Thursday, June 10, 2021

RAIS DK.MWINYI AFUNGUA MKUTANO MKUU WA MADAKTARI WA UPASUAJI TANZANIA.(TSA)

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akisalimiana na Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Madaktari wa Upasuaji (TSA) Tanzania alipowasili katika Viwanja vya Hoteli ya Madinat -Al-Bahar Mbweni nje ya Jiji la Zanzibar kufungua Mkutano wa Mkuu wa madaktari wa Upasuaji Tanzania (TSA) leo (katikati) Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Nassor Ahmed Mazrui.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akifuata na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Nassor Ahmed Mazrui (katikati) pamoja na Viongozi wengine mara alipowasili katika Hoteli ya Madinat -Al-Bahar Mbweni nje ya Jiji la Zanzibar kuufungua Mkutano wa Mkuu wa Madaktari wa Upasuaji Tanzania (TSA) ulioanza leo .

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (mbele wa tatu kushoto) akitoa hutuba yake wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Mkuu wa madaktari wa Upasuaji Tanzania (TSA) alioufungua leo katika ukumbi wa Hoteli ya Madinat -Al-Bahar Mbweni nje ya Jiji la Zanzibar(kushoto mbele) Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Nassor Ahmed Mazrui (kushoto)alipokuwa akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (wa pili kulia) kuufungua rasmi wa Mkutano wa Mkuu wa madaktari wa Upasuaji Tanzania (TSA) leo katika ukumbi wa Hoteli ya Madinat -Al-Bahar Mbweni nje ya Jiji la Zanzibar (katikati) Rais wa Chama cha  Madaktari wa Upasuaji Tanzania (TSA) Prof. Catherine Mngongo. 

 Baadhi ya washiriki katika Mkutano Mkuu wa madaktari wa Upasuaji Tanzania (TSA) wakiwa katika ukumbi wa Mkutano wa Hoteli ya Madinat AL Bbahar wakimsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani ) alipokuwa akitoa hutuba yake ya ufunguzi  rasmi wa Mkutano huo ulioanza leo.

Mkurugenzi katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Dk.Marijani Msafiri alipokuwa akitoa maelezo  wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 26 wa Madaktari wa Upasuaji Tanzania (TSA) ulioanza leo katika Hoteli ya Madinat Al Bahar, Nje ya Jiji la Zanzibar na kufunguliwa rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati). [Picha na Ikulu

 

No comments :

Post a Comment