Tuesday, November 16, 2021

MAKAMU WA RAIS AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI MKUU WA SINGAPORE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akimkabidhi zawadi ya picha yenye mchoro wa Mlima Kilimanjaro Naibu Waziri Mkuu wa Singapore Mhe. Heng Swee Keat mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao yaliofanyika eneo la Shenton Way Nchini Singapore. Novemba 16,2021.

Naibu Waziri Mkuu wa Singapore Mhe. Heng Swee Keat akimuonesha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango Mandhari pamoja na namna nchi ya Singapore ilivyopangiliwa katika ujenzi wa Majengo na Miundombinu katika eneo la Shenton Way. Novemba 16, 2021.



Naibu Waziri Mkuu wa Singapore Mhe. Heng Swee Keat akimkabidhi zawadi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao yaliofanyika Shenton Way nchini Singapore. Novemba 16,2021.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza na Naibu Waziri Mkuu wa Singapore Mhe. Heng Swee Keat, mazungumzo yaliofanyika katika Ukumbi wa Treasury 100 eneo la Shenton Way Nchini Singapore. Makamu wa Rais yupo nchini Singapore kuhudhuria Mkutano wa Jukwaa la Majadiliano ya Kiuchumi (Bloomberg New Economy Forum 2021 ). Novemba 16,2021.

No comments :

Post a Comment