Friday, August 7, 2015

OFISI YA WAZIRI MKUU YAENDELEA NA URATIBU WA SHUGHULI ZA SERIKALI NDANI YA MAONESHO YA NANE NANE – LINDI

xxx1
Mratibu  wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Edgar Senga akieleza uratibu wa shughuli za maafa kwa  wananchi waliotembelea Banda hilo katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi, Tarehe 7 Agosti , 2015.
xxx3
Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Wavulana ya Ndada wakipata maelezo juu ya sera baina ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi kutoka kwa Mchumi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Maendeleo ya Sekta Binafsi, Uwekezaji na Uwezeshaji , Vedastus Manumbu walipotembelea Banda hilo katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi, Tarehe 7 Agosti , 2015

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, SEIF SHARIF HAMAD, ashiriki Uvunaji wa Matikiti

Makamu wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akizindua uvunaji wa
matikiti maji kwa wakulima wa shehia ya Donge Muwanda.
 
Makamu wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akizindua uvunaji wa
matikiti maji kwa wakulima wa shehia ya Donge Muwanda.
       
Mkulima wa
matikiti maji na pilipili boga Bw. Salum Khamis Kiregu akitoa maelezo mbele ya
Makamu wa Kwanza wa Rais kuhusiana na changamoto zinazowakabili katika kilimo
hicho.
 
Makamu wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiwa pamoja na badhi ya
wakulima wa Donge Mchangani na Muwanda, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini “A”
(kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Affan Othman Maalim (wa pili
kushoto). Picha na OMKR.
 
                                 
Na:Hassan Hamad (OMKR)
…………………………
Makamu wa Kwanza wa
Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amesifu juhudi zinazochukuliwa
na wananchi wa Donge katika kuendeleza kilimo cha matunda na mboga mboga.
Amesema iwapo kilimo
hicho kitawekeza mikakati imara, kinaweza kuwa mkombozi wa kweli kwa wakulima
na kuweza kuweza kuongeza kipato chao.
Maalim Seif ameeleza
hayo wakati akizindua uvunaji wa matikiti maji na pilipili boga katika shehia
za Donge mchangani na Muwanda katika Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja.
Amesema katika siku
za hivi karibuni, kilimo hicho kimepata mafanikio makubwa na kupunguza
uagiziaji wa bidhaa hizo nje ya Zanzibar kutoka asilimia 80 hadi asilimia 20.
Amefahamisha kuwa
lengo la Serikali ni kuimarisha zaidi kilimo cha matunda na mboga mboga ili
kuweza kukidhi soko la ndani na kuacha kuagizia bidhaa hizo kutoka nje ya
Zanzibar.
Amesema
kinachohitajika hivi sasa ni kwa Serikali kuongeza mashirikiano na wakulima,
ili kusaidia kuwatatulia kero zinazowakabili ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa
maji pamoja na pembejeo.
Makamu huyo wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar ameiagiza Wizara ya Kilimo kupeleka mabwana na mabibi
shamba wa kutosha katika shehia hizo za Mchangani na Muwanda, ili kusaidia
utaalamu kwa wakulima hao na kuweza kuzalisha zaidi.
Nae Katibu Mkuu
Wizara ya Kilimo na Maliasili Zanzibar Bw. Affan Othman Maalim, amesema tayari
Serikali imeanza kufanya utafiti kujua maeneo ya kuchimba visima ili kuwasaidia
wakulima hao kuondokana na tatizo la upungufu wa maji.
Hata hivyo
amewashauri wakulima hao kujikusanya pamoja ili kurahisisha miundombinu ya maji
kuweza kuwafikia walengwa.
Kuhusu tatizo la
pembejeo, Bw. Affan amesema Wizara ya Kilimo inaandaa utaratibu wa kulipeleka
suala hilo katika ngazi za juu, ili kuwawezesha wakulima wa matunda na mboga
mboga kuweza kupatiwa ruzuku za pembejeo za kilimo kama wanavyopatiwa wakulima
wa mpunga.
Mapema mmoja kati ya
wakulima hao Bw. Salum Khamis Kiregu, amemueleza Makamu wa Kwanza wa Rais kuwa
licha ya mafanikio wanayoyapata, bado wanakabiliwa na tatizo la soko la kuuzia
bidhaa hizo, na kuiomba serikali kuandaa mazingira bora ya soko kwa wakulima
hao.
Amesema hivi sasa wanalazimika kuuza bidhaa zao kwa bei ya chini kupitia kwa wafanyabiashara,
jambo ambalo limekuwa likipunguza kipato chao licha ya kuzalisha bidhaa hizo
kwa wingi.
Bw. Kiregu ameeleza matatizo mengine yanayowakabili kuwa ni pamoja wadudu
waharibifu na maradhi ya mimea, na kuwaomba wataalamu wa kilimo kuwa karibu na
wakulima ili kusaidia kukabiliana na changamoto hizo.

TGDC yaendelea na Kampeni ya kuelimisha Umma kuhusu Jotoardhi mkoani Mbeya.

xx2
Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (aliyesimama) akielimisha Umma wa Kata ya Swaya wakati walipotembelea eneo la kata hiyo ikiwa ni sehemu ya Kampeni ya uelimishaji kuhusu manufaa ya Jotoardhi hivi karibuni mkoani Mbeya. Kushoto ni Mkurugenzi wa masuala ya Ufundi wa TGDC, Bwana Karamaeli Mnjokava.
xx4
Mkurugenzi wa masuala ya Ufundi wa TGDC, Bwana Karamaeli Mnjokava.(aliyesimama mbele) akichangia mada kuhusu jotoardhi na manufaa yake kwa wakazi wa Kata ya Swaya hivi karibuni mkoani Mbeya.
xx5 xx7
Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Swaya pamoja na baadhi ya Watendaji wa Kampuni ya Uendelezaji Nishati ya Jotoardhi (TGDC) wakifuatilia uwasilishwaji wa mada toka kwa Meneja Mkuu wa TGDC hivi karibuni mkoani Mbeya.
………………………………………………………………………………….
Habari Picha na Benedict Liwenga, Maelezo-Mbeya.
 
Mkoa wa Mbeya unasemekana kuwa ni moja ya maeneo yaliyobarikiwa kuwa miongoni mwa maeneo ambayo Shirika la Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC) linatarajia kuanza shughuli ya uchimbaji jotoardhi kutokana na tafiti za awali kuhusu nishati hiyo kuanza katika mkoa huo.
Kauli hiyo imetolewa na Meneja Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe wakati wa Kampeni ya Uelimishaji kuhusu Jotoardhi kwa viongozi katika ngazi za Kata za Ilomba katika Vijiji vya Ituha, Tonya pamoja na Kata nyingine ya Nanyala iliyoko Mbozi Mkoani Mbeya.
Mhandisi Njombe amesema kuwa, TGDC ina malengo ya kuzalisha zaidi ya megawati 200 kwa mkoa huo licha ya mkoa huo kwa sasa kutumia megawati 40 jambo ambalo linaweza kupelekea nishati hiyo itakayozalishwa kupeleka katika mikoa mingine ya jirani kwani kiasi hiko cha umeme kitakuwa ni kikubwa.
Aidha, amewataka wakazi wa Mbeya kuonyesha ushirikiano kati ya Serikali yao pamojana TGDC ili zoezi hilo lenye manufaa kwao liweze kufikiwa kwa maendeleo ya mkoa na vijijini ambako kuna changamoto ya ukosefu wa nishati ya umeme pia kutatua tatizo la mgao wa umeme katika mkoa huo.
“Tuunge mkono jitihada hizi za Serikali ili walau nishati hii izidi kuendelezwa na ituokoe dhidi ya hali ya umeme isiyokuwa na uhakika kwani tukishakuwa na uelewa na kuelimisha wananchi na kutoa ushirikiano, tutakaa mkao wa kula kutokana na nishati hii”, alisema Njombe.
Kwa upande wake Mjiolojia Mwandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Bwana Jacob Mayalla ameeleza kuwa kutokana na juhudi za Serikali, tafiti za jotoardhi nchini zilizanza miaka ya 1976 hadi mwaka 1978 zikiwa kama tafiti za awali ambazo ziliweza kubainisha maeneo katika nchi ya Tanzania kwenye maeneo yaliyopitiwa na Bonde la Ufa ambapo viashiria vya jotoardhi vipo.
“Kwa Mkoa wa Mbeya, tafiti za jotoardhi zilifanywa na Serikali kwa kushirikiana na Wakala wa Jiolojia Tanzania”, alisema Mayalla.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa masuala ya Kiufundi toka  Kampuni ya TGDC, Bwana Taramaeli Mnjokava ameyataja baadhi ya matumizi ya moja kwa moja ya jotoardhi nchini ikiwemo matumizi ya kiutalii ambapo maji ya jotoardhi huwekwa kwenye mabwawa hivyo huvutia watalii wa ndani na nje ya nchi kwa kuyaoga na kuyaangalia jambo ambalo linaongeza pato la taifa.
Aliongeza kuwa, maji ya jotoardhi hufaa kwa matumizi ya uzalishaji wa samaki kwani samaki hupenda maji yenye hali ya uvuguvugu kuliko yenye baridi hasa kwa maeneo yenye baridi kama mkoa wa Mbeya, hivyo pindi mabwawa ya samaki yanapotengenezwa na kuwekewa maji ya jotoardhi yanasaidia kuzalisha samaki kwa wingi jambo ambalo nalo litakuza pato kwa taifa na kwa eneo husika ambalo uzalishaji unafanyika.
“Maji ya jotoardhi yanaweza kutumika katika uzalishaji wa mboga mboga au maua kwa njia ya Vitalu Nyumba kwa Kiingereza huitwa Green Houses lakini ni vitalu hutengenzwa kwa plastiki au kioo, hivyo watu hutumia vitalu hivi jambo ambalo linavutia sana soko la nje kwani huwa hawapendi mboga zilizopigwa dawa wala maua yaliyopigwa dawa, niwahamasishe kujiandaa kwa kuupokea mradi huu kwani utawanufaisha vyakutosha nyie wakazi wa Mbeya na taifa kwa ujumla,” alisema Mnjokava.
Mnamo tarehe 19 Disemba, 2013 Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) ilisajiri kampuni ya kuendeleza nishati itokanayo na Jotoardhi, jina la kampuni likiitwa “Tanzania Geothermal Development Company Limited (TGDC).
Kampuni hii ilianzishwa kama kampuni tanzu ya Shirika la TANESCO ambalo linamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100 na mnamo mwezi Julai 2014 TGDC ilianza kazi zake rasmi ikipewa jukumu la kuharakisha uendelezaji wa nishati ya jotoardhi nchini.

MTANGAZAJI WA RADIO FREE AFRICA APITA KURA ZA MAONI UDIWANI SASA KUSUBIRI KURA ZA UBUNGE.

1525677_749904191774263_4961655255847640040_nWilliam Bundala (KIJUKUU CHA BIBI K)
……………………………………………………………..
SHINYANGA
Mwandishi wa habari na mtangaaji wa Radio Free Africa William Bundala (KIJUKUU CHA BIBI K) ameshinda kura za maoni katika nafasi ya Udiwani katika kata ya Ulowa jimbo la Ushetu.
 
Akitangaza matokeo hayo Msimamizi wa uchaguzi huo Sangoma amesema kuwa Bundala ameshinda nafasi hiyo kwa kupata kura 46 dhidi ya Wagombea wenzake Charles Bahati aliyepata kura 14 na Marco Matheo ambaye hakupata kura yoyote katika kinyang’anyiro hicho.
 
Kuelekea uchaguzi mkuu Bundala alitangaza nia ya Kugombea Ubunge katika jimbo la Ushetu na udiwani katika kata ya Ulowa huku akisimamia kauli mbiu yake kuwa “Tunahitaji mawazo na nguvu mpya za vijana kuleta mabadiriko ya maendeleo”.
 
Akiongea kwa njia ya simu akiwa jimboni Bundala amesema kuwa huu ni mwanzo na kuongeza kuwa kwa sasa anasubiri kura za maoni za ubunge ili kuchaguliwa kupeperusha bendera ya Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
 
Sambamba na hayo Bundala amesema kuwa Tanzania ilipofikia kwa sasa inahitaji viongozi wazalendo wenye uchungu na rasilimali za wananchi na siyo kiongozi mwenye uchu wa madaraka anayetaka uongozi kwa rushwa.
 
Kwa upande wao wagombea waliokuwa katika kinyang’anyiro hicho cha udiwani wamesema kuwa wameridhika na matokeo na kwamba lengo la CHADEMA ni moja kuleta mabadiriko katika jimbo la Ushetu na kata ya ulowa kwa Ujumla.
 
Kwa sasa Bundala anasubiri kura za maoni za Ubunge zinazotarajiwa kufanyika wiki ijayo huku akiwa katika kinyang’anyiro hicho na watia nia wengine wawili ambao ni Mabula Nkwabi na John Kitibu ambaye alipata kura 45 katika kura za maoni za jimbo la Kahama Mjini katika uchaguzi ambao James Lembeli aliibuka mshindi.

ADC YAFANYA MKUTANO WA HADHARA KUWATAMBULISHA WAGOMBEA WA URAIS KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

 Mgombea urais wa Tanzania  kupitia Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC),  Lutasola Yemba (katikati), akimtambulisha kwa wananchi mgombea mwenza Said Miraj (kulia) na mgombea urais wa chama hicho, Zanzibar, Hamad Rashid Hamad  kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Buguruni Sheli Dar es Salaam jana. 
 Mgombea urais wa Tanzania  kupitia Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC),  Lutasola Yemba (katikati), akimtambulisha kwa wananchi mgombea mwenza Said Miraj (kushoto), baada ya kuchukua fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Dar es Salaam leo. Kulia ni mke wake, Mwanaisha Lutasola.
 Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama hicho, Hamad Rashid Hamad akizungumza na wananchi katika mkutano huo.
  Mgombea urais wa Tanzania  kupitia Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC),  Lutasola Yemba, akihutubia katika mkutano huo Buguruni Sheli jana.
Wanachama wa chama hicho na wananchi wakisikiliza sera za viongozi hao watakao peperusha bendera ya ADC kwenye uchaguzi mkuu. 

Rais Kikwete azindua benki ya kwanza ya Wakulima Tanzania-Agosti 7, 2015

  03
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wadau wa kilimo na taasisi za fedha wakati akizindua rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam.
01
 Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo, Thomas Samkyi akizungumza wakati wa uzinduzi wa benki ya wakulima Tanzania (TADB), uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu JK Nyerere.
05
Mwenyekiti wa Bodi ya benki ya Maendeleo ya Kilimo, Bi Rosebud Kurwijila, akizungumza wakati wa uzinduzi wa benki.
04 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akifuatilia uzinduzi wa benki ya Maendeleo ya Kilimo, kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya benki hiyo Bi Rosebud Kurwijila, akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa benki, bwana Thomas Samkyi, na kutoka kushoto ni Waziri wa Kilimo, Stephen Wasira akifuatiwa na Waziri wa Fedha, Bi Saada Mkuya.
06
 Wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi wa benki ya Maendeleo ya Kilimo
02
Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akizindua rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam.
………………………………………………………………………………………
Na Mwandishi wetu-Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete leo amezindua benki ya kwanza ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, ambayo inalenga kuanzisha mtizamo mpya wa kukiendeleza kilimo kupitia kushirikisha wadau mbali mbali, kuangalia kila mnyororo wa thamani kwa ukamilifu wake, pamoja na kuwa na ubunifu katika kuchangia kifedha kwenye miradi ya muda mrefu, ya kati na muda mfupi kwenye sekta ya kilimo. Benki hiyo inatarajiwa kutoa mchango mkubwa katika ukuzaji wa sekta ya kilimo ambayo imeajiri zaidi ya aslimia 70 ya Watanzania.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Rais Kikwete amesema changamoto zinazowakabili wakulima nchini ndizo zilizosababisha serikali yake kuanzisha benki hii ili kuwakomboa wakulima kwenye umaskini ili waweze kuzalisha kibiashara na sio kwa kwa kujikimu.
‘Awali huduma za kifedha na mikopo kwa wakulima hazikuwepo kabisa na hivyo kupelekea tija kwenye kilimo kuwa chini, uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo nao ukawa chini ya viwango vya Afrika na hata dunia, hivyo ya uzinduzi wa benki hii unafungua ukurasa mpya wa mapinduzi ya kilimo nchini’ alisema Rais Kikwete.
Rais Kikwete pia aliwaasa wakulima kutumia vyema fursa ya uanzishwaji wa benki hii akisema kwa sasa kilimo kinachangia asilimia 25 ya pato la taifa, huku asilimia 35 ya bidhaa tunazouza nje ni za kilimo.
‘Serikali imetoa mtaji wa kuanzisha benki wa jumla ya shilingi bilioni 60, na tunatarajia kuingia hati fungani ili kuiongezea benki mtaji kwa jumla ya shilingi bilioni 800’ anasisitiza Waziri wa Fedha, Saada Mkuya.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa benki, Bwana Thomas Samkyi, alisema dhumuni kuu la uanzishaji wa benki hiyo ni kuboresha tija katika uzalishaji kwenye sekta ya kilimo kwa kuunganisha nguvu za wadau mbalimbali ili kuwezesha uendelezaji wa miundombinu ya kilimo kama miradi ya umwagiliaji, usafirishaji, uhifadhi, mindombinu ya masoko, n.k. ambayo inachangia maendeleo ya sekta ya kilimo.
‘Uanzishwaji wa benki hii unalenga kuziba mianya mikubwa ya ukopeshaji kwenye kilimo ambayo inaachwa na benki za biashara, ili kuchochea kukua kwa sekta ya kilimo, kwa kutoa mikopo na huduma nyingizezo za uwezeshaji wa kilimo kwa wakulima, ambao wengi wao hawana uwezo wa kupata huduma za kibenki’ alisema Bw. Samkyi.
Akieleza zaidi kuhusu uanzishwaji wa benki hiyo, Bwana Samkyi alisema Benki ya Wakulima itakuwa msitari wa mbele katika kusukuma shughuli za kilimo pamoja na kuchagiza benki na taasisi nyingine za kifedha kushiriki katika kuwezesha shughuli za kilimo.
‘Benki hii imeundwa ili kutoa mikopo kwa masharti nafuu, pamoja na kutoa huduma nyinginezo zitakazoongeza uwezo wa wakulima kukopa na kuzalisha. Ili kufanikisha haya, benki inabidi iwe na vyanzo endelevu vya fedha za kutosha kwani nchi hii ni kubwa na wadau wa benki ni wengi sana. Lengo kuu ni kubadili kilimo cha Tanzania kutoka kilimo cha kujikimu kwenda kilimo cha kibiashara’ alisema Bw. Samkyi.
Benki hii pia inatarajiwa kuwa ni kiungo muhimu cha utekelezaji wa mageuzi ya awamu ya pili ya sekta ya kifedha, na vile vile kuboresha maendeleo ya kilimo nchini ikizingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025 pamoja na mipango mbalimbali ya maendeleo ya miaka mitano mitano, Mkakati wa Maendeleo wa Sekta ya Kilimo, na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUKUTA), pamoja na sera mbali mbali za Serikali zinazohusu sekta ya kilimo.

KAMATI MAALUM YA HALMASHAURI KUU YA CCM NEC ZANZIBAR

x1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) mara walipoingia katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo katika kikao cha kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM NEC ya Zanzibar,(kulia) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi(kushoto)
Picha zote na Ikulu.
x2
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai alipokuwa akitoa taarifa ya kikao kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM NEC ya Zanzibar kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein  katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo kbla ya kukifungua kikao hicho,
x3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akikifungua  kikao cha kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM NEC ya Zanzibar leo katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja,(kulia) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi(kushoto)
x4
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM NEC ya Zanzibar wakifuatuilia kwa makini ratiba ya kikao hicho kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja,
x5
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM NEC ya Zanzibar wakifuatuilia kwa makini ratiba ya kikao hicho kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja,

Naibu waziri wa Viwanda na Biashara Janet Mbene atembeleakiwanda cha kutengeneza vigae mkoani mbeya

unnamed (40)
Naibu waziri wa Viwanda na Biashara Janet Mbene akizungumza, mmoja wa viongozi wa kampuni ya Marmo and Garnito Mines wakati alipokuwa kwenye ziara ya viwanda mkoani mbeya hivi karibuni.
unnamed (41) unnamed (42)
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara,Janet Mbene,akiangalia  baadhi ya bidhaa zilizotengenezwa na kampuni ya Marmo and Garnito Mines kwa ajili ya matumizi mbalimbali
unnamed (43)
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara , Janet Mbene, akitembelea sehemu ya kiwanda cha Marmo anda Granito Mines
 

TOTO AFRICAN KUCHAGUANA OKTOBA 2015

download (11)
Klabu ya Toto African ya Mwanza inatarajiwa kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi zilizo wazi katika kamati yake ya utendaji ifikapo tarehe 11 Oktoba 2015. Katika barua yake kwa Katibu Mkuu wa Toto African, Katibu Mkuu wa TFF ameuagiza uongozi wa Toto African kuwasiliana na Kamati yao ya Uchaguzi ili tangazo la uchaguzi litolewe si chini ya siku sitini (60) kabla ya tarehe ya kufanyika uchaguzi.
Kwa muda mrefu kumekuwa na mvutano katika klabu ya Toto na suala kubwa likiwa ni kuhusu ujazaji wa nafasi zilizo wazi. Awali TFF ilipokea maombi ya wanachama na wadau wa Toto African wakitaka ufanyike uchaguzi ili kumaliza mvutano ndani ya klabu.
TFF ilishauri uchaguzi huo kusubiri klabu kukamilisha mchakato wa usajili.
Vilevile TFF imewataka wadau wote wa klabu hiyo kongwe ya mjini Mwanza kuheshimu uongozi uliopo madarakani kwani ndio unaotambulika na ndio utaendelea kuiongoza Toto African katika kipindi cha kuelekea uchaguzi uchaguzi.

TWIGA STARS YAELEKEA ZANZIBAR

unnamed (38)
Timu ya Twiga Stars ikiondoka kwenda Zanzibar kwa ajili ya kambi ya mazoezi
unnamed (39)
Wachezaji wa Tiga Stars wakiwa Feri wakisubiri boti ya kwenda Zanzibar kwa ajili ya kupiga kambi ya mazoezi.
……………………………………………………………………
Kikosi cha timu ya Timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) kimeodoka leo saa 6 mchana jijini Dar es salaam kuelekea kisiwani Zanzibari, ambapo kitaweka kambi ya mwezi mmoja kujiandaa na fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) mwezi Septemba.
Msafara wa Twiga Stars umeondoka na boti ya Azam (Kilimanjaro) ukiwa na watu 32, wakiwemo wachezaji 25, benchi la ufundi 6 pamoja na kiongozi wa msafara, ambapo TFF imegharamia kambi hiyo ya mwezi mmoja
Wachezaji waliosafiri leo ni Fatuma Omari, Belina Julius, Happiness Hezron, Fatuma Hassan, Anastazia Anthony, Fatuma Bashiru, Fatuma Issa, Fatuma Khatibu, Maimuna Hamis, Donizia Daniel, Sofia Mwasikili, Etoe Mlenzi.
Wenigine ni Amina Ally, Thereza Yonna, Mwanahamisi Omari, Stumai Abdallah, Shelder Boniface, Asha Rashid, Najiat Abbas, Estha Chabruma, Mwajuma Abdallah na Fatuma Mustapah.
Twiga Stars itakua kambini kisiwani Zanzibar kwa kipindi cha mwezi mmoja, kujiandaa na fainali hizo za michezo ya afrika, ambapo imepangwa kundi A pamoja na wenyeji Congo – Brazzavile, Ivory Coast na Nigeria.
Fainali za Michezo ya Afrika  (All Africa Games) zinatarajiwa kuanza kutivua vumbi Septemba 4 – 19 nchini Congo-Brazzavile.

MABONDIA RAMA SHAURI NA LULU KAYAGE WAPAA KWENDA AFRIKA KUSINI

Rais wa TPBO Yassin Abdallah ‘Ustaadhi’ katikati akiwa na mabondia Lulu Kayage kulia na Ramadhani Shauri wakienda kupanda ndege kwenda Afrika ya Kusini mabondia hawo wanapanda uringoni agost 9 Picha naSUPER D BOXING NEWS
Rais wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yassin Abdallah Othadhi katikati akiwa uwanja wa ndege wa kimataifa na mabondia Ramadhan Shauri kushoto na Lulu Kayage kabla hawajapaa kwenda Afrika ya Kusini kwa ajili ya mchezo wao utakaopigwa Agosti 9

EUROPEAN UNION STATEMENT

images (1)
Declaration by the High Representative, Federica Mogherini, on behalf of the European Union on the occasion of the International Day of the World’s Indigenous Peoples, 9 August 2015.
…………………………………………………………………..
While we celebrate today the International Day of the World’s Indigenous Peoples, we take stock of the progress achieved towards ending all forms of discrimination and in ensuring that indigenous peoples’ rights are respected, protected and fulfilled. In September of last year, the EU contributed to the success of the World Conference on Indigenous Peoples and promoted equal participation of indigenous peoples in preparation of this meeting. We supported the Outcome Document of the conference which serves as a blueprint for actions at international and national level, bringing positive changes to the lives of indigenous peoples. As follow up to the World Conference, the EU is further developing its policy in line with the United Nations Declaration on the Rights of Indigenous Peoples and in close consultation with their representatives. Despite the many positive examples of progress achieved around the world, indigenous peoples, particularly women and girls, continue to experience multiple forms of discrimination, vulnerability and marginalisation in their lives. We are therefore committed to their empowerment. By reaffirming its support to the UN declaration on the Rights of Indigenous Peoples, the EU restates its determination to work closely with indigenous peoples, along with other partners and stakeholders in its endeavour to promote the recognition that human rights are equally guaranteed to all men and women.

RAIS KIKWETE AZINDUA RASMI BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO TANZANIA (TADB)

unnamed (30)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wadau wa kilimo na taasisi za fedha wakati akizindua rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
unnamed (31)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wadau wa kilimo na taasisi za fedha wakati akizindua rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
unnamed (32)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akizindua rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
unnamed (33)
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akizindua rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
unnamed (34)
Vifijo baada ya  Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuzindua  rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
unnamed (35)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na Waziri wa Kilimo, Mhe Stephen Wasira, Waziri wa Fedha Mhe Saada Mkuya na viongozi na watendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
unnamed (36)
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na Waziri wa Kilimo, Mhe Stephen Wasira, Waziri wa Fedha Mhe Saada Mkuya, Katibu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, Mkurugenzi Mkuu wa TIB Bank Bw. Peter Noni  na viongozi na watendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
unnamed (37)
Msanii akiburudisha kwa ngoma kutoka Zanzibar baada ya  Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuzindua  rasmi Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) leo Agosti 7, 2015 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam
PICHA NA IKULU

TFDA YAWATAKA WAFANYABISHARA KUZINGATIA SHERIA YA CHAKULA NA VIPODOZI NA MWANDISHI WETU, ARUSHA

download (10)
NA MWANDISHI WETU, ARUSHA
Mamlaka ya chakula na dawa hapa nchini TFDA imewataka wafanya biashara kuzingatia sheria ya chakula na vipodozi kwa kutoingiza nchini bidhaa ambazo hazidhibitishwa na mamlaka hiyo ili kulinda afya za watumiaji
 
Hayo yamesema na mkurugenzi wa mmalaka hiyo hapa nchini Hiiti Baran Sillo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari wakati akitoa elimu kwa wananchi na wafanyabaishara katika maonesho ya nane nane
 
Amesema kuwa wafanyabishara na wananchi wanapaswa kuwa makini wanaponunua vipodozi venye sumu pamoja na vyakula vilivuyuopita muda wake kwani kwa kufanya hivyo wanavunja sheria za mamlka hiyo huku wauzaji nao wakiwa wanahatarisha usalama wa watumiaji.
  
Ameeeleza kuwa ameona umhimu wa kushiriki katika maonesho ya nane nane ili watoe elimu kwa wananchi na wafanyabiashara ambao wanaingiza bidhaa zenye sumu au ambazo zimepita muda wake kwani zimekuwa zikihatrarisha maisha ya binadamu 
 
Amedai kuwa kupitia maonesho hayo wananchi wataelewa bidhaa bora na salama pamoja na kubaini zile ambazo zimepigwa marufuku kwa matumizi ya binadamu kwani wapo wanaozituimia kwa kutokuwa na elimu ya kutosha.
 
Aidha Baram amewataka wananchi kuhakikisha kuwa wananunua bidhaa  ambazo zimedhibitishwa na mamlaka hiyo na kuepuka kununua bidhaa ambazo zimepia muda wa uhai wake na endapo kama watabaini wafanyabishara wanaouza bidhaa zilizopita basi watoe taarifa katika mamlaka hiyo ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

KAMISHNA CHAGONJA AWAPOKEA WANAMICHEZO WALIOTOKA SWAZILAND NA KUWAHUTUBIA

HP1
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo  wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja akiwa katika picha ya pamoja na wanariadha wa Jeshi la Polisi walioshiriki Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO).Wengine ni Viongozi wa Michezo wa Jeshi la Polisi (Picha na Alexander Mpeka-Jeshi la Polisi)
HP2
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo  wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja akizungumza na Wanariadha wa  Jeshi la Polisi, Wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza iliyofanyika Makao Makuu ya Polisi Jana baada ya kufanya vizuri katika Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO).Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Jonas Mahanga (Picha na Alexander Mpeka-Jeshi la Polisi)
HP3
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja akimpongeza Mwanariadha wa  Jeshi la Polisi, PC Basil John aliyeshinda medali tatu za dhahabu katika Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO), Wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza iliyofanyika Makao Makuu ya Polisi Jana.(Picha na Alexander Mpeka-Jeshi la Polisi)
……………………………………………………………………………………….
Michezo ya SARPCCO ilianzishwa kwa lengo la kuwakutanisha Maafisa na Askari Polisi ili kuweza kubadilishana mbinu za kukabiliana na uhalifu pamoja na kuwasaidia kujenga afya na kuwa wakakamavu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
Michezo ni sehemu ya kuitambulisha nchi yoyote kama Taifa huru lenye utamaduni wake. Michezo ni mojawapo ya viungo muhimu katika utamaduni wa kila jamii ya binadamu duniani. Michezo ni chombo muhimu sana katika kuiendeleza jamii. Aidha, michezo huweza kuwa kielelezo na utambulisho wa Taifa kwa kutoa burudani, kujenga na kukomaza afya ya mwili na akili, kujenga nidhamu, kujitangaza kiuwezo na vipaji. Ushiriki katika michezo ya kimataifa husaidia kulitangaza Taifa nje ya mipaka yetu. Vile vile michezo huwaweka pamoja Askari na kuwawezesha kufahamiana na kuondoa misongo ya mawazo “STRESS”. Hivyo Ni wazi kuwa mmetumia vyema fursa mliyoipata katika michezo hiyo ikiwemo ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika kutenda kazi za polisi, Hongereni sana.
Nimepewa taarifa kuwa kulikuwa na ushindani mkubwa katika michezo hiyo na ninyi pamoja na uchache wenu  mmfenakiwa kupata medali 12, 6 za dhahabu, 4 za fedha na 2 za shaba, Pia timu yetu ya riadha (wanaume) ya mbio ndefu imefanikiwa kuwa timu bora katika mashindano hayo na Askari PC Basil John aliibuka mchezaji bora wa mashindano baada ya kushinda medali 3 za dhahabu katika mbio za mita 800, 1500 na mbio za nyika (Km 12 cross country).Nawapongeza sana walioshinda
Mmefanya kazi kubwa  na mmehakikisha kuwa heshima ya Jeshi letu la Polisi iliyojijengea katika michezo hiyo tangu kuanzishwa kwake inaendelea kudumu pamoja na uchache wenu kutokana na wanamichezo wengine kutofanikiwa kwenda kutokana na sababu mbalimbali.
Aidha nawapongeza sana kwa nidhamu mliyoionyesha katika kipindi chote cha michezo hiyo, Nidhamu na kujituma kwa juhudi ndio msingi wa kufanikiwa katika mchezo wowote hivyo ninyi mmekuwa mabingwa katika kipengele hicho.
Aidha, napenda pia kutumia fursa hii kuwashukuru wadhamini waliotuwezesha kwa kutupatia vifaa vya michezo ambao ni Benki ya CRDB, NMB, African Life Assuarance, na PPF, kwani kwa ufadhili wao walioutoa umefanyiwa kazi na hivyo kupata mafanikio ya ushindi, Hivyo wakati mwingine wasisite kuiunga mkono timu yetu ya Polisi.
 napenda kuwaahidi kuwa tutaendelea kuipa kipaumbele michezo ili kuweza kuwaimarisha kiafya na kuwakutanisha na wenzenu katika mataifa mengine na nawatakieni maandalizi mazuri katika michezo mingine iliyopo mbele yenu na safari njema ya kurudi katika mikoa yenu.
AHSANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA.

UTUMISHI YAKABIDHIWA ZAWADI YA USHIRIKI WA TANZANIA KATIKA MAONYESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA BARANI AFRIKA YALIYOFANYIKA CONGO BRAZAVILLE

UT1
Kaimu Katibu Mkuu Utumishi Bw.HAB Mkwizu (wa pili kutoka kushoto) akipokea zawadi ya Tanzania kutoka kwa mmoja wa Washiriki wa Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Barani Afrika Bw. William Budoya yaliyofanyika nchini Congo Brazaville hivi karibuni. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw.Aloyce Msigwa (kushoto) na Mkurugenzi wa Mipango Ofisi ya Rais- Utumishi Bw. Cosmas Ngangaji (wa pili kutoka kulia).
UT2
Kaimu Katibu Mkuu Utumishi Bw.HAB Mkwizu (katikati) akipokea cheti cha ushiriki wa Tanzania kutoka kwa Mmoja wa Washiriki wa Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma  Barani Afrika Bw. William Budoya yaliyofanyika nchini Congo Brazaville hivi karibuni. Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Florence Temba (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw.Aloyce Msigwa (wa pili kutoka kushoto) na Mkurugenzi wa Mipango Ofisi ya Rais- Utumishi Bw. Cosmas Ngangaji (wa pili kutoka kulia).
UT3
Kaimu Katibu Mkuu Utumishi Bw.HAB Mkwizu (katikati) akionyesha cheti cha ushiriki wa Tanzania katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika nchini Congo Brazaville hivi karibuni.  Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Florence Temba (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw.Aloyce Msigwa (wa pili kutoka kushoto),  Mkurugenzi wa Mipango Ofisi ya Rais- Utumishi Bw. Cosmas Ngangaji (wa pili kutoka kulia) na mmoja wa washiriki wa maonyesho hayo kutoka Wizara ya Uchukuzi Bw. William Budoya (wa kwanza kulia).

MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA UZINDUZI WA MFEREJI MPYA WA SUEZ

B2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Balozi wa Tanzania, nchini Misri, Balozi Mohammed Hamza, wakati wakitoka kwenye Boti baada ya kuhudhuria hafla ya uzinduzi wa Mfereji mpya wa Suez Canal, kwa ajili ya meli za mizigo. Hafla hiyo ilifanyika jana Agosti 6, 2015 jijini Ismailia. Picha na OMR
B3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Balozi wa Tanzania, nchini Misri, Balozi Mohammed Hamza, wakati wakitoka kwenye Boti baada ya kuhudhuria hafla ya uzinduzi wa Mfereji mpya wa Suez Canal, kwa ajili ya meli za mizigo. Hafla hiyo ilifanyika jana Agosti 6, 2015 jijini Ismailia. Picha na OMR

BI1

ISIMAILIA AGOSTI 06, 2015
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal jana ameiwakilisha Tanzania katika uzinduzi wa mfereji mpya wa Suez unaounganisha mabara ya Ulaya, Afrika na Asia. Mfereji huu mpya ambao Misri inauita “zawadi mpya kwa Dunia” unalenga kukuza uchumi katika usafiri wa maji na utarahisisha usafirishaji wa mizigo kwa mabara haya matatu, huku Misri ambayo kijiografia iko jangwani ikitegemea kukuza uchumi wake kutokana na meli zitakazopita katika mfereji huo.
Mradi wa ujenzi wa Mfereji huu mpya umejengwa kwa mwaka mmoja licha ya kupangwa kukamilika baada ya miaka mitatu na umetumia kiasi cha dola za Marekani Bilioni Nane ambazo zimechangwa kwa njia ya Hisa na wananchi wa Misri kwa kipindi kisichozidi siku tisa. Mfereji huu ambao umezinduliwa jana, unatoa fursa kwa Meli kupita bila usumbufu tofauti na zamani ambapo ilipaswa Meli kusimama ili kupishana lakini sasa kila upande wa Meli utapita bila kuathiri upande mwingine.
Sherehe hizo za aina yake zimehudhuriwa na viongozi kadhaa wa nchi mbalimbali na kupata kuripotiwa na vyombo vyote vikubwa duniani na hivyo kutoa picha ya kuwa Afrika inapiga hatua katika kukuza uchumi wake pamoja na kuonesha dunia kuwa fursa mpya za maendeleo zipo Afrika.
Sherehe hizo za  aina yake zilipambwa na maonesho ya ndege za kivita zilizotanda anga la Mfereji mpya wa Suez huku zingine zikiruka kwa kasi na kutoa moshi ulioakisi bendera ya Misri, zingine zikipeperusha bendera ya nchi hiyo.
Katika tukio hilo la kuathimisha tukio hilo la kihistoria   serikali ya Misri ilitangaza kuwa  siku hiyo ni ya mapumziko huku ulinzi mkali ukiimarishwa katika miji yote mikuu ya nchi hiyo huku jiji la Cairo walipofikia  viongozi mbalimbali wa kimataifa likiwa chini ya uangalizi wa kijeshi kwenye maoneo yote muhimu. Barabara ya kwenda eneo la Islamelia zilikofanyika sherehe hizo ilifungwa kwa siku nzima,  walioruhusiwa kupita  ni viongiozi na wageni mbalimbali  waalikwa waliotakiwa kuhudhuria tukio hilo la kihistoria.
 Rais wa Misri Abdel  Fatah  Sisi alisema kufunguliwa kwa Mfereji  ni uthibitisho kwamba Misri inaweza na kueleza kwamba njia hiyo itaimarisha zaidi shughuli za usafirisha na kufungua fursa zaidi kwa mataifa  duniani.
Katika moja ya matukio ya  uzinduzi huo Rais Fatah na viongozi mbalimbali waliohudhuria sherehe hizo walisafiri katika meli za kifahari huku kiongozi huyo wa Misri akivalia mavazi maalumu ya kijeshi akiwa juu ya sehemu ya uwazi wa meli hiyo pamoja na kijana mdogo mwanafunzi wa miaka tisa aliyevalia kijeshi na kupeperusha bendera ya  Misri kama ishara ya kufunguliwa rasmi kwa mfereji huo.
Shughuli  ilimazika usiku  kwa  maonesho mbalimbali ya sanaa na utamaduni wa Misri  na kuhudhuriwa na viongozi na wageni wote waalikwa.
Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais
Cairo Misri Agosti 7, 2015

TCRA YAWAHIMIZA WANANCHI KUTUMIA KWA USAHIHI MAWASILIANO

Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano(TCRA) Kanda ya Kaskazini,Annette Mahimbo Matindi.……………………………………………………………………………….
Wananchi wanaofika kwenye maonesho ya wakulima na wafugaji(Taso)Nane nane Njiro jijini Arusha wametakiwa kufika kwenye banda la TCRA kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na Mamlaka hiyo muhimu kwa wananchi na uchumi kwa ujumla. 
Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano(TCRA) Kanda ya Kaskazini,Annette Mahimbo Matindi amesema kuna umuhimu mkubwa wananchi kufahamu utendaji kazi wa taasisi hiyo badala ya kuilalamikia bila kujua mipaka na wajibu wake.
Amesema wakulima na wafugaji ili kunufaika katika shughuli zao hawana budi kutumia kwa usahihi  huduma za mawasilino ili kukuza biashara zao.
“Nitumie fursa hii kuwataka wananchi wote kutumia kwa usahihi huduma za mawasiliano badala ya matumizi yasiyofaa na ambayo wakati mwingine watajikuta kwenye mikono ya vyombo vya dola,”amesema Annette
Amesema wakulima na wafugaji ni sehemu muhimu katika kukuza uchumi wa Tanzania hivyo  mawasiliano ni nyenzo muhimu kwao. 

TBL YAFANIKISHA UPIMAJI AFYA ZA MADEREVA WA MASAFA MAREFU WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI

 Mganga kutoka kitengo cha afya makao makuu ya jeshi la polisi Tanzania, Dk Issa Ndimila akimchukua damu dereva wa magari makubwa, Benedicti Samuel kwa ajili ya kumpima magonjwa katika uzinduzi wa upimaji wa afya kwa madereva wa mabasi na malori ya masafa marefu ikiwa sehemu ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani katika kituo cha mizani cha Mikese mkoa wa Morogoro mpango ulioanzishwa na TBL na jeshi la polisi nchini.
 Mganga kutoka kitengo cha afya makao makuu ya jeshi la polisi Tanzania, Dk Issa Ndimila akimchukua damu dereva wa magari makubwa, Kanai John kwa ajili ya kumpima magonjwa katika uzinduzi wa upimaji wa afya kwa madereva wa mabasi na malori ya masafa marefu ikiwa sehemu ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani katika kituo cha mizani cha Mikese mkoa wa Morogoro mpango ulioanzishwa na TBL na jeshi la polisi nchini.
 Katibu Tawala wilayaa ya Morogoro, Emmanuel Nzunda akimkabidhi zawadi ya fulana na cheti dereva wa magari makubwa baada ya kupima afya wakati wa maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani katika kitucha mizani cha Mikese mkoa wa Morogoro, mpango ulioanzishwa na
TBL na jeshi la polisi nchini.
 Askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Morogoro, Silve Massawe akijaza taarifa za dereva Edward Sanga baada ya kupima afya katika uzinduzi wa upimaji wa afya kwa madereva wa mabasi na malori ya masafa marefu ikiwa sehemu ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani katika kituo cha mizani cha Mikese mkoa wa Morogoro mpango ulioanzishwa na TBL na jeshi la polisi nchini.
Askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Morogoro, Silve Massawe akijaza taarifa za dereva Abdallah Rajabu baada ya kupima afya katika uzinduzi wa upimaji wa afya kwa madereva wa mabasi na malori ya masafa marefu ikiwa sehemu ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani katika kituo cha mizani cha Mikese mkoa wa Morogoro mpango ulioanzishwa na TBL na jeshi la polisi nchini.

KATA YA MWASANGA NA TEMBELA MKOANI MBEYA ZAPATIWA ELIMU KUHUSU JOTOARDHI

JO1
Afisa Mawasiliano wa Kampuni ya Kuendeleza Jotoardhi Tanzania (TGDC) Bi. Johari Kachwamba akiwaelimisha Viongozi wa Kata ya Mwasanga na Tembela kuhusu majukumu ya TGDC leo 7 Agosti, 2015 Mkoani Mbeya.
JO2
Mhandisi Mwandamizi toka Wizara ya Nishati na Madini, Bwana. Jacob Mayalla akiwaelimisha Viongozi wa Kata ya Mwasanga na Tembela kuhusu historia ya tafiti za jotoardhi kwa mkoa wa Mbeya leo 7 Agosti, 2015 Mkoani Mbeya.
JO3
Baadhi ya Viongozi wa Kata ya Mwasanga na Tembela wakifuatilia kwa makini elimu ikiyotolewa na Wayendaji wa TGDC leo 7 Agosti, 2015 Mkoani Mbeya.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA.
………………………………………………………………………………………………………..
NA BENEDICT LIWENGA, MAELEZO, MBEYA.
Nishati ya jotoardhi imeelezwa kuwa ni nishati usiyokuwa na kikomo kwani pindi inapovunwa huwa haiishi na matumizi yake yanakuwa endelevu kwasababu pindi mvuke unapopatikana toka katika maji ya jotoardhi, maji yake hutumiwa kwa shughuli za moja kwa moja ikiwemo ukaishaji wa mazao, uzalishaji samaki ikiwemo na utalii.
Hayo yameelezwa leo na Mhandisi Mwandamizi toka Wizara ya Nishati na Madini, Bwana Jacob Mayalla wakati Timu ya Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC) ikiendelea na kampeni yake ya kuelimisha viongozi pamoja na wanavijiji kuhusu faida ya jotoardhi nchini.
Mayalla amesema kuwa utafiti kuhusu upatikanaji wa jotoardhi ulianza miaka ya nyuma ya 1976 hadi 1978 ambapo mkoa wa Mbeya umekuwa miongoni mwa mikoa ambayo jotoardhi inasemekana ipo kutokana na tafiti hizo.
“Mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa iliyobarikiwa kuwa na jotoardhi, hivyo Serikali kupitia Kampuni hii ya TGDC inakusudia kuanza shughuli za upimaji ili kuweza kupata nishati hii na kuweza kutatua changamoto za upatikanaji wa umeme katika mkoa huu”, alisema Mayalla.
Akitaja baadhi ya matumizi ya moja kwa moja, Mhandisi Mipango toka TGDC, Bwana Chagaka Kalimbia ameeleza kuwa, jotoardhi ina matumizi mbalimbali ikiwemo kupadha nyumba joto, kuzalisha mazao ya mbogamboga kwa kutumia Vitalu Nyumba, vyanzo vya kitalii kwa nchi pamoja na matumixi mengineyo ambayo yanapelekea kuongeza vipato vya wananchi na taifa kwa ujumla.
“Mradi huu una manufaa kwa wananchi kwa mfano kwa mkoa wa Mbeya ambao kuna baridi kali, jotoardhi inaweza kutatua changamoto hii kwa kutengeneza miundombinu ambayo itasaidia kupasha nyumba joto, lakini pia kwasababu mkoa huu unategemea kilimo, basi jotoardhi hii itakuwa mkombozi kwa uzalishaji mkubwa wa mazao mbalimbalu kwa kukaushia maxso yao kwani nishati ya jua katika maeneo haya siyo ya uhakika”.
Naye Afisa Mawasiliano wa TGDC, Bi. Johari Kachwamba ameeleza mandhari nzima wa madhumuni ya TGDC kwa wananchi na kwa Taifa zima ikiwemo hali ya uzalishaji wa umeme hapa nchini, historia ya TGDC, Dira na dhamira kuu ya TGDC ili kuifanya jamii ipate uelewa mzuri kuhusu majukumu ya Kampuni hiyo.
Kwa upande wake Afisa Sayansi ya Jamii, Bi. Eva Nyantori ameeleza masuala mbalimbali kuhusu namna gani jamii inashitikishwa na mradi huo kwa manufaa ya wananchi hususani fursa mbalimbali ambazo jamii inatarajiwa kuzipata zikiwemo fursa za ajira ambazo huleta kipato hali ambayo inapelekea uchumi wa eneo kukua kwa kasi kutokana na na nishati hiyo.
“Jamii itarajie kupata fursa mbalimbali mfano sekta za barabara, ajira kwa wananchi, kodi itokanayo na mradi huo, upatikanaji wa umeme wa nafuu kwa wakazi wa eneo husika, hivyo ni matumaini yetu kuwa nishati hii itapunguza gharama kwa wananchi wa mkoa huu”, alisema Nyantori.
Akizitaja changamoto za mradi huo, amesema kuwa kuna Sheria namba 4 na 5 ya 1999 ili kuweza kufanya fidia kwa maeneo yayaksyohusika na mradi ambapo Sheria hiyo inaitaka kufanya fidia hiyo ndani ya miezi Sita kabla ya mradi huo kuanza rasmi kuchimbwa, lakini elimu kuhusu fidia hiyo itatolewa ili kumfanya mwananchi apate kuelewa.
TGDC inatarajia kuzalisha zaidi ya Megawati 200 za nishati ya umeme kwa mkoa wa Mbeya ambao utatokana na nishati ya jotoardhi ambapo kwa sasa mkoa huo unatumia Megawati 40.

MBUNIFU WA MITINDO AMINA PLUMMER ATOA MADA NAMNA KUJITAMBUA KWENYE SEMINA YA KUWAWEZESHA WANAWAKE WAJASIRIAMALI

   
Mbunifu na Mmiliki wa Maduka ya Amina Design  Ambaye pia ni   Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation Amina Plummer Akitoa Mada kwenye Semina ya Kuwawezesha  Wanawake Kuwa Wajasiriamali kupitia Vipodoz Vya Luv Touch Manjano Iliyoandaliwa na Manjano Foundation Kwa Lengo la Kuwajengea Udhubutu Wanawake  Kufanya biashara pia namna ya Kujiwekea Akiba na Kutumiza Malengo yao. Taasisi ya Manjano Foundation, ambayo imeanzisha jukwaa kwa ajili ya kuandaa Miradi  ambayo itamuinua mwanamke wa Kitanzania kwa kumwondolea umasikini wa kipato na ambayo itakuwa ni chachu ya kubadili yale yote yaliyoyazunguka maisha yake. Taasisi hii  limekwishazindua mradi wenye kubeba bendera yake, Manjano Dream-Makers, mradi unaokusudia kuzaa kizazi kipya cha wajasiriamali wanawake kwa kutumia kipodozi cha LuvTouch Manjano tu
Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions Ltd  Mama Shekhar Nasser (Katikati) Akiwa na Mbunifu Amina Plummer (Kushoto ) Pamoja Afisa Mtendaji Mkuu wa Women an Youth  Empowerment Program Kutoka Uganda Dada Remmie Male.
Mbunifu na  Mmiliki wa maduka ya Amina Design Amina Plummer  ni mmoja kati ya Mentors 15 watakao wapa muongozo washiriki 30 wa mradi wa Manjano Foundation. Amina aliwapa somo la kujifahamu kama wajasiriamali chipukizi kuwa wasilimbuke pale ambapo mafanikio yanapo anza kuja. Aliwaeleza kuhusu umuhimu wa kujiamini, kumuamini Mungu, kuwakarimu wateja, kuweka akiba Akiwa Sambamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Women an Youth  Empowerment Program Kutoka Uganda Dada Remmie Male
Mbunifu  Amina Plummer  ni mmoja katika Picha ya Pamoja na Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo inayoandaliwa na Taasisi ya Manjano  Kupitia Bidhaa za Luv Touch Manjano.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Shear illusions Ltd  Mama Shekhar Nasser na Mbunifu Amina Plummer  Pamoja Afisa Mtendaji Mkuu wa Women an Youth  Empowerment Program Kutoka Uganda Dada Remmie Male. Katika Picha ya Pamooja na Washiriki wa Semina hiyo..

NISHATI YA JOTOARDHI KUNUFAISHA BAADHI YA VIJIJI MKOANI MBEYA

e
Mkurugenzi wa masuala ya Kiufundi toka TGDC, Bwana Karamaeli Mnjokava akiwaeleza wanakijiji cha Ituha na Itonyajuu ya faida za jotoardhi nchini 6 Agosti, 2015 mkoani Mbeya.
q
Meneja Mkuu wa Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi, Mhandisi Boniface Njombe  akiwaelimisha wanakijiji cha Ituha na Tonya juu ya jotoardhi nchini 6 Agosti, 2015 mkoani Mbeya.
r
Mjiolojia Mwandamizi toka Wizara ya Nishati na Madini, Bwana Jacob Mayalla akiwaelezea wanakijiji wa Ituha na Tonya hitoria ya tafiti za jotoardhi nchini 6 Agosti, 2015.
w
Baadhi ya wanakijiji wa Ituha na Tonya wakifuatilia mada kwa makini zikizotolewa na watendaji wa TGDC 6 Agosti, 2015 mkoani Mbeya.
……………………………………………………………………………..
NA BENEDICT LIWENGA, MAELEZO, MBEYA.
Nishati ya Jotoardhi imeelezwa kuwa muhimu kwa maeneo ambayo utafiti ulishafanywa hapo awali kwani ina faida lukuki kwa maendeleo ya nchi hususani katika kutatua changamoto ya ukosefu wa nishati ya umeme ikiwemo umeme wa mgao ambao unazikumba baadhi ya mikoa hapa nchini.
Akiongea wakati wa Kampeni endelevu kuhusu jotoardhi 6 Agosti, 2015 katika Kata za Ilomba vijiji vya Ituha na Tonya pamoja na Kata ya Nanyala iliyopo Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya, Meneja Mkuu wa Shirika la Uendelezaji wa Jotoardhi (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe amesema kuwa jamii hainabudi kuonyesha ushirikiano na Serikali pamoja na Kampuni ya TGDC ili kuwepo na uelewa juu ya nishati hiyo na kuleta maendeleo nchini.
“Niwahakikishie kuwa nishati hii ni nzuri kwani itasaidia kutatua changamoto tulizonazo katika uoande wa nishati, hivyo niwasihi kuonyesha ushirikiano baina ya Serikali yetu pamoja na Kampuni hii ili juhudi hizi zizidi kuendelea na kutuletea maendeleo katika maeneo yetu”, alisema Njombe.
Mhandisi Njombe aliongeza kuwa TGDC imedhamiria kuzalisha umeme wa Megawati 200 jambo ambalo litasaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuuondoa mgao kwani kwa sasa mkoa wa Mbeya pekee unatumia Megawati 40.
Naye Mkurugenzi wa Masuala ya Kiufundi toka TGDC, Bwana Taramaeli Mnjokava ameeleza kuwa, jotoardhi ina matumizi mengi ikiwemo matumizi ya moja kwa moja kama vile katika uzalishaji wa samaki kwani samaki hupendelea maji yenye uvuguvugu kiasi, hivyo endapo wanambeya watajikita katika kutengeneza mabwawa ya samaki, maji ya jotoardhi yanasaidia katika kuzalisha samaki kwa wingi na hatimaye kuongeza pato kwa taifa.
“Matumizi mengine ya maji yatokanayo na jotoardhi ni kwamba, maji haya yanaweza kutumika katika Vitalu shamba kwa kiingereza huitwa Green Houses, sasa kwa maji haya tunaweza kuzalisha mboga mboga pamoja na maua jambao ambalo litaweza kutuongezea kipato.

WENGI WAJIUNGA NA NSSF MAONYESHO YA NANENANE

 Meneja Kiongozi wa Masoko na Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume akiwaelezea faidaza kujiunga na mfuko huo wakazi wa Mkoa wa Lindi waliofika kwenye banda la NSSF kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa mkoani humo.
 Meneja Kiongozi wa Masoko Na Uhusiano Eunice Chiume akiwapa Maelezo ya Faida za kuwa Mwanachama wa NSSF wanachama waliotembelea banda la NSSF mkoani Lindi.
 Mwanachama wa Hiari, Mrisho Mpoto akilipia michango yake kwenye maonesho ya Nanenane Mkoani Lindi.
Afisa Uendeshaji
Muandamizi Kabona Kandoro akimkabidhi zawadi mmoja wa wanachama waliotembelea
banda la NSSF kwenye maonesho ya nanenane mkoani Lindi.
Mwanachama mpya wa NSSF akipigwa picha kwa ajili ya kadi ya uanachama baada ya kujiunga na mfuko huo.

UMOJA WA WASANII WA FANI MBALIMBALI WAMTANGAZA RAIS DR. JAKAYA KIKWETE KUWA SHUJAA WA SANAA YA MUZIKI NCHINI

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani),waliofika ndani ya ukumbi wa Mlimani City  katika hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10 na pia kumtambulisha Mgombea wa Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli,Dkt Jakaya Kikwete alizungumza mambo mbalimbali zikiwemo haki na hatimiliki za wasanii wa muziki pamoja na Bongomovie na pia alikubali kuwa mlezi wa tasnia hizo na kuhakikisha mambo yanakwenda sawa ndani ya tasnia hizo mbili adhimu kwa sasa hapa nchini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete katikati pichani akiserebuka na wadau wa muziki na huku akipiga nao picha,ndani ya ukumbi wa Mlimani City  katika hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10 na pia kumtambulisha Mgombea wa Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akipiga ngoma huku akishirikiana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipiga gitaa ndani ya ukumbi wa mlimani City jijini Dar.
Mwanadada Wema Sepetu akimtunza midola Dkt John Magufuli alipokuwa akipiga ngoma jukwaani kwa ustadi mkubwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete akiwa ameambatana na Mgombea Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Katibu wa NEC Itikadi na Uuenezi Nape Nnauye na pamoja na Januari Makamba wakifurahia jambo kwa pamoja na wageni waalikwa mbalimbali waliofika ndani ya ukumbi wa Mlimani City kushiriki hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Jakaya Kikwete akiwa ameambatana na Mgombea Urais wa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli pamojoa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  (mwisho kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh.Paul Makonda wakiwasili ndani ya ukumbi wa Mlimani City kushiriki hafla ya kuagwa kwake ilioandaliwa na Muungano wa Wasanii kwa ajili ya kumshukuru kwa namna alivyowasaidia tangu alivyoingia madarakani kwa miaka 10.
PICHA NA MICHUZI JR.
 

SELEMANI RASHIDI MKAZI WA KITONGOJI CHA LUGONGONI (A) NGURUKA MKOA WA KIGOMA ANAOMBA MSAADA WA MATIBABU KWA MWENYE KUGUSWA

 Selemani Rashidi,  naomba msaada  kwa yeyote anisaidie niweze kufanyiwa matibabu kwa kinyama kilicho jitokeza kichwani mwangu toka nilipo zaliwa.
 Selemani Rashidi, anapoishi na mama yake mzazi
Selemani Rashidi (kushoto), akiwa na mama yake mzazi pichani, ambaye alisimulia mkasa mzima wa mwanaye, alizaliwa akiwa mzima na baada ya kuzaliwa alipatwa na matatizo ya ugonjwa wa Degedege na alimpeleka kwa mganga wa kienyeji na kupona matatizo hayo na ndipo kikaota kipele kichwani cheusi na kikawa kinakuwa na kushikana na sikio, kutokuwa na uwezo wa kipesa hakuweza mpeleka popote, Baba yake yapata Miaka kumi na tano toka afariki na ukizingatia ni pesa inayo hitajika, hayo yalisemwa na mama yake mzazi ambaye anaitwa Zamda  Kibosha, wakiwa wamekaa kwao maeneo ya kitongoji cha  Lugongoni, (A)  Kataa ya Nguruka Wilaya ya Uvinza Mkoa wa Kigoma, Mama yake anasema mwanaye baada ya kuota kinyama hicho, kauli kutoka ni kwa shida, akijibu maramoja harudii tena kuongea na chooni anakwenda mwenyewe na kula anakula kama kawaida, mama anaomba kwa mtu yoyote mwenye kuona na kusia anaomba msaada wa hali na mali ili mwanaye apate matibabu, kwa mawasiliano mwenye chochote kitumwe kwenye namba 0687946492, Mariam Hamza Thabiti, Nguruka kigoma.
(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Mmiliki wa ujijirahaa blog.

Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayofanyika mkoani Lindi yafikia siku ya sita.

1
Wananchi wote mnakaribishwa kutembela banda la Wizara ya Fedha na taasisi zilizo chini yake ikiwemo UTT AMIS, Mfuko wa Pensheni PPF, GPSA na UTT PID uwanja wa maonesho ya kilimo ya Nane Nane Kitaifa Ngongo mkoani Lindi.
3
Mwenyekiti wa Chama cha Kilimo Taifa (TASO) Englebert Moyo akiuliza swali kuhusu masuala ya pensheni kwa Mhasibu kutoka Idara ya Pensheni Wizara ya Fedha Imelda Mzatulla wakati alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha.
5
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) Josephat Mwambega akiongea na Afisa Msoko na Uhusiano Rahimu Mwanga kutoka taasisi ya UTT AMIS kwenye Uwanja wa  maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Ngongo Mkoani Lindi.
6 7
Mhasibu kutoka Idara ya Pensheni Wizara ya Fedha Imelda Mzatulla akiongea na baadhi ya wageni waliofika kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Wizara ya Fedha wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi. Continue reading →

VIJANA WAJITUME ZAIDI ASEMA DIAMOND

TFF YATUMA SALAM ZA RAMBIRAMBI

TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetuma salam za rambi rambi kwa familia ya Muro, kufutia kifo cha Mzee Cornel Muro kilichotokea mwishoni mwa wiki jijini Dar s salaam na mazishi kufanyika Machame mkoani Kilimanjaro.
Katika salamu zake za rambirambi kwa familia ya marehemu Muro, TFF imewapa pole wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kusema wako pamoja katika kipindi hiki cha maombelezo na kuomba mwenyezi Mungu awajilie nguzu wafiwa
Marehemu Cornel Muro ni baba mzazi wa Afisa Habari wa klabu ya Young Africans, Jerry Muro.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

WASANII WAMUAGA DR. JAKAYA KIKWETE NA KUMKARIBISHA DR JOHN POMBE MAGUFULI MLIMANI CITY

1
Rais Dr. Jakaya Kikwete akifurahia jambo  na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kupitia CCM wakati alipowasili Mlimani City jijini Dar es salaam kwa ajili ya kushiriki hafla ya chakula cha jioni kilichondaliwa na Muungano wa wasanii Kumshukuru Mh. Dr. Jakaya Kikwete kwa jinsi alivyowasaidia katika uongozi wake wa miaka 10 kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kumkaribisha Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. John Pombe Magufuli, Hafla hiyo imehudhuriwa na wasanii mbalimbali  wakiwemo waigizaji wa filamu, wachezaji na wanamuziki wakishiriki kwa pamoja kumshukuru Dr. Jakaya Kikwete, Kulia ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh. Januari Makamba(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MLIMANI CITY-DAR ES SALAAM)
3
Rais Dr. Jakaya Kikwete akiongozana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto, Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. John Pombe Magufuli na Mwigizaji Jacob Steven JB wakati alipowasili kwenye ukumbi wa Diamond.  
4
Rais Dr. Jakaya Kikwete akiongozana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanawa pili kutoka  kushoto ar es salaam Mh Meck Sadik na Muigizaji Jacob Steven JB.
5
Mwanamuziki Nasib Abdul aka Diamond Platnumz akiwasili na Meneja wake wa Shughuli za kimataifa Bw.Salam.
6
Rais Dr. Jakaya Kikwete akiongozana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto wakati wakiigia ukumbini.
7
Rais Dr. Jakaya Kikwete akiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto,Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. John Pombe Magufuli wa pili kutoka kulia na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Mh. Januari Makamba.
8
Rais Dr. Jakaya Kikwete akiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto,Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. John Pombe Magufuli kulia na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye wakipiga makofi wakati wimbo maalum ukiimbwa.
9
Davis Mosha kulia akiwa pamoja na Mboni Masimba wa The Mboni Show wakiperuzi kwenye simu. 
10
Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na Davis Mosha na Mboni Masimba
11
Rais Dr. Jakaya Kikwete akina baadhi ya viongozi wa bendi za muziki wa Taarab.
Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na Bw. Godfrey Kusaga mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Primetime.
16
Rais Dr. Jakaya Kikwete akisalimiana na Adam Mchomvu mtangazaji wa kipindi cha XXL cha Clouds Radio.
17
Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dr. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkurugenzi wa mtandao huu Bw. John Bukuku kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadik Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam.
19
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Davis Mosha kushoto ni msanii Mwana FA.
20
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wasanii mbalimbali kutoka kushoto ni Mwigizaji Jacob Steven, Mwanamuziki Jose Mara na Mwana FA.
21
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifurahia jambo na wasanii mbalimbali kutoka kushoto ni Mwigizaji Jacob Steven, Mwanamuziki Jose Mara, Mwigizaji Monalisa aka Yvone Cherry na Mwana FA, kulia ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadik.
22
Kutoka kulia ni Mama Monalisa . Juma Kaseja, Dokii na Monalisa wakiwa katika hafla hiyo.
23
Ali Choki kushoto na anayefuatia ni msanii Kitale pamoja na wasanii wenzao wakiwa katika hafla hiyo.
24
Kutoka kushoto ni Mabosi wangu Edward Mpogole, Daniel Chongolo na Juma Kengele wakipozi kwa picha.

TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI KUTOKA CHAMA CHA WANANCHI CUF KUHUSU KUJIUZULU KWA PROFESA LIPUMBA

Leo tarehe 6 Agoimagessti, 2015 Profesa Ibrahim Lipumba aliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Hoteli ya Peacock, mjini Dar es Salaam na kutangaza kwamba amejizulu nafasi yake kama Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF).
Sisi kama Chama tumezipokea taarifa hizo na tunayaheshimu maamuzi yake. Ni haki yake ya kikatiba na haki ya kidemokrasia kufanya maamuzi anayoyaona yana maslahi kwake.
Bila shaka, Profesa Ibrahim Lipumba amekifanyia kazi kubwa Chama chetu katika miaka 16 ambayo alikuwa Mwenyekiti wetu, nafasi iliyomfanya awe kiongozi wetu mkuu. Kwa nafasi yake hiyo, pia ametoa mchango mkubwa katika ujenzi wa demokrasia katika nchi yetu. Tunaithamini kazi hiyo na tutaendelea kumheshimu kwa utumishi wake mkubwa kwa Chama chetu na nchi yetu. Tunamtakia kila la kheri katika mipango yake ya baadaye.
Chama Cha Wananchi (CUF) ni taasisi na kinaendeshwa kitaasisi. Ndiyo maana maamuzi yake yote yamekuwa yakifanywa kitaasisi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chama. Kwa msingi huo, pamoja na ukweli kwamba kuondoka kwa Profesa Lipumba katika safu ya uongozi kutaacha pengo hasa katika kipindi hichi ambacho tunaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu, tunawahakikishia wanachama na wapenzi wa CUF na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kwamba Chama hichi hakitayumba.
Katika historia yake, CUF imepita katika dhoruba na misukosuko mingi lakini mara zote kimeonesha uwezo mkubwa wa kuhimili dhoruba na misukosuko hiyo na kukabiliana na athari zake. Hatuna chembe ya wasiwasi kwamba hata mtihani huu tutauvuka na tunaamini tutaibuka tukiwa Chama imara zaidi.
Katibu Mkuu ameagiza kuitishwa kwa vikao vya dharura vya Kamati ya Utendaji ya Taifa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa siku ya Jumapili, tarehe 9 Agosti, 2015 ili kujadili hatua hiyo na kufanya maamuzi juu ya hatua muafaka zinazopaswa kuchukuliwa katika kipindi hiki hadi hapo Chama kitakapomchagua mwanachama mwengine kujaza nafasi hiyo ya Mwenyekiti.
Katika kipindi hiki, Chama kinawataka wanachama na wapenzi wake wote kuwa watulivu na wavumilivu na kusubiri maelekezo ya vikao vya juu vya kitaifa vya Chama.
Mwisho kabisa, tunawahakikishia wanachama wetu na Watanzania wote kwa ujumla kwamba CUF itaendelea na shughuli zake kama Chama na pia kama mshirika katika UKAWA ambayo CUF ilikuwa ni katika waasisi wake. Tunawahakikishia wanachama wetu na Watanzania wote kwa ujumla kwamba CUF itatumia nguvu, uwezo, juhudi na maarifa yake yote kuhakikisha kwamba inaulinda UKAWA ambao unaonekana kuwa mwiba kwa CCM. Tunatambua kwamba kuna njama na mbinu kubwa na nyingi zinazofanywa na watawala kutaka kuuvuruga na kuuhujumu UKAWA wakidhani kwamba watapata manusura. Tumesema na tunaendelea kusema CCM mwaka huu hawana manusura. Watanzania wameamua kuwan’goa, na watan’goka Tanzania Bara na Zanzibar kupitia sanduku la kura tarehe 25 Oktoba, 2015. Wimbi hili kubwa la mabadiliko halizuiliki tena.
HAKI SAWA KWA WOTE
ISMAIL JUSSA
KAIMU MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA MAWASILIANO NA UMMA
06 AGOSTI, 2015

No comments :

Post a Comment