Mkurugenzi Mtendaji wa DART Dk.Edwin Mhede akizungumza wakati Kamati ya Bunge ya Utawala wa Serikali za Mitaa na Serikali za Mikoa (USEMI) ilipotembelea Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Utawala wa Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa Abdallah Chaurembo wakifurahi jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa DART Dk.Edwin Mhede mara baada Dk.Mhede kumkabidhi zawadi ya kikombo kwa niaba ya Kamati nzima
Kamati ya Bunge ya Utawala wa Serikali za Mitaa na Serikali za Mikoa (USEMI)wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa DART Dk.Edwin Mhede wakati wa ziara ya kamati katika Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam.
Kamati ya Bunge ya USEMI ikiwa katika ziara ya miundombinu mbalimbali ya DART.
Kamati ya Bunge ya Utawaka Serikali za Mitaa na Tawala Mikoa (USEMI) wakipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Usafirishaji wa DART Mhandisi Fanuel Kalugendo akitoa maelezo huhusiana na miundombinu ya huduma za usafirishaji wa abiria katika jiji la Dar es Salaam.
Kamati ya Bunge ya Utawala wa Serikali za Mitaa na Serikali za Mikoa (USEMI) wakiwa katika usafiri wa mabasi yaendayo haraka wakati kamati hiyo ilipotembelea Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam.
*Wajumbe wa Kamati wapongeza DART kwa ufanisi wa kazi, DART na UDART watakiwa kukutana na kamati hiyo kunoana
Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
Wakala wa Usafiri wa Mabasi yaendayo Haraka (DART) umesema kuwa usafiri wa mabasi yaendayo haraka kwa Barabara kuanzia Mbagala kuelekea Gerezani kuanza Machi 23.
Hayo ameyasema Mkurugenzi Mtendaji wa DART Dk.Edwin Mhede wakati Kamati ya Bunge ya Utawala wa Serikali za Mitaa na Serikali za Mikoa ilipotembelea mradi huo jijini Dar es Salaam kwa kuangalia mifumo mbalimbali ya Wakala huo.
Dk.Mhede amesema wakala huo unajivunia mifumo ya ukusanyaji mapato ambapo imeongezeka kutoka sh.bilioni 1.8 hadi kufikia sh.bilioni Tatu kwa Mwezi.
Amesema mifimo hiyo imetengenezwa na wataalam ambao ni watanzania ambapo umesaidia kuokoa fedha ya serikali.
Aidha Dk.Mhede amesema kuwa malengo ambayo wamejiwekea ni kuhakikisha wanakwenda kutoa huduma bora ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam ambayo itachochea na uchumi kukua.
Kamati hiyo baada ya kupata taarifa za DART imeiagiza DAR na UDART kukutana na kamati hiyo na kuwapa maelezo ya kina pamoja na sheria ilioanzisha mradi huo ambapo ndipo wanaweza kushauri serikali kama kuna jambo la kufanya.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Abdallah Chaurembo ambaye ni Mbunge wa Mbagara amesema kuwa mradi huo uko vizuri na kushauri waendelee kuboresha baadhi ya kasoro.
Mjumbe wa Mjumbe wa Kamati na Mbunge wa Urambo Magreth Sitta ameiopongeza DART kwa kazi nzuri wanayoifanya katika utoaji wa huduma ya usafiri katika jiji Dar es Salaam.
Nae Mjumbe wa Kamati hiyo Mwantum Haji amesema kuwa DART wanafanya kazi nzuri ambayo matokeo yake yanaonekana katika usimamizi wa maradi huo na kuongeza kuwa wanaupiga Mwingi.






No comments :
Post a Comment