SERIKALI imetaja hatua inazokusudia kuchukua ili kupunguza bei za bidhaa nchini.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt.Mwigulu Lameck Nchemba wakati wa mkutano wa pamoja (joint press conference) na
Waziri wa Uwekezaji, viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji jijini Dar es Salaam.Baadhi ya hatua hizo Dkt. Nchemba alitaja "Tutapunguza kodi ya sukari kwa kiwango so chini ya asilimia 10%, baada ya hapo tutaangalia mwezi mmoja au miwili na tutakapokuwa tunapitisha sheria mpya ya kodi tutaangalia mambo yanaendeleaje." Alisema.
"Tutapunguza sehemu ya gharama ambayo ilikuwa inaongezeka katika vifaa vya usafiri, tukipunguza gharama kwenye mafuta na vifaa hivyo moja kwa moja tunaamini itashusha gharama na bei za bidhaa nyingine,"alisisitiza Mhe. Waziri wa Fedha.
Pia alisema, Serikali itaangalia gharama ambazo zinaihusu kwenye mafuta ili kuona kiwango ambacho itapunguza.
"Timu yetu ya wataalamu itakaa ndani ya wiki moja na inaweza kuwa imeshapata jibu ili tuweze kuchukua hatua." Alibainisha Dkt. Nchemba.


No comments :
Post a Comment