Friday, September 4, 2015

RAIS KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA MFUMO WA TAKWIMU HURIA BARANI AFRIKA, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na washiriki (hawapo pichani) wa Mkutano wa Kimataifa wa Mfumo wa Takwimu Huria Barani Afrika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake Rais Kikwete alisema jukumu la utoaji wa taarifa kwa umma si kwa serikali pekee bali hata kwa Sekta binafsi pamoja na taasisi zingine zisizokuwa za serikali zinatakiwa kufuata mfumo huo ili kuleta maendeleo katika nchi husika. Mkutano huo ambao unaudhuriwa na mamia ya washiriki unalengo la kutoa elimu pamoja na kuhamasisha umma kuhusu utoaji wa taarifa kwa uwazi katika sehemu mbalimbali barani Afrika. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

TBS KUFANYA MSAKO MKALI NCHI NZIMA KUWABAINI WAUZAJI WA UMEME NURU 'SOLAR POWER PANELS' ZILIZO CHINI YA KIWANGO

 Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Nishati Jadidifu (TAREA), Mhandisi Mathew Matimbwi (katikati), akiwaonesha wanahabari Dar es Salaam leo asubuhi Umeme Nuru (Solar Power panels) ambazo hazina ubora zilizokamatwa zikiwa katika soko la Tanzania baada ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikiana na Taasisi hiyo, kufanya uchunguzi na kubaini kuwepo katika soko solar hizo. Kulia ni Ofisa Viwango wa TBS, Henry Massawe na Ofisa Uhusiano, Roida Andusamile.
 Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Nishati Jadidifu (TAREA), Mhandisi Mathew, akiwaonesha wanahabari Solar Power panels zinazotakiwa kuwa kwenye soko ambazo ni bora.
Ofisa Uhusiano wa TBS, Roida Andusamile (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Ubungo Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu shirika hilo kuanza msako mkali wa kuwabaini wafanyabiashara wanaouza Umeme Nuru (Solar Power Panels), zilizochini ya kiwango. Kulia ni Ofisa Viwango wa TBS, Henry Massawe na Ofisa Udhibiti Ubora wa TBS, Ashura Katunzi.

MAKAMU WA RAIS DKT. AFUNGUA KONGAMANO LA AFRIKA KUHUSU MAKUBALIANO YA RASIMU MPYA YA DUNIA, JIJINI DAR ES SALAAM.

3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Kongamano la Afrika kuhusu Makubaliano ya Rasimu mpya ya Dunia inayohusu Usimamizi wa Masuala ya Tabianchi. Kongamano hilo lilianza jana Sept 3, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar esSalaam. Picha na OMR
unnamedunnamedb

BALOZI WA KUWAIT NCHINI AMTEMBELEA WAZIRI CHIKAWE OFISINI KWAKE, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

AVIC LASEMA LIPO TAYARI KUSHIRIKIANA NA SHIRIKA LA NDEGE ZANZIBAR
Picha na – OMPR – ZNZ.

Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya usafiri na matengenezo ya Ndege la avic kutoka Jamuhuri ya Watu wa China limejitolea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuanzisha mradi wa Kiuchumi wa pamoja wa Shirika la Ndege la Zanzibar.

Naibu Mkurugenzi wa Shirika hilo lenye Makao Makuu yake Mjini Beijing China Bwana Duan Bao Rong alieleza hayo wakati alipokuwa akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Ofisini kwa Balozi Seif Vuga Mjini Zanzibar.

Bwana Duan Bao Rong alisema Uongozi wa Shirika hilo hivi sasa uko katika hatua za awali za kuwasiliana na Viongozi Waandamizi wa Taasisi zinazohusika na Sekta ya Mawasiliano na Uwekezaji kwa nia ya kuandaa taratibu zinatakazofanikisha kuanzishwa kwa Shirika hilo katika mfumo wa Ubia na Serikali.

Alisema Wataalamu wa Shirika hilo kwa kushirikiana na wale wa Zanzibar wataendelea kufanya utafiti wa pamoja katika kuona namna gani mradi huo mkubwa unatekelezwa ili kusaidia kuongeza mapato ya Taifa ambapo pia alieleza kuwa Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China itakuwa tayari kuunga mkono uanzishwaji wa mradi huo.

PAPA FRANCIS AKUSANYA WATU BAADA YA KUTOKA KWENDA KUNUNUA MIWANI

SECRETARY GENERAL ON A WORKING VISIT TO ROOFINGS GROUP UGANDA

The Secretary General of the East African Community, Amb. Dr Richard Sezibera, on Thursday paid a working visit to Roofings Group Uganda at its 2nd plant located in Namanve, Uganda's upcoming Industrial Area on the outskirts of the capital, Kampala.
The Secretary General was accompanied by Hon. Dr. James Shinyabulo Mutende, Uganda's Minister of State for Industry; Mr. Dennis Karera, the Chair of the East African Business Council (EABC) and the Ag. CEO, Ms. Lilian Awinja; Mr. Hussein Omar, the EABC Uganda Chapter Chair; Dr. Samuel M. Nyantahe, Chairman of Confederation of Tanzania Industries; Amb. Jean Rigi, Burundi's Permanent Secretary for EAC Affairs, and; Commissioner Rona Sserwada from Uganda's Ministry of EAC Affairs.

Welcoming the Secretary General to the Plant, the Chairman and Managing Director of the Roofings Group, Mr. Sikander Lalani, said it was gratifying that Amb. Sezibera's visit to the plant came immediately after the 1st East African Manufacturing Business Summit held from 1st to 2nd September, 2015 in the Ugandan capital.

TIMU YA TAIFA YA WANAWAKE YAONDOKA KUELEKEA CONGO BRAZAVILLE KATIKA MASHINDANO YA ALL AFRICAN GAMES

x4
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Leonard Thadeo (kushoto) akimkabidhi mmoja wa wanariadha Bendera ya Taifa tayari kwa safari yakuelekea nchini Congo Brazaville kwenye mashindano ya Afrika (All African Games), Timu hiyo iliondoka jana jioni na ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania.   (Pichana Benjamin Sawe- WHVUM)
1x
Afisa Michezo Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Gordon Nsajigwa akimpatia mmoja wa wachezaji wa Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake tiketi jana jioni tayari kwa safari yakuelekea Congo Brazaville kwenye mashindano ya Afrika (All African Games), kushoto aliyevaa sutini Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Leonard Thadeo.
x2
Wachezaji wa Timu ya Taifa wakipanda ndege ya Shirikia la Ndege la Tanzania (Air Tanzania) jana jioni tayari kwa kuanza safari ya kuelekea nchini Congo Brazaville kwaajili ya Mashindano ya Afrika (All African Games).
A BAADA YA KUMTUMIA MENEJA UHUSIANO PICHA ZA UTUPU
Mwanaume mmoja huko Chicago Marekani amepoteza nafasi ya kupata ajira baada ya kumtumia kimakosa picha za utupu meneja uhusiano wa kampuni aliyoomba ajira.

Polisi wamesema mwanaume huyo ambaye jina lake limehifadhiwa alituma picha za utupu kati ya Agosti 11 na 13 kwa meneja uhusiano huyo mwanamke na baadae kumpigia simu.

Meneja huyo mwanamke wa kampuni mojawapo ya St Charles alipokea picha hizo zilizotumwa kama ujumbe wa simu mara mbili akiwa nyumbani na kuwasiliana na polisi.

Msemaji wa polisi amesema mwanaume huyo alikiri kutuma jumbe hizo lakini amesema picha hizo alikuwa amelenga kumtumia mtu mwingine.

KT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA WAJUMBE WA JUMUIYA YA WAZAZI YA CCM
1
Mgombea wa Urais kupitia Tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akiingia kwenye Ukumbi wa Karemjee kuzungumza na Wajumbe wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi CCM.
2
Mgombea wa Urais kupitia Tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wajumbe hao. Dkt. Magufuli amewaomba wajumbe hao kufanya kazi kwa uadilifu na kuihubiri Amani ya nchi yetu ili maendeleo bora yaweze kupatikana.
5
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Abdalah Majura akizungumza katika mkutano huo.
3
Wajumbe wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi Taifa wakimshangilia Mgombea wa CCM-Dkt. John Magufuli.

MUIGIZAJI FILAMU EMMA THOMPSON ADAI KUWA UK WABAGUZI

Muigizaji filamu Emma Thompson amedai kuwa Uingereza haichukui kiasi kikubwa cha wakimbizi kutoka mataifa ya Ulaya kutokana na umma wake kuwa ni wabaguzi.

Mshindi huyo wa tuzo ya Oscar, amesema namna Uingereza inavyoshughulikia mgogoro wa wahamiaji ni aibu, na kusema kuna nafasi ya kutosha kuhifadhi maelfu ya wakimbizi.

Hatua hiyo ya muigizaji huyo nyota imekuja huku kukiwa na shinikizo kwa serikali ya Uingereza kutoa hifadhi kwa familia zaidi za wakimbizi wa Syria wanaokimbilia mataifa ya Ulaya.

No comments :

Post a Comment