Waziri wa Fedha na Mipango Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba na Mwakilishi wa Benki ya Dunia nchini, Bw. Nathan Belete (kushoto), wakiwaonesha wanahabari, mikataba ya mikopo nafuu ya dola za Marekani milioni 535 sawa na shilingi trilioni 1.24, kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo. Kulia ni Waziri wa Nishati Mhe January Makamba.
Benki ya Dunia imeipatia Tanzania mikopo nafuu ya jumla ya dola za Kimarekani Milioni 535 sawa na shilingi za Kitanzania trilioni 1.24 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya
maendeleo.Hafla ya kutia saini mikataba hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Hazina jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba na Mwakilishi wa Benki ya Dunia hapa nchini Bw. Nathan Belete ambapo pia Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba alihudhuria.
No comments :
Post a Comment