Saturday, December 4, 2021

Shemdoe - Wanaofanya Kazi Za Ununuzi Na Ugavi Wasajiliwe Na Bodi Ya PSPTB

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe  akizungumza na Wataalam wa Ununuzi na Ugavi pamoja na wafanyakazi wa Bodi hiyo kuhusu namna walivyojipanga kuwasimamia na kuisimamia taaluma hiyo ili kuwa na tija kwenye maendeleo ya Taifa wakati wa kufunga Kongamano la 12 Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi  lililokuwa na kauli mbiu ya  kujadili ubunifu wenye suluhisho katika utekelezaji wa Ununuzi na Ugavi kwa kutambua ushindani na mapinduzi ya Viwanda kwa maendeleo ya Jamii. Kongamano hilo lililoanza Novemba 30 hadi Desemba 03 mwaka 2021.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) Godfred Mbanyi akizungumza wakati na Wataalam wa Ununuzi na Ugavi pamoja na kumkaribisha mgeni rasmi Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe aliyemwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Ummy Mwalimu kwa ajili ya kufunga Kongamano la 12 la mwaka la Wataalam wa Ununuzi na Ugavi.
Baadhi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi  wakifuatilia mada kwenye Kongamamo la 12 la wataalam hao lililoanza Novemba 30 hadi Desemba 03 mwaka 2021 likiwa na kauli mbiu ya  kujadili ubunifu wenye suluhisho katika utekelezaji wa Ununuzi na Ugavi kwa kutambua ushindani na mapinduzi ya Viwanda kwa maendeleo ya Jamii. 
Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma ( PSPTB), Shamim Mdee akizungumza jambo kwenye kongamano la 12 la mwaka la Wataalam wa Ununuzi na Ugavi 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe akiwa kwenye picha ya pamoja na makundi mbalimbali mara baada ya kufunga Kongamano la 12 la Mwaka la  Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi  lililofanyika jijini Arusha.

No comments :

Post a Comment