Wednesday, December 9, 2015

HAPA KAZI TU WANANCHI WATEKELEZA AGIZO LA RAIS


so1
Wasanii wa bongo movie wakishiri kufanya usafi
katika eneo la mnara wa askari makutano ya barabara ya Samora na Azikiwe jijini Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON-FULLSHANGWEBLOG
so2
Wasanii wa bongo movie wakishiri kufanya usafi
katika eneo la mnara wa askari makutano ya barabara ya Samora na Azikiwe jijini Dar es Salaam.
so3
Mbunge wa jimbo la Ilala,Mhe. Mussa Azzan Zungu , akihojiwa na waandishi wa habari wakati aliposhiriki siku ya usafi kitaifa, katika eneo la mnara wa askari makutano ya barabara ya Samora na Azikiwe jijini Dar es Salaam .
so4
Wasanii  wa Bongo Muvie,  wakishiriki kupakia taka kwenye gari lenye namba za usajili Su 39012 mali ya shirika la Nyumba Taifa NHC katika eneo la Posta jijini Dar es Salaam.
so5
Wauza matunda wakiendelea na biashara hiyo mtaa wa Zanaki jijini Dar es Salaam.
so6
Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Temeke wakifanya usafi katika dampo lililopo Mwembe yanga ambalo limekuwa kero kwa wakazi wake kutokana na kutoa harufu kali na kupelekea wasiwasi wa wakazi kupata ugonjwa wa kipindupinndu kama walivyokutwa na kamera yetu jijini Dar es Salaam leo.
so8
Baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha madawa ya binadamu, bohari kuu, wakifanya usafi wa mazingira kandokando mwa jengo hilo kama walivyonaswa na kamera yetu jijini Dar es Salaam jana, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Brigedi ya Chui Brigedia Jenerali Sharif Othman wakishiriki kufanya usafi maadhimisho ya uhuru

17251e86-84ab-450c-b736-78ef7de38e42
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange(kulia), Mkuu wa Brigedi ya Chui Brigedia Jenerali Sharif Othman(kushoto) pamoja na Maafisa na Askari wakishiriki zoezi la usafi katika kambi ya Lugalo, jijini Dar es Salaami wakati wa  kuadhimisha miaka 54 ya Uhuru kama alivyoagiza Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli

MABONDIA ZUMBA KUKWE NA SELEMANI GALILE WATAMBIANA KUZIDUNDA JANUARR 2, MANZESE

Mabondia Seleman Galile kushoto na Zumba Kukwe wakitunishiana misuli baada ya kusaini makubaliano ya kupigana january 2 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
Mabondia Seleman Galile kushoto na Zumba Kukwe wakitunishiana misuli baada ya kusaini makubaliano ya kupigana january 2  kwenye mpambano wa kufungulia mwaka utakaofanyika katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Hussein Mbonde kushoto wakitunishiana misuli na Shomari Milundi wakati wakitambulisha mpambano wao utakaofanyika january 2 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Hussein Mbonde kushoto wakitunishiana misuli na Shomari Milundi wakati wakitambulisha mpambano wao utakaofanyika january 2 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam katikati ni Pembe Ndava  Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Hussein Mbonde kushoto wakitunishiana misuli na Shomari Milundi wakati wakitambulisha mpambano wao utakaofanyika january 2 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
Mabondia Hussein Mbonde wa pili kulia na Shomari Milundi wakiwa na makocha wao kushoto ni Cristopher Mzazi na Mohamed Mbade mbade wakati wa utambulisho wa mpambano wao utakaofanyika january 2 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS

DK. SHEIN AJUMUIKA WATANZANIA KATIKA WAZANZIBARI KUADHIMISHA DISEMBA 9KWA KUFANYA USAFI LEO

df1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Zanzibar Khatib Abrahman Khatib wakati alipowasilikati eneo la Malindi Mjini Zanzibar katika zoezi ka Usafi wa mazingira katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililoshirikisha Viongozi na Wananchi mbali mbali nchini.[Picha na Ikulu.]
df2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizoa taka katika  zoezi ka Usafi wa mazingira katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania eneo la Malindi Mjini Unguja leo zoezi ambalo liliwashirikisha Viongozi na Wananchi mbali mbali nchini (kushoto) Waziri wa Ardhi,Maji,Makaazi na Nishati Ramadhan Abdalla Shaaban,[Picha na Ikulu.]
df3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizoa taka katika  zoezi ka Usafi wa mazingira katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania eneo la Malindi Mjini Unguja leo zoezi ambalo liliwashirikisha Viongozi na Wananchi mbali mbali nchini (kushoto) Waziri wa Ardhi,Maji,Makaazi na Nishati Ramadhan Abdalla Shaaban,[Picha na Ikulu.]
df6
Baadhi ya Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ walishiriki katika zoezi ka Usafi wa mazingira katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania eneo la Malindi Mjini Unguja leo zoezi ambalo liliwashirikisha Viongozi na Wananchi mbali mbali nchin,[Picha na Ikulu.]
df7
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati)  akimimina taka katika kontena  baada ya kufanya usafi wa madhingira leo wakati wa  zoezi hilo lililofanyika nchi nzima  katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo eneo la Malindi Mjini Unguja,ambapo viongozi mbali mbali walijumuika katika kufanikisha kazi hiyo,[Picha na Ikulu.]
df8
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati)  akitoa nasaha zake baada ya kumalizika kwa zoezi la kufanya usafi  wa madhingira leo wakati wa  zoezi hilo lililofanyika nchi nzima  katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo eneo la Malindi Mjini Unguja,ambapo viongozi mbali mbali walijumuika katika kufanikisha kazi hiyo,(kushoto)Mstahiki Meya wa Manispaa ya Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, [Picha na Ikulu.]
df9
Baadhi ya Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ walishiriki katika zoezi ka Usafi wa mazingira katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania eneo la Malindi Mjini Unguja leo zoezi ambalo liliwashirikisha Viongozi na Wananchi mbali mbali nchin,[Picha na Ikulu.]

Wizara ya Fedha yaadhimisha sherehe za Uhuru kwa kufanya usafi

fe1
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (wa tatu kulia) akielekea eneo la kufanya usafi kuzunguka maeneo ya ofisi za wizara hiyo leo jijini Dar es salaam ikiwa ni mwitikio na utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kufanya usafi katika eneo ya kazi wakati wa maadhimisho ya sherehe za Uhuru mwaka huu.
fe2
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (DHRM) Wizara ya Fedha Deodata Makani akitoa maelekezo ya kufanya usafi kuzunguka ofisi za Wizara hiyo leo jijini Dar es salaam.
fe3
Baadhi ya watumishi wakikata matawi ya miti kwa makini bila kuharibu nya za simu yaliyokuwa kizuizi katika barabara eneo la ofisi za wizara ya fedha kwa lengo la kufanya usafi leo jijini Dar es salaam.
fe4
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile akiendelea kufanya usafi katika moja ya sehem ya kuzunguka maeneo ya ofisi za wizara hiyo leo jijini Dar es salaam ikiwa ni mwitikio na utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kufanya usafi katika eneo ya kazi wakati wa maadhimisho ya sherehe za Uhuru mwaka huu.
fe7
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile akiongea na watumishi wa wizara hiyo leo jijini Dar es salaam mara baada ya kumaliza zoezi la kufanya usafi ikiwa ni mwitikio na utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kufanya usafi katika eneo ya kazi wakati wa maadhimisho ya sherehe za Uhuru mwaka huu.
…………………………………………………………………………………………..
 
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile leo ameiongoza wizara hiyo katika kuitikia na kutekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kufanya usafi katika eneo lao la kazi katika maadhimisho ya sherehe za Uhuru ya mwaka huu.
Akiongea na watumishi wa Wizara hiyo, Dkt. Likwelile alisema kuwa maadhimisho ya siku ya uhuru yaendelee kutumika kama kichocheo cha kujenga tabia ya kufanya kazi ikizingatiwa dhana iliyokuwepo tangu uhuru ilikuwa “Uhuru na Kazi” ambapo kwa sasa kaulimbiu ya Rais Dkt. Magufuli inasema “Hapa Kazi Tu”
“Ni uamuzi mzuri wa Rais, ni wa busara na unaendana na tulipotoka ambapo Tanzania inaamini katika “Uhuru na Kazi”, huu ni mwanzo wa kusimama kwa miguu yetu wenyewe ili kujiletea maendeleo kwa kuendelea kuwapiga vita maadui watatu wa taifa” alisema Dkt. Likwelile.
Dkt. Likwelile aliwataja maadui hao kuwa ni ujinga, maradhi na umasikini ambao ndiyo wamekuwa chanzo cha kurudisha nyuma juhudi za maendeleo, kwa kuimarisha suala la usafi katika mazingira yote nchini, itakuwa mwanzo wa kupambana na suala magonjwa milipuko ikiwemo kipindupindu ambao asili yake ni uchafu.
Aidha, Dkt. Likwelile aliwaasa watumishi wa wizara hiyo na Watanzanaia kwa ujumla kuenzi kazi iliyonzishwa na Mhe. Rais Dkt. Magufuli ya kufanya usafi na zoezi hilo liwe  endelevu na la kudumu ambapo ameahidi kuwa wizara yake itapanga siku ya kufanya usafi mara kwa mara katika maeneo ya kazi ili kudumisha usafi ambao ni suala muhimu katika kuimarisha afya zao na ikizingatiwa watumishi hutumia muda mwingi wakiwa katika maeneo ya kazini.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (DHRM) Wizara ya Fedha Deodata Makani alisema kuwa mwitikio wa watumishi katika zoezi la usafi umekuwa mkubwa na wanapendekeza zoezi hilo liwe endelevu maana watumishi hutumia muda mwingi katika maeneo ya kazini hivyo ni vema kuyaweka mazingira hayo katika hali ya usafi ili yawe rafiki wakati wote wa kutekeleza majukumu yao.
Naye mmoja wa watumishi wa Wizara hiyo William Muhoja alisema kuwa zoezi la kufanya usafi katika maeneo ya kazi linatakiwa kufanywa kila wakati ambapo itakuwa ni sehemu ya watumishi kuwajibika kwa jamii katika maeneo yao wanapoishi na wanapofanya kazi.
Sherehe za uhuru mwaka huu nchini zimeadhimishwa kwa namna tofauti na ilivyozoeleka miaka iliyopita ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa mamlaka aliyonayo kikatiba alitangaza maadhimisho ya Sherehe za Uhuru na Jamhuri ya 9 Disemba mwaka huu,  Watanzania wote waitumie kwa kufanya kazi mbalimbali kama vile, mashambani, maofisini, sokoni, viwandani na usafi wa miji yao katika kutimiza dhana ya Uhuru na Kazi kwa vitendo.
Maadhimisho hayo yanaendelea nchi nzima ambapo kila halmashauri inatekeleza agizo la Mhe. Rais kwa vitendo kwa kufanya usafi katika maeneo yao, zoezi linashirikisha Wizara, idara, taasisi za Kiserikali na zisizo za kiserikali, maeneo ya viwanda, shule, vyuo, maeneo ya biashara, masoko na kuzunguka maeneo yote ya makazi ya watu.
 

TAMASHA KUBWA LA MSAFARA LINALOWAHUSISHA VIJANA KUFANYIKA JUMAMOSI HII IFAKARA MOROGORO.

Kutoka kushoto ni Manoah William Waziri wa Elimu Serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Agnes Inocent wa YFF, James Isdore Mwenyekiti wa Msafara,Fadhiri Meta kutoka Youth can na  Batseba Modest kutoka Ngao youth wakiongea katika mkutano huo na waandishi wa Habari leo 9.12.2015
 James Isdore Mwenyekiti wa Msafara akizungumzia Shughuli ya msafa kwa ujumla
 Fadhiri Meta kutoka Youth can akizungumzia jinsi Msafara ulivyopokelewa vizuri na mpaka sasa wamepata zaidi ya vijana 500 ambao wanajifunza ujasiliamali na kuibua vipaji na ubunifu mbalimbali.
 Agnes Inocent akizungumzia jinsi watakavyo hamasisha wanawake wengine kujitambua na kuwa wanaweza.
 Batseba Kassanga (Kulia) akitoa wito kwa vijana namna wanavyoweza kujikomboa kupitia Msafara
 Noah William akifafanua jambo kuhusiana na Msafara
Mkutano ukiendelea 
Programu ya
Msafara inayoendeshwa asasi tano za kiraia ambazo ni; YouthCAN, TYDC, DARUSO,
NGAO YOUTH na Young Feminist Forum kwa uratibu wa Shirika la Oxfam, inatarajiwa
kufanyika mapema kesho kutwa katika Mkoa wa  Morogoro wilayani Ifakara.
Programu
inayolenga kuwahamasisha vijana kubuni njia za kujikwamua kiuchumi kupitia
wenzao waliofanikiwa, itafanyika kwa njia ya tamasha kubwa katika eneo la
Uwanja wa Taifa, Ifakara mkoani Morogoro ambapo ndani ya tamasha hilo mitaji na
motisha ya kukabidhiwa vitendea kazi itagaiwa kwa vijana wenye umri kuanzia
miaka 15 hadi 24.
 
Mbali na
kutoa elimu na motisha hiyo, tamasha hilo litapambwa na burudani za aina mbalimbali
huku pia kukiwa na vijana waliofanikiwa watakao wahamasisha wenzao kupitia kauli
mbiu ya Inspire, Aspire and Activate.

Bayport yamuunga mkono Dr Magufuli kwa vitendo, yapaka rangi, yafagia shule ya msingi Hekima

Mkurugenzi Mkuu wa Bayport Financial Services, John Mbaga, akipaka rangi katika ukuta wa shule ya Msingi Hekima, iliyopo Tandale, wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo mchana. Picha zote kwa Hisani ya Bayport Financial Services.

Meneja wa Oparasheni wa Bayport Financial Serviices, Charles Mgeta, akizungumza na waandishi wa habari juu ya taasisi yao kuamua kufanya usafi, kutunza mazingira na kuipaka rangi shule ya msingi Hekima, iliyopo Kata ya Tandale, Wilaya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo, kushoto mwenye kofia na miwani akishiriki kufanya usafi katika shule ya Msingi Hekima, iliyopo Tandale, wilayani Kinondoni, jijini Dar es Salaam, asubuhi.

Wafanyakazi wa Bayport, walimu na wanafunzi wakijiandaa kufanya usafi mbele ya jengo la shule ya Hekima, kabla ya kuanza kupakwa rangi.

Mchambuzi wa Miradi wa Bayport Financial Services, Joseph Munga, kulia akishiriki kupaka rangi katika shule hiyo ya msingi Hekima.
………………………………………………………………………………….
TAASISI ya
Kifedha ya Bayport Financial Services inayojihusisha na utoaji wa mikopo, jana
imemuunga mkono kwa vitendo Rais wa Jamhuri ya Muungano Dr John Pombe Magufuli
kwa kufanya usafi, kutunza mazingira na kupaka rangi shule ya Msingi Hekima,
iliyopo Kata ya Tandale, wilaya Kinondoni, jijini Dar es Salaam, huku wakianza
kwanza kusafisha eneo la Makao Makuu ya ofisi yao, kabla ya kuelekea hapo.
Tukio hilo
liliongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Bayport, John Mbaga, pamoja na zaidi
ya wafanyakazi 80 kwenye taasisi hiyo inayotoa mikopo ya fedha kwa watumishi wa
umma na wafanyakazi wa kampuni binafsi, bila kusahau wajasiriamali katika mradi
wao wa mikopo ya viwanja vilivyopo Vikuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani.
Shughuli
hiyo Ilianza mishale ya saa tatu asubuhi ambapo Mkurugenzi huyo na wafanyakazi
wa Bayport walianza kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya shule hiyo,
pamoja na upakaji wa rangi katika baadhi ya madarasa katika shule hiyo yenye
wanafunzi zaidi 1900, ukiacha idadi kubwa ya wanafunzi wa darasa la kwanza
watakaonza shule mapema mwakani.
Wafanyakazi wa Bayport Financial Services wakiendelea na usafi katika shule ya msingi Hekima.

Akizungumza
katika tukio hilo leo asubuhi, Mkurugenzi wa Bayport Financial Servivces, John Mbaga,
alisema kwamba wameamua kuchagua shule ya Tandale kwa sababu inahitaji kuungwa
mkono kutokana na eneo iliyopo pamoja na changamoto mbalimbali za kimaisha.
Alisema
baada ya rais kuagiza kwamba Sikukuu ya Uhuru 9 Desemba iendane na kazi ya
kufanya usafi na utunzaji wa mazingira, Bayport iliamua kwenda mbali zaidi kwa
kuhakikisha kwamba wanaipaka rangi shule hiyo ili ionekane safi, tofauti na
ilivyokuwa awali.
Usafi ukiendelea shuleni hapo
Usafi ukiendelea
“Tunamuunga
mkono Dr Magufuli na serikali yake kwa vitendo, hivyo si usafi tu, ila
tumeirudisha shule ya Msingi Hekima kwenye upya wake, huku tukiamini kuwa
tutaendelea kujikita zaidi katika mambo ya kijamii, hususan katika suala zima
la elimu kwa kusaidia kila kilichokuwa ndani ya uwezo wetu” alisema Mbaga.
 
Naye Meneja
Masoko na Mawasiliano wa Bayport, Ngula Cheyo, alisema kwamba wamefurahia
kushirikiana na walimu na wanafunzi wa shule ya Msingi Hekima kufanya nao usafi
na kutunza mazingira ya eneo la shule hiyo inayotumiwa na watoto wengi kutoka
kwenye Kata hiyo ya Tandale.
“Bayport ni
taasisi ya Watanzania wote, wakiwamo watumishi wa umma na wafanyakazi wa
kampuni binafsi, hivyo naamini itaendelea kutoa huduma bora zenye kuwakwamua
wateja wetu,” alisema Cheyo.
 
Naye Mwalimu
Mkuu wa shule ya Msingi Hekima, Hussein Mohamed, aliishukuru Bayport kwa
kujitolea kurudisha upya wa shule yao kwa kuamua kuipaka rangi, pamoja na
kushirikiana nao katika 9 Desemba kufanya usafi, jambo ambalo ni muhimu ili
kujiepusha na magonjwa ya miripuko, ukiwamo ugonjwa wa Kipindupindu.
 
“Hatuna cha
kuwalipa Bayport kwa kujitolea kwao kwetu, hivyo tunawaombea kwa Mungu, ingawa
tunazidi kuwaomba waendelee kuwa karibu na sisi kwa kutusaidia mambo mbalimbali
ili tufanikishe kwa vitendo kuwapatia watoto wetu elimu bora ili kuwaandalia
maisha bora wanafunzi hawa ambao licha ya changamoto kadhaa zinazotukabili, ila
ufaulu wao umekuwa ni mkubwa, jambo linalotutia moyo,” alisema Mohamed.
Bayport ni
moja ya taasisi zinazofanya juhudi kubwa kuwakwamua wateja wao, wakiwamo
watumishi wa umma na wafanyakazi wa kampuni binafsi kwa kupewa mikopo isiyokuwa
na amana wala dhamana, huku huduma hizo zikipatikana kwa urahisi kutokana na
kuenea kwa matawi zaidi ya 80 katika wilaya na mikoa mbalimbali ya Tanzania
Bara.

WAFANYAKAZI WA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII WAFANYA USAFI MAENEO MBALIMBALI JIJINI DAR ES SALAAM

WI1
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakifanya usafi katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road ikiwa ni kutekeleza agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kufanyika kwa usafi wa mazingira nchi nzima ikiwa ni maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
WI2
Makatibu  wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt .Donan Mmbando (wapili kulia) na  Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Seikali za Mitaa (TAMISEMI) Ndg. Jummanne Sagini (watano kulia) wakifanya usafi katika Soko la Samaki la Feri jijini Dar es Salaam. Wengine walioshirikia kazi ya kufanya usafi ni  wafanyakazi wa wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
WI3
Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakifanya usafi wa mazingira leo katika soko la samaki la Feri ikiwa ni kutekeleza agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kufanyika kwa usafi wa mazingira nchi nzima ikiwa ni maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
WI4
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donan Mmbando akiongea na waandishi wa Habari waliofika katika soko la samaki la Feri jijini Dar es Salaam kuona jinsi usafi wa mazingira ulivyokuwa unafanyika sokoni hapo.
WI5
Baadhi ya wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakifanya usafi wa mazingira leo katika soko la samaki la Feri ikiwa ni kutekeleza agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kufanyika kwa usafi wa mazingira nchi nzima ikiwa ni maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
WI6
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii  Dk.Donan Mmbando   akiongea na wafanyakazi wa wizara hiyo mara baada ya kumalizika kwa kazi ya  kufanya usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa wizara hiyo walifanya usafi  katika mahabusu ya watoto Kisutu, Makazi ya Wazee ya Nunge, Taasisi za Mifupa MOI na Saratani ya Ocean Road, Hospital ya Taifa Muhimbili, Masoko ya Kariakoo na Feri, na Mbagala Zakhem.
WI7
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakiwa na nyuso za furaha mara  baada ya kumaliza kazi ya  kufanya usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa wizara hiyo walifanya usafi 
Picha na Anna Nkinda – Maelezo

Kwaya ya Kinondoni Revival Tamasha la Krismasi

images (2) 
Na Mwandishi Wetu
KWAYA mahiri ya nyimbo za Injili, Kinondoni Revival ni mojawapo ya watakaosindikiza Tamasha la Krismasi linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama maandalizi ya kuelekea tamasha hilo yanaendelea kufanyika kupitia kamati yake.
Msama alisema waimbaji kadhaa wameshathibitisha kushiriki kufikisha ujumbe wa neno la Mungu ambao ni wa Shukrani baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Msama alisema kabla ya uchaguzi Mkuu aliandaa Tamasha la Kuombea Amani uchaguzi Mkuu , lililofanyika Oktoba 4 uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
“Tunaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi katika tamasha la Krismasi ambalo linalwenda sambamba na shukrani kwa Mungu baada ya kupita kwenye uchaguzi Mkuu uliofanyika kwa amani na utulivu, tukio ambalo limefanikishwa kupitia maombi ya waimbaji na viongozi wa dini waliopiga magoti kumuomba Mungu,” alisema Msama.
Aidha Msama aliwataja waimbaji waliothibitisha kushiriki tamasha hilo ni pamoja na Rebecca Malope, Ephraim Sekeleti, Sarah K, Rose M
uhando, Upendo Nkone, Christina Shusho, Kwaya ya Wakorintho Wapili na Joshua Mlelwa.

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE ASHIRIKI ZOEZI LA USAFI SOKO KUU LA CHALINZE

KJ1
Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng. Evarist Welle Ndikilo wakielekea soko kuu la Chalinze kushirikiana na wananchi kufanya usafi wa mazingira leo Desemba 9, 2015 ikiwa ni kuadhimisha miaka 54 ya UHURU kama ilivyoagizwa na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli
KJ2
Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakifanya usafi katika soko kuu la Chalinze leo Desemba 9, 2015 ikiwa ni kuadhimisha miaka 54 ya UHURU kama ilivyoagizwa na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli
KJ3
Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakifanya usafi katika soko kuu la Chalinze leo Desemba 9, 2015 ikiwa ni kuadhimisha miaka 54 ya UHURU kama ilivyoagizwa na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli
KJ4
Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na wananchi wa Chalinze baada ya kushirikiana nao kufanya usafi wa mazingira ya soko kuu la Chalinze leo Desemba 9, 2015 ikiwa ni kuadhimisha miaka 54 ya UHURU kama ilivyoagizwa na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli

Mkuu wa Mkoa azindua kampeni ya upigaji dawa mabasi ya mikoani

images (1)
Na Immaculate Makilika, MAELEZO
Mkuu  wa Mko wa Dar es Salaam  Saidi  Meck Sadick  leo  katika eneo la Standi ya mabasi Ubungo, amezindua  kampeni ya upigaji dawa ya kuuwa wadudu kwa mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani.
Uzinduzi huo umefanyika  ikiwa ni sehemu ya  kuunga mkono jitihada  za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John  Magufuli  ambaye aliamua maadhimisho ya sherehe za miaka 54 kwa mwaka huu yafanyike kwa wananchi kushiriki kufanya usafi katika maeneo yao.
Hatua hiyo imefikiwa baada ya kuwa na ongezeko kubwa la idadi ya wagonjwa wa kipindupindu ambapo imefikia idadi ya zaidi  ya  vifo  165 nchi nzima, na  kupelekea Mheshimiwa Rais kufikia uamuzi huo.
Aidha, zoezi hilo la upigaji dawa ya kuuwa  wadudu  kwa mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani  limeanza tangu tarehe 7/12/2015  ambapo hadi sasa mabasi zaidi ya 70 tayari yameshapigwa dawa, huku matarajio ni kufikia mabasi 1,000.
Mkuu wa  Mkoa alipongeza jitihada zilizofanywa na Chama cha wamiliki wa mabasi Tanzania  (TABOA)  kwa kuandaa  utaratibu huu kwa kushirikian na  Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi  Kavu  na Majini (SUMATRA) pamoja na Jeshi la Polisi  kikosi cha Usalama Barabarani   na kusema kuwa  “ usafi huu ni endelevu  usisubiri matukio kama haya peke yake, anagalau ufanyike kila  baada ya miezi 4 au 6”.
Aliendelea kwa kusema kuwa,  baadae utaratibu huo  utafanyika pia  kwa daladala zote zinazofanya safari zake  katika jiji la Dar es salaam ili kuhakikisha afya za wasafiri zinakuwa katika hali ya usalama,  na pia aliwataka  wamiliki kuweka vifaa vya kutupa taka katika daladala zao.
Naye,   Kamanda wa Polisi wa kikosi cha usalama Barabarani Mohammed  Mpinga  amesema zoezi hili ni zuri kwa kuwa linasaidia kuhakikisha  usalama  wa abiria kwa kuzuia kupata magonjwa kutokana na maambukizi yanayotokana na wadudu kama kunguni na mende.
Aidha, mmoja wa wamikili wa mabasi Bwana.  Issa  Nkya  amesema zoezi hili linaendelea vizuri, na kuhakikisha kuwa mabasi yote yatapigwa dawa kufikia tarehe 15/12/2015 hadi tarehe  20/12/1015, pia  ametoa wito kwa kwa wamiliki wa mabasi kuhakikisha mabasi yao yanapigwa dawa.
Huku, mmoja wa abiria Bwana. Thabiti  Mfaume  naye amesema amefurahishwa na zoezi hilo na kuomba liwe endelevu.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekua ikiadhimisha sherehe za Uhuru kila mwaka tangu Uhuru wa nchi hii tarehe 9 Desemba, 1961. Ambapo mwaka huu imekua tofauti baada ya Rais John Magufuli kuwataka  wananchi kushiriki katika kampeni ya usafi kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali nchi nzima.
Ambapo, wananchi  katika maeneo yao  nchi nzima wameitikia  wito wa kampeni hiyo kwa kushiriki kwa kufanya usafi na kuungwa  mkono na viongozi  mbalimbali akiwemo Rais Magufuli  ambaye amefanya usafi katika eneo la soko la samaki Feri, Waziri Mkuu Mheshimiwa Majaliwa  Khasim Majaliwa naye  ameshiriki kufanya usafi katika eneo la soko kuu la Kariakoo jijini Dar es salaam.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo afungua maoyesho ya 10 ya filamu za Asia.

OLE1
: Balozi wa Japan nchini Tanzania Bw,Masaki Okada(wa kwanza kushoto) akizungumza jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel(katikati) wakati wa uzinduzi  wa maonyesho ya 10 ya filamu za Asia.Aliyesimama pembeni yao ni katibu mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Tanzania Bi.Joyce Fisoo.
OLE2
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel(wa tano  kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wa nchi za Asia katika uzinduzi wa maonyesho ya 10 ya filamu za Asia.
OLE3
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akifungua maonyesho ya 10 ya Filamu za Asia.Pembeni yake ni mabalozi wa nchi mbalimbali za Asia walihoudhuria uzinduzi huo.Maonyesho Hayo  yatafanyika  kuanzia tarehe 8-17 desemba katika ukumbi wa Century Cinemax Dar Free Market Oysterbay.
OLE4
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bi.Joyce Fisoo akifurahia jambo wakati  wa ufunguzi wa maonyesho ya 10 ya Filamu za Asia katika ukumbi wa Dar free Market jijini Dar es salaam.

TPB YASAFISHA SOKO LA FERI, YATOA VIFAA VYA USAFI, NI KATIKA KUUNGA MKONO UAMUZI WA RAIS MAGUFULI WA UHURU NI KAZI

Kaimu
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania, TPB, Henry Bwogi, akizibua
chemba ya kupitisha maji taka kwenye zoni 3 ya soko la samaki la kimataifa Feri
jijini Dar es Salaam Desemba 9, 2015. TPB imeungana na watanzania katika kuunga
mkono agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwataka wananchi
kusherehekea sikukuu ya Uhuru wa Tanganyika kwa kufanya usafi ili kutekeleza
zana ya “Uhuru ni Kazi” badala ya kufanya sherehe na matamasha huku nchi
ikakabiliwa na ugonjwa wa Kipindupindu
 ………………………………………………………………………
Na
K-Vis Media/Khalfan Said)
KATIKA
kuunga mkono maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa wananchi
na taasisi za serikali kufanya usafi siku ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru
wa Tanganyika, Benki ya Posta Tanzania, TPB, nayo iliungana na wananchi hususan
eneo la soko la kimataifa la samaki Feri, katika kutekeleza agizo hilo.
Wakati
Mh. Rais alishirikiana na majirani zake, wavuvi na wachuuzi wa samaki pale nje
kidogo ya uzio wa Ikulu, hali ilikuwa hivyo hivyo kwenye maeneo mengi, ya nchi
ambapo katika eneo hilo la soko la Feri, TPB walipewa eneo la kufanyia usafi
kwenye zoni namba 1 na eneo la kuegeshea mitumbwi maarufu kama “Lebanon” ambapo
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Bw. Henri Bwogi, aliwaongoza
wafanyakazi wa benki hiyo katika kufagia, kuzibua mitaro na chemba za maji
taka, hali kadhalika kupakia taka kwenye malori ya kubebea taka.
Katika
hatua nyingine Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo Bw. Bwogi, alikabidhi
vifaa vya kufanyia uasafi viliovyokuwa vikitumiwa na wafanyakazi wa benki hiyo
kwa uongozi wa soko ili waendelee na kazi ya usafi siku za usoni.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli,
aliagiza sherehe za mwaka huu za Uhuru wa Tanganyika, zisherehekewe kwa kufanya
kazi ili kutekeleza zana ya “Uhuru ni Kazi” badala ya kufanya matamasha na shamra
shamra kwenye viwanja mbaklimbali nchini.

Nimefurahishwa sana na wananchi jinsi walivyojitokeza kwa wingi kwenye maeneo
mbaklimbali ya nchi katika kufanya usafi ili kuiweka nchi yetu safi na
kujikinga na maradhi kama Kipindupindu.” Rais Magufukli aliwaambia majirani
zake baada ya zoezi la kufanya usafi.
Naye
Kaimu Afisa Myendaji Mkuu wa TPB, Bw. Bwogi, alisema TPB kama taasisi ya
serikali iliamuru wafanyakazi wake, wafike kazini na kushiriki katika kufanya
usafi na sisi tumeona tuje kuungana na wenzetu wa feri ili kutekeleza maelekezo
ya Rais wetu.” Alisema.
 Mfanyakazi wa TPB, akizibua chemba katika kutekeleza zana ya Uhuru ni Kazi

Usafi wa Disemba 9 wang’arisha Soko la Tandale

bei
Na Jacquiline Mrisho
Mazingira ya Soko la Tandale jijini Dar r es salaam yamekua safi  baada ya usafi mkubwa kufanywa leo na wafanyabiashara pamoja na Makampuni mbalimbali yaliyojitolea kusaidia kusafisha mazingira hayo.
Akiongea na mwandishi, Mtendaji  wa Kata ya Tandale Bw.Ole Losai amesema kuwa usafi wa kawaida huwa unafanyika sokoni hapo ila changamoto kubwa ni ukosefu wa vifaa pamoja na magari ya kubebea uchafu kutokuja kwa wakati kwakua soko la Tandale linapokea zaidi ya tani 28 za uchafu kwa siku kutoka kwenye vifungashio vya  bidhaa mbalimbali ziletwazo sokoni hapo.
“Tamko la Muheshimiwa Rais ni zuri sana maana sherehe za uhuru zimesherehekewa na watu wote kwa kufanya usafi wa mazingira “alisema Bw. Losai.
Aliongeza kuwa ,kwa Wilaya ya Kinondoni hasa Kata ya Tandale usafi ulianza kufanyika tangu Disemba 1 baada ya kufanya uzinduzi wa usafi katika Wilaya hiyo ambapo Mtendaji wa Kata pamoja na watendaji wa Manispaa ya Kinondoni walipita kila mtaa kuwahamasisha wananchi kufanya usafi katika maeneo yao.
Aidha Mwenyekiti wa Soko hilo,Bw.Mohamedi Mwekya ametoa salamu za pongezi  kwa Muheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutoa tamko la kufanya usafi wa mazingira pamoja na kulisimamia hadi kukamilika kwake hivi leo.
“Matamko mengi huwa yanatamkwa na viongozi mbalimbali lakini hayafanyiwi utekelezaji ila hili la Muheshimiwa Rais,watu wamelipokea na wamefanya usafi kwa bidii hata hali ya soko letu inaridhisha”amesema Bw. Mwekya.
Pia Bw. Mwekya aliyapongeza makampuni na vikundi mbalimbali vya kijamii ambavyo vimejitolea kusaidia  kufanya usafi katika Soko la Tandale ambapo aliyataja baadhi ya Makampuni na vikundi hivyo vya Kijamii vilivyoshiriki  kuwa ni chombo cha habari cha Clauds Media Group, Msalaba Mwekundu,Max Malipo, Benki ya Biashara ya Akiba (ACB), Watendaji wa Manispaa,Shirika la Afya Duniani (WHO) na Kliniki ya tiba mbadala ya Ifakara Herbalist Clinic iliyopo Tandale.
Akiongea na mwandishi,mmoja wa wafanyabiashara wa soko hilo Bw.Gasper Muhumba alisema,wito wa wananchi umekua mkubwa na wamewahi kuanza usafi kabla hata ya muda uliopangwa (sa moja asubuhi) na hii inaonyesha kuwa watu wamependa na wamekubaliana na wazo la Muheshimiwa Rais John Pombe Magufuli ndio maana wamefanya kazi ya kusafisha mazingira kwa juhudi.
Tamko hili lilitolewa na Rais John Pombe Magufuli kuwa badala ya wananchi kujumuika uwanjani kuazimisha siku ya Uhuru,maadhimisho hayo yatafanyika kwa kufanya usafi katika maeneo yetu yanayotuzunguka ili kuzuia magonjwa ya milipuko kama kipindupindu.

Wananchi wazingatie Mipango Miji kudumisha Usafi

index 
Diwani wa kata ya Kawe Mhe. Muta Rwakatare akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu usafi katiak kata ya ya kawe ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais Dkt Magufuli kufanya usafi siku ya Disemba 9.
……………………………………………………………………………………………..
Na Raymond Mushumbusi -Maelezo
Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Bw. Alphayo Kidatu aliposhiriki kufanya usafi katika eneo la mto Mbezi maarufu kwa jina la darajani kwa Malecela ikiwa ni kuunga mkono tamko la Mhe Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli la kuitangaza siku ya Disemba 9 kuwa ni siku ya uhuru na kazi.
Katibu Mkuu Alphayo Kidatu amesema kuwa  usafi sio kusafisha maeneo tu ya makazi na sehemu za huduma pia ni kuzingatia mipango miji kwa kutovamia maeneo ya wazi, kujenga kiholela bila mipango na kuvamia sehemu za vyanzo vya maji kwa kuchimba mchanga na kufanya yale yote yanayohatarisha usafi wa mazingira.
“  kwa sasa wizarani tunahakikisha tunatoa ramani za mipango miji kwenda mpaka serikali za mitaa ili wananchi na watendaji wa serikali za mitaa wajue maeneo ya wazi yako wapi ili waweze kuyasimamia.” Alisema Kidatu.
Naye Diwani wa kata ya Kawe Mhe. Muta Rwakatare amesema kata yake inachangamoto za kukosa huduma ya kukusanya taka na kwa sasa wameamua kufunga dampo ndogol ililopo pembezoni mwa mto Mbezi ili kuepusha magonjwa ya mlipuko.
“ kama viongozi hatuwezi kusubiri Manispaa waleta magari ya kuzoe taka mimi kama diwani nitahakikisha anakuwepo mkandarasi wa kuzoa taka katika kata yangu na swala hili nitalisimamia kwa karibu” Alisema  Rwakatare.
Naye mtendaji wa kata ya kawe Bw. Raymond Chimbuya amesema wanaunga mkono siku ya leo na halitaishia leo tu bali watajiwekea utaratibu kwa kushirikia na diwani na wananchi kufanya usafi kuwa ni desturi na sio mpaka walazimishwe.
Akizungumza mmoja ya wananchi wa kata yak awe Bw. Hussein Bana amesema wanapenda kufanya usafi ila changamoto zimekuwa ni vifaa vya usafi, watu kutojitoa kufanya usafi maeneo yao na ufatiliaji mbovu katika serikali za mitaa hivyo watendaji wafatilie kwa karibu ili kunusuru afya za wa watanzania na watanzania tuwe na desturi ya usafi.
Disemba 9 ilitangazwa rasmi na Mhe rais dkt John Pombe Joseph Magufuli kuwa ni siku ya uhuru na kazi na wananchi wafanye usafi katika maeneo yao ili kupiga vita ugonjwa wa kipindipindu unaoenea kwa kasi nchini.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN ASHIRIKI NA WANANCHI WA ENEO LAKE KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA, MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU

SM1 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan, akishiriki kufagia na baadhi ya wananchi wakazi wa eneo lake la Oysterbay Karume Raod, wakati wa zoezi la kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan, akishiriki kufagia na baadhi ya wananchi wakazi wa eneo lake la Oysterbay Karume Raod, wakati wa zoezi la kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM4 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan, akishiriki kuzoa taka na baadhi ya wananchi wakazi wa eneo lake la Oysterbay- Karume Raod, wakati wa zoezi la kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM5 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili eneo la Kituo cha Daladala cha Morocco, kwa ajili ya kuendelea kushiriki na wananchi wa eneo hilo kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM6 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiingia kukagua eneo la kuhifadhia Taka lililopo eneo la Kituo cha Daladala cha Morocco, wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kuendelea kushiriki na wananchi kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM7 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan, akishiriki kuzoa taka na baadhi ya wananchi wa eneo Morocco, wakati wa zoezi la kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote hii leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi na wasanii mbalimbali waliojitokeza kushiriki naye katika zoezi hilo baada ya kuhitimisha zoezi la usafi eneo la Morocco, jijini Dar es Salaam, leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM9 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi na wasanii mbalimbali waliojitokeza kushiriki naye katika zoezi hilo baada ya kuhitimisha zoezi la usafi eneo la Morocco, jijini Dar es Salaam, leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM11 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi na wasanii mbalimbali waliojitokeza kushiriki naye katika zoezi hilo baada ya kuhitimisha zoezi la usafi eneo la Morocco, jijini Dar es Salaam, leo Dec 9, 2015. Picha na OMR
SM13 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiondoka eneo la Morocco, baada ya kushiriki zoezi hilo na wananchi wa eneo hilo la kufanya usafi wa mazingira leo Dec 9, 2015. Picha na OMR

KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO AKIFANYA USAFI NA WANANCHI WA UPANGA MASHARIKI

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika toroli akishiriki zoezi la usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika toroli akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika toroli akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika toroli akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika koleo akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika koleo akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel anayeendesha toroli akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel anayeendesha toroli akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyechuchumaa akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika koleo akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyeshika toroli akishiriki zoezi la
usafi na wananchi wa Kata ya Upanga mashariki ikiwa ni kuitikia wito wa
kutikia agizo la Mh. Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi siku ya
Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania
 
PIcha na Benjamin Sawe

MH. NAPE NNAUYE ASHIRIKI KUFANYA USAFI MTAMA

 Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akishiriki kufanya usafi jimboni kwake ikiwa sehemu ya kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli inayowataka wananchi kushiriki usafi wa mazingira kwenye siku ya kilele cha kusheherekea uhuru wa Tanzania, Desemba 9.
 Wakazi wa jimbo la Mtama wakijitokeza kufanya usafi
 Wakazi wa jimbo la Mtama wakishiriki usafi
  Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Yahaya Nawanda (mwenye fulana nyeusi) akishiriki usafi pamoja Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye na wakazi wa jimbo hilo ikiwa sehemu ya kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli inayowataka wananchi
kushiriki usafi wa mazingira kwenye siku ya kilele cha kusheherekea
uhuru wa Tanzania, Desemba 9.

 Usafi ukiendelea Mtama ambapo wananchi wamesafisha mitaro yote pamoja na maeneo ya sokoni.
  Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akishiriki kufanya usafi
jimboni kwake ikiwa sehemu ya kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli inayowataka wananchi
kushiriki usafi wa mazingira kwenye siku ya kilele cha kusheherekea
uhuru wa Tanzania, Desemba 9.

 Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akizungumza na wananchi wa jimbo lake waliojitokeza kushiriki usafi

WAFANYAKAZI NHC WAUNGA MKONO AGIZO LA RAIS DK MAGUFULI, WASHIRIKI KWA VITENDO KUSAFISHA MITAA NHC UPANGA


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiongoza kwa vitendo zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC na maeneo yanayozunguka barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore UPANGA jijini Dar es Salaam leo. Menejimenti ya NHC imeamua kuwa kufanya usafi kwenye majengo ya Shirika ili kuonyesha kwa vitendo utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli wa kuitumia Sikukuu ya Uhuru na Jamhuri ambayo hufanyika kila ifikapo Desemba 9 ya kila mwaka kwa gwaride na shamrashamra za halaiki, kufanya usafi wa mazingira. 

Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Issack Peter na Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi TAMICO, NHC, Lilian Reuben wakishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiongoza kwa vitendo  zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiongoza kwa vitendo zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiwa amebeba reki kushiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Wafanyakazi wa NHC wakishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Yamlihery Ndullah wa NHC akishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC na maeneo yanayozunguka barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

 Wafanyakazi wa NHC wakishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa NHC, Haikamen Mlekio  akishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC na maeneo yanayozunguka barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

 Mkurugenzi wa Fedha wa NHC, Felix Maagi akishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC na maeneo yanayozunguka barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

  Mkurugenzi wa Fedha wa NHC, Felix Maagi akishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC na maeneo yanayozunguka barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Wafanyakazi wa NHC wakiwa na zana za usafi wakielekea kwenye wakishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Issack Peter na Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi TAMICO, NHC, Lilian Reuben wakishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo

  Mkurugenzi wa Fedha wa NHC, Felix Maagi akishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC na maeneo yanayozunguka barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

  Mkurugenzi wa Fedha wa NHC, Felix Maagi akishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC na maeneo yanayozunguka barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo. 


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiongoza kwa vitendo zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

Kutoka kushoto Meneja wa Fedha wa NHC, Albinus Manumbu, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi TAMICO, NHC, Lilian Reuben, Meneja wa Huduma kwa Jamii, Muungano Saguya na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu wakishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiongoza kwa vitendo zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

 Mojawapo ya majengo ya NHC yaliyopo katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi lililofanyiwa usafi a wafanyakazi wa NHC.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiwa na wadau walioshiriki katika zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiongoza kwa vitendo  zoezi la kufanya usafi katika majengo ya NHC yaliyopo barabara za Ali Hassan Mwinyi, Alikhan, Barak Obama na Magore jijini Dar es Salaam leo.

NHIF YAADHIMISHA 9 DESEMBA KWA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

????????????????????????????????????
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Michael Mhando akikabidhi mashuka  100 kwa Hospitali ya Jeshi la Polisi Kilwa Road baada ya kuwaongoza watumishi wa mfuko NHIF kwa  kufanya usafi maeneo yanayozunguka makao makuu ya Mfuko na hatimaye kutoa mashuka 100 kwa jeshi la Polisi
????????????????????????????????????
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Michael Mhando akishiriki kufanya usafi pamoja na wafanyakazi wa mfuko wa NHIF  kuzunguka maeneo ya majengo ya mfuko hu.
????????????????????????????????????
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Michael Mhando akiwaelekeza wafanyakazi wa NHIF mahali pengine ambapo panatakiwa kufanyiwa usafi.
????????????????????????????????????
Wafanyakazi hao wakiendelea na kazi ya kuzoa taka.
????????????????????????????????????
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko Michael Mhando wa pili kutoka kushoto akiongozana na maofisa wa shirika hilo kuelekea ofisini baada ya kumalizika leo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wafanyakazi wakiendelea ksafisha mitaro.
????????????????????????????????????

WAKAZI WA KITUNDA JIJINI DAR ES SALAAM WAITIKIA WITO WA KUFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA UHURU 9 DESEMBA MWAKA HUU.

index 
Baadhi ya Wakazi wa Kitunda jijini Dar es Salaam wakiitikia wito wa Rais John Pombe Magufuli wa kuadhimisha siku ya Uhuru wa Tanzania Bara unafanyika kila mwaka tarehe 9 Desemba kwa kufanya usafi katika maaeneo yao.
index2 
Mmoja wa  Wakazi wa Kitunda jijini Dar es Salaam akiitikia wito wa Rais John Pombe Magufuli wa kuadhimisha siku ya Uhuru wa Tanzania Bara unafanyika kila mwaka tarehe 9 Desemba kwa kufanya usafi katika maaeneo yao.
…………………………………………………………………………………………
Na Benedict Liwenga
 
Wakazi wa Kata ya Kitunda Kati Jijini Dar es Salaam wameitikia wito wa kufanya usafi katika maeneo yao ikiwa ni siku ya Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania inayofanyika kila mwaka tarehe 9 Desemba.
Akiongea leo kwa niaba ya wakazi wa eneo lake, Mjumbe wa Nyumba Kumi Bi. Zahara Idrissa ameeleza kuwa kauli ya Mhe. Rais John Pombe Magufuli la kuwataka Watanzania wote nchini kuadhimisha Sherehe za Siku ya Uhuru kwa kufanya usafi katika maeneo yao ni suala muhimu kwakuwa linasaidia katika kuepukana na magonjwa ya milipuko ukiwemo ugonjwa wa Kipundipindu ambao umeshika kasi nchini.
Bi. Idrissa amesema kuwa kwa kufanya usafi katika maeneo ya makazi kutawafanya watu wengi kujitambua na kuachana na tabia ya kutupa taka ovyo ili kuepukana na magonjwa hatari, hivyo wao wameamua kuitikia wito huo kwa dhati na kushirikiana kwa bidiii kuifanya kazi hiyo.
Ameongeza kuwa, suala la kufanya usafi katika makazi nchini kote liwe endelevu kwani haitakuwa na maana kufanya hivyo siku moja tu ya Uhuru kama kumpendezesha Rais.
‘’Hili suala la usafi ni zuri sana na linaboresha mazingira yetu na linawafanya watu wajielewe kwa kuishi katika mazingira yaliyosafi na salama ili kujikinga na maambukizi ya magonjwa hasa ya milipuko, lakini kuna watu wengine wanakuwa wabishi wa kufanya usafi hivyo  hatunabudi kuwahimiza watu wa namna hii’’, alisema Bi. Idrissa.
Aidha, ametoa ushauri kwa Serikali ya Awamu ya Tano ya kutaka suala la usafi liwe la mara kwa mara ikiwezekana kila siku za Jumamosi watu wawe wanafanya usafi na kwa kufanya hivyo magonjwa kama vile Kipindupindu na malaria vitatoweka.
Makzi wa Kivule Bwana Yusuph Mateka ambaye ni Fundi pikipiki katika eneo la Kitunda Shule anafafanua kuwa, suala la kufnya usafi ni jambo zuri lakini changamoto iliyopo ni magari ya kuzoa taka yamekuwa hakuna katika maeneo yao hali ambayo inawafanya wafanya usafi kulindika taka eneo moja bila kuzipeleka kunakohusika.
‘’Kwa kifupi hali iliyoko ya uchafu jijini Dar es Salaa imekithiri lakini kama zoezi hili la ufanyaji wa usafi litakuwa enedelevu basi litasaidia kuondokana na maradhi hasa ya kipindupindu, hivyo mimi nampa pongezi sana Mhe. Magufuli kwa wazo hili zuri alilotuletea sisi Watanzania.
Watanzania leo wanashiriki katika kufanya usafi kwenye maeneo yao ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania Bara ambayo kwa mwaka huu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliamua itumike kwa kufanya usafi nchini kote ili kuepukana na magonjwa ya kipindupindu yatokanayo na uchafu.

FILAMU YA ‘Going Bongo’ KUZINDULIWA MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM

FILAMU mpyaindex inayokwenda kwa jina la ‘Going Bongo’ ambayo iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa filamu ndani na na nje ya nchi  imekamilika  sasa kuzinduzliwa rasmi kesho  Ijumaa kwenye ukumbi wa sinema wa Century Cinemax uliopo Mlimani City, Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jijini Dar es Salaam kuhusu uzinduzi huo mtunzi na muandishi ambaye pia ameisimamia  katika kuitengeneza na kuigiza filamu hiyo,Ernest Napoleon  alisema, “Naamini kuonyeshwa kwa filamu hii kutaandika historia muhimu kwenye tasnia ya filamu  nchini Tanzania”
“Tunashukuru kupata  nafasi hii kwani tunategemea tutaweza kubadilisha utamaduni wa kuangalia filamu haswa pale filamu nyingi za hapa nyumbani zikipana nafasi ya kuonyeshwa kwenye majumba ya majumba ya sinema” alisema.
Filamu hiyo ambayo mpaka sasa imetwaa tunzo kadhaa, ina maudhui ambayo yanonyesha maisha ya Daktari aliyejitolea kwenda kufanya huduma  nchini Tanzania kwa muda wa  mwezi mmoja.
Filamu hii imerekodiwa   majiji makubwa mawili ambayo ni Dar es Salaam na California  Marekani, inaelezea sehemu ya maisha ya kweli aliyonayo Daktari  mwenye asili ya nchini Ufaransa  aliyeondoka Ulaya na kwenda kufanya kazi  barani Afrika.
Kati ya tuzo ambazo filamu hii imeshinda ni pamoja na, Filamu Bora Afrika Mashiriki katika tamasha la Zanzibar International Film Festival (Ziff)  na Filamu Bora ya Kimataifa katika tamasha la ‘Black Entertainment Fashion’,  ‘Film and Television Awards’  (BEFTA)
Amewaomba mashabikmi wa filamu kujitokeza kwa wingi kesho kwenye uzinduzi huo ambapo tiketi zimeshaanza kuuzwa Century Cinemax Theaters Mlimani City.

WAFANYAKAZI HOSPITALI YA MUHIMBILI WAFANYA USAFI

VE1 
Baadhi ya Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakifanya usafi leo nje ya jengo la Kibasila akiwamo Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithnashery Jamaat ya jijini Dar es Salaam, Dewji Azim (katikati).
VE2 
Kushoto ni Mwanasheria wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Veronica Hillary, Mkuu wa Idara ya Upasuaji,  Dk Julieth Magandi, Mkurugenzi wa Upasuaji, Dk John Kimario na Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithnashery Jamaat ya jijini Dar es Salaam, Dewji Azim wakifanya usafi leo Desemba 9 ambayo ni siku ya kuadhimisha Uhuru wa Tanzania. Usafi huo umefanyika katika Jengo la Kibasila.
VE3 
Mkurugenzi wa Upasuaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk John Kimario akisomba takataka ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la Rais John Pombe Magufuli kwamba leo Desemba 9, siku ya Uhuru watu wote wajumuike kufanya usafi.
VE4
VE5 
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Aminiel Aligaesha (wa pili kulia) akishiriki kufanya usafi katika hospitali hiyo leo Desemba 9, 2015.
VE6 
Mkuu wa Idara ya Sheria, Veronica Hillary, Ofisa Uhusiano Msaidizi, John Stephen, Mkurugenzi wa Upasuaji, Dk John Kimario na Mkuu wa Idara ya Upasuaji, Dk Julieth Magandi wakijumuika pamoja kufanya usafi leo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ikiwa ni kuitikia agizo la Rais John Pombe Magufuli la kufanya usafi leo Desemba 9, siku ya Uhuru.
VE7 
Mwenyekiti wa Khoja Shia Ithnashery Jamaat ya jijini Dar es Salaam, Dewji Azim akifanya usafi leo katika hospitali hiyo.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AFANYA USAFI SOKO KUU LA KARIAKOO

mal2 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisafisha mtaro wa maji machafu kwenye soko kuu la Kariakoo jijini Dar es salaam Desemba 9, 2015.  Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Meck Sadiki.(Pichana Ofisi ya Waziri Mkuu)
mal3 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akielekea eneo la shimoni kwenye soko kuu la Kariakoo kufanya usafi Desemba 9, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mal4 
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akitoka eneo la shimoni kwenye soko kuu la  Kariakoo kufanya usafi Desemba 9, 2015. Kulia kwake ni Mkuu wa wilaya ya Ilala, Raymond Mushi. (Picha na Ofisi ya  Waziri Mkuu)
mal6 mal7 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na umati ulioshiriki katika kufanya usafi kwenye soko kuu la Kariakoo jijini Dar es salaam Desemba 9, 2015.  kushoto  kwake ni  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Meck Sadiki na Kulia kwake ni Mkuu wa wilaya ya Ilala, Raymond Mushi.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mal8 
Baadhi ya washiriki wa zoezi la usafi kwenye soko kuu la Kariakoo jijini Dar es salaam wakipiga picha kwa kutumia simu wakati Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa alipozunguza nao baada ya kufanya usafi  sokoni hapo  Desemba 9, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mal10 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na umati ulioshiriki katika kufanya usafi kwenye soko kuu la Kariakoo jijini Dar es salaam Desemba 9, 2015.  .(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mal13 
Gari alilopanda Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa likitoka kwenye eneo la soko kuu la Kariakoo alikokwenda kushiriki katika kufanya usafi Desemba 9, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
mal15…………………………………………………………………………
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema zoezi la usafi lililofanyika leo nchini kote lisiishie hapo bali liwe endelevu ili Tanzania iwe na taswira nzuri kwa wageni wanaoingia nchini.
Ametoa wito huo leo kwenye soko la Kariakoo wakati akishiriki zoezi la kufanya usafiikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Pombe Magufuli la kutaka maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru yasiwepo na badala yake watu wote washiriki kufanya usafi katika maeneo mbalimbali.
Waziri Mkuu Majaliwa pia amewataka viongozi wa soko la Kariakoo wafike ofisini kwake Jumatatu ijayo (Desemba 14, 2015) saa 4 asubuhi ili wamueleze wana mikakati gani ya kuboresha utoaji huduma kwenye soko hilo.
“Natambua kuwa siyo sahihi kupanga chini biashara tulizonazo. Nataka hawa viongozi waje wanieleze wana mpango gani endelevu wa kuboresha soko hili,” alisema Waziri Mkuu huku akishangiliwa.
Waziri Mkuu ambaye alienda kufanya usafi kwenye soko hilo,  alilazimika kuzungumza na mamia ya wananchi waliofika kushiriki zoezi hilo. Pia alikagua maeneo mbalimbali ya soko hilo hadi shimoni na kusema aneridhika na usafi uliofanyika bali amesisitiza usafi huo uendelezwe.
“Kaulimbiu ya Mheshimiwa Rais Magufuli ya HAPA KAZI TU inatupa ari ya kufanya kazi. Fanyeni kazi. Watanzania mko huru kufanya kazi yoyote lakini cha msingi fuateni taratibu na kanuni. Serikali hii tumamua kuwajali watu wa chini. Tutahakikisha wajasiriamali wadogo, akinamama lishe na wamachinga mnafanya kazi kwa amani na utulivu, ” alisema.
Rais Magufuli aliamua kuitangaza siku ya leo (Desemba 9, 2015) ambayo ni maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru iwe ni siku ya kufanya usafi nchi nzima ili kuepukana na magonjwa mbalimbali na hasa kipindupindu..

Rais Magufuli afanya usafi katika Ufukwe wa Ferry jijini Dar es Salaam

guf1 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mama Janeth Magufuli wakielekea eneo la ufukwe wa Ferry kufanya usafi katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru tarehe 9 Desemba.
guf2 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizoa taka katika eneo la ferry jijini Dar es Salaam.
guf3 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizoa taka katika eneo la ferry jijini Dar es Salaam.
guf4 guf6 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizoa taka katika eneo la ufukwe wa ferry jijini Dar es Salaam.
guf7 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka taka ndani ya ndoo ya Taka katika eneo la Magogoni jijini Dar es Salaam.
guf8 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kulia akiwa pamoja na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakifanya usafi katika eneo la ufukwe wa ferry jijini Dar es Salaam.
guf9 guf10 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka taka taka kwenye dastibin wakati akifanya zoezi la kufanya usafi katika eneo la ufukwe wa Ferry jijini Dar es Salaam.
guf11 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiokota takataka katika eneo la Ferry katika zoezi la kufanya usafi nchi nzima.
guf12 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiokota takataka katika eneo la Ferry katika zoezi la kufanya usafi nchi nzima.
guf13 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wavuvi wa ferry huku akiwa ndani ya Mtumbwi. Rais Magufuli alizisikiliza kero zao na kuahidi kuzitatua ndani ya muda mfupi.guf14 
Rais Magufuli akifanya usafi pamoja na wavuvi wa eneo la ferry waliojitokeza kuungamkono zoezi hilo. Rais Magufuli amewataka Watanzania kuwa na Utamaduni wa kufanya Usafi kila wakati ili kuweka mazingira katika hali nzuri. PICHA ZOTE NA IKULU

Matukio ya picha za usafi siku ya Uhuru kutoka Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira

um1 
Katibu wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi (katikati) akiwaongoza watumishi wa ofisi yake Kufanya usafi eneo la Maktaba Kuu ya Taifa ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania.
um2 
Watumishi wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma wakiwa katika Picha ya pamoja baada ya kumaliza zoezi la usafi katika eneo la Maktaba kuu ya Taifa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanzania.
um3 
Sehemu ya Watumishi wa Sekretarieti ya Ajira wakishiriki katika zoezi la usafi kuadhimisha siku ya Uhuru.

SSRA emerged the First winner in the National Board of Accountants and Auditors (NBAA) – Best presented Financial Statements Competitionusing IPSAS

 THE Social Security Regulatory Authority (SSRA) has emerged the First winner in the National Board of Accountants and Auditors (NBAA) Best presented financial statements competition. SSRA competed in the International Public Sector Accounting Standards (IPSAS)   category with other public entities using IPSAS.
 
It’s the fourth year consecutively since SSRA started
participating in the competition and throughout the period the Authority became
number one for the all four years. It’s the Authority’s pleasure to be
associated and acknowledged in this prestigious and highly recognized best
financial statements competition.
 
SSRA Board Chairman( at the
center) with SSRA staff in a jovial mood after emerging theFirst winner in the
National Board of Accountants and Auditors (NBAA) Best presented Financial
Statements Competition from left Ms. Lightness Mauki Director of  Compliance and Registration; Mr. Emil Mkaki –
Finance Manager; Mr. Mohamed Nyasama –Director of Finance & Administration
& Mr. Peter Mbelwa – Chief Internal Auditor.
SSRA Director of Compliance &
Registration Ms. Lightness Mauki receiving award trophy from   Dr. Hamis Mwinyimvua Deputy Permanent Secretary-
Ministry of Finance looking from left is Mr. Peter Mbelwa – Chief Internal
Auditor.
SSRA Director of Compliance & Registration Ms. Lightness
Mauki receiving award trophy from   Dr.
Hamis Mwinyimvua Deputy Permanent Secretary- Ministry of Finance.
SSRA Director of Finance & Administration Mr. Mohamed Nyasama in a jovial mood holding a trophy with Ms. Lightness Mauki – Director of Compliance and Registrations.
SSRA Director of Finance & Administration Mr. Mohamed Nyasama in a jovial mood holding a trophy with Ms. Lightness Mauki – Director of Compliance and Registrations.

MASHINDANO BAISKELI KILOMITA 115 YAKUZA VIPAJI VYA VIJANA

Washindi wa kwanza wa
mashindano.ya baiskeli, ya  Rift Valley
Odyssey  ya liyofanyika  jijini arusha  DEC 6 Mwaka huu Sophia Husseni wa kwanza
(kulia) na Sophia Adson wa (pili) kutoka kulia wakiwa na Mkurugenzi wa 6degrees
Simone Paine wa pili kutoka kulia yaliyo fanyika Arusha ambapo wachezaji
toka ndani nan je ya nchi wameshirikai kwa takriban siku mbili kuendesha kwa
umbali wa kilomita 115. Masindano ambayo yanawapa ushindi timu ya Warriors
ambao wametumia masaa matano na dakika 28
 Mshindi wakwanza wa mashindano ya
kuendesha baiskeli  ya   Rift Valley Odyssey  Sophia Husseni ya liyofanyika  jijini arusha  DEC  Jijini Arusha
Washiriki wa mashindano ya baiskeliya  Rift Valley Odyssey  yaliyofanyika
jijini arusha ambapo wachezaji toka ndani nan je ya nchi wameshirikai
kwa takriban siku mbili kuendesha kwa umbali wa kilomita 115
 Mkurugenzi wa 6degrees
Simone Paine akizungumza na washiriki wa shindano hilo.
Mshindi wakwanza wa mashindano ya
kuendesha baiskeli  ya   Rift Valley Odyssey  Sophia Husseni

NAPE AWAPA PIKIPIKI MAKATIBU KATA WA JIMBO LAKE

 Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akimkabidhi Katibu wa kata ya Mtua Kilimahewa funguo ya pikipiki kwa niaba ya makatibu kata 20 wa jimbo hilo ambao wote wamewezeshwa usafiri wa pikipiki ili kurahisisha ufanisi wa kazi zao.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM) Nape Nnauye akijaribu moja ya pikipiki kati ya 20 alizowapa makatibu kata ili ziweze kuwasaidia kufanya kazi kwa ufanisi kwenye shughuli zao za kujenga na kuimarisha Chama Cha Mapinduzi.
 Sehemu ya pikipiki zilizotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye kwa makatibu kata 20 wa jimbo hilo.
Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akizungumza mbele ya viongozi wa CCM wilaya ya Lindi vijijini ambapo aliwaambia viongozi hao kuwa amejipanga kufanya kazi katika jimbo hilo zenye kuleta tija na kuhakikisha anatekeleza ahadi zote alizozitoa wakati wa kampeni na kuwata makatibu kata waliokabidhiwa pikipiki 20 kuzitumia katika kazi za kujenga na kuimarisha chama.

No comments :

Post a Comment