Wednesday, November 18, 2015

PSPF YAWAPONGEZA WABUNGE WA BUNGE LA 11 LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

DSC_1602
Rais wa klabu ya Rotary Dar es Salaam Oyster Bay kwa mwaka huu wa 2015-2016, Mohamed Versi akizungumza na waandishi wa Habari (Hawapo pichani) katika mji wa Kerege jana Novemba 15. wakati wa zoezi hilo la kambi ya bure ya upimaji wa afya. (Picha zote na Andrew Chale ).
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[BAGAMOYO] Klabu ya Rotary ya Dar es Salaam Oyster Bay, kwa mara nyingine tena imeendesha matibabu katika kambi maalum ya matibabu ya bure katika mji wa Kerege uliopo Bagamoyo, Mkoani Pwani.
Kambi hiyo iliyofanyika siku ya Jumapil Novemba 15.2015 ambapo zaidi ya wahudumu 50 wa Afya walipima na kutibu magonjwa kwa wakazi hao wa Kerege waliojitokeza kwa wingi wanaokadiriwa kufikia zaidi ya 700.
Kambi hiyo ya matibabu bure imedhaminiwa na benki ya Diamond Trust Bank (DTB) imeweza kuwa faraja kubwa kwa wananchi na wakazi wa Kerege kupata Huduma hiyo kwani imeweza kuwafikia muda muafaka kwao kupata fursa za matibabu na vipimo bure.
Akizungumza na wanahabari Rais wa klabu hiyo ya Rotary Dar es Salaam Oyster Bay kwa mwaka huu wa 2015-2016, Mohamed Versi amebainisha kuwa wito mkubwa kwa wananchi wa Kerege kujitokeza kunawapa faraja kuendelea kutembelea na kuweka kambi kwa mwaka mara moja katika mji huo.
“Mwaka huu ni wa tano tokea kuanza kutoa matibabu bure kwa kuweka kambi hizi za matibabu. Kwa hapa Kerege huu ni mwaka wa nne tunafika hapa na kuhudumia wananchi huku zaidi ya wananchi, 600 hadi 700 wanahudumiwa ikiwemo vipimo na matibabu” alisema Versi.
Aidha, Rais huyo alibainisha kuwa, mbali na kutoa matibabu bure pia wameweza kutoa dawa pamoja na neti za kuzuia mbu kwa kila mwananchi aalijitokeza kwenye kambi hiyo.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Masoko kutoka benki hiyo ya DTB, Bw. Sylvester Bahati amebainisha kuwa kujitokeza kudhamini kambi hiyo ni miongoni mwa taratibu za benki hiyo kuweza kusaidia jamii.
“Tunawapongeza Rotary Klabu kwa kuona umuhimu wa kusaidia kambi hii ya Kerege matibabu bure na ufadhili wetu hapa unaendana na sawa na taratibu tulizojiwekea za kutoa gawio kwa jamii kama zilivyotaratibu nyingine tulizonazo” alibainisha Bw. Bahati.
Aidha, ameeleza kuwa Benki hiyo ya DTB ina matawi zaidi ya 20 nchini huku ikitarajia kufungua matawi zaidi kwa nchi nzima ikiwemo Zanzibar.
Kwa upande wake daktari na mratibu wa magonjwa ya Kisukari, Dk. Bashiru Rajab ameeleza kuwa, wengi wa wa wagonjwa walipatikana katika kambi hiyo ni wale wa matatizo ya mapigo ya moyo (Blood pressure ).
“Katika kambi hii wengi wa wananchi wanaofika hapa wanakabiriwa na matatizo ya Presha na ugonjwa wa Maralia huku wa kisukari wakiwa wachache. Inatia faraja sana kwani wamepata kujua hali ya afya zao za mwili na tunawashahuri wawe na taratibu ya kupima afya mara kwa mara” alibainisha Dk. Bashiru.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi walipongeza waandaaji wa kambi hiyo ambapo imewasaidia kujua afya zao hivyo kuchukua hatua ikiwemo suala la kuzingatia kanuni za kufuata pamoja na ushahuri wa kitabibu.
Matibabu, sehemu mojawapo ya Miradi ya Afya ya Jamii, ambayo hufanyika kila mwaka toka ilipozinduliwa mwaka 2011 katika kitongoji cha Chanika jijini Dar es Salaam ambapo takribani wananchi 600 walijitokeza kupima malaria, VVU, Kisukari, magonjwa ya mfumo wa upumuaji, macho na viashiria vya magonjwa sugu na baadae kuamia katika mji huo wa Kerege kwa mwaka wa nne sasa huku wakitoa dawa na miwani bure.
Kwa mwaka huu imedhaminiwa na benki ya Diamond Trust Bank, Rotary Club of Seattle4 huku ikiandaliwa kwa kushirikiana na Shree Hindu Mandal Hospital, Vital Supplies, Kids Care Tanzania, Elite Dantal Clinic, Whitedent, Sayona, Ultimate Security na wengine wengi.
DSC_1655
Mkuu wa kitengo cha Masoko kutoka benki ya Diamond Trust Bank [DTB] akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa zoezi hilo la kambi ya matibabu bure. DTB ndio wadhamini wakuu katika kambi hiyo.
DSC_1629
DSC_1630
Daktari na mratibu wa magonjwa ya Kisukari, Dk. Bashiru Rajab akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo la kambi ya bure ya Matibabu katika mji wa Kerege,Bagamoyo Pwani.
DSC_1640
Mkazi wa Kerege akiwa katika mstari wa kwenda kumuona Daktari kwa ajili ya kupima afya zake sambamba na mtoto wake wakati wa kambi hiyo Novemba 15.2015.
DSC_1644
Zoezi la Kambi hiyo ya matibabu bure likiendelea katika mji huo wa Kerege..
DSC_1727
Mmoja wa wananchi wa Kerege (kulia) akimwelezea Daktari wa kambi hiyo..
DSC_1730
Upande wa huduma za macho...katika kambi hiyo
DSC_1759
Kitengo cha dawa wakiwa tayari kwa kutoa huduma hiyo wakati wa kambi hiyo..
DSC_1754
Wananchi wakipatiwa dawa bure wakati wa kambi hiyo..
Rotary Medical Camp-44
Huduma ya kinywa ikiendelea..
DSC_1714
Baadhi ya vifaa maalum kwa ajili ya matibabu ya kinywa ikiwemo meno kutoka Elite Dental Clinic wakati wa kambi hiyo..
DSC_1718
Baadhi ya madaktari wa magonjwa ya kinywa wakiwa tayari kwa ajili ya kutoa huduma kwa mmoja wa wakazi wa Kerege aliyefika katika kambi hiyo. Huduma ya Kinywa ilitolewa na Elite Dental Clinic.
DSC_1721
Huduma hizo za kinywa zikiendelea..
DSC_1712
DSC_1710
Picha za juu na chini ni eneo la upimaji wa magonjwa wa kinywa na meno iliyokuwa ikitolewa na Elite Dental Clinic
DSC_1700
Rotary Medical Camp-62
Mtaalamu wa tiba ya macho akiendelea na uchunguzi kwenye kambi hiyo
DSC_1742
Zoezi hilo la upimaji likiendelea katika vitengo mbalimbali wakati wa kambi ya upimaji na matibabu bure katika mhi wa Kerege.
Rotary Medical Camp-108
zoezi likiendelea kwa wananchi kupitia hatua moja hadi nyingine...
DSC_1d684
Baadhi ya wanachama wa Rotary Klabu ya Dar es Salaam Oyster Bay wakiwa katika kambi hiyo kutoa huduma..
DSC_1690
Rotary Medical Camp-7
DSC_1723
DSC_1664
Baadhi ya wananchi wa Kerege waliojitokeza wakiwa kwenye foleni katika Kambi hiyo huku wakipatiwa maelezo mbalimbali juu ya afya..
DSC_1666
Baadhi ya wananchi upande wa wanawake waliojotokeza kwenye kambi hiyo..
DSC_1673
Wananchi wakipata kusajiliwa kwa lengo la kuelekea kumuona Daktari na vipimo..
DSC_1681
Baadhi ya waanachi hao wakiwa kwenye moja ya foleni kuingia kwa madaktari na vipimo mbalimbali wakati wa zoezi hilo.
Rotary Medical Camp-2-3
Wananchi hao wakiwa katika kambi hiyo..
Rotary Medical Camp-15
Huduma na somo likiendelea wakati wa kambi hiyo..
Soma zaidi hapa:

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Diamond Trust (DTB), Viju Cherian (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Hoteli ya Serena Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu benki hiyo kuuza hisa zenye thamani ya sh. bilioni 30 na kusherehekea miaka 70 ya uwepo wake tangu ianzishwe hapa nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa benki hiyo, Joseph Mabusi.
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa benki hiyo, Joseph Mabusi (kulia), akizungumzia mafanikio mbalimbali  na shughuli zinazofanywa na benki hiyo.
 Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Uzalishaji na Masoko wa benki hiyo, Sylvester Bahati (kushoto), akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu masuala mbalimbali ya benki hiyo.
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua  taarifa hiyo.
Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo.
 ........................................................................................................................................

Benki ya Diamond Trust (DTB Tanzania) hivi karibuni imefanikiwa kuuza hisa stahili (Rights Issue) zenye thamani ya shilingi 30 billion kwa wanahisa wake kwa bei ya shilingi 5,200 kwa kila hisa. Hii ni mara ya tatu kwa DTB Tanzania kuuza hisa stahili ambapo mwaka 2007 iliuza hisa kama hizo zenye thamani ya shilingi bilioni 5.3 na mwaka 2012, shilingi bilioni 12.4
Uuzaji wa hisa unaimarisha mtaji wa benki na kuendelea kuwekeza kwenye matawi mapya, teknolojia na uanzishwaji wa huduma mpya.  DTB Tanzania imeendelea kukua ikianza na matawi manne (4) mnamo mwaka 2007 wakati wa hisa stahili za kwanza hadi matawi 24 hivi sasa.
Mwaka huu, DTB Tanzania imezindua akaunti maalum za akiba kwa ajili ya kuwasaidia watu wenye kipato tofauti kutimiza malengo yao. Akaunti hizi ni pamoja na Akaunti ya watoto (Smart Saver), akaunti ya akina mama (Amani), akaunti ya wazee (Faraja) na akaunti ya wanafunzi wa sekondari na vyuo (Kisomi Zaidi).
Pia uongezaji wa mtaji wa benki unakusudia kuendana na matakwa ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), juu ya kanuni za mitaji ya mabenki. DTB Tanzania ni benki ambayo siku zote imukuwa mstari wa mbele kutimiza matakwa ya sheria juu ya mitaji ya mabenki ikiwa ni pamoja na ongezeko la viwango vya mitaji (core /total capital ratios). Benki ya DTB Tanzania imekuza mtaji utakaoendena na mipango ya kibiashara kwa miaka ijayo.
DTB Tanzania ambayo inasherehekea miaka 70 ya uwepo wake Tanzania, imepata mafanikio ya kuridhisha kwa kipindi cha miezi tisa iliyoishia tarehe 30 Septemba 2015. Faida bila kodi imefikia shilingi 20.0 bilioni; ikiwa ni ukuaji wa asilimia 30.1 ikilinganishwa na shilingi 15.4 bilioni iliyopatikana katika kipindi kama hicho mwaka jana. DTB Tanzania ni miongoni mwa benki chache nchini Tanzania, zilizofanikiwa na ongezeko kabla ya faida ya zaidi ya asilimia 31 kwa miaka mitano sasa.
Amana za wateja imekua kwa asilimia 30 kutoka shilingi 504 bilioni Septemba 2014, hadi shilingi 720 bilioni mwishoni mwa Septemba 2015. Mali za Benki (Total Assets) zimefikia shilingi 858 bilioni ikilinganishwa na shilingi 632 bilioni mwezi Septemba 2014, ikiwa ni ukuaji wa asilimia 26. Mali za Benki (Total Assets) ziliongezeka kwa asilimia 24 mwaka 2012, asilimia 26 mwaka 2013 na asilimia 36 mwaka 2014. 
Amana zisizo na riba (Casa deposits) zilikuwa shilingi 372 bilioni, ongezeko la asilima 40.5 toka shilingi 265 bilioni mwezi Septemba 2014. Mikopo kwa wateja ilikuwa shilingi 512 bilioni ikilinganishwa na shilingi 391 bilioni kwa kipindi kama hicho mwaka 2014, ikiwa ni ongezeko la asilimia 23. 
Kwa sasa DTB Tanzania ina mtandao wa matawi 24 nchi nzima. Matawi 10 yakiwa Dar es Salaam (Tawi Kuu la Dar, Kariakoo, Magomeni, Masaki, Mbagala, Mbezi, Morocco, Nelson Mandela na Upanga iliyopo barabara ya Umoja wa Mataifa. DTB Tanzania pia ina matawi 14 kwenye miji mikubwa nchini, ikiwa ni matawi 2 jijini Arusha, matawi 2 Jijini  Mwanza na tawi moja moja katika miji ya Dodoma, Iringa, Kahama, Mbeya, Morogoro, Moshi, Mtwara, Tabora, Tanga na Zanzibar. 
DTBT ni kampuni tanzu ya Diamond Trust Bank Group yenye matawi  zaidi ya 115 katika nchi za Tanzania, Kenya, Uganda na Burundi. DTB ni mshirika wa Mfuko wa Maendeleo ya Uchumi wa Aga Khan (Aga Khan Fund for Economic Development -AKFED), ambayo ni sehemu ya Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (Aga Khan Development Network).
DSC_1839
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki akizungumza mbele ya wanahabari, madaktari na baadhi ya akina mama waliokuwa na watoto waliozaliwa kabla ya wakati maarufu kama Njiti (Hawapo pichani). Kushoto ni DoriS Mollel ambaye ni Mwanzilishi na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation (DMF) na wengine ni maafisa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[DAR ES SALAAM] Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepongeza juhudi binafsi zinazofanywa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation (DMF) katika harakati zake za kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) na mambo ya elimu hapa nchini huku ikiahidi kuendelea kushirikiana nayo kufikia malengp yake.
Kauli hiyo imetolewa mapema leo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki wakati wa kupokea vifaa maalum vya kusaidia watoto njiti vilivyotolewa na taasisi hiyo ya Doris Mollel Foundation tukio lililofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jengo la Watoto.
“Tunatambua mashine hizi ni bei kubwa na Serikali pekee yake haina pesa hivyo kwa kusaidiana na wadau kama hivi n faraja sana na tunapongeza juhudi hizi za taasisi ya DMF kwa kujitokeza kusaidia mashine kwa watoto njiti” ameeleza Mkuu wa Mkoa huyo.
Mkuu wa Mkoa huyo aliongeza kuwa, Mashirika mengine yaendelee kujitokeza kusaidia huduma za kijamii ikiwemo vifaa kama taasisi ya Doris Mollel kwani asilimia 100 ya wagonjwa na watu wengine wenye mahitaji katika tiba wanakimbilia Dar es Salaam hasa Hospitali ya Muhimbili.
“Tunaomba tena mukipata nyingine musisite kutiletea hapa maana Mkoa huu unapokea wagonjwa wengi kutoka maeneo mengi ya Tanzania na vifaa vya tiba mara nyingi vinakuwa ni vichache, Huko mikoani wanapewa rufaa waanakuja hapa pia hivyo DMF musisite kuja tena” alimalizia Mkuu wa Mkoa huyo.
Hata hivyo kwa upande wake Mwanzilishi na mtendaji Mkuu wa DMF, Doros Mollel amemweleza Mkuu wa Mkoa Meck Sadik kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega katika juhudi za kusaidia watoto njiti nchini ikiwemo kutoa elimu, vifaa na usaidizi kwa jamii dhidi ya kukabiliana na watoto njiti nchini.
Katika tukio hilo, Mkuu wa Mkoa alishudia vifaa hivyo na kupokea kutoka DMF sambamba na kutembelea wote ya watoto njiti pamoja na ile ya Kangaroo ambayo wamama wenye watoto njiti wanakuwa wanapatiwa uangalizi maalum dhidi ya watoto wao ikiwemo kupata joto la Mama na baadae alipanda mti maalum mbele ya jengo hilo la Watoto kama kumbukumbu na juhudi za wadau katika kusaidia jamii dhidi ya watoto njiti.
DMF imeweza kusaidia vifaa katika wodi hiyo ya watoto Muhimbili vikiwemo (Suction machines, Oxygen Concentrators na Feeding tubes). Aidha Doris Mollel amebainisha kuwa baada ya hapo wanatarajia kuelekea mikoa ya Kanda ya Ziwa kutoa vifaa kama hivyo huku lengo ikiwa ni kufika mikoa yote ya Tanzania.
DSC_1855
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Muhimbili wakishuhudia tukio hilo maalum la taasisi ya DMF ilipotoa vifaa hivyo katika kitengo cha Jengo la Watoto.
DSC_1865
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadik akipata maelezo juu ya vifaa hivyo vilivyotolewa na Taasisi ya DMF.
DSC_1870
Msimamizi wa wodi ya akina mama wanaopatiwa huduma ya Kangaroo dhidi ya watoto wao ambao walizaliwa njiti, akimpatia maelezo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alipotembelea wodi hiyo leo.
DSC_1924
Picha ya juu na chini Mkuu wa Mkoa wa Dar e Salaam akiwafariji baadi ya wakinamama waliojifungua watoto kabla ya wakati maarufu njiti wakati alipotembelea wodi hiyo ya watoto mapema leo.
DSC_1929
DSC_1939
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimpatia zawadi ambayo ni jozi ya soksi kwa ajili ya kusaidia watoto njiti kwa mmoja wa wamama waliokuwa katika wodi hiyo ya watoto njiti.
DSC_1873
Keki maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya siku maalum ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati maarufu njiti
DSC_1885
Mtoto Amne Salim (3) ambaye ni njiti akikata keki maalum kwa niaba ya watoto wenzake katika tukio hilo mapema leo.
DSC_1890
DSC_1891
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akimlisha keki mtoto Amne Salim katika tukio hilo.
DSC_1897
Mtoto Amne Salim akimlisha keki Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadik katika tukio hilo.
DSC_1954
Baadhi ya akina mama waliokwenye mpango maalum wa kutunza watoto wao waliozaliwa njiti ujulikanao kama Kangaroo wakiwa wodini mapema leo wakati wa ugeni wa DMF na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam walipotembelea wodi hiyo.
DSC_1882
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaamm Meck Sadik akipokea na kukabidhi vifaa maalum kwa ajili ya kusaidia watoto njiti katika Hospitali ya Taifa Muhimbili vilivyotolewa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation mapema leo.
DSC_1907
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Meck Sadik akipanda mti maalum baada ya zoezi hilo la Taasisi ya Doris Mollel Foundation kutoa misaada ya vifaa vya watoto njiti.
DSC_1912
DSC_1921
DSC_1918
Shughuli hiyo ya upandaji mti wa kumbukumbu ikiendelea..
DSC_1900
Mama mzazi wa Doris Mollel akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

No comments :

Post a Comment