Waziri
Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa
kadhaa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi baada ya
kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo
hakuyafurahia.
Maafisa
hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze
kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.
Habari kamili inaandaliwa. Fanya subira....
Kwa sasa anza na picha....
Kwa sasa anza na picha....
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.
Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere, jijini Dar es Salaam, Bw.Injinia Thomas Haule, (katikati), akizungumza
kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa uwanja huo
leo Ijumaa Novemba 27, 2015. Utawala wa uwanja huo ulio chini ya Mamlaka ya
Viwanja vya Ndege Tanzania, TAA, umejipanga upya katika kuimarisha ulinzi
ambapo kuanzia sasa, vifurushi na mizigo yote kutoka posta itakaguliwa kwa mara
ya pili kabla ya kupakiwa ndani ya ndege, ikiwa ni hatua ya kudhibiti vifurushi
na mizigo haramu kupenya kwenye ndege. Kushoto ni Kaimu Meneja Usalama wa
Uwanja huo, Bw.David Ngaragi, (kushoto) na Afisa Usalama Mwandamizi wa Uwanja
huo, Dorice Uhagile. (Picha na K-Vis Media/Khalfan Said)
Na K-Vis Media
UONGOZI
wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere unaomilikiwa na
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, TAA, umetangaza leo Ijumaa
Novemba 27, 2015 kuwa kuanzia sasa vifurushi na mizigo mingine yote ya
Shirika la Posta Tanzania, itakaguliwa kwa mara ya pili kama mizigo
mingine yoyote kabla ya kupakiwa ndani ya ndege.
Uamuzi
huo umetangazwa na Mkurugenzi wa Uwanja huo, (JNIA), Injinia Thomas
Haule, wakati akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye
ukumbi wa mikutano wa VIP ulioko uwanjani hapo.
Alisema,
uamuzi huo ni baada ya Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege, TAA, kutoa maonyo
kadhaa, kwa Shirika la Posta, kuimarisha ukaguzi wa vifurushi na mizigo
itokayo Posta kwa vile imekuwa ikikamatwa na mizigo ambayo ni tofauti na
iliyokusudiwa.
Alitaja
mizigo hiyo kuwa ni pamoja nabangi, na kwamba, Uholanzi wamekuwa
wakilalamika mara kadhaa kuwa wamekuwa wakikamata vifurushi vya Posta
vikiwa na mizigo iliyoharamishwa.
"Sisi
Kama Mamlaka, wajibu wetu mkubwa ni kuzuia kitu au vitu vyovyote
vinavyoweza kuhatarisha usalama wa abiria wawapo ndani ya ndege au ndege
yenyewe haviingii ndani ya ndege." Alianza kwa kusema Injinia Haule na
kuongeza kuwa, vitu vingine kama madawa ya kulevya, pembe za ndovu, na
vingine vingi, , vinashughulikiwa na mamlaka nyingine ambazo zina
maafisa wake hapa JNIA wakishirikiana na maafisa wetu.
Hata
hivyo makosa yafanywayo na idara Fulani ya serikali yenye afisa wake
hapa JNIA, ni wazi kwamba watakaonyooshewankidole ni TAA, alisema na
kubainisha kuwa Mamlaka haitavumilia tena uzembe utakaofanywa na taasisi
nyingine ya serikali katika kuhakikisha zinatekeleza wajibu wake
ipasavyo
Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, Injinia Thomas Haule, akizungumza kwenye mkutano huo
Meneja wa Usalama wa Mamlaka ya Viwanja
vya Ndege Tanzania, TAA, kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere jijini Dar es Salaam, Bw.David Ngaragi, akifafanua jambo kwenye
mkutano huo na waandishi wa habari
Waandishiw a habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, JNIA, Injinia Thomas Haule
Injinia Haule akiteta jambo na Afisa
Habari wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Bw. Godfrey Lutego,
muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano huo
| Mteja wa muda mrefu wa bemki ya Amana Bw Masoud Khalfan ambaye akizindua wiki ya huduma kwa wateja katika tawi la Main la benki ya Amana jijini Dar ka kukata utepe. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa benki hiyo Dk Muhsin Masoud, Kulia ni mkuu wa idara ya masoko Bw Dassu Mohamed Mussa, kushoto ni mteja wa siku nyingi wa benki hiyo Bw Dossa. |
Mkuu wa idara ya masoko Bw. Dassu Mussa
kushoto akiwa na mkuu wa kitengo cha fedha Bw. Fahad Hamid siku ya
uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja.
|
Benki ya kwanza ya kiislamu Tanzania, Amana Bank imeadhimisha miaka minne tangu kuanza rasmi kutoa huduma zake kwa wateja mnamo 24 Novemba 2011. Wakuu wa idara Mameneja na wafanyakazi siku ya jumatatu wote walikutana na wateja na kuwapatia huduma mbalimbali kupitia matawi yetu yote ya Dar es salaam, Arusha na Mwanza.
Meneja wa tawi la Main, Bi Aisha Awadh akimwelekeza kitu mteja wa benki hiyo mama Sangawe.
|
Amana Bank ambayo kwa sasa ina wateja zaidi ya 20,000 na matawi 7 Tanzania nzima, inachukua
fursa katika maadhimisho haya kuwashukuru wateja wake wote kwa kuwa
wazalendo na kuichagua Amana Bank kama pendekezo lao kwa huduma za
kibenki. Amana Bank inaahidi kuendelea kuwekeza na kukuza
mtandao wake na kuleta bidhaa na huduma bora Zaidi na za kisasa. Amana
Bank mpaka sasa ina matawi saba ambapo manne yapo jijini Dar nayo ni
Tandamti, Lumumba, Nyerere na main ambapo ndipo makao makuu ya benki
hiyo ya aina yake nchini.
| Mfanyakazi wa benki ya Amana (Kushoto) akiwahudumia wateja kwa viburudisho katika siku ya wiki ya huduma kwa wateja wiki hii. |
Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Amana wakipata picha ya pamoja.
|
Mkurugenzi Mtendaji wa Amana Bank, Dr. Muhsin Salim Masoud amesema, “Katika kipindi hiki maalum kwa benki yetu, tutashirikiana na wateja wetu wa ndani na wa nje kwa kuwapatia huduma bora zaidi. Tunaamini wateja wetu ndio muhimili wa mafanikio yetu, lengo letu kubwa ni kuwaridhisha wao hivyo tumejidhatiti kuwapa huduma bora muda wote bila kujali mahali walipo. Tunawaahidi wateja wetu huduma za kiwango cha juu kwa ajili ya mahitaji yao ya binafsi au kibiashara muda wote.
| Mtoa huduma kwa wateja Bi. Zainab wa tawi la Mwanza akimhudumia kwa viburudisho mteja wa benki hiyo. |
| Mteja huyu akijipatia huduma katika tawi la Mwanza |
Huduma kwa wateja.
|
Maadhimisho haya yatahitimishwa ijumaa ya 27/11/2015, kwa
hafla ya kuwazawadia wateja na wafanyakazi katika matawi ya Amana Bank
ambapo mkurugenzi wa benki hiyo Dk Muhsin Masoud atakuwa katika tawi
la jijini Mwanza mjini kukutana na wateja na kupokea maoni na ushauri wa
kila aina utakaotolewa na wateja wao.
![]() |
| Baadhi ya wateja wakijipatia huduma katika benki ya Amana tawi la jijni Arusha. |

![]() |
| Huduma kwa wateja zikiendelea jijini Arusha. |
JAMII YA WAHADZABE, WABARABAIG, WAMASAI WAIOMBA SERIKALI YA TANZANIA KUWATAMBUA KAMA JAMII NYINGINE!
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki
za Binadamu, Mh. Idd Ramadhan Mapuri (katikati) akizindua taarifa ya
Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kuhusu utafiti wa Hali ya
Haki za watu wenye kuishi maisha asilia Tanzania. kushoto kwake ni
Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi. Mary
Massay na (kulia) ni mmoja wa wajumbe walioshiriki kuandaa ripoti
hiyo, kutoka nchini Kenya katika taasisi ya ACHPR, Dk. Naomi Kipuri.(Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[DAR ES SALAAM-TANZANIA] Jamii ya
watu wa asili na makundi yao wameiomba Serikali ya Tanzania kutambua
uwepo wao hapa nchini ikiwemo kuwatangaza kwa mema na kuwasaidia kwa
misingi ya haki, hutu na kimaendeleo kama watu wengine wanaotambulika
ndani na nje ya mipaka yao.
Hayo yameelezwa mapema leo jijini
hapa wakati wa uzinduzi wa taarifa ya Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu
na Watu kuhusu utafiti wa Hali ya Haki za watu wenye kuishi maisha
asilia Tanzania wakiwemo makabila ya Wa-Akiye,Wa- Hadzabe,Wa-
IIparakuyio Masai na wengine wengi.
Akielezea katika uzinduzi huo mmoja
wa wajumbe walioandaa taarifa ya Tume hiyo, ambaye anatoka nchini
Kenya, katika taasisi ya African Commission on Human and Peoples Rights
(ACHPR), Dk. Naomi Kipuri amebainisha kuwa jamii ya watu asilia
wamekuwa na kilio cha muda mrefu cha kutaka kupata haki zao zao msingi
na kutambulika zaidi.
“Utafiti tuliofanya jamii ya watu
asilia wamekuwa katika malalamiko ya muda mrefu ikiwemo kutaka haki zao
za msingi. Ikiwemo masuala ya elimu, makazi na haki zingine. Pia
wameomba Serikali kuwatangaza watu hawa wa asilia ili wasionekane
wageni kwani jamii nyingi bado hazijawatambua na hata kupelekea
kuwavunjia hutu wao” alieleza Dk. Naomi.
Aidha, Dk. Naomi katika uwakilishi
wake wa mada kwenye mkutano huo amelezea namna ya jamii inavyoendelea
kuwaona watu hao ni tofauti kiasi cha kupelekea watu hao kudumaa na
maisha yale yale ya asilia.
Mtangazaji wa radio Deutsche
Welle (DW) ya Ujerumani, George Njogopa akifanya mahojiano na Katibu
Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi. Mary Massay.
Kushoto ni Mratibu wa NGONET Ngorongoro, Samweli Nangiria
“Jamii zingine zinawatenga watu wa
jamii ya Wamasai, tumeshuhudia lugha na matamshi kwenye mizunguko ya
watu ikiwemo kwenye madaladala, mitaani huku wakimuona Mmasai kama mtu
tofauti, sasa katika ripoti hii imeweza kuelezea mambo mengi sana.
Ikiwemo suala la Haki ya kuishi, kufanya kazi na mambo yote kama watu
wengine” alimalizia Dk. Naomi.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa
Tume ya Haki za Binadamu, Mh. Idd Ramadhan Mapuri ameeleza kuwa kupitia
ofisi yake itahakikisha inashughulikia suala hilo la kuwa karibu na
watu asilia na kutambua misingi ya haki zao ambapo amebainisha watu hao
wa asilia kwa Tanzania wanafikia makundi zaidi ya sita.
Kwa upande wao baadhi ya wawakilishi
wa watu hao wa watu asilia wakielezea katika mkutano huo, waliomba na
wao na wapate wawakilishi maalum ikiwemo Bungeni ama sehemu za maamuzi
ikiwemo Halmashauri na maeneo mengine ya Serikali ilikutambua michakato
ya Kimaendeleo kwa kina.
“Jambo la ardhi, ndilo linalotuumiza
kwa sasa. Sie tunaporwa ardhi yetu kila siku na kesi nyingi ni za
kuporwa ardhi na migogoro ya wakulima na wafugaji, ndani ya migogoro hii
ina siri kubwa bila kujua kiini chake ni wakati wa kufika kule na
kupata ukweli zaidi” alielezea Adam Ole Mwarabu
Kwa upande wake, Mratibu wa NGONET
Ngorongoro, Samweli Nangiria ambaye anawakilisha watu hao asilia
anaeleza kuwa, wao wamekuwa wakitambuana kwa desturi ikiwemo suala la
ufugaji na maisha mengine, Jamii nyingine imekuwa wakiwaona wao ni watu
wa tofauti kiasi cha kupora mali zao ikiwemo ardhi, mifugo na mambo
mengine ya msingi.
Baadhi ya wawakilishi wa Jamii za
watu asilia wakiwemo Wahadzabe, Masai, Wabarabaig na wakiwa katika
picha ya pamoja na viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
na wadau wengineo wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa
ripoti hiyo juu ya usawa na kutambulika kama jamii asilia yenye tamaduni
na desturi zake.
“Sie watu asilia tuna mahusiano
mbalimbali na jamii zetu za kifugaji licha ya jamii zingine kutuingilia
kwenye maeneo yetu na kupora ardhi yetu. Watu asilia tunahitajika
kutambulika zaidi na hata kupatiwa huduma muhimu ikiwemo kujengewa
shule, vyuo na mahitaji mengine ikiwemo haki na hutu kama watu wengine.”
Alieleza Samweli Nangiria.
Kwa upande wake, .. ameweza
kuipongeza tume ya Haki za Binadamu kwa kuweza kushughulikia suala hilo
na hata kuandaa tukio hilo kwa kushirikisha wadau wengine wakiemo wao wa
asilia.
“Tanzania ndio nchi ya kwanza
kuaandaa kikao cha Afrika kwa watu hawa wa makundi maalum wa asilia,
kilichofanyika mwaka uliopita. Hili ni jambo bora sana kwani watu asilia
tunaendelea kutambulika zaidi.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa ya
taarifa ya Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kuhusu utafiti wa
Hali ya Haki za watu wenye kuishi maisha asilia Tanzania, imeweza
kuangalia mambo mbalimbali ikiwemo suala la haki ya kuishi, Utawala bora
na namna ya jamii hizo zinapotokea katika maeneo yao hapa nchini.
Wadau wa haki za binadamu wakiwa
katika picha ya pamoja katika mkutano huo baada ya uzinduzi wa ripoti
hiyo ya kuwatambua watu wa makundi asilia. Mkutano unaofanyika katika
ukumbi wa mikutano wa Blue Pearl Ubungo jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa washiriki wa mkutano huo
Mhifadhi Mkuu, kutoka ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Seleman Kisimbo
akichangia mada juu ya hali iliyopo sasa ikiwemo jamii hiyo ya watu
asilia na changamoto za Mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo suala la ukame
inayowakabili katika maisha yao ya vijijini.
Dk. Naomi Kipuri wa taasisi ya
ACHPR, ya nchini Kenya akijadiliana jambo na Mhadhiri wa Sheria Chuo
Kikuu cha Tumaini-Makumira, Bw. Elifuraha Laltaika.
Baadhi ya wawakilishi wa Jamii za
watu asilia wakiwemo Wahadzabe, Masai, Wabarabaig na wengineo wakiwa
kwenye picha ya pamoja kwenye mkutano huo.








No comments :
Post a Comment