Wednesday, September 1, 2021

CHAMURIHO AWATAKA TANROADS KUTOA ELIMU

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akizungumza na menejimenti na mameneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), kutoka mikoa yote Tanzania (hawapo pichani), katika kikao kazi cha wakala huo kilichofanyika jijini Dodoma.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mhandisi. Rogatius Mativila, akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho (hayupo pichani), kufungua kikao kazi cha uongozi na Mameneja wa TANROADS kutoka mikoa yote nchini, jijini Dodoma.
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Nkolante Ntije, akichangia mada katika kikao kazi cha menejimenti na mameneja wa TANROADS kutoka mikoa yote nchini na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, jijini Dodoma
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akiwa katika picha ya pamoja na menejimenti na mameneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), kutoka mikoa yote nchini mara baada ya kufungua kikao kikazi, jijini Dodoma

No comments :

Post a Comment