Friday, November 27, 2015

BREAKING NEWZZZZZ….WAZIRI MKUU MAJALIWA AVAMIA BANDARI LEO, AAMRISHA KUKAMATWA KWA MAAFISA KIBAO WA TRA

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa  wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi  baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia.
Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri.
Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.
Habari kamili inaandaliwa. Fanya subira….
Kwa sasa anza na picha….
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi.
 Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa 
akiagana na viongozi wa TRA na TPA.

MWILI WA MAWAZO KUAGWA KITAIFA KATIKA UWANJA WA FURAHISHA JIJINI MWANZA.

Mkutano wa Naibu Katibu Mkuu Chadema Salum Mwalimu na Wanahabari Jijini Mwanza hii leo.
Na:Binagi Media Group
Mwili wa aliekuwa
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Geita Marehemu
Alphonce Mawazo, kesho unatarajiwa kuagwa Jijini Mwanza kabla ya kusafirisha
kwenda Mkoani humo kwa ajili ya Mazishi.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema Salum Mwalimu, amesema Marehemu Mawazo
ataagwa Kitaifa kwa taratibu za chama hicho, katika uwanja wa Furahisha Jijini
Mwanza.
Amesema ratiba hiyo itatanguliwa na ratiba ya kifamilia ya kuuaga
mwili huo, ambayo itafanyika asubuhi Nyegezi Jijini Mwanza ambako ni nyumbani
kwa Mchungaji Charles Lugiko ambae ni baba mdogo wa Marehemu Mawazo hiyo ikiwa
ni baada ya mwili wake kutolewa katika Hospitali ya Rufaa Bugando
ulikohifadhiwa.
Mwalimu amebainisha kwamba mwili huo utasafirishwa hiyo kesho
kwenda Mkoani Geita kuanzia majira ya saa nane mchana ambapo wakazi wa Mkoa huo
pia watapata fursa ya kuuagwa kesho kutwa jumapili.
Ameeleza kwamba kuanzia majira ya saa mbili asubuhi, shughuli za
kuuaga mwili huo zitafanyika Kimkoa katika Uwanja wa Magereza Mjini Geita na
baadae kusafirisha kwenda Katoro ambapo wakazi wa Jimbo lake la Busanda
watapata fursa ya kuuaga mwili huo.
Mwalimu ametanabaisha kwamba, baada ya shughuli zote hizo
kukamilika, mazishi ya Marehemu Mawazo yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatatu
katika Kijiji cha Chikobe Jimbo la Busanda Mkoani Geita.
Shughuli zote hizo zinatarajiwa kuongozwa na Mwenyekiti wa Chadema
Taifa Freeman Mbowe, Viongozi waandamizi wa Chama hicho akiwemo Frederick
Sumaye, aliekuwa mgombea urais wa Ukawa Edward Lowasa, wabunge pamoja na makada
wa Chadema.
Ratiba za Mazishi ya Marehemu Mawazo ambae aliuawa Novemba 14
mwaka huu na watu wasiojulikana, zimejiri baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza
jana kuondoa zuio la Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza, lililokuwa zinazuia mwili
huo kuagwa Jijini Mwanza kutokana na hofu ya kiusalama pamoja na uwepo wa
mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambapo zuio hilo liliondolewa katika kesi
iliyofunguliwa na baba mlezi wa Mawazo, Mchungaji Charles Lugiko baada mvutano
mkali wa siku nne mahakamani hapo.

BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA

Naibu Katibu Mkuu Chadema, Salum Mwalimu akionyesha kibali kilichotolewa na Manispaa ya Ilemela ili kuruhusu ibada ya kumuaga Marehemu Mawazo Kufanyika kesho katika Uwanja wa Furahisha
Mkutano wa Naibu Katibu Mkuu Chadema Salum Mwalimu na Wanahabari Jijini Mwanza hii leo (hawapo pichani).
Kushoto ni Ezekiel Wenje na Kulia ni Grace Kihwelu ambae ni Mbunge Viti Maalumu Chadema Mkoani Kilimanjaro
Singo Kigaila Benson ambae ni Mkurugenzi wa Mafunzo Chadema (Kushoto) akiwa na Peter Mekele ambae ni Mwenyekiti Chadema Kanda ya Ziwa Victoria (Kulia)
Husna Amri Said ambae ni Mwenyekiti BAWACHA Wilayani Geita
Viongozi na Makada wa Chadema
Mkutano wa kutoa ratiba za kuuaga mwili wa Marehemu Mawazo kwa wanahabari Jijini Mwanza hii leo
Wanahabari

KAMPENI YA ABIRIA PAZA SAUTI YAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Mkuu wa Kitengo cha Elimu kwa Umma wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Abel Swai (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo, kuhusu kampeni ya Abiria Paza Sauti iliyozinduliwa Dar es Salaam leo asubuhi.
…………………………………………………………………………….
Na Dotto Mwaibale
MKUU wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna wa Polisi, Mohamed Mpinga amesema kila mwananchi anawajibu kuzuia ajali za barabarani badala ya kudhani kazi hiyo ni ya polisi pekee.
Mpinga alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Abiria Paza Sauti iliyozinduliwa Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam leo asubuhi, ambao ulikwenda sanjari na mabalozi wa Usalama barabarani  (RSA) ambao walitoa elimu  kwa abiria kuhusu usalama barabarani.
“Abiria pazeni sauti pale mtakapoona dereva anaendesha gari lake ndivyo sivyo na kama mtapaza sauti itasaidia kupunguza ajali hapa nchini” alisema Kamanda Mpinga.
Mwakilishi  wa Mwenyekiti wa Usalama Barabarani ambaye ni Mratibu wa kampeni hiyo , Jackson Kalikuntima, alisema kampeni hiyo itaendelea nchini kote kwa njia ya kutoa elimu, haki na wajibu wa raia wanapokuwa safarini.
Alisema abiria wanaowajibu wa kuzuia ajali wakishirikiana na mabalozi watakao kuwa ndani ya mabasi kuhimiza abiria kupaza sauti.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Elimu kwa Umma wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Abel Swai alisema kumekuwa na changamoto kubwa kwa baadhi ya madereva kukiuka sheria na kusababisha ajali kwa makusudi.
Alisema kampeni hiyo inalengo la kutoa elimu kwa abiria waweze kujiamini na kutoa taarifa pale wanapoona dereva anakwenda kinyume na sheria kwa kutumia namba za kutoa taarifa kwa polisi na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) ambazo ni 0800110019 au 0800110020.
Swai alisema madereva wanapaswa kutii sheria bila shuruti na kuwa wana amini kila mmoja atakuwa makini na kuzingatia sheria ajali zitapungua kama sio kuisha kabisa.

NHIF Yakabidhiwa Kituo cha Matibabu cha Mfano Dodoma

re1
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa Bw. Michael Muhando akionyesha funguo za majengo ya kituo chake cha matibabu kilicho katika Chuo Kikuu cha UDOM mkoani Dodoma.
re2
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa Bw. Michael Muhando akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhiwa majengo ya kituo chake cha matibabu kilicho katika Chuo Kikuu cha UDOM mkoani Dodoma.
re3
Majengo yenyewe yanavyoonekana.
re5
Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa Bw. Michael Muhando akikagua majengo hayo.
……………………………………………………………………………………………………..
MFUKO wa taifa wa bima ya afya (NHIF) umekabidhiwa kituo chake cha
matibabu cha mfano mara baada ya ujenzi wa kituo hicho kukamilika.
Makadhiano hayo yamefanyika mjini hapa jana (leo) katika hafla fupi
iliyohudhuriwa na Uongozi wa nhif, hospitali ya mkoa na timu ya
wakandarasi akiwemo mshauri mkuu wa mradhi huo kampuni ya Nosuto
Associates.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Michael Mhando amesema kukamilika kwa
jengo hilo ni hatua kubwa iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na kazi
iliyoko sasa ni ya ununuzi wa vifaa na samani za jengo ili lianza
kutoa huduma kabla ya sikukuu ya Krismasi.
Amesema timu ya wataalamu kutoka Sekteratarieti ya mkoa tayari iko
jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuchagua vifaa tiba mbalimbali
vitakavyotumika. Ameongeza kuwa vifaa vyote hivyo pamoja na samani za
jengo hili vitalipiwa na Mfuko wa NHIF.
Kituo hicho cha matibabu cha kisasa kinayo mifumo mbalimbali ya TEHAMA
katika utoaji wake wa huduma ikiwemo miito kwa wauguzi,  utayarishaji
wa madai na utambuzi wa wagonjwa.
Amesema malengo makuu ya ujenzi wa kituo hicho ni kuwa na kituo cha
kisasa kitakachowezesha wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na
umma wa watanzania kwa ujumla kupata huduma bora za matibabu
wanapokuwa Dodoma katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa.
Naye Mkurugenzi wa fedha,mipango na uwekezaji wa nhif bw Desudedit
Rutazaa amesema Kituo hicho vilevile kitasaidia kuwepo na watalamu
wenye uzoefu nchini kwani itakuwa ni sehemu ya kujifunzia kwa
wataalamu wa kada mbalimbali za udaktari na utabibu wawapo masomoni
katika mkoa wa Dodoma na mikoa mingine ya Tanzania.

KAMANDA MPINGA AZINDUA OPERESHENI PAZA SAUTI,JIJINI DAR ES SALAAM LEO

mp1 
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani,DCP  Mohamed Mpinga, akisalimiana na Mabalozi wa Usalama Barabarani, muda mfupi kabla ya kuzindua Operesheni ijulikanayo kwa jina la “Paza Sauti” yenye lengo la kuwaelimisha abiria ili waweze kutoa taarifa mara wanapoona kuna viashiria vya uvunjifu wa sheria za barabarani. Operesheni hii ilizinduliwa jijini Dar es Salaam leo.
mp2 
Kamanda  wa Kikosi cha Usalama Barabarani, DCP Mohammed Mpinga, akitoa maelekezo ndani ya moja ya basi linalofanya safari  zake mkoani wakati wa  kuzindua  wa Operesheni Paza Sauti yenye lengo la kuwaelimisha abiria ili waweze kutoa taarifa mara wanapoona  viashiria vya uvunjifu wa sheria za  barabarani. Operesheni hii ilizinduliwa jijini Dar es Salaam leo.
mp3 
Wadau wanaotumia  usafiri wa barabara, wakiwemo madereva na abiria wakimsikiliza Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga(hayupo pichani) alipozindua  Operesheni Paza Sauti, yenye lengo la kuwaelimisha abiria ili waweze kutoa taarifa  wanapoona kuna viashiria vya  uvunjifu wa sheria za barabarani,Operesheni hii ilizinduliwa jijini Dar es Salaam leo.
mp4 
Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo na Matukio wa Mabalozi wa Usalama Barabarani,Jackson Kalikumtima(kulia), akitoa elimu kuhusiana na Operesheni ya Paza Sauti kwa mmoja wa wadau wanaotumia  usafiri wa barabara, Operesheni hii ilizinduliwa Stendi ya Mabasi yaendayo mikoani ya Ubungo, jijini Dar es Salaam leo.(Picha zote na Abubakari Akida,Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

MAHAKAMA YA TANZANIA YAFUNGUA MILANGO KWA WANAHABARI.

index 
Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila akitoa ufafanuzi kuhusu Kichwa cha Habari ya Mahakamani kilichoandikwa bila kuzingatia Weledi na moja ya Gazeti la Kila siku  wakati wa mafunzo ya  siku mbili ya Waandishi wa Habari za Mahakama yaliyofanyika jijini Dar es salaam. Picha/Aron Msigwa –MAELEZO.
…………………………………………………………………………………….
Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
.Dar es salaam.
Mahakama ya Tanzania imesema kuwa itendelea kufanya kazi na vyombo vya Habari nchini katika kuuhabarisha umma kuhusu utekelezaji wa jukumu la Kikatiba ililonalo la kutafsiri sheria mbalimbali na kuzitolea maamuzi ili kuwawezesha wananchi kujua na kupata Haki zao kwa wakati.
Akifunga Mafunzo ya siku 2 ya waandishi wa Habari za Mahakama jana jijini Dar es salaam Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila aliwataka waandishi hao kutimiza wajibu wao wa kuueleza umma taarifa sahihi za mashauri mbalimbali yanayotokea mahakamani kwa kuzingatia sheria.
Alisema vyombo vya habari na mahakama vinahitajiana, vinafanya kazi pamoja kwa manufaa ya umma huku akieleza kuwa mikutano ya mara kwa mara kati ya wanahabari na mahakama kunaongeza kuaminiana na kujenga mahusiano mazuri.
Alifafanua kuwa kazi ya Mahakama kikatiba ni kutafsiri sheria mbalimbali na kuzitolea maamuzi kwa mujibu wa sheria kulingana na mashauri yananayowasilishwa Mahakamani na kuongeza kuwa hakuna Jaji wa Mahakama ya Tanzania anayeamua kesi bila nje ya utaratibu wa sheria zilizopo.
Alisema wao kama majaji hutumia sheria zilizopo katika kutoa maamuzi hata kama haziwapendezi wahusika na kuongeza kuwa jambo wanalolifanya ni kutoa maoni na mapendekezo kwa mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa hatua zaidi.
” Sisi kama Majaji hutumia sheria zilizopo kutoa maamuzi,hatutungi sheria jukumu letu kikatiba ni kutafsiri sheria mbalimbali na kuzitolea maamuzi pia tunatumia fursa ya maamuzi tunayoyatoa  kuelimisha jamii kuhusu sheria iliyotumika kutoa haki katika kesi husika” Alisema.
Aliwataka waandishi wa Habari za Mahakama kujipa muda wa kutosha pindi wanapofika Mahakamani kufuatilia mashauri yanayoendeshwa ili waweze kuwa na taarifa za kutosha pindi shauri linapofunguliwa na kutolewa hukumu ili kuwawezesha wananchi kupata taarifa za kutosha za mwenendo wa Mashauri.
Aliongeza kuwa Mahakama ya Tanzania imedhamiria  kufanya kazi na waandishi wa habari nchini kwa kuzingatia kwamba wakati majaji wanapotoa hukumu mahakamani kunakuwa na idadi ndogo ya wananchi wanaoshuhudia kuliko ile iliyo nje ila vyombo vya habari kutokana na umuhimu wake huwapasha habari mamilioni ya watanzania  walio nje ya Mahakama.
Alisema Mahakama itaendelea kujenga mahusiano mazuri na Vyombo vya Habari hususan waandishi wa Habari za Mahakama kwa kutenga maeneo ndani ya Mahakama yatakayotumiwa na waandishi hao kuwawezesha kufanya kazi zao bila vikwazo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo.
Pia alieleza kuwa Mahakama, itaendelea kutoa taarifa za ufafanuzi wa hukumu mbalimbali zitakazotolewa kwa vyombo vya habari pia Nakala za taarifa za Hukumu kwa waandishi wa habari ili kuwawezesha wananchi kujua ukweli wa yale yanayojili mahakamani kuondoa upotoshaji unaotokea.

Majaliwa azindua ununuzi wa hisa za Benki ya Walimu- MCB

tr1 
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majliwa akigonga kengelle kuashiria uzinduzi wa ununuzi wa hisa za Benki ya Walimu- MCB kwenye soko la hisa la Dar es salaam. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es salaam Novemba 27, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
tr2 
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua uuzaji wa hisa za Benki ya Walimu MCB kwenye soko la hisa la Dar es salaam, uliofanyika jijini Dar es salaam Novemba 27, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
tr4 
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa akiteta na baadhi ya Viongozi wa Benki ya Walimu- MCB baada ya kuzindua uuzaji wa hisa za Benki hiyo katika soko la hisa la Dar es salaam. Uzinduzi huo uliyofanyika jijini Dar es salaam Novemba 27, 2015 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
tr5 
Waziri Mkuu,Majaliwa Kassim Majlaiwa akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile baada ya kuzindua mpango wa Benki ya Walimu MCB – MCB kuanza kuuza hisa zake kwenye soko la hisa la Dar es salaam Novemba 27, 2015. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dares salaam.3065 (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU AWASIMAMISHA KAZI MAAFISA ​WATANO WA TRA

tr6 
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa  akisalimiana na Kamishina Mkuu wa  Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade na Naibu wake, Lusekelo Mwaseba (wapili kulia ) baada ya kuwasili kwenye bandari ya Dar es salaam kutaka maelezo kuhusu upotevu wa makontena 349 yenye kodi ya serikali ya thamani ya shilingi bilioni 80, Novemba 27, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
tr7
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa  akimwonyesha orodha ya makontena 349 yenye kodi ya serikali ya thamani ya shilingi bilioni 80 yaliyotoka kwenye bandari ya Dar es salaam bila kulipiwa kondi, Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania , Rished Bade wakati alipotaka maelezo kuhusu upotevu  wa makontena hayo, bandarini jijini Dar es slaam Novemba 27, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
tr9 
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa  akimkabidhi Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade orodha ya makontena  349 yenye kodi ya serikali ya thamani ya  shilingi bilioni 800 yalitoka kwenye bandari ya Dar es salaam bila kulipiwa kodi. Mheshimiwa Majaliwa alikwenda kwenye bandari ya Dar es salaam Novemba 27, 2015 kutaka maelezo kuhusu kupotea kwa makontena hayo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
tr10 
Waziri Mkuu, Majliwa Kassim Majaliwa akizungumza kwenye bandari ya Dar es salaam alikokwenda Novemba 27, 2015 kutaka maelezo ya makontena 349 yaliyotoka kwenye bandari ya Dar es salam bila kulipiwa kodi na kuikosesha serikali shilingi billioni 80. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
…………………………………………………………………………
*Ni kwa upotevu wa makontena 349, yana thamani ya sh. bilioni 80/-
WAZIRI MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi maafisa watano na watumishi watatu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutokana na upotevu wa makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni 80/-.
Akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari pamoja na viongozi wa TRA katika ziara ya kushtukiza leo mchana (Ijumaa, Novemba 27, 2015), Waziri Mkuu amewataka Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Rished Bade na Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Lusekelo Mwaseba wahahakikishe wanashirikiana na polisi kufuatilia upotevu huo na kwamba fedha hizo zinapatikana na zinarudi Serikalini.
Akitangaza uamuzi huo baada ya kufanya kikao na baadhi ya viongozi wa Serikali bandarini hapo, Waziri Mkuu aliwataja maafisa waliosimamishwa kazi kuwa ni Kamishna wa Forodha, Bw. Tiagi Masamaki na Mkuu wa Kituo cha Huduma kwa Wateja, Bw. Habibu Mponezya.
“Hawa wanasimamishwa kazi. IGP ninaagiza hawa watu wakamatwe na kuisaidia polisi. Hati zao za kusafiria zikamatwe na mali zao zikaguliwe kama zinaendana na utumishi wa umma,” alisema Waziri Mkuu.
Maafisa wengine waliosimamishwa kazi ni Mkuu wa kitengo cha TEHAMA, Bw. Haruni Mpande, Bw. Hamisi Ali Omari (hakutaja ni wa idara gani), na Mkuu wa Kitengo cha Bandari Kavu (ICD In-Charge), Bw. Eliachi Mrema. “Hawa wanasimamishwa kazi hadi uchunguzi utakapokamilika na pia wawe mikononi mwa polisi,” alisema.
Pia aliagiza watumishi watatu wa mamlaka hiyo wahamishwe kutoka Dar es Salaam na kupelekwa mikoani. Watumishi hao ni Bw. Anangisye Mtafya, Bw. Nsajigwa Mwandengele na Bw. Robert Nyoni.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemwagiza Katibu Mkuu wa Hazina, Dk. Servacius Likwelile ambaye alikuwepo kwenye kikao hicho, kuhakikisha kuwa anapeleka wataalamu kutoka Wakala wa Serikali Mtandao (e-Govt) haraka iwezekanavyo ili wakakague mifumo ya taarifa na kubaini jinsi ambavyo wizi huo unafanyika.
“Ninataka uchunguzi uanze kufanyika mara moja, tafuteni njia ambazo zinatumika kama mianya ya wizi kutokea hapa bandarini hadi kwenye ICDs. Nataka hayo makontena yatafutwe hadi yajulikane yako wapi, na fedha hiyo ihakikishwe inarudi serikalini,” alisema.
Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Bw. Ernest Mangu, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Florens Turuka, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM, Suleiman Kova, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Bw. Awadh Massawe na viongozi mbalimbali kutoka TRA na TPA.
Mapema akijibu maswali ya Waziri Mkuu, Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Bade alikiri kwamba kuna upotevu wa makontena ambao huwa unafanyika kati ya bandarini na ICDs na hasa ICD ya Ubungo. Akitoa ufafanuzi, alisema kwamba walifanya ukaguzi kwenye ICD moja na kukuta makontena 54 yamepotea kwa njia za wizi. “Hata hivyo, tulipoendelea na ukaguzi, namba iliongezeka na kufikia 327. Tunaendelea kufuatilia kwa kushirikiana na TAKUKURU. Mmiliki wa ICD ametakiwa kulipa faini sh. bilioni 12.6/- na ameshalipa sh. bilioni 2.4/-,” alifafanua.
Alipoulizwa na Waziri Mkuu kama ana majina ya watumishi wanaohusika na wizi huo, Bw. Bade akakiri kwamba anayo lakini siyo kwa wakati huo labda ayapate kutoka kwa wasaidizi wake. Ndipo Waziri Mkuu akamuonyesha orodha ya makontena 349 yenye taarifa zote hadi namba za magari yaliyobeba mizigo hiyo na Bw. Bade akakiri kwamba orodha hiyo ni ya kweli.
“Kwa utaratibu huo hatuwezi kufika, labda baadhi ya watu waondolewe kazini”. Ndipo akaanza kutaja majina ya maafisa hao waliosimamishwa kazi.

…………………………………

KITUO CHA KILIMO N AUFUGAJI KUJENGWA WILAYANI KIBAHA KUUNGA JUHUDI ZA SERIKALI KATIKA SEKTA YA KILIMO

images 
NA VICTOR MASANGU,KIBAHA
KATIKA kuunga mkono juhudi za serikali katika kukuza sekta ya kilimo Chama cha wakinamama wataalamu katika sekta za kilimo mifugo  pamoja na mazingira Tanzania (TAWLAE) wamejiwekea mikakati ya kujenga kituo maalumu  cha kilimo na ufugaji  katika kata ya Pangani iliyopo Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI

 DSC00212 
MZEE WA MIAKA 70 MKAZI WA KIJIJI CHA MPELANGWASI WILAYA YA RUNGWE ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA MWANYAPU MWAKASEGE ALIKUTWA AMEUAWA KWAKUPIGWA MCHI KICHWANI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA.

Makumbusho ya Taifa yazindua maonyesho ya picha za matukio yanayohusu Albino nchini

al1 
Mratibu wa Maonyesho ya Picha za Alibino kutoka Makumbusho ya Taifa Bibi. Flora Vicent akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa maonyesho hayo jana jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo yanafanyika kuanzia tarehe 26 Novemba 2015 hadi tarehe 26 Januari 2016
al2 
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Profesa Audax Mabulla (kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa Under The Same Sun Bw. Peter Ash, Mwakilishi wa Benki ya Dunia Dkt. Yutaka Yoshino wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maonyesho ya Picha za matukio ya watu wa jamii ya Albino zilizo pigwa katika kambi ya kuwahudumia Albino ya Kabanga.
al3 
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Profesa Audax Mabulla (kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa Under The Same Sun Bw. Peter Ash, Mwakilishi wa Benki ya Dunia Dkt. Yutaka Yoshino wakipongezana mara baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maonyesho ya Picha za matukio ya watu wa jamii ya Albino zilizo pigwa katika kambi ya kuwahudumia Albino ya Kabanga.
al4 
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Profesa Audax Mabulla (kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa Under The Same Sun Bw. Peter Ash, Mwakilishi wa Benki ya Dunia Dkt. Yutaka Yoshino wakifurahia mara baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maonyesho ya Picha za matukio ya watu wa jamii ya Albino zilizopigwa katika kambi ya kuwahudumia Albino ya Kabanga
al5 
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu akifuatilia maelekezo ya Picha wakati hafla ya uzinduzi wa mmaonyesho ya picha maonyesho ya Picha za matukio ya watu wa jamii ya Albino zilizopigwa katika kambi ya kuwahudumia Albino ya Kabanga.
al6 
Wakiwa katika picha ya pamoja.

Tigo yazindua mtandao wenye kasi zaidi wa 4G LTE jijini Tanga.

goz1 
Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Mashariki, Goodluck Charles (wa pili kulia) akimkabidhi zawadi ya simu, James Marwa ambaye aliibuka mshindi wa kwanza wa bahati nasibu iliyochezeshwa jana sambamba na uzinduzi wa intaneti yenye kasi zaidi ya 4G LTE jijini Tanga.
goz2 
Wadau mbalimbali wakimsikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa mfumo wa intaneti wenye kasi zaidi wa 4G LTE, uliozinduliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, jijini Tanga jana.
goz3
Mkuu wa kitengo cha biashara (B2B) katika kampuni ya simu za mkononi ya Tigo Rene Bascope, akihutubia hadhira iliyohudhuria uzinduzi wa mfumo wa intaneti wenye kasi zaidi (4G LTE) uliozinduliwa jana jijini Tanga.
goz4 
Wadau mbalimabli wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, wakihudumiwa na watoa huduma wa kampuni hiyo sambamba na uzinduzi wa huduma ya intaneti yenye kasi zaidi (4G LTE) uliofanyika jijini Tanga jana.
goz5 
Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Tanga, Nassor Sisiwaya (wa pili kushoto) akibadilishana mawazo na Meneja Mawasiliano ya Umma wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo John Wanyancha (wa kwanza kulia) wakati wa uzinduzi huo.
goz6 
Mkuu wa wilaya ya Tanga, Abdullah Lutavi akihutubia wakati wa uzinduzi huo.

No comments :

Post a Comment