Baadhi ya wanachama wakishauri mifuko ya hifadhi ya jamii
kuanzisha mikataba ya huduma bora yenye
misingi ya uwazi na uwajibikaji na kufahamu matarajio na viwango vya mafao yao
Unafikiri kwa nini kuna
umuhimu mkubwa kwa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii kuwekea maanani sana
juu ya huduma kwa wanachama, wastaafu pamoja na wategemezi wao na hata kwa
waajiri. Kwa sasa kampuni na taasisi nyingi zinaendeshwa kwenye mazingira ya
ushindani ambao kila siku unaongezeka.
Na ushindani huu ni wa kimataifa na wakati huo huo na masoko ulimwenguni
yanaendelea kuongezeka.
Leo gharama za kumpata
mwanachama au mteja mpya mara nyingi zinazidi hata gharama za kumbakiza
mwanachama au mteja wa siku nyingi. Mteja aliyeridhika na huduma huwa habishana
na bei za huduma au bidhaa unazotoza na kwa maana hiyo kunakuwepo na shughuli
au kazi ndogo sana za kufanya masoko na za uuzaji za kumhudumia mteja wa namna
hii kuliko utekelezaji au shughuli ambazo ungefanya kwa kumtafuta mteja mpya.
Matokeo yake kwa sasa wakati
wa teknolojia na habari na mawasiliano shughuli za biashara zaidi humgusa
mteja. Kwa kuongezeka kwa ushindani mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii
inahitaji kuunganisha aina zote za mitandao ili kuboresha mawasiliano na
hatimaye kumridhisha mteja. Mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii lazima iweke
malengo na mikakati ya rasilimali zao kwa nguvu zote kwa ajili ya kuwalenga na
kuwabakisha wateja bora na wanaovutia na kuhakikisha ya kuwa wanapanua msingi
wa wateja ambao wataleta faida kubwa ndani ya mfuko hasa kukusanya michango
itakayotunisha mfuko kwa muda marefu ili kutimiza ahadi za mafao ya muda mrefu
na ya muda mfupi. Faida kubwa kwa mwanachama kama atapatiwa huduma bora anakuwa
amezoea na huduma ya hali juu kwa kuridhika na kiwango cha huduma na jinsi
mfuko unavyomjali.
Matokeo yake ni kwamba mteja
anakuwa hana muda wa kuhangaika wa kutafuta mfuko mwingine wa pensheni wa
hifadhi ya jamii wa kuhamia wa kumpatia huduma bora zaidi hiyo anayopata.
Gharama au bei ya huduma au bidhaa siyo
kwa kila kitu, mteja yaani mwanachama anabaki kuwa mwaminifu wa mfuko wa
pensheni wa hifadhi ya jamii unaomridhisha na huduma anazotaka hata kama
kutatokea na mfuko mwingine wa pensheni wa hifadhi ya jamii unaotoa huduma na
bidhaa zinazofanana na kwa bei au gharama za chini. Na faida kubwa kwa mfuko wa
kutoa huduma bora na hali ya juu ya kumjali mteja ni kwamba mteja aliyeridhika
mara nyingi ni mtu ambaye atabaki kuwa mteja wako. Na jinsi ya kumpata mteja au
mwanachama mpya kwa kawaida ni gharama za hali ya juu sana kuliko kumtunza na
kumbakiza mteja au mwanachama uliyekuwa nawe tangia muda mrefu
Hivyo Mifuko ya Pensheni ya
hifadhi ya jamii nchini inatakiwa kujiwekea malengo na mikakati mbalimbali ili
kuleta ufanisi na tija katika shughuli za ulipaji wa mafao. Kwa mfano mfuko wa
pensheni wa PSPF tangu kuundwa kwake umejiwekea malengo na mikakati mbalimbali
ili kuleta tija na ufanisi katika shughuli za ulipaji mafao. ili kuweza
kulibainisha hili, mfuko umeona ni muhimu kuwepo na mapatano ya utoaji wa
huduma baina yake na mteja kwa kuanzisha mkataba wa huduma kwa wateja.
Mkataba huu wa PSPF unasema
mapatano haya ni hatua muhimu sana katika utoaji wa huduma bora katika misingi
ya uwazi na uwajibikaji. Kwa kufanya hivyo wateja wa PSPF watapata uhuru na
uelewa wa kufahamu matarajio yake katika huduma fulani na hasa viwango vya muda ambavyo vitamwezesha
mwanachama kupanga mambo yake vyema badala ya kusubiri huduma bila kufahamu
upatikaji wa huduma hizo na kwa viwango vipi.
Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa
PSPF ndugu Adam Mayingu anasema mapatano haya yatamwezesha mwanachama kufahamu
huduma za mfuko, viwango vya huduma na hatua atakazoweza kuzichukua iwapo
viwango vya huduma vitakuwa kinyume na matarajio ya mkataba.
“Hata hivyo, ili mfuko uweze
kutoa huduma bora kwa wakati kama ilivyokusudiwa katika mapatano haya,
tunategemea zaidi kupata mwitikio na ushirikiano kutoka kwa wateja ili kutimiza
makubaliana haya. Mteja ndiyo kiungo muhimu katika kufanikisha utekelezaji wa
malengo ya kila siku ya mfuko, kwa kuwa taarifa anazotoa ndizo zinazouwezesha mfuko
kutoa huduma stahiki” Mayingu anasema.
Mkurugenzi mkuu anasema wana
imani ya kwamba, kila mwanachama atatimiza wajibu wake ipasavyo ili aweze
kupata huduma bora zinazotolewa kwa wakati muafaka, kwa heshima na kwa
unyenyekevu. Hivyo, maoni ya mteja yatauwezesha mfuko kuongeza ubora wa huduma
unazozitoa.
Mfuko wa pensheni wa PSPF
ulianzishwa kwa sheria ya mafao ya hitimisho la kazi kwa watumishi wa umma
namba 2 ya mwaka 1999, sura ya 371. Tangu kuundwa kwake mfuko umejiwekea
malengo na mikakati mbalimbali ili kuleta tija na ufanisi katika shughuli za
ulipaji mafao ili kuweza kulibainisha hili, mfuko umeona ni muhimu kuwepo mapatano ya utoaji wa huduma baina yake na
mteja kwa kuanzisha mkataba wa huduma kwa mteja. Dira ya mfuko ni “kuwa mtoa huduma bora kwa
huduma za hifadhi ya jamii nchini”, wakati kwa upande wa dhima ni “kutoa huduma
zenye ushindani katika sekta za hifadhi ya jamii kwa wateja kwa kutumia
watumishi wenye ari ya kazi na teknolojia inayofaa”.
No comments :
Post a Comment