Friday, May 3, 2013

Changamoto za mfanyakazi mpya wakati wa kuchangua mfuko wa pensheni wa kujiunga nao










 



















na christian gaya -majira
kwa mujibu wa kifungu cha 30 cha Sheria ya usimamizi na udhibiti wa sekta ya hifadhi ya jamii na sheria za mifuko kama zilivyorekebishwa, mfanyakazi ambaye hajawahi kujiunga na mfuko wowote wa pensheni au anayeajiriwa kwa mara ya kwanza anao uhuru wa kuchagua mfuko wowote kati ya mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii. Hii ina maana mfanyakazi anapaswa kuwa mwanachama wa mfuko mmoja tu wa pensheni. Kifungu hicho kinaendelea kusisitiza ya kuwa ni makosa makubwa kwa mfanyakazi mpya kujiunga au kujiandikisha kwenye mifuko zaidi ya mmoja wa pensheni. 



Hiki ni kitu kizuri ili kuleta ushindani  zaidi kwa mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii nchini na kuleta uwiano wa wanachama. Na huenda hii inaweza kusaidia changamoto ya kuongezea idadi kubwa ya wanachama kwenye mifuko hii ya hifadhi ya jamii hasa kutoka katika sekta isiyokuwa rasmi  ambayo kwa muda mrefu imesahaulika na badala ya kuegamia sheria zilizoanzisha mifuko hii ya pensheni. Kwa sababu mpaka inakisiwa  kuwa idadi ya watanzania wote inakisiwa kuwa ni milioni 45.


Je mfuko wa pensheni una mpango wa kutoa angalau theluthi mbili ya mafao ya pensheni ya mwanachama kama amana ya kupatiwa mkopo wa nyumba? 


Kati ya hawa asilimia 70 wako maeneo ya vijijini. Na idadi ya nguvu kazi ya watanzania inakisiwa kuwa ni milioni 16 ambapo asilimia 5.4 ya nguvu kazi au asilimia 2.7 ya idadi yote ya watanzania ndiyo iliyojiunga na mfumo kamili wa lazima wa hifadhi ya jamii. Na asilimia 93 ya nguvu kazi yaani ya watu wanaojiweza kufanya kazi imejikita kufanya kazi kwenye sekta isiyo kuwa rasmi kwa sehemu zote za mijini na vijijini. Na asilimia 80 ya hao ambao wamo kwenye sekta isiyo rasmi wanashughulika na kilimo


Inayokisiwa kuwa ni milioni 1.0 hii ni asilimia 5.4% ya nguvu kazi yote ambayo ni kama milioni 16 ya Watanzania wote. Hii ina maana yakuwa karibu milioni 15 ya nguvu kazi inashughulika na sekta isiyo rasmi na wote wako katika hali hatarishi kwa vile hawana kinga yeyote ya hifadhi ya jamii


Hifadhi ya jamii ina maana ni aina ya hatua madhubuti au shughuli zilizobuniwa za kuhakikisha kuwa wananchi wa jamii hiyo wanapata mahitaji yao ya lazima na ya msingi  na wanapewa kinga ya hifadhi ya kutokana na majanga ili kuwawezesha kuwa na kiwango cha maisha ya kuishi kulingana na mila na desturi za jamii


Na lengo kubwa la hifadhi ya jamii ni kuzuia umasikini, kupunguza au kuondoa umasikini, kuifidia jamii, kugawanya mapato sawasawa kwa wanajamii. Masuala mengi yanayogusa hifadhi ya jamii ni ya nyeti sana, yanagusa ni kiini muhimu sana cha wafanyakazi kwenye sekta rasmi na sekta zisizo rasmi hasa za watu masikini pamoja na sekta ya bima za jumuiya za waajiri


Mfumo wa hifadhi ya jamii ambayo ni ya lazima kisheria ambayo wafanyakazi pamoja na mwajiri wanachangia pamoja na kupeleka michango kwenye chombo cha mfuko wa pensheni (pension fund) au mfuko wa akiba ya wafanyakazi (provident fund). 


Taasisi za hifadhi ya jamii ya jamii nchini Tanzania zimekuwa zikiwekeza orodha ya fedha kwa faida kwenye mikopo, nyumba za kupangisha, hatifunganishi, kuweka akiba benki zote hizi zimechangia maendeleo.
Kumekuweko na ongezeko dogo sana la kuelewa juu ya mfumo wa hifadhi ya jamii hasa juu ya mafao yanayotolewa, jinsi ya kujiunga kuwa wanachama, vitega uchumi na shughuli mbalimbali za sekta. Mapungufu yaliyomo kwenye mfumo huu wa hifadhi ya jamii ambayo yanahitajika kutatuliwa na sera hii ya hifadhi ya jamii. Watu waliomo katika mifuko hii ya hifadhi ya jamii ni wale tu ambao wameajiriwa kwenye sekta iliyo rasmi 
 

Hivyo kama mfanyakazi utahitaji kujifunza ili kujua na kuzingatia mambo muhimu kabla ya kufanya maamuzi ya kujisajili na mfuko wa pensheni wa hifadhi ya jamii wowote ule. Najua kila mmoja wetu anaweza kuwa na lengo lake la kutaka kujiunga na mifuko hii ya pensheni. Na wawekezaji wengi mara nyingi hutumia vigezo vya takwimu au vigezo vya kifedha, na vigezo vingine au taarifa nyinginezo mbali na fedha. Hivyo kuna vigezo muhimu hata kama utasikia habari au ripoti kwenye runinga, magazeti, rafiki, redio n.k. kutoka sehemu tofauti kuhusu uzuri wa mfuko fulani wa pensheni ya hifadhi ya jamii hakikisha kwanza unaupima kwanza kwa vigezo vyako.

No comments :

Post a Comment