Saturday, December 17, 2022

MHE. JENISTA AKEMEA TABIA YA WAAJIRI SERIKALINI KULIPA MADENI YA WAKUU WA IDARA PEKEE NA KUYAACHA YA WATUMISHI WENGINE

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na watumishi wa umma katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika halmashauri hiyo. 

Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukamba akitoa salamu za mkoa wake kabla ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama kuzungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika halmashauri hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Mhe. Jerry Muro akieleza hali ya Utumishi wa Umma katika wilaya yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya waziri huyo iliyolenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi katika Wilaya ya Ikungi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Bi. Martha Mlata katika Ofisi za CCM mkoani humo, mara baada ya Waziri huyo kuwasili mkoani Singida kwa ajili ya ziara ya kikazi.

No comments :

Post a Comment