
Mmojawapo
wa wajasiriamali wa maduka ya nguo nchini akijaza fomu ya kujiunga kuwa
mwanachama wa mpango wa hiari wa mfuko wa pensheni wa PSPF ili kunufaika na
mafao ya muda mrefu na mafao ya mfupi kama vile mikopo ya kukuza biashara na
mikopo ya ada za shule na chuo
Idadi
kubwa ya watanzania hawana elimu ya hifadhi ya jamii inayoweza kuwaelemisha juu
ya mafao yanayotolewa, wajibu wao, na haki zao za pensheni kwa ujumla. Hivyo kuna
haja kubwa hata kuelemishwa umma juu ya kujiunga na mifuko ya pensheni ya ziadi
ya kujiunga kwa hiari hata kama ni wanachama wa wachangiaji wa mifuko hii ya
lazima kisheria.
Kufuatia kupitishwa na sheria ya
mamlaka ya usimamizi na udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Sheria Na. 8 ya
mwaka, 2008 mtu yeyote anaweza kujiunga na mfuko wowote wa pensheni ya hifadhi
ya jamii.
Uanachama kwenye mifuko ya ziada iliyoruhusiwa na SSRA kuanzishwa na mifuko hii
ya pensheni ya hifadhi ya jamii ni ya hiari kwa mtu yeyote aliyeajiriwa au
kujiajiri mwenyewe, mwanachama aliye katika mifuko mingine, na kwamba
mwanachama wa mpango wa hiari anayo fursa ya kuhamia kwenye mpango wa
uchangiaji kwa mujibu wa sheria.
Kila binadamu ana uhusiano mkubwa na hifadhi ya
jamii iwe kinadharia au kivitendo kutoka kuzaliwa kwake mpaka kufa, binadamu
mwenyewe lazima ajishughulishe na kazi hatarishi na kuugua magojwa mbalimbali na kwa hiyo binadamu lazima akumbane na
majanga mbalimbali kama vile majanga ya kiuchumi na ya kijamii yanayosababishwa
na kukoma au kupungua kipato kutokana na maradhi, kujifungua mtoto, ajali za
kuumia kazini, ukosefu wa ajira, ulemavu, uzee, kifo na kuongezeka kwa gharama
za matibabu haya majanga yote ni matukio ya kila siku kwa binadamu ambayo
hayatabiriki na yote yanaaangukia kwenye mpango wa hifadhi ya jamii. Hivyo ni
kitu cha asili ya kwamba kila mtu lazima apewe hifadhi ya jamii na lazima aijue
inamsaidiaje katika maisha yake ya kila siku kama sehemu ya maisha ya mwanadamu
Pamoja
na hayo ikumbukwe ya kuwa pensheni zinazotolewa na mifuko iliyopo hapa nchini hazitoshelezi
mahitaji ya watanzania wakiwemo wastaafu na familia zao. Takwimu zilizotolewa mwaka 2012 zinaonesha ya
kuwa ni watu milioni 1.7 tu ndio waliojiunga na
mifuko ya hifadhi ya jamii wakati idadi ya watanzania wote ni milioni 44.9 hii
ikiwa ni asilimia 6.5 tu ya nguvu kazi yote ya watu milioni 23.7. Hivyo ni kwamba asilimia 93.5 ya watanzania
wote wanaotegemewa kuwa ni milioni 44.9 hawana kinga ya hifadhi ya jamii ya
aina yeyote.
Hifadhi ya Jamii ni haki ya kila Mtanzania. Haki hii imeanishwa wazi katika Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 11(1) na Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003.
Haki
hii pia imeiainishwa kwenye mkataba wa kimataifa wa haki za binadamu wa mwaka
1948 pamoja na mikataba ya shirika la kazi duniani (ILO) ibara ya 102 ya mwaka
1952.
Mfuko wa pensheni wa PSPF ni taasisi
ya hifadhi ya jamii iliyoanzishwa kwa sheria Namba 2 ya mafao la hitimisho la
kazi kwa watumishi wa umma ya mwaka 1999
Mabadiliko katika sekta ya hifadhi
ya jamii nchini yamepelekea kuwepo na mabadiliko ya sheria ya mfuko wa
pensheni wa (PSPF). Sheria ya Mfuko wa pensheni wa
PSPF sasa unaruhusu kusajili wanachama katika sekta zote za umma na binafsi. Na
kwa sasa mfuko una mipango miwili ya uchangiaji wa lazima yaani PSPF Mandatory Scheme na mpango
wa uchangiaji wa hiari yaani PSPFSupplementary
Scheme yaani kwa kifupi PSS
Mwanachama wa mpango huu anastahili kulipwa
michango pamoja na faida itakayopatikana kutokana uwekezaji ambayo huwekwa
katika akiba mara mbili kwa mwaka yaani kwa mwezi wa Januari na Julai.
Mpango huu wa hiari ni mahususi kwa ajili ya kuwapatia
huduma ya hifadhi ya jamii wale wote ambao awali kutokana na matakwa ya kisheria
hawakuweza kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii. Watanzania wanatakiwa kuitumia fursa hii kujiwekea akiba ya ziada hata
kwa wale ambao tayari wamo katika mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii hii
itawasaidia kujiongezea na kutunisha na hivyo kunufaika na mafao ya muda mrefu
na ya muda mfupi wakati wanapoendelea kufanya kazi na kuweza kuwa na akiba za ziada baada ya kustaafu.
.
Katika mpango huu wa uchangiaji wa
hiari wa wa pensheni wa PSPF, mwanachama
anapaswa kuchangia si chini ya Tshs 10,000 au zaidi kwa mwezi. Michango inaweza
kuwasilishwa kwa siku, wiki, mwezi au awamu. Mwanachama anawekewa gawio la
akiba yake kwa kila mwaka mara moja. Uanachama ni kwa watanzania wote na wasio
watanzania wanaofanya kazi nchini na hata waliopo nje ya nchi.
Mpango huu wa hiari umeanzishwa na
mfuko wa pensheni wa PSPF kwa ajili ya kupanua wigo wa uwanachama kwa
kuandikisha wananchi waliojiajiri au kuajiriwa katika sekta rasmi na isiyo
rasmi na kuwawezesha wale wote ambao hapo awali hawakuweza kupata huduma ya
hifadhi ya jamii kutokana na kutokua na ajira
Hifadhi ya jamii ni haki ya kila mtu na si kwa
wale tu walio katika ajira rasmi ila hata kwa wale waliojiajiri wenyewe na hata
kwa wale ambao ni wanachama wa katika mifuko ya hifadhi ya jamii nchini kuweza
kuwa na akiba ya ziada.
Kwa sababu mpaka sasa kulingana na takwimu
zilizotolewa mwaka 2012 idadi ya watanzania wote ni milioni 44.9 ambao kati yao
watu milioni 1.7 tu ndio waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii, hii ikiwa
ni asilimia 6.5 tu ya nguvu kazi yote ya watu milioni 23.7 na ndiyo
maana mfuko wa pensheni PSPF wana mpango wa uanachama wa hiari kama mkakati wa
makusudi juu ya kupanua wigo wa hifadhi ya jamii ili kuhakikisha ya kuwa hata
wale waliojiajiri kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii kwa hiari na hata wale
wanachama wa mifuko iliyopo kuweza kuwa na akiba ya ziada ya kutosha kwa
baadaye.
Uanachama
wa mpango huu wa hiari wa PSPF ni kwa raia na asiye raia wa Tanzania anayefanya
kazi nchini na nje ya nchi hivyo hauna ubaguzi nchi wala wa rangi ya mtu. Mfanyakazi
anapaswa kuwa mwanachama wa mfuko mmoja tu katika mpango wa lazima, lakini ana
haki ya kujiunga na mpango wa hiari zaidi ya mmoja kama huu wa mfuko wa
pensheni wa PSPF.
Aina
za mafao yanayo tolewa na mpango huu wa hiari chini ya mfuko wa pensheni wa
PSPF ni kama vile fao la uzeeni, fao ya kuumia kazini, fao la kifo, fao la
elimu, fao la ujasiriamali, fao ya urithi, fao ugonjwa/ulemavu, na fao la
kujitoa. Mafao haya hutolewa na kunufaika sawasawa bila kujali ya kuwa
mwanachama anachangia kwa hiari au kwa lazima kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii.
Hivyo
mtu yeyote aliyejiajiri, mkulima, mvuvi, mfanyakazi wa ndani, wafanya biashara
wadogo wanaweza kujiandikisha kwa hiari na kulipa kadri ya uwezo wake wa mapato
kwenye mfuko wa pensheni wa PSPF. Uchangiaji katika mpango huu wa hiari wa PSPF
wanachama wana uhuru wa kuchagua
jinsi ambavyo wanaweza kuwasilisha michango yao, iwapo ni kwa wiki Mwezi au kwa
msimu kutegemea na upatikanaji wa kipato cha ziada kwa ajili ya akiba na
michango huwasilishwa moja kwa moja kupitia akaunti ya benki au wakala wa
malipo wa M-pesa, Tigo-pesa na Airtel money.
“Nimejiunga kuwa mwanachama wa hiari katika Mfuko
wa Pensheni wa PSPF, kwa kuwa kuna utaratibu baada miezi 12 ambapo unaweza
kuchukua fedha zako za kuanzishia biashara au kulipia ada za watoto shuleni au
chuoni,” anaanza kueleza mfanyakazi wa shirika la bandari Tanzania ambaye hakutaka kutaja jina
lake alipozungumza na gazeti hili la majira
Mwanachama huyu ambaye ni mwanachama wa mfuko wa
hiari wa PSPF ambaye yuko kituo cha bandari ya Mtwara, anasema ni muhimu kwa
wajasiriamali na watu wengine walio katika sekta isiyo rasmi kujiunga na mfuko
huu wa PSPF ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zilizopo kwa kwamba
yeye ana wasilisha michangi yake kwa wiki, mwezi au msimu kutegemeana na
upatikanaji wa kipato cha ziada kwa ajili ya akiba.
Mtu yeyote anaweza kuwa mwanachama kwa
kujiunga na mpango huu wa hiari kwa kujaza formu PSS FN.1 na kuambatanisha picha
moja ya rangi yaani passport size pamoja na taarifa muhimu za wanachama kama
vile; majina; tarehe ya kuzaliwa; anwani
na nambari za simu; shughuli au kazi na mara baada ya kukamilisha usajili,
mwanachama hupewa kitambulisho na nambari ya uanachama
Katika mpango huu wa
uchangiaji hiari wa mfuko wa pensheni wa PSPF mwanachama akisha anza kuchangia
naye anakuwa na haki ya kupata mafao yote yatolewayo na mpango huu wa hiari wa
PSPF.
Mafao katika mpango huu wa hiari
mwanachama huwa anastahili kulipwa michango pamoja na riba inayokokotolewa kwa
mujibu wa viwango vya riba vilivyoko katika soko kulingana na mfumuko wa bei na
kwamba riba ambayo ni asimilia sita (6) huongezwa katika akiba ya mwanachama
mara mbili kwa mwaka katika miezi ya Januari na Julai. Mwanachama wa mpango huu wa hiari wa
PSPF anapolazimika kuchukua michango yake yote na faida kutokana na sababu
zozote zile, anaweza tena kuchangia upya bila masharti yoyote.
No comments :
Post a Comment