Tuesday, June 8, 2021

WADAU WA JUKWAA LA MAJI BONDE LA PANGANI WATAKIWA KUTOA ELIMU YA KUTOSHA KWA WANANCHI.

KATIBU mkuu wa wizara ya maji,Antony Sanga akizungumza katika mkutano huo wa jukwaa la wadau wa bonde la Pangani Leo jijini Arusha (Happy Lazaro).

Mkurugenzi wa bonde la Pangani ,Segule Segule akizungumza na wadau mbalimbali katika mkutano huo unaofanyika jijini Arusha leo.(Happy Lazaro)
**********************************
Happy Lazaro, Arusha.
Arusha.Wadau  wa jukwaa  la Bonde la Pangani wametakiwa kuhakikisha wanatoa ushirikiano  katika kutoa elimu ya kutosha kuwaelimisha wananchi juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji katika maeneo yao.
Hayo yamesemwa leo na Katibu wa wizara ya Maji ,Antony  Kasanga wakati akifungua mkutano wa wadau wa jukwaa la bonde la Pangani linalofanyika jijini Arusha na kuwashirikisha wadau mbalimbali.
Aidha mkutano huo una lengo la kujadiliana matatizo na fursa zilizopo katika bonde la Pangani huku akisema kazi ya bodi hiyo ni kubwa ,hivyo bila ushirikiano wa wadau  ni ngumu kufanyika kwa utekelezaji wenye tija.
“kazi ya Bodi ni kupima, kutunza na kugawa maji lakini kila mmoja wetu ana wajibu wa kutoa ushirikiano katika hili hasa tukikumbuka kuwa vyanzo vya maji haviongezeki ila vizazi vinaongezeka hivyo mahitaji ya matumizi ya maji ni makubwa ,tunachopaswa kufanya ni kuvilinda kwa kuwaelimisha wananchi juu ya uvamizi na uchafuzi wa vyanzo hivi” amesema  Kasanga.
Kasanga ameongeza kuwa,jukumu la wizara ya maji ni kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama lakini pia uendelezaji wa rasilimali maji  kuwa endelevu ili kuhakikisha uhaba wa maji unakuwa historia ambapo amesema wizara pekee haitatosha kubeba majukumu hayo bali ni kila mmoja kuwajibika katika hayo.
Naye Mwenyekiti wa jukwaa  hilo Taifa Mhandisi Mbogo Futakamba amesema ni hatua kubwa kuwa na jukwaa ambalo kwa sasa limeanza mikutano yake kisheria huku akisema mkutano huo ndio wa kwanza  tangu kuundwa kisheria kwa jukwaa hilo ambalo kupitia jukwaa hilo wanatarajia kujadili namna bora ya utatuzi wa migogoro katika mabonde tisa huku na kuwa  tayari mabonde saba yameshaanza mpango wa utekelezaji wa  hatua hizo.
Mkurugenzi wa rasilimali za maji ,George Lugomela  alitaja malengo mengine ya mkutano  huo kuwa ni kujenga uelewa  wa rasilimali za maji , kujadili upatikanaji wa fedha za kuendesha jukwaa hilo na Usimamizi wa maji, pamoja na  kuchangiza utunzaji wa vyanzo vya maji.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bonde la Pangani ,Segule Segule amesema halmashauri 22 zipo chini yake kwa maana ya kanda ya kaskazini  ambazo zinahitajika kusimamiwa vizuri ili kuwa na rasilimali maji endelevu hivyo umuhimu wa mkutano huo una nafasi kubwa kwa  wadau wa maji. 
” lengo letu ni kutunza rasilimali ziwe endelevu katika Halmashauri zote za kanda , lakini pia tunalenga kushirikishana matatizo na fursa zilizopo katika Bodi ya Maji bonde la Pangani katika Jukwaa hili” amesema Segule.

 

No comments :

Post a Comment