO ZA INJILI YA SOGEA NA BARAKA ZA BWANA YAZINDULIWA RASMI DAR E S SALAAM NA MHE. ANGELA KAIRUKI
Aliyekuwa
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo na Makazi, Angela Kairuki
(kushoto), akionesha DVD ya nyimbo za injili iitwayo Sogea wakati wa
uzinduzi wa albamu mbili za
nyimbo
hizo ikiwepo na ya Baraka za Bwana zilizoimbwa na muimbaji Anna Shayo
Dar es Salaam juzi. Kulia ni Mwanaharakati Hoyce Temu na mwimbaji na
mmiliki wa albam hizo, Anna Shayo. Kairuki alikuwa mgeni rasmi katika
uzinduzi huo.
Aliyekuwa
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo na Makazi, Angela Kairuki
(kushoto), akionesha DVD ya nyimbo za injili iitwayo Sogea wakati wa
uzinduzi wa albamu mbili za
nyimbo
hizo ikiwepo na ya Baraka za Bwana zilizoimbwa na muimbaji Anna Shayo
Dar es Salaam juzi. Wa pili kulia ni Mwanaharakati Hoyce Temu na
mwimbaji na mmiliki wa albam hizo, Anna Shayo. Kairuki alikuwa mgeni
rasmi katika uzinduzi huo. Kulia ni mdogo wake Hoyce Temu.
Mwimbaji na mmiliki wa albam hizo, Anna Shayo (kulia), akimkabidhi Kairuki risala yake.
Waziri Kairuki akimkabidhi Anna Shayo kitita cha sh.milioni moja.
Mwimbaji wa nyimbo za injili, Juvenalister Mabumba akitoa burudani katika uzinduzi huo.
Mwimbaji wa nyimbo za injili, Ulimbaga Mwakatobe akiimba wakati wa uzinduzi huo.
Mwimbaji Andrew Kihwelu (kushoto), akitoa burudani.
Mwimbaji Supa Belgano (kulia), akitoa burudani.
Mhe. Kairuki akisalimiana na waimbaji wa nyimbo za injili.
MKUTANO WA MWAKA WA WATAALAMU WA MANUNUZI NA UGAVI WAFUNGULIWA JIJINI ARUSHA.
|
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi nchini(PSPTB)Dk Hellen
Bandiho akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Wataalamu
unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa AICC jijini Arusha
na kusisitiza miiko ya uadilifu katika manunuzi ya umma na sekta
binafsi.
|
|
Mjumbe
wa Bodi ya Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi nchini(PSPTB)Ahmed Kilima
akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Wataalamu
unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa AICC jijini
Arusha.
|
|
Mkurugenzi
Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Manunuzi nchini(PSPTB)Dk Clemence
Tesha akizungumza jambo na wajumbe wa mkutano wa mwaka wa Wataalamu wa
taaluma ya Manunuzi na Ugavi unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya
kimataifa wa AICC jijini Arusha na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka mikoa
mbalimbali nchini na wageni kutoka nchi jirani.
|
|
Wajumbe wakiwa kwenye ukumbi wa Simba
|
|
Wajumbe wa mkutano ambao ni wana taaluma ya Manunuzi na Ugavi wakifatilia mada kwenye mkutano huo leo.
|
|
Baadhi ya wajumbe wa mkutano wa Manunuzi na Ugavi wakifatilia mada kwenye mkutano huo leo.
|
|
Wajumbe wa mkutano wa mwaka wa PSPTB
|
|
Mgeni
rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB,Dk Charles
Kimei(katikati)akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu wa fani
Manunuzi na Ugavi nchini baada ya kufungua mkutano wa mwaka ambao
amesisitiza umuhimu wa kufanya manunuzi sahihi yenye lengo la kuokoa
fedha za umma.
|
CHINA KUPITIA JIMBO LA JIANGSU YATOWA MSAADA WA DAWA WENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 500
Balozi
mdogo wa China aliyepo Zanzibar Xie Yunliang akitoa maelezo wakati wa
sherehe ya kukabidhi msaada wa dawa zenye thamani ya zaidi ya shilingi
milioni 500 zilizotolewa na Jimbo la Jiangsu kwa ajili ya Wananchi wa
Zanzibar. Sherehe hiyo ilifanyika Bohari Kuu ya Madawa Maruhubi Mjini
Zanzibar. na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Baadhi
ya Madaktari wa China na waalikwa wakifuatilia sherehe ya makabidhiano
ya msaada wa dawa mbali mbali za binaadamu katika sherehe iliyofanyika
Bohari Kuu ya Madawa Maruhubi.
Kamishna
wa Afya na Uzazi wa Mpango ambae pia ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Jimbo
la Jiangsu Hong Hao akizungumza wakati wa makabidhiano ya dawa zenye
thamani ya shilingi milioni 500 (kulia) Naibu Waziri wa Afya Mahmoud
Thabiti Kombo.
Balozi
mdogo wa China aliyepo Zanzibar Xie Yunliang na Naibu Waziri wa Afya
Mahmoud Thabit Kombo wakitia saini makabidhiano ya dawa hizo
zilizotolewa na Jimbo la Jiangsu.
Naibu
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo na Balozi mdogo wa China
wakibadilishana hati za makabidhiano ya msaada wa dawa zenye thamani ya
zaidi ya shilingi milioni 500 katika sherehe zilizofanyika Bohari Kuu ya
Madawa Maruhubi.
Balozi
mdogo wa China akimkabidhi Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo
sehemu ya Dawa zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China
kupitia Jimbo la Jiangsu (kati) Naibu Mkurugenzi Mkuu ambae pia ni
Kamishna wa Afya na Uzazi wa Mpango wa Jimbo hilo Hong Hao. Picha na
Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Wasanii SHIWATA kumpa Magufuli ufagio wa chuma
MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) umeamua kutekeleza kwa
vitendo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano, John Magufuli la kufanya
usafi nchini siku ya sherehe za Uhuru 9/12/2015 kufagia, kulima, kuzoa
taka na kusafisha maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema jana Dar es
Salaam kuwa usafi huo utaanzia makao makuu yao Ilala Bungoni, soko la
Ilala,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mmachinga Complex, Soko la
Mitumba Karume, Kariakoo, Mnazi Mmoja, Soko la Kisutu, Posta ya zamani,
soko la samaki Feri mpaka Ikulu.








No comments :
Post a Comment